Facebook Comments Box

Friday, May 30, 2014

KIBONZO: USTAADH NA MASHARTI YA KUOA YA SIKU HIZI




ZITTO KABWE ATOA UFAFANUZI JUU YA TUHUMA ZA KUOKOTEZA ZA SUGU


"Maelezo yangu kuhusu kazi za Kigoma AllStars/LEKADUTIGITE kwa NSSF na TANAPA.

Leo tarehe 29 Mei, 2014 Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu Habari, Michezo, Vijana na Utamaduni amenituhumu kuhusika na kinachoitwa ufisadi katika Shirika la TANAPA na NSSF.
Nasikitika kwamba katika hali niliyonayo ya kumwuguza mama yangu naingizwa kwenye siasa za majitaka. Kwa sasa nitatoa maelezo kwa ufupi ili kuondoa upotoshaji.
Kampuni ya LekaDutigite inamilikiwa na wasanii 15 ambapo kila mmoja ana hisa 5% ambazo niliwalipia ili waweze kushirikiana katika kazi zao. Hisa 25% zilizobakia zinamilikiwa na kampuni ya Gombe Advisors ambayo ni kampuni isiyofanya faida (Company limited by guarantee) na haina maslahi yeyote ya kibiashara (not for profit company). Hivyo Mimi binafsi sina maslahi yeyote ya kifedha zaidi ya kuwasaidia wasanii hawa katika kazi zao mbalimbali.
Wasanii wa Kigoma AllStars wamefanya kazi na TANAPA na NSSF, kazi ambazo zinajulikana na zipo. Kwa upande wa TANAPA wasanii hawa waliandaa kazi ya kuitangaza Hifadhi ya Saadani na walilipwa. Kwa upande wa NSSF wasanii hao walitunga wimbo na video yake ( http://m.youtube.com/watch?v=sMl8T-RkIdM ) na wimbo huo unatumika katika Shirika hilo.
Vile vile walifanya matamasha mbalimbali ya kuhamasisha watu kujiunga na NSSF. Wasanii wa Kigoma All Stars wote ni wanachama wa Mfuko huo.
Katika kazi zote hizi Mimi binafsi sijafaidika kwa namna yeyote ile kifedha. Kauli yeyote ya kujaribu kuonyesha kazi hizi za wasanii ni ufisadi ni kauli za kusikitisha na kukatisha tamaa kwa mtu ambaye anajaribu kusaidia wasanii kufaidika na kazi zao za sanaa.
Toka mwaka 2012 nilipoanza kujitokeza kusemea wasanii watu kadhaa wenye maslahi na tasnia hii wamekuwa wakinikatisha tamaa na hata wengine kuona nimewaingilia kazi zao.
Hivi sasa wasanii wa Kigoma AllStars ni wanahisa katika kampuni ya PERA Africa limited ili kufaidika na biashara ya miito ya simu. Yote haya nilifanya kwa uchungu nilionao kwa vijana wetu na sio kwa kutaka kufaidika kifedha. Nimeumizwa sana na tuhuma hizi za kuokoteza okoteza.
Inaniumiza zaidi kutokana na ukweli kwamba ninamwuguza mama yangu mzazi, kipindi ninachohitaji kutiwa moyo na kuombewa hata na maadui zangu kisiasa. Kipindi ambacho mama yangu yupo mahututi, tena mjumbe wa kamati kuu ya chama ambacho watoa tuhuma wanatoka, pole ninayopewa ndio hiyo. Hakuna namna ya kukosa ubinaadamu zaidi ya hivi.
Najua wajibu wangu ni kusimamia Mashirika ya Umma na nikiwa mpigania uwajibikaji nipo makini sana kuhakikisha sina mgongano wa maslahi katika mambo yangu. Ndio maana sina biashara yeyote ile ili kuhakikisha natimiza wajibu wangu kwa uadilifu mkubwa. Napata 'moral authority' ya kutaka uwajibikaji kwa sababu nafanya kazi zangu kwa misingi hiyo 'at arms length'.
Hivyo ninataka mara moja CAG afanye ukaguzi wa kazi za wasanii hao kwenye NSSF na TANAPA. Pia achunguze kama Gombe Advisors ( company limited by guarantee) ina maslahi yeyote ya kifedha katika kazi hizo za wasanii. Nataka pia Shirika la NSSF na TANAPA waweke wazi mchakato wa kazi zao na wasanii hawa kupitia LEKADUTIGITE Limited.
Zitto Kabwe
Mei 29, 2014
Dar Es Salaam.


MZUNGU AMLAZIMISHA MSICHANA KUFANYA MAPENZI NA MBWA JIJINI DAR




Mzungu huyo ambaye jina tunalihifadhi, alidaiwa kufanya tukio hilo la kinyama Mei 26, mwaka huu na inadaiwa Aneth alipomkatalia, alimtimua nyumbani hapo kwa kumtupia virago.
Chanzo makini kilidai kuwa, baada ya kutupiwa virago bila kupewa mshahara wake sambamba na kipigo, Aneth aliripoti tukio hilo katika Kituo Kidogo cha Polisi cha Tabata, Dar na muda mfupi polisi walifika nyumbani hapo lakini Mzungu huyo hakutoka ndani, akakataa kuzungumza chochote
Taarifa zilidai kuwa, baada ya polisi kukutana na kizingiti hicho, walimpigia simu kiongozi wao ambaye aliwaamuru warudi kituoni wajipange upya.
Akisimulia zaidi ishu hiyo, Aneth alisema polisi walipoondoka eneo hilo, umati uliochukizwa na kitendo hicho ulikusanyika nje ya nyumba ili kumdhibiti ‘mtasha’ huyo kwa lolote.
    Kuna jirani mmoja alipiga simu tena kituo cha polisi alipoona hali ya hewa imechafuka ndipo polisi wakafika kwa mara nyingine na difenda na kufanikiwa kuingia ndani kwa kutumia geti kubwa, walipofika walikuta milango imefungwa lakini ilisemekana aliruka ukuta na kutimkia kusikojulikana.
    Polisi waliniambia nimpigie simu ajisalimishe lakini nilipompigia alisema hayupo na kama tunamhitaji tukutane sehemu huku na yeye akiwa na polisi wake
kilisema chanzo.



Mmiliki wa nyumba hiyo anayeishi Kigamboni, Mr. Cris alipoulizwa kuhusiana na ishu hiyo, alikiri kupokea malalamiko na manyanyaso kutoka kwa Aneth.
Akisimulia zaidi maisha anayoishi na Mzungu huyo, Aneth alisema:
     Alikuwa akinitafutia sababu za kunitimua kwani hivi karibuni kwa bahati mbaya nilipoteza ufunguo wa ndani, akanipiga mateke na kunisababishia maumivu makali mwilini kiasi cha kushindwa kutembea.

    Lakini lililoniuma zaidi ni hili la kunilazimisha eti nifanye mapenzi na mbwa wake, amekuwa akifanya hivyo mara kwa mara mimi nikaona siyo sawa na nilipokataa ndipo yakanikuta hayo.
Aneth aliripoti matukio hayo katika Kituo Kidogo cha Polisi Tabata na kupewa fomu ya matibabu (PF-3) sambamba na kufunguliwa jalada la kesi namba TBT/RB/3132/2014/ SHAMBULIO na jalada la uchunguzi lenye namba TBT/IR/1829/2014/UCHUNGUZI.



Thursday, May 29, 2014

MTOTO WA MFALME WA SAUDIA RABIA AMENUNUA NDEGE YA KIFAHARI 'AIR BUS A380' KWA $500 MILIONI

Mtoto wa Mfalme wa Saudia Rabia ameonesha jeuri ya pesa pale aliponunua ndege ya kifahari aina ya AIR BUS A-380 kwa dola za kimarekani 500 Milioni. Ndege hiyo ya kifahari ina vyumba ambavyo ndani yake vina malu malu na kila aina ya Nakshi nakshi kama uonavyo hapo pichani:-



Monday, May 26, 2014

HAWA NDIO VIJANA WA PANYA ROAD NA MBWA MWITU WALIO KAMATWA

Hawa ndio viongozi wa panya road na mbwa mwitu ambao tayari
wameshakamatwa
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanya msako
wa nyumba kwa nyumba, mtaa na maeneo yaliyoathirika kwa
hofu ya vijana ambao ni vibaka maarufu kama Mbwa mwitu au
Panya Road.  Msako huu uliofanyika ndani ya masaa 24 hadi
alfajiri ya tarehe 26/5/2014 kwa lengo la kuwaondolea hofu na
uhalifu dhidi ya makundi ya vijana wadogo wasio na ajira ambao
uliibuka hivi karibuni.
Maeneo yaliyoathirika ni Kigogo, Magomeni, Tabata, maeneo
yote yanayozunguka mto Msimbazi, maeneo ya Mbagala nk.
Msako huu unaendelea kufanywa na askari wa vikosi maalum
ambao wamepewa kazi ya kuhakikisha kuwa vikundi hivyo
haviibuki tena na vinatokomezwaa kabisa kwa  kuwakamata wale
wote wanaojihusisha na vitendo vya kuvamia kwa mkundi
wananchi ambao hawana hatia

Kamishna kova ambaye amezungumza na wanahabari muda
mfupi uliopita
Kati ya watuhumiwa 149 waliokamatwa mmoja amegundulika
kuwa ni kiongozi aitwaye ATHUMANI SAIDI miaka 20, Mkazi wa
Kigogo na amekiri anaongoza kundi la watu zaidi ya 15 ambao
baadhi yao ni kati ya waliokamatwa.
Imegundulika pia kwamba vijana hawa wanatumia dawa za
kulevya aina ya bangi na wengine hujichoma sindano na
kuwafanya iwe rahisi kujihusisha na matukio ya uhalifu.  Vijana
hao hupenda kushiriki katika ngoma kama Mnanda, Mchiriku,
Kigodoro, Kanga moja nk. ambazo kwa kawaida huchezwa hadi
usiku wa manane.
Wakitoka katika ngoma hizo hujikusanya pamoja na kufanya
matukio ya uporaji kwa mtu wanayekutana naye, kufanya uvunjaji
katika majumba na wakati mwingine wana mtindo wa kugema
mafuta ya diesel au petrol katika matanki ya malori
yanayosafirisha mafuta.
Operesheni kali inafanyika katika maficho ya wahalifu hao
ikiwa ni pamoja na daraja la River side, Kigogo darajani, Manzese,
maeneo ya Tandale pamoja na maeneo mengine ya maficho mkoa
wa Kipolisi Temeke.
Tunawasiliana na Maafisa utamaduni wa Wilaya zote za Mkoa
wa D’Salaam kusimamisha utoaji wa vibali wa ngoma za usiku
ambazo hazina tija.  Pia Jeshi la Polisi linafuatilia na kuwavizia
vijana wanaopora  watu wanaotoka katika sherehe za usiku kama
vile Harusi na wanaotoka katika mikesha ya Ibada na sehemu
zozote zenye mikusanyiko.
Aidha Jeshi la Polisi wanapambana na vijana wanaowavizia
watu katika vituo vya mabasi pindi wanapotoka alfajiri kwenda
katika shughuli zao za kila siku.
Zipo taarifa kwamba baadhi ya wazazi wasio waaminifu
wamewasafirisha watoto wao wahalifu katika makundi haya
kwenda mikoani ili kukwepa wasinaswe na msako huu mkali.
Hata hivyo Jeshi la Polisi lina mtandao wa kutosha kati yake na
mikoa mingine na nchi jirani hivyo litawatafuta popote walipo na
kuwakamata.
Oparesheni hii ni endelevu na ya kudumu hadi kero hii ya
vibaka itakavyokwisha kabisa. Baadhi ya majina waliokamatwa ni
kama ifuatavyo:-
1. DANIEL PETER @ MALUNDE, miaka 25, mkazi wa Yombo
Kigunga
2.    MWISHEHE ADAM, miaka 35, mkazi wa Mtoni mashine ya
maji
3. MOHAMED SAID, miaka 32, mkazi wa Mtoni
4.    JAKAMA ALPHONCE, miaka 23, mkazi wa Mtoni Kilakala
5.    HAMADI MDUDU, miaka 25, mkazi wa Mbagala
6.    SALUM MUSA, miaka 25, mkazi wa Kiwalani
7.    ANTHONY DANIEL, miaka 20, mkazi wa Mashine ya maji
8.    FIDELIN ANTHONY, miaka 18, mkazi wa Kigogo
9. HAMZA MAZUMA, miaka 19, mkazi wa Kigogo
10.           MGANGA ABEID, miaka 20, mkazi wa Kigogo
11. SAID ABEID, miaka 19, mkazi wa Kigogo
12.           SALUM NYENJE, miaka 36, mkazi wa Chamazi
13.           DOMINICK PETER miaka 22, Mkazi wa Kigogo
14.           KULWA ABEID, miaka 20, mkazi wa Mabibo
15.           MUSA IBTRAHIM, Miaka 20, mkazi wa Magomeni
16.           HUSSEIN SHABAN, miaka 22, Mkazi wa Magomeni
S. H. KOVA
KAMISHNA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAAM


VIONGOZI WA MBWA MWITU NA PANYA ROAD WATIWA MBARONI.

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limefanikiwa
kuwakamata viongozi sita wa makundi ya uhalifu maarufu kwa
majina ya Mbwa Mwitu na Panya Road.Akizungumza na waandishi
wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamishna wa Polisi wa kanda
hiyo, Suleiman Kova, aliwataja viongozi hao kuwa ni Athumani Said
(20), Joseph Ponela, Clement Petter (25) na Romans Vitus (18)
wakazi wa Kigogo.Wengine ni Mwinshehe Adamu (37) mkazi wa
Temeke na Daniel Petter (25) mkazi wa Yombo, huku kamanda
huyo akibainisha kwamba maeneo yenye vijana hao wahalifu ni
Kigogo,
Magomeni, Tabata, Manzese na Mbagala ambapo askari wa
kutosha wapo kwa lengo la kuwadhibiti. aliwaonya wanaoeneza
uzushi kwamba makundi hayo ya wahalifu yamevamia maeneo
hayo jambo alilodai kuwakosesha wananchi amani huku akisisitiza
kuwa si kweli.Alisema uchunguzi wa jeshi hilo umebaini kwamba
chanzo cha uvumi huo ni baada ya mauaji ya vibaka wawili
walihusishwa na makundi hayo yaliyotokea Mei 18 na Mei 20
mwaka huu eneo la Kigogo Sambusa.
CHANZO:FREEMEDIA


Sunday, May 25, 2014

MAXIMO KUJA KUINOA YANGA?

Kuna habari za kurejea tena kwenye soka la Bongo kwa aliyekuwa
kocha wa timu ya Taifa Mbrazil Marcio Maximo lakini safari hii sio
kuinoa Taifa Stars, ni watoto wa Jangwani timu ya Dar es salaam
Young Africans maarufa kama Yanga.
Maximo ni kocha ambaye atakumbukwa kwa mambo mengi kwenye
soka la Bongo na machache kati ya hayo, ni namna alivyokuwa na
msimamo kwa wachezaji waliokuwa na utovu wa nidhamu,
kuhamasisha watanzania kuipenda timu yao ya taifa na kubwa
kuliko yote, ni kuipeleka Taifa Stars kwenye michuano ya kombe la
Afrika kwa wachezaji wa ndani maarufu kama CHAN.
Baada ya mkataba wa aliyekuwa kocha wa timu ya Yanga Hans Ven
Der Pluijm kumalizika mwishoni mwa msimu uliomalizika hivi
majuzi, kumekuwa na habari za wanajangwani hao, kumsaka mtu
ambaye atakuja kuungana na kocha msaidizi wa timu hiyo Boniface
Mkwasa ili kuirejesha timu hiyo kwenye makali yake baada ya
msimu huu, kujikuta wakipoteza ubingwa wao mbele ya watoto wa
mjini timu ya Azam dakika za lala salama.
Kama Mbrazil huyo atafikia makubaliano na kuja kuinoa timu hiyo,
ni wazi kuwa atakuwa na faida kutokana na kuyafahamu vema
mazingira na utamaduni wa watanzania. Maximo anajua kiwango
cha wachezaji wa kibongo na umuhimu wa mechi kubwa kama
“Kariakoo Derby” ambayo huwakutanisha timu za Simba na Yanga.
Kwa siku za hivi karibuni, Yanga ni mahali ambapo makocha
wamekuwa hawakai muda mrefu kutokana pengine na sababu
mbalimbali kama vile, maslahi na kutofikia malengo ya timu.
Mashabiki wa timu hiyo kwa muda mfupi, wamemuona kocha
Mbelgiji Thom Saintfiet na waholanzi Ernie Brands na Hans Van Der
Pluijm ambaye amemaliza mkataba wake wa miezi sita.
Pamoja na kufanya mawasiliano na kocha Maximo, bado Yanga
wanaendelea kusaka kocha mwingine ambaye atakuja kuwaletea
mafanikio endapo makubaliano na Mbrazil huyo hayatofikiwa.Huu
ni muda ambao mashabiki wa Jangwani wana hamu ya kujua
mwalimu wao mpya kuelekea kuanza kwa ligi kuu ambayo
inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 24 mwaka huu.
CHANZO: TANZANIA SPORTS


Wednesday, May 21, 2014

MAMA AMFUNGIA MTOTO KWENYE BOX MIAKA MINNE

Mtoto huyu ana miaka minne alikuwa amefungiwa ndani tangu akiwa na miezi mitatu na  mama yake mdogo, mama yake mzazi alifariki Kwa kipindi chote hicho alikuwa anamfungia kwenye box anamtupia chakula humohumo Mara ya mwisho kumuogesha ilikuwa mwaka jana mwezi wa tisa
Alikuwa anajinyea na kujikojolea hiyo rangi nyeusi ni taka hajawahi kukatwa kucha wala nywele.
Amepata ulemavu wa mikono na miguu Kwa sababu ya kukaa kwenye box. Inadaiwa mama wa Mtoto huyo alikufa Kwa ugonjwa unao ambukiza ndio maana huyo mama yake mdogo alikuwa anaogopa kuambukizwa.
Hajawahi kupewa chanjo yoyote tangu azaliwe




Tuesday, May 20, 2014

BALOZI AFA AKIWA NA KIMADA

Balozi wa Togo nchini Nigeria amefariki akiwa na kimada. Balozi huyo inasemekana walikuwa wametoka klabu ya usiku na binti huyo na bahati mbaya ndio wakadumbukia baharini na mauti yakawafika.
Wapasha habari wanasema walikuta wawili hao wakiwa wamesema ndani ya maji






MUUGUZI MWENYE HIV AFUNGWA JELA UGANDA

Nchini Uganda mahakama imempata na hatia muuguzi mwenye HIV,
aliyeshitakiwa kwa kumdunga mtoto mchanga sindano, ambayo
awali ilimchoma yeye mwenyewe.
Muunguzi huyo, Rosemary Namubiru, mwenye umri wa miaka 64,
mwathiriwa wa virusi vya HIV, amefungwa miaka mitatu jela, kwa
kile hakimu amekiita, 'uzembe wa weledi'.
Hukumu hio imetolewa wiki moja baada ya bunge la Uganda
kupitisha muswada, unaomtia hatiani mtu yeyote ambaye kusudi
anamuambukiza mtu mwengine virusi vya ukimwi.
Mtoto huyo hata hivyo hakuambukizwa virusi vya HIV na
wanaharakati wamekosoa mahakama kwa kumfunga jela
mwanamke huyo.
Babake mtoto huyo hata hivyo alielezea kufurahishwa na uamuzi wa
mahakama.
Baba huyo, Daniel Mushabe, amesema kuwa anatumai kesi hiyo
itampa motisha Rais Museveni kuidhinisha mswada uliopitishwa na
wabunge wa kuwachukulia hatua za kisheria watu
wanaowaambukiza wengine HIV kusudi.
Adhabu ya kosa hilo ni faini ya dola 1,900 au miaka kumi jela.
Sheria hiyo ikiwa itapitishwa itawaadhibu wanaotenda uhalifu huo
kwa maksudi.
Wananchi bila shaka walionyesha kuudhiwa na kitendo cha muuguzi
huyo ingawa wanaharakati wamemtetea mama muuguzi.
Hakimu aliyetoa hukumu alisema kuwa Namubiru alikosa
kuonekana kama aiyesikitishwa na kosa lake.
Namubiru, muuguzi mwenye uzoefu wa kazi wa miaka 30, alisisitiza
kwamba hana hatia na kuwa mtoto huyo hakuambukizwa HIV.
Namubiru aliamua kumdunga sindano mtoto huyo kutafuta mshipa
lakini kapata ugumu na hivyo kujidunga mwenye kwa bahati mbaya
lakini amesisitiza kuwa hakuwa na nia yoyote ya kumuambukiza
mtoto huyo virusi vya HIV.
CHANZO: BBC SWAHILI


Wednesday, May 14, 2014

TV IMAAN NDANI YA STARTIMES DAR ES SALAAM LEO.

TV Imaan kituo cha televisheni chini ya Islamic Foundation,
Morogoro hii leo In Sha Allah kitaanza kurusha matangazo
yake kupitia Startimes kwa Mkoa wa Dar es Salaam.
Fuatilia kipindi ''Walioacha Alama Katika Historia ya
Tanzania,'' ambamo Mohamed Said atafanya mahojiano na
wale waliosukuma gurudumu la historia ya Tanzania.
Patakuwa na vipindi vingine vingi vya kuuelewa Uislam
kwa watazamaji wa kila rika vipindi ambavyo vinaelimisha,
kuburudisha, kutuliza akili ya mja na kumjengea uwezo
mkubwa wa kuijua dini yake kwa wepesi na kumjua Allah
Subhana wa Taala.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU