Facebook Comments Box

Monday, May 5, 2014

HUU NDIO MSHAHARA WA SENETA MIKE SONKO.



USTAADH ILUNGA HASSAN KAPUNGU AFARIKI DUNIA

Nchi ya Tanzania imezizima kwa huzuni baada ya mwanaharakati wa kiislam Ustaadh Ilunga Hassan Kapungu kuaga dunia jana kwenye saa tano usiku.

Mwili wa marehemu utaswaliwa leo Alasir katika msikiti wa kichangani magomeni. Mwili utazikwa kwenye makuburi ya Mwinyi mkuu

Inna lilayh wa inna ilayhi rajiuun.

Allahuma ghfirlahu warhamhu waskanahu filjannah




Saturday, May 3, 2014

WARIOBA NI "BWANA KERO" KWA SERIKALI TOKEA ZAMANI

Kama alivyoandikika Edson Kamukana katika makala yake moja
"ukiachilia mbali wasomi kadhaa walioamua kulamba matapishi
yao na kumtusi Jaji Warioba na wana-CCM wengi wanaotukana
bila kujua wanamtusi nani, katikati yake utaona wanaosalia si bure
wana jambo na sababu za kufanya hivyo, hawa bila shaka
wanalipa kisasi."
Mnamo tarehe Julai 17, 1997, Rais Mkapa alimteua Jaji Warioba
kuongoza Tume ya Rais (Warioba Commission) kuchunguza na
kubainisha mianya na vyanzo vikuu vya rushwa nchini. Baada ya
kufanya mapitio ya sheria, kanuni na taratibu ndani ya serikali na
kuonyesha mianya ya kukua na kuongezeka kwa rushwa nchini,
Tume ya Warioba ilichapisha ripoti yake (Ripoti ya Warioba) tarehe
7 December 1997.
Baadhi ya mambo ambayo Tume ya Warioba iliyakuta ni pamoja
na baadhi ya wafanyakazi wa umma kuchukua rushwa kama
sehemu ya kujazia mishahara yao (petty corruption) midogo.
Lakini pia Tume ya Warioba ilikuta kuwa kulikuwa na rushwa
nyingine (grand corruption) aka ufisadi iliyohusisha maafisa wa
ngazi za juu na baadhi ya wafanyakazi wa serikali walio na ulafi wa
kujilimbikizia mali.
Tume ya Warioba ilitoa mapendekezo ya hali ya juu yaliyogusa
wizara na idara zote za serikali. Ripoti ya Warioba iligusa mioyo ya
walalahoi na wengi waliotoa maoni ya kumtaka Rais Mkapa
awafikishe mahakamani wale wote waliohusishwa na ufisadi
kwenye Ripoti ya Warioba. Hata hivyo, ripotii hiyo iliwekwa
kabatini na kutiwa kofuli. Ripoti ya Warioba ni imekuwa adimu
sana kupatika ilivyokuwa kwa Hati ya Muungano.
Japokuwa ripoti hiyo iliwekwa kabatini, iliwagusa moja kwa moja
vigogo kadhaa hasa wa CCM na wengi wao au watoto, ndugu na
jamaa zao ndio wanaoshika madaraka leo. Kama mnakumbuka
baada ya ile ripoti, ndipo vyombo vya habari vilianza kuripoti
masuala ya rushwa, ikiwemo ile skendo ya IPTL iliyomfanya
Mwalimu Nyerere aseme kuwa "kama huu ndiyo ushirikiano wa
nchi za kusini, basi bora ukoloni urudi." Waliounga mkono au
kuipinga IPTL wanajulikana. Wengine mtakuwa mnawakumbuka
hata watawala wa miaka hiyo na wizara/idara walizokuwa
wanaziongoza.
Akihojiwa na gazeti la Raia Mwema Mei 13, 2008, Jaji Warioba
alisema kuwa "Baadhi yetu tumepiga kelele muda mrefu kuhusu
hali ya rushwa nchini mpaka ikafika mahali ikawa watu wanatoa
dhihaka tu. Kuna rafiki yangu mmoja, yeye alinipachika jina la
‘Bwana Kero’ kwa sababu ya taarifa ile ya Tume ya Kero ya
Rushwa. Alisema mimi nimegeuka kuwa kero kwa kuzungumzia
rushwa kila wakati." Bado anaendelelea kuwa "Bwana kero" kwa
kutetea Rasimu ya Katiba Mpya.
Kama alivyouliza Edson Kamukana, inawezekana kweli hao vigogo
au watoto wao, ndugu na jamaa zao walioguzwa moja kwa moja
na ile ripoti wakamsifu "Bwana Kero" wakati alishawaharibia
kitumbua chao? Hatuoni vigogo hao wanautumia mchakato
mzima wa Katiba mpya kama mwanya pekee was kumdhoofisha
"Bwana Kero" na kujaribu kuendelea kuficha madhambi yao
yaliyoyafichuliwa na "Bwana Kero" kwenye ile ripoti yake ya kero
za rushwa 1997?
Kwa wale ambao hawakuwahi kuisoma Ripoti ya "Bwana Kero"
itafuteni muisome halafu muone "kero" ambazo "Bwana Kero"
aliziodhoresha kwenye ripoti yake. Halafu muunganishe the dots
kwa kujiuliza ni kwa nini kigogo A na B au mtoto/ndugu/jamaa wa
Kigogo C "anakereka" sana mpaka kumtusi "Bwana Kero"? Mara
ya mwisho nilisoma muhtasari wa ripoti kwenye maktaba ya
HakiElimu. Ilikuwa imejaa vumbi kweli kweli. Inaitwa " The Report
of the Presidential Commission of Inquiry Against Corruption",
kwa kifupi "The Warioba Report".
CHANZO: JAMII FORUM


Thursday, May 1, 2014

MBUYU TWITE NAE KUJIUNGA NA AZAM?

Uongozi wa klabu ya Young Africans unapenda kuwajulisha
wanachama wake, wapenzi wa soka na wadau kwa ujumla kuwa
taarifa za kuhama kwa wachezai wake Didier Kavumbagu na Frank
Domayo kwenda kujiunga na Azam FC zisiwakatishe tamaa, ni
mapenzi ya wachezaj wenyewe kwani walishakubaliana na uongozi
kila kitu juu ya kuendelea kuitumikia Yanga kabla ya siku mbili hizi
kuonekana wakiwa wamejiunga na wana ramba ramba.
Yanga tayari ina wachezaji watatu wenye mikataba inayoendelea na
kama kanuni za VPL kwa wachezai wa kimataifa kuwa watatu
zitatumika wachezaji Haruna Niyonzima, Hamisi Kizza na Emmanuel
Okwi ndio watakaoendelea, hivyo uongozi uliomba mwongozo kwa
TFF juu ya taratibu zitakazotumika kwa msimu ujao kabla ya
kuwasainisha Kavumbagu na Twite.
Awali uongozi wa Yanga ulikuwa kwenye mazungumzo na wachezaji
hao tangu mwanzoni mwa msimu wa 2013/2014 juu ya kuongezewa
muda wa mikataba yao ili waweze kuendelea kuitumika Yanga kwa
ajili msimu mpya ujao 2014/2015.
Didier Kavumbagu na Mbuyu Twite ambao mikataba yao ilikuwa
mwishoni waliongea na uongozi tangu mapema mwaka jana mwezi
wa Septemba juu ya kuweka sahihi zao na kuendelea kuitumikia
Yanga na kukubaliana mambo yote ya msingi kikubwa kilichokuwa
kinasubiriwa ni maamuzi ya TFF juu ya usajili wa wachezaji wa
kigeni msimu mpya wa 2014/2015 kwani Azimio la Bagamoyo
linapaswa kuanza kutekelezwa msimu huu
Uongozi wa Yanga uliandikia TFF barua mapema kuomba kupewa
mwongozo wa kanuni zitakazotumika kwenye usajli kwa wachezaji
wa kimataifa kwa msimu mpya kufuatia Azimio la Bagamoyo
kuelekeza msimu huu kila timu inapasa kuwa na wachezaji watatu
wa kigeni, mpaka sasa uongozi wa Yanga haujapata majibu juu ya
utaratibu utakaotumika kwenye msimu wa Ligi Kuu ijayo.
Hivyo makubaliano ya wachezaji Didier Kavumbagu, Mbuyu Twite
na uongozi wa Yanga SC yalikua yakisubira majibu ya TFF juu ya
kanuni zipi zitakazotumika kwenye usajili msimu wa 2014/2015 kwa
wachezaji wa kigeni na katika hali ya kushangaza Kavumbagu
akaonekana tayari ameshasaini kuichezea timu ya Azam FC.
Kuhusu Frank Domayo aliyeripotiwa jana kujiunga na Azam FC pia
alikuwa katika makubaliano ya kuongeza mkataa tangu mwezi Julai
2013, alikubaliana na uongozi juu ya mambo yote ya msingi na
kilichobakia ilikuwa ni kuweka sahihi kwenye mkataba mpya, lakini
Domayo alisema hawezi kusaini mpaka siku atakapokuja mjomba
wake ambaye ndie wakala wake na ahadi hiyo iliendelea kwa muda
wa mwaka mzima kabla ya jana kusikia ameshasaini timu nyngine.
Habari hizi zimewashitua wapenzi, wanachama na washabiki wa
Young Africans lakini ukweli ni kuwa wachezaji wenyewe walisindwa
kuwa wakweli kwa viongozi na mwisho wa siku walikua na mipango
yao ya kuondoka, hivyo uongozi ulijtahid kadri ya uwezo wake lakini
wachezaji wanaonekana hawakua tayari kuendelea kuichezea Yanga
SC.
Taarifa kamili kuhusu mipango ya timu kwa msimu ujao pamoja na
ripoti ya kocha mkuu Hans pamoja na benchi lake la Ufundi
zitatolewa hivi karibuni baada ya benchi la ufundi na uongozi kukaa
kwa pamoja na kuafikiana mipango ya msimu ujao.
Aidha uongozi wa Yanga SC unawaomba wanachama wake,
wapenzi na washabiki wasiwe na wasi wasi juu ya kuondoka kwa
wachezaji hao kwani Yanga bado ina nafasi wachezaji wengi wenye
vipaji na itaendelea kuboresha kikosi chake kwa kuzingatia
maelekezo ya kocha mkuu Hans katika usajli wa msimu ujao.
Kwa maelezo hayo hapo juu inaonesha Mbuyu twite hana nafasi tena maana azimio la Bagamoyo limetiliwa mkazo sana na TFF.
Na kuna habari kocha wa Azam ameuambia uongozi uhakikishe imemsajili 


Saturday, April 26, 2014

WILAYA MBILI KUUNDWA MKOA WA DAR ES SALAAM

Mkuu wa Mkoa wa DarEs Salaam
Said Mecky Sadick.
Wilaya mbili zinatarajiwa kuongezwa na kufanya idadi ya
wilaya kuwa tano katika jiji la Dar Es Salaam. Wilaya hizo
ni Kigamboni na Ubungo.
Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Said
Mecky Sadick wakati wa kuhitimisha kikao na baraza la
Mashauri jijini Dar Es Salaam siku ya Jumanne ambapo
wilaya ya Kigamboni itagawanywa na kuwa na majimbo
mawili ya Mbagala na Kigamboni.
“Mapendekezo hayo yatafikishwa kwenye serikali kuu na
uamuzi wake utatolewa mwezi ujao’, alisema Mkuu wa
Mkoa , ambaye alikuwa mwenyekiti wa baraza hilo,
lililokuwa likijadili pia muswada wa bajeti wa mwaka wa
fedha wa 2014/2015.
Wilaya hizo zitaungana na Manispaa za Kinondoni, Ilala na
Temeke za jijini Dar Es Salaam linalokadiriwa kuwa na
watu zaidi ya milioni 4.5 .


MKUTANO WA TAASISI YA DHI NUREYN WAANZA ARUSHA

Wajumbe kutoka sehemu mbalimbali duniani wamefika jijini Arusha kwa ajili ya mkutano mkubwa ulio andaliwa na taasisi ya Dhi Nureyn Tanzania yenye makao makuu mkoani Iringa.
Taasisi hiyo huji usisha na utoaji wa misaada na uendelezaji wa dini.
Sasa hivi taasisi hiyo inamiliki radio inayosikika mikoa ya nyanda za juu kusini.



Thursday, April 24, 2014

MACHOZI YA SHEIKH HAMID JONGO BUNGENI.


Mashekh wa BAKWATA hakika wana mambo sana.Kuna kitu
kinaitwa ''theatrics,'' masheikh wa BAKWATA ni mabingwa na wana
medali za dhahabu. Sheikh Mkuu wa BAKWATA Shaaban
Simba aliwahi kutoa medali kumpa Reginald Mengi kwa utumishi
wake uliotukuka kwa Waislam. Hakika umma ulipigwa na butwaa.
Umma ukajiuliza. Sheikh Shaaban Simba hajapata kumsikia Sheikh
Hassan bin Amir bingwa wa tafsir ya Qur'an na bingwa wa lugha ya
Kiarabu aliyeandika vitabu lukuki mpaka akapewa shahada ya
heshima na Al Azhar, Cairo mwaka 1964?Ukiachia sifa yake ya
kupigania uhuru wa Tanganyika nk. nk.
Umma ulijiuliza Sheikh Shaaban Simba hajamsikia Sheikh Mohamed
Ayub aliyesomesha dini maisha yake yote na ana wanafunzi Afrika
ya Mashariki nzima na hao wote wanafunzi wake wana vyuo
wanaisomesha Qur'an? Sheikh Shaaban Simba hivi kweli hajapatapo
hata siku moja kumsikia Sheikh Aboud Maalim aliyejenga misikiti
chungu mzima kwa kuwahamasisha Waislam matajiri na masikini
wachangie ujenzi kila mtu kwa uwezo wake alojaaliwa na
Allah? Sheikh Aboud Maalim akaweza kujenga Msikiti wa Manyema,
Msikiti wa Ngazija, Msikiti wa Maamur, Msikiti wa Mwinjuma
Mwinyikambi na mingine tusiyoijua. Achilia mbali kuanzisha
scholarship kwa vijana wa Kiislam kusoma Udaktari na Uhandisi
Uturuki chini ya taasisi aliyoanzisha, Tanzania Muslim Trust Fund.
Sheikh Shaaban Simba hawa wote hakuwaona ila kamuona
Reginald Mengi?
Kwa wasiowajua masheikh wa BAKWATA hakika wanapata tabu.
Kwa wanowajua masheikh wa BAKWATA hawashangazwi.
Wakati mwingine hakika huwa vioja na vichekesho khasa mtu
unatamami kucheka lakini kinachokuzuia ni kuwa jambo lenyewe si
la kuchekesha.
Kuna msemo wa Kiarabu unaosema,''Sababu ikijulikana ajabu
huondoka.'' Naamini Sheikh Jongo anaujua msemo huu.
Sasa hili la kulia Sheikh Jongo ni mlolongo tu wa hizo ''theatrics'' za
masheikh wa BAKWATA.


Wednesday, April 23, 2014

JE, HUU NDIO MWISHO WA WENGER ARSENAL?


Baada ya Manchester United kumfungashia virago kocha wao fununu,tetesi,masikio na macho yote yamehamia  kwa washika bunduki wa London

Wengi wanasema kuwa huu ndio mwisho wa enzi za mzee huyo hapo kilabuni

Baada ya Moyes kuachia ngazi,kocha
anayetajwa sana kurithi mikoba yake ni
boss wa timu ya taifa ya Uholanzi Luis
van Gal. 
Lakini Van
Gal amehusishwa kuhamia Arsenal na
gazeti moja maarufu la kwao uholanzi
liitwalo Vuetbal international state kwa
kutaja sababu kadhaa.

1:Wenger amebakiza wiki 6 tu katika
mkataba wake wa sasa na hajaongeza
bado.

2:Arsenal imemuajiri aliyekuwa msaidizi
wa Van Gal walipokuwa Bayern
Munich. Adries Jonker kama Director
of academy. (Mkurugenzi wa vipaji) hili likitafsiriwa kama
matayarisho ya ujio wa Van Gal.

3:Kama hilo halitoshi,Arsenal pia
imeshawaajiri makocha wadachi wa
vijana wa miaka chini ya 18 na 16 wanaoitwa Jans de kaart
na Luis van Hoon. Kitu
kinachotafsiriwa kwamba ni maandalizi
ya kumnyakua kocha mkuu mdachi.




WANASAYANSI WAGUNDUA MIWANI INAYOGUNDUA MIHEMKO YA MTU.

Mwanasayansi nchini Japan anaitwa Osawa amegundua miwani ambayo imeitwa miwani ya kipelelezi "AgencyGlass"

Wakati akifanya mahojiano na shirika la habari la AFP amesema kuwa "nilikuwa nataka kutengeneza kitu ambacho kitaeleza tabia halisi za kijamii za binaadamu"


organic light-emitting diode (OLED) ambayo imewekwa kwenye miwani hiyo inaunganishwa na kifaa cha kugundua mihemko "emotion" ambacho kimewekwa nyuma kidogo ya miwani hiyo

Mwanasayansi huyo ambae anafanya kazi katika chuo kikuu cha Tsukuba anasem. miwani hiyo itasaidia kugundua wasafiri wakorofi au wanafunzi wakorofi na sehemu ya kazi ambapo mahusiano sio  mazuri

Miwani hiyo ina uzito wa gram 100 na inauzwa  kwa dollar za kimarekani 290.





AKUTWA NA VIPANDE 12 VYA DHAHABU TUMBONI.

Madaktari nchini India wamepatwa na mchangao baada ya kukuta vipande 12 vya dhahabu katika tumbo la mgonjwa ambae alikuja na maumivu ya tumbo.

Dr  C.S. Ramachandran anasema kuwa mgonjwa huyo alikuja na maumivu ya tumbo na akasema kuwa alimeza mfuniko wa chupa

Dr C.S Ramachandran alikataa kuweka wazi jina la mgonjwa ila vipande hivyo vya dhahabu wamevikabidhi polisi

Nae afisa wa polisi anasema vipande hivyo vitakuwa vimeibiwa na wanafanya uchunguzi.

Kila kipande cha dhahabu kilicho kutwa tumboni lilikuwa na uzito wa gram 33.



Tuesday, April 22, 2014

HIZI NDIO REKODI ALIZOVUNJA MOYES AKIWA MAN U

Baada ya bodi ya wakurugenzi kumfungashia virago kocha wake hizi ndio rekodi alizovunja akiwa anaifundisha timu hiyo.



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU