Baada ya Manchester United kumfungashia virago kocha wao fununu,tetesi,masikio na macho yote yamehamia kwa washika bunduki wa LondonWednesday, April 23, 2014
JE, HUU NDIO MWISHO WA WENGER ARSENAL?
Baada ya Manchester United kumfungashia virago kocha wao fununu,tetesi,masikio na macho yote yamehamia kwa washika bunduki wa LondonWANASAYANSI WAGUNDUA MIWANI INAYOGUNDUA MIHEMKO YA MTU.
Mwanasayansi nchini Japan anaitwa Osawa amegundua miwani ambayo imeitwa miwani ya kipelelezi "AgencyGlass"AKUTWA NA VIPANDE 12 VYA DHAHABU TUMBONI.
Madaktari nchini India wamepatwa na mchangao baada ya kukuta vipande 12 vya dhahabu katika tumbo la mgonjwa ambae alikuja na maumivu ya tumbo.
Dr C.S. Ramachandran anasema kuwa mgonjwa huyo alikuja na maumivu ya tumbo na akasema kuwa alimeza mfuniko wa chupa
Dr C.S Ramachandran alikataa kuweka wazi jina la mgonjwa ila vipande hivyo vya dhahabu wamevikabidhi polisi
Nae afisa wa polisi anasema vipande hivyo vitakuwa vimeibiwa na wanafanya uchunguzi.
Kila kipande cha dhahabu kilicho kutwa tumboni lilikuwa na uzito wa gram 33.
Tuesday, April 22, 2014
HIZI NDIO REKODI ALIZOVUNJA MOYES AKIWA MAN U
Baada ya bodi ya wakurugenzi kumfungashia virago kocha wake hizi ndio rekodi alizovunja akiwa anaifundisha timu hiyo.
Monday, April 21, 2014
DAVID MOYES KUFUKUZWA MUDA WOWOTE.
Habari za ndani zinasema kocha wa Manchester United David Moyes atafukuzwa muda si mrefu.
Hii inatokana na familia ya Glazer kuchoshwa na vipigo inayopata timu hiyo.
Inasemekana familia hiyo imesikitishwa na kukasirishwa sana na kipigo cha mwisho ambacho timu hiyo ilipata kipigo cha bao mbili kwa bila.
Na habari zaidi zinapasha wiki hii inawezekana isiishe kocha huyo atakuwa amefungiwa virago.
MZEE WA MIAKA 61 AKATWA SEHEMU ZAKE ZA SIRI MBEYA
HUYU NDIO MKUU WA WILAYA ALIE FARIKI
HISTORIA YETU: KANALI ALI MAHFOUDH
Kanali Ali Mahfoudh ni Mmoja wa Wanajeshi wa Jeshi la Wananchi wa
Tanzania, JWTZ waliotajika sana kwa Miaka hii 50 ya Jeshi letu hili,
viza Ushupavu, Ushujaa na Umahiri wake Vitani zikielezewa kwa Vijana
na kuwashajiisha wengi kutamani kuingia Jeshini kufuata njia yake
njema ya Utumishi wa Kutukuka, Kujituma, Weledi, Ushupavu na
Ushujaa.
Akifanya kazi njema ya Ukombozi tokea Mapinduzi ya Zanzibar
ambapo vipawa vyake na Umahiri wake Jeshini lionekana mwanzoni
tu, japo kwa kuwa naye alisomea Ukomandoo wa Kijeshi Nchini Cuba
alihusishwa zaidi na kundi la Makomredi wa Umma Party chini ya
Profesa Abdulrahman Mohammed Babu na Mzee Ali Sultan Issa.
Mara baada ya Mapinduzi na kuundwa Muungano wa Nchi za
Tanganyika na Zanzibar, Kanali Ali Mahfoudh na wengi wa Makomredi
wenziwe waliingizwa kwenye Serikali ya Muungano na kuondolewa
kabisa Zanzibar kwa kukhofiwa kwa Ujemedari wao, Usomi wao na
"Utata" wao.
Kanali Ali Mahfoudh alikuwa Mkurugenzi wa Operesheni wa Jeshi la
Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, JWTZ kuanzia Mwaka 1964
alipohamishiwa Bara mpaka Mwaka 1972. Mwanajeshi huyu ni mmoja
wa askari waliopata umaarufu sana katika JWTZ kwa utumishi wao,
Wengi wamesikia jina lake, lakini wachache wamepata kumuona kwa
sura na hao waliobahatika kumuona wakikiri kwamba "alikuwa na sura
nzuri" lakini alikuwa Shupavu hasa.
Kanali Mahfoudh alipata Umaarufu zaidi kati ya Mwaka 1964 - 1972
katika kuvisaidia Vyama vya Ukombozi vya Afrika kama FRELIMO,
ZANU, ZAPU na MPLA katika vita vyao vya Msituni vya Ukombozi wa
Nchi zao, na pia akitajwa kuwa ndiye aliyeongoza Kikosi cha JWTZ
katika RABSHA moja Maarufu dhidi ya Uchokozi wa Rais Kamuzu
Banda wa Malawi.
Wakati wa Mapambano ya Frelimo kudai Uhuru kutoka kwa Waremo
Kanali Mahfoudh alijichimbia Nachingwea akiwasapoti Majemedari wa
Msumbiji Albarto Sipande na Raymundu Pasinuwapa katika ukombozi
wa nchi hiyo kutoka Mikononi mwa Wakoloni hao waonevu.
Kati ya Mwaka 1972 mpaka mwaka 1978 aliwekwa kizuizini Jijini Dar
es salaam kwa Tuhuma za kuhusika na Mauaji ya Rais wa Kwanza wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Makamo wa Rais wa Kwanza wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheikh Abedi Amani Karume na
akahukumiwa Kifo katika Kesi ambayo iliendeshwa Zanzibar bila yeye
kuwepo.
Wengine waliotiwa Kizuizini pamoja naye ni Profesa Abdulrahman
Mohammed Babu, Tahir Ali Salim, Hashil Seif Hashil, Salim Saleh
Salim, Ali Yusuf Baalawi, Hemed Hilal Mohammed, Suleiman
Mohammed Abdullah, Amour Mohammed Durgheish, Ahmed
Mohammed Habib, Haji Omari Haji, Saleh Abdallah, Abdallah Juma
Khamis, Ali Salim Hafidh, Shaaban Salim Mbarak, Badru Said, Ali
Mohammed Ali na Abdulaziz Abdulkadir Ahmed, Makomredi wengine
kama Ali Sultan Issa, Sharifu Ahmad Badawy Qullatein na wenziwao
walishikiliwa Zanzibar.
Baada ya Mbinyo mkali wa Shirika la Haki za Binaadam la Amnesty
International na Mataifa ya Kigeni juu ya kushikiliwa kwao, Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu Julius Kambarage Nyerere
alitoa amri ya kuachiwa kwa Kanali Ali Mahfoudh na Makomredi
wenzie Tarehe 26, Mwezi Aprili Mwaka 1972.
Mara baada ya kutolewa Gerezani Kanali Ali Mahfoudh alichukuliwa na
Serikali ya Msumbiji kwa Ombi Maalum la Rais Samora Machel kwa
kuthamini mchango ambao Nguli huyu alitoa kwa Nchi hiyo, japo
ikidaiwa kuwa kulikuwa na Makubaliano Maalum ya Kuhakikisha
Kanali Ali Mahfoudh hakanyagi tena Ardhi ya Tanzania.
Nchini Msumbiji Kanali Mahfoudh alikuwa Mshauri Mkuu wa Mambo
ya Kijeshi wa Rais Samora Machel na kwa kiasi kikubwa ndiye
anayetajwa kuisaidia Msumbiji kimbinu kupambana na Waasi wa
Renamo waliokuwa wakipewa Msaada wa Mbinu za Kijeshi, Silaha na
Fedha kwa Dhahiri na Makaburu wa Afrika ya Kusini pamoja na
Mataifa mengi makubwa ya Magharibi. Kwa kutambua Ushujaa na
Ujuzi wa Mbinu mbalimbali za Vita wa Kanali Ali Mahfoudh, Makaburu
walijaribu Mara tatu kutaka kumuua lakini Mara zote walishindwa
katika Majaribio yao hayo.
Kanali Ali Mahfoudh aliendelea kuishi Msumbiji hata mara baada ya
kustaafu kazi yake ya Ushauri wa Mambo ya Kijeshi kwa Serikali ya
Msumbiji, Baadaye alijiingiza kwenye Biashara, mara nyingi alikuwa
Akipatikana katika Klabu ya Watanznia iliyokuwa katika Jengo la
Ubalozi wa Tanzania Nchini Msumbiji ambalo tulipewa zawadi na
Serikali ya Msumbiji kwa msaada wetu kwao. Hata alipofariki Dunia
Nchini humo bado Kanali Ali Mahfoudh hakurudishwa Tanzania na
alizikwa Katika Makaburi ya Mashujaa (Heroes Cemetary) Jijini
Maputo huko huko Msumbiji.
Aliyekuwa Mke wa Kanali Ali Mahfoudh, Mama Naila Majid Jiddawi
aliendelea kubaki Tanzania ambapo baadaye naye alikuja kuwa Mtu
Maarufu na Nguli mno katika Siasa za Tanzania hasa kwa Upande wa
Zanzibar, ambapo alipambana sana katika siasa kupitia Vyama vya
CUF na NCCR Mageuzi (aliwahi kuwa Mgombea Mwenza wa Urais wa
Chama hicho) lakini naye kama Mumewe alikutana na Rungu la
Serikali kwa kufanyiwa Hujuma za wazi katika Biashara zake kiasi cha
kufikia Mpaka kuchomewa Hoteli anayoimiliki.
Wakati Rais Amani Abedi Amani Karume akiwa Madarakani
alishutumiwa sana kwa kutoa Msamaha kwa Wafungwa ambao
walifungwa kwa kosa la kuchoma hoteli ya Mama Naila Majid Jidawwi,
ikionekana ni kama vile Serikali ilikuwa inatoa Msamaha kwa watu
ambao ilidhanika kwamba iliwatuma wachome Hoteli ya Mama huyu.
Mama Naila Majid Jiddawi bado yuko hai huko Zanzibar, akifarijika
kwa Mtoto wake mwema aliyefanikiwa kuzaa katika ndoa yake na
Kanali Ali Mahafoudh, Mtoto huyo anaitwa Mahfoudh au kwa jina
Maarufu "CHE" Mahfoudh kwa kuwa kama baba yake naye kafanana
sana na Mwanamapinduzi Enersto "Che" Guvara wa Amerika ya
Kusini.
Pichani ni Rais wa Kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akimvisha medali ya Ushujaa wa
Vita vya Ukombozi wa Nchi za Afrika Mwanajeshi Mkakamavu,
Komandoo aliyeogopwa na Maadui wa Tanzania na Afrika na
Mpiganaji Shupavu aliyejitolea kupigania Ukombozi, Kanali Ali
mahfoudh, Picha hii ilipigwa mwaka 1969.
Saturday, April 19, 2014
PICHA: YANGA NA SIMBA ZILIVYOKUTANA LEO.
| Akiwa mbele kuwaongoza wachezaji wenzake katika kushangilia bao lake la kusawazisha ni Saimon Msuva |
| mshambuliaji wa Yanga Kavumbagu akiwatoka mabeki wa Simba |
| Akitafuta mbinu sahihi za kuwatoka mabeki wa simba ni mfungaji wa bao safi la kusawazisha la Yanga Simon Msuva |
![]() |
| Shabiki wa Yanga |
AZAM WATOA KIINGILIO MECHI YA LEO.
Tanzania Bara, Azam FC unatarajia
kutowalipisha kiingilio mashabiki katika
mchezo wa kesho dhidi ya JKT Ruvu kwenye
Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Katibu Mkuu wa timu hiyo, Nassor Idrissa
alisema sababu ya kufanya hivyo ni kuwapa
fursa mashabiki wao kuingia kwa wingi ili
kushuhudia timu yao ikikabidhiwa kombe la
ubingwa huo ambalo wanalitwaa kwa mara
ya kwanza tangu ilipopanda kucheza Ligi
Kuu.
“Natarajia kukutana na viongozi wenzangu
halafu tuzungumze na Mwenyekiti wa Bodi
ya Ligi, Silas Mwakibinga tuone kama
tunaweza kuruhusiwa kuwaingiza mashabiki
wetu bure kwenye mchezo wetu wa mwisho
dhidi ya JKT Ruvu, ili washuhudie timu yao
ikikabidhiwa kombe,” alisema Idrissa.
Idrissa alisema kama yangekuwa mamlaka
yao wenyewe na siyo sheria za Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF), wangechukua uamuzi
Ni
Thursday, April 17, 2014
MABADILIKO YA UELEKEO WA BARABARA KATIKATI YA JIJI LA DAR ES SALAAM
1. RANGI YA NJANO - Njia ya Uelekeo Mmoja {One Way}.
UBUNGO PLAZA GHOROFA YA KWANZA.
OFISI YA MHANDISI WA MANISPAA YA ILALA
MABALA NA SHOPRITE SUPEEMARKET JIRANK NA KAMATA



