Facebook Comments Box

Saturday, August 9, 2014

WABUNGE WA YANGA WALIVYO WANYANYASA WABUNGE WA SIMBA

Kikosi cha Yanga kilichokwaana na Simba na kuibuka na ushindi wa 3-2.

Kikosi cha Simba kilichopigwa 3-2 na Yanga.
Mechi ya wabunge mashabiki wa Simba na Yanga iliyopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini 2014 imemalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-2. 

Wafungaji Simba: Maji Marefu na Yusuf Gogo. 

Yanga: Idrissa Kitwana, Ahmed Ngwali na Mark Tanda.
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akishangilia na shabiki wake baada ya ushindi wa Yanga.
Mwigulu Nchemba akiwarushia skafu yake mashabiki wa Yanga.
Ridhiwan Kikwete akishangilia ushindi wa Yanga dhidi ya Simba.
Mbunge wa Jimbo la Chalinze ambaye ni shabiki wa Yanga, Ridhiwan Kikwete akivua jezi yake kwa ajili ya mashabiki mara baada ya ushindi wa timu yake wa mabao 3-2 dhidi ya Simba leo.
Hekaheka wakati wa mtanange huo.
Mashabiki wakifuatilia mtanange huo.
Timu zikiingia uwanjani.
Ridhiwan akiwapa hi mashabiki.
Waamuzi wakiingia uwanjani.

Mwamuzi Othman Kazi akiongea na manahodha wa Yanga na Simba (Wabunge).


RAIS KIKWETE NA MAMA SALMA WATEMBELEA MAKTABA YA KIRAIS YA RAIS BUSH

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea Maktaba ya Kirais ya Rais Bush (Bush Presidential Library) sehemu ambayo imejengwa kwa mfano wa Ikulu ya Marekani, White House, hususan katika bustani y a Waziri (Rose Garden) pamoja na ofisi ya Rais wa Marekani, Oval office
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea Maktaba ya Kirais ya Rais Bush 

 (Bush Presidential Library) sehemu ambayo imejengwa kwa mfano wa Ikulu ya Marekani, White House, hususan katika bustani y a Waziri (Rose Garden) pamoja na ofisi ya Rais wa Marekani, Oval office

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea Maktaba ya Kirais ya Rais Bush (Bush Presidential Library) na kujionea nafasi kubwa iliyotolewa kwa Tanzania na zawadi ambazo Rais Bush alizipata katika ziara yake rasmi ya Tanzania wakati akiwa Rais wa Marekani. Maktaba hiyo ya kuvutia inaendeshwa kwa teknolojia ya kisasa kabisa ya habari na mawasiliano.

Rais Kikwete alikuwa amesimama mjini Dallas kwa muda akiwa njiani kutoka Washington D.C., kwenda Houston, jimbo hilo la Texas kuhudhuria mkutano wa wafanyabiashara wa mafuta na gesi ambao wanataka kuwekeza katika sekta hiyo hapa Tanzania.

Rais Kikwete amekuwa Marekani kwa ziara ya kikazi ya siku tisa, ambako miongoni mwa mambo mengine, amehudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Marekani na Afrika uliofikia kilele chake jana kwa kikao kilichoendeshwa na Rais Barack Obama wa Marekani katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani mjini Washington D.C.



Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea na kujionea vitu mbalimbali ambavyo Rais mstaafu George W. Bush alipewa kama zawadi kutoka Tanzania ambavyo vimehifadhiwa katika Maktaba ya Kirais ya Rais Bush (Bush Presidential Library)

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea na kujionea vitu mbalimbali ambavyo Rais mstaafu George W. Bush alipewa kama zawadi kutoka Tanzania ambavyo vimehifadhiwa katika Maktaba ya Kirais ya Rais Bush (Bush Presidential Library)

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea sehemu ya mfano wa ofisi ya kupangia mikakati ya Ikulu ya Marekani iliyotumika na Rais MStaafu George W. Bush kwenye Maktaba ya Kirais ya Rais Bush (Bush Presidential Library)





BONGO FLEVA WAWANYAYASA BONGO MOVIES

Mchezaji wa Bongo Fleva, Ali Kiba akimtoka msanii wa Bongo Movies, Issa Mussa ‘Cloud 112′.

Mwanamuziki H-Baba akijaribu kuwatoka wachezaji wa Bongo Movies.
Nyomi ndani ya Uwanja wa Taifa ikifuatilia mechi hiyo.
 Kikosi cha Bongo Movies.
Kikosi cha Bongo Fleva.
 Bongo Fleva wakisalimiana na Bongo Movies kabla ya mechi.

 Bongo Movies kabla ya kuanza mtanange dhidi ya Bongo Fleva.

Kikosi cha timu ya Bongo Fleva kimeibuka kidedea katika mtanange wao dhidi ya Bongo Movies kwenye Tamasha la Usiku wa Matumanini 2014 ndani ya Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Mfungaji wa bao pekee la Bongo Fleva ni mwanamuziki Ali Kiba.


LORI LAPINDUKA KIBAHA





KIBONDE MBARONI

Kibonde akiwa chini ya ulinzi
Na mwandishi wetu mtaani;

Kibonde wa Clouds anadaiwa kusababisha ajali asubuhi hii eneo la Makumbusho, amemgonga dereva mwingine kwa nyuma. Trafiki walipofika kupima ajali, Kibonde karudi nyuma kaendesha gari lake kasepa! Trafiki katumia gari lililogongwa kumfukuzia. 

Walifanikiwa kumkamata eneo la Mwenge. Trafiki aliingia ktk gari lake nakumwomba arudi eneo la ajali ili wakapime na kuchora mchoro wa ajali. 

Kibonde kagoma na kumtaka trafiki ashuke ktk gari lake, trafiki naye kagoma kushuka. Mchezo ulioendelea Kibonde aliondoa gari na kuanza kupiga misele, akizunguka mitaa akiwa na trafiki huyo! Trafiki aliwasiliana na wenzake ambao walianza kuifuatilia gari hiyo ya Kibonde kila kiunga cha jiji hususani eneo la Mwenge na Ubungo.

kunifuatafuata sio dili achana na mimi
Hayawi, hayawi yakawa, Kibonde akatokea maeneo ya mataa ya Ubungo, hapo nikashuhudia senema ya Kibonde na trafiki! Trafiki wa kike aliyekua eneo hilo akaipiga mkono gari ya Kibonde iliyokuwa kasi, gari hiyo haikuonesha dalili za kupunguza mwendo.

 Trafiki alikomaa kusimama mkono wake ukiwa juu kuashiria kumtaka Kibonde asimame huku akipaza sauti ktk radio call akisema ananigonga, afande, ananigonga! Akiwa ktk hali hiyo, kuna gari ilikotokea sikujua ikakatisha kati ya trafiki na gari ya Kibonde ndiyo ikawa kigingi cha gari ya Kibonde na kutiwa mbaroni! 

Aligoma kuendesha gari ikabidi livutwe hadi polisi Urafiki ambapo kwa sasa amepelekwa Oystabay! Kwa utafiti wangu kidogo nilioufanya nikifukuzana na muda kuwahi kanisani, ni kwamba Kibonde na watu wengine aliokuwanao ndani ya gari lake walikuwa 'TINGASI'!


Wednesday, July 30, 2014

ALICHOAMUA KINGWENDU BAADA YA MKEWE KUBAKWA


Muigizaji wa filamu za Kiswahili, mchekeshaji Kingwendu yuko katika wakati mgumu baad aya mkewe kubakwa na jirani yake wakati akiwa amelewa pombe.

Muigizaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa alizipata habari hizo wakati ambapo yuko safarini na majirani walimueleza kilichotokea kuwa mkewe na jirani huyo aliyembaka mida ya saa tano usiku wote walikuwa wamelewa.

”Kama ulivyosikia hiyo habari, mimi nilikuwa sipo ndo nimerudi jana, nataka nianze kufuatilia sheria sema sasa hivi nimefiwa na dada yangu tunapeleka msiba kijijini na baada ya hapo ninapumzika kesho tu halafu ninasafiri Nairobi, nikirudi Nairobi tarehe tano kuanzia tarehe sita ndo naanza kufuatilia.” Amesema Kingwendu.

Mchekeshajihuyo ameumizwa na kitendo hicho na ameamua kufuata taratibu za kisheria ili haki itendeke.
“Kutokana na kitendo alichokifanya na mimi nimejisikia vibaya, inanibidi nimtafute huyu bwana nimpate ili nimpeleke mahakamani, mke wangu bado niko naye, sema huyu jamaa aliyefanya unyamaa huu yupo jirani.

Mke wangu alikuwa amelewa na jamaa naye  alikuwa amelewa. Mke wangu sijui alikuwa anatoka wapi saa tano usiku ndo akakutana na huyo jamaa, majirani ndio walivyoniambia hivyo, walinipigia simu wakati nipo Shinyanga huko.”

  Source: Bongo5


PICHA: MORO BEST YAPATA AJALI

Basi la Moro Best Mpwapwa kuja Dar limepata ajali na kuua watu 15 hapohapo.




Tuesday, July 29, 2014

TAMASHA LA IDD TABATA SHULE:MECHI WALIO OA NA AMBAO HAWAJAOA

Washindi watarajiwa walio oa wakipanga timu na mikakati.  Hawa ni kutoka misikiti yote ya tabata ya Ansari suna.
Kipa wa walio oa akipangua shuti lilokuwa likielekea langoni kwake.
Beki wa wasela Ustaadh Ramadhan Kabange akienda kuvaa tayari kwa mpambano.



Saturday, July 26, 2014

MAJINA 70 YA WALIOPATA AJIRA YA UHAMIAJI

MAJINA 70 YA WALIOPATA AJIRA
YA MKAGUZI MSAIDIZI WA
UHAMIAJI.

TANGAZO KUITWA KWENYE AJIRA
NAFASI YA MKAGUZI MSAIDIZI WA
UHAMIAJI (ASSISTANT INSPECTOR OF
IMMIGRATION)

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi, anawatangazia wafuatao
waliofaulu usaili wa kujaza nafasi ya
Mkaguzi Msaidizi wa Uhamiaji
(Assistant Inspector of Immigration)
wanatakiwa kuripoti Makao Makuu ya
Idara ya Uhamiaji, Mtaa wa Loliondo
Kurasini, Dar es Salaam tarehe 29 Julai
2014, saa 2:00 asubuhi. Aidha,
wahusika wote wanaelekezwa kufika
kwa wakati wakiwa na vyeti halisi vya
masomo na vya kuzaliwa.
Na
1 Abel Md. Maganya
2.Absolum Stafford Bashigwa
3 Agnes P. Mlay
4 Ali Musa Abdallah
5 Angela Kagaruki
6 Antony J. Nyagilo
7 Asteria Kiyanga
8 Awadhi Issa
9 Aziza Kaku
10 Bakari M. Khamis
11 Baraka Estomihi
12 Beatrice K. John
13 Bernard K. Mwampashe
14 Binasra J. Sabri
15 Charles M. Swai
16 Cosmas J. Mbuguni
17 Dativa J. Ndyetabura
18 David Muna
19 Doroth Ngai
20 Dotto Tabu
21 Emmanuel Gelison
22 Ezekiel A. Kibona
23 Fahamu Saidi
24 Farida Sued
25 Felix Mkemwa
26 Forget N. Charles
27 Frida N.Masomhe
28Gabriel M. Kamugisha
29 Gath E. Nyansambo
30 Gerald Moses
31 Gideon Kihoko
32 Godson Mwanawima
33 Grace C. Nyarata
34 Hamza Sanga
35 Hassan A. Mziray
36 Ibrahim Ally
37 Idd Mgoi
38 Joachim Joseph
39 John G. Mgayambasa
40 Joseph Gregory
41 Kennedy John
42 Khamis Moh'd Khamis
43 Kombo M. Ame
44 Kwame Charles
45 Lawi E. Kumburu
46 Mabrouk H. Thabit
47 Mangunda A. Kaporo
48 Marco Zacharia
49 Maria Agapith
50 Mateso Msigala
51 Meshack Mwaisela
52 Michael John
53 Miriam Mwakamele
54 Mlalama Fortinatus Amlima
55 Mussa Hemedi
56 Mwita Mwikwabe
57 Neema R. Mrope
58 Nyangoma Martin
59 Oscar Philip
60 Pasaka Wilson
61Pastory Packshard Mkongwa
62 Reagan H. Kawa
63 Rose Nseka
64 Senga Ally
65 Silvia Ngasoma
66 Sixtus Stephano Burashahu
67 Steven L. Kweka
68 Wendy Y. Mwalukasa
69 Witness Lwambo
70 Zulu P. Charles
Aidha, ni muhimu kufahamu kuwa
uchaguzi wa walioitwa kwenye ajira
umezingatia yafuatayo:
• Vipaumbele vya Idara ya Uhamiaji;
• Kutoa nafasi kwa waombaji kutoka
Zanzibar;
• Ufaulu kuanzia alama 50 asilimia na
kuendelea;
• Jinsia
Wasailiwa ambao majina yao hayamo
kwenye orodha hii wafahamu kuwa
hawakufanikiwa.
Atakayesoma tangazo hili amjulishe na

mwenzake.
Tangazo hili limetolewa na:
Katibu Mkuu
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
4 Mtaa wa Ohio
11483 Dar es Salaam



Friday, July 25, 2014

TV IMAAN WAPATA LESENI YA KURUSHA MATANGAZO


Hatimae TCRA leo watoa leseni ya urushaji wa matangazo ya Tv kwa TV Imaan na kuwa television ya kwanza afrika mashariki na kati kurusha matangazo yake kwa lugha ya kiswahili.
Tunawatakia mafanikio mema na Allah awaongoze katika kuwatoa watu kwenye giza na kuwapeleka kwenye nuru.
Br Arif Nahad akitoa hutuba
     
Br Arif Nahad na Br Ally ajiraan wakibadilishana mawazo katika hafla ya utoaji wa leseni


Mwenyekiti wa The Islamic Foundation akihojiwa na Jaffar Mponda



Tuesday, July 22, 2014

VIDEO NA PICHA:MABAKI YA MIILI YA BINAADAMU ZAIDI YA 20 YAKAMATWA BUNJU

Hii ndio gari iliyokutwa na mabaki ya miili ya binaadamu ambayo hutumika na wanafunzi wa udaktari kwa mafunzo "cadaver". Miili hiyo ilikuwa inaenda kutupwa kwenye jalala la kawaida.
Haya ndio mabaki ya viungo hivyo
Ki kawaida mabaki ya miili ya binaadamu ambayo hutumiwa na wanafunzi wa udaktari kwa ajili ya upasuaji huchomwa na moto na kuisha yote. ila haya yalikuwa yanatumiwa na wanafunzi  wa udaktari wa IMTU yalipelekwa muhimbili kwa ajili ya kuchomwa ila inasemekana hawakuwa na hela ndio maana muhimbili wakashindwa kuchoma na mwenye gari akaamua kwenda kutupa kwenye jalala la

Hili tatizo linaletwa na serikali kukubali kuzipa ruhusa taasisi na vyuo ambavyo havijajitosheleza. Chuo hakina hospital yake ambayo inaweza kutumika kuwafundishia wanafunzi wake ila unakuta kimepewa ruhusa na kinafanya kazi.

Ushauri wetu serikali ikague upya vyuo vyote vya udaktari ambavyo havina sifa na havijitoshelezi wavifunge.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU