

Mahakama nchini India imewahukumu wanaume wote wanne kifo baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka na kumuua mwanamke katika basi katika mji mkuu wa India Delhi mwezi Desemba mwaka jana.
Mmoja wao aliangua kilio na kuanguka baada ya kutangazwa kwa hukumu dhidi yao .
Taarifa zinazohusiana
afya
Msichana huyo aliyekuwa na umri wa miaka 23 aliumizwa sana na baada ya wiki moja alifariki kutokana na majeraha .
Karibu miezi 9 baada ya ubakaji ulioitikisa India, jaji ametoa hukumu kwa wanaume wote wanne ambao tayari walikuwa wamepatikana na hatia ya uhalifu .
Wendesha mashtaka walikuwa wamewaombea hukumu ya kifo wakisema ingetoa ishara muhimu kwamba uhalifu wa aina hiyo hautakubalika kamwe .
Familia ya mwanamke huyo pia waliomba wanaume hao wanyongwe .
Lakini mawakili watetezi wa wanaume hao walipinga mapendekezo ya hukumu ya kifo , wakisema wateja wao hawakuwa na rekodi za uhalifu awali na kwamba wanastahili kusamehewa .
Kifo cha mwanafunzi huyo mwezi Disemba mwaka jana kilisababisha maandamano makubwa ya upinzani kote nchini India , yaliyoilazimisha serikali kubadili sheria zilizokuwepo za uhalifu wa ngono
|
Makao Makuu ya Jeshi,
Simu ya Upepo : “N G O M E” Simu ya Mdomo : DSM 22150463 Sanduku la Posta 9203, DAR ES SALAAM, 12 Septemba, 2013. |
TAARIFA za kukamatwa na unga kwa mabondia wawili Mbwana na Mkwinda wa familia maarufu ya mchezo wa ngumi nchini ya Matumla, zimeishangaza familia na jamii nzima ya Tanzania.
Bondia Rashid ‘Snake man’ Matumla ambaye ni kaka wa Mbwana na Mkwanda, amedai endapo itathibitika wadoeo zake wanajihusisha kusafirisha dawa za kulevya, watakuwa ameipa fedheha familia yao.
Mbwana Matumla ambaye ni mkubwa, ameelezwa kukamatwa mpakani mwa Uswisi na Ujerumani wakati Mkwanda Matumla amekamatwa Addis Ababa nchini Ethiopia.
Akikaririwa kuzungumza na wanahabari kadhaa, Rashid, bingwa wa zamani wa dunia wa WBU amesema:
Tumesikia Mkwanda hadi ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia umethibitisha, lakini Mbwana bado hatuna uhakika ingawa hakuna anayeweza kumpata kwa sasa.
Ni mwezi sasa umepita sina taarifa naye na hata wakati anaondoka hakuniaga, nimesikia kupitia
vyombo vya habari. Kitendo cha mdogo wangu kukamatwa kimenisikitisha mno, siyo siri nimekwazika na ninarudia kusema hii ni fedheha kwenye familia yetu.
Mimi mwenyewe nashangaa ni lini amejiingiza kwenye kazi hiyo, hata wakati anaondoka hakuniaga, mimi kaka yao na familia hatuelewi chochote.
Unajua Mbwana hakumuaga hata mkewe, kweli inatusikitisha sana na tunasikia maumivu makubwa. Kama kweli itakuwa ni hivyo, basi watakuwa wameiangusha sana familia ambayo ilipigana kujenga jina. Lakini hatuwezi kuwatenga kwa kuwa ni ndugu zetu, tutawapigania.
Maisha:
Mkwanda alikuwa akiishi nchini Sweden ambako alikuwa na mpenzi wake aliyejaaliwa naye kupata mtoto mmoja aitwaye Liam aliyezaliwa mwaka 2010. Mpenzi wake huyo raia wa Sweden alikuwa mwanafunzi katika chuo kimoja mjini Norrkoping wakati Mkwanda alikuwa mwanafunzi katika chuo kingine akisomea Lugha ya Kiswidi. Alisema mdogo wake huyo alikuwa amebadilisha uraia na kuchukua uraia wa Sweden licha ya kwamba hapa Tanzania alikuwa amepanga Mbagala, Dar es Salaam na alikuwa anakuja na kukaa kwa muda na kisha kuondoka.
Kurejea:
Hivi karibuni inaelezwa alirejea jijini Dar es Salaam na alionekana ni mtu mwenye furaha na mishemishe kibao. Alikuwa anamiliki gari aina ya Toyota Vitz ambalo pia aliliuza lakini kuna taarifa kuwa, alinunua kiwanja katika moja ya maeneo ya Jiji la Dar.
Ngumi:
Katika familia ya Matumla, Mkwanda ndiye alikuwa bondia mdogo kuliko wote baada ya wengine sita. Kwa mujibu wa Rashid alipumzika kucheza ngumi miaka kadhaa iliyopita kutokana na kusumbuliwa na maradhi. Rekodi zinaonyesha kabla ya kupumzika kwa muda kucheza ngumi, Mkwanda alishinda mapambano manane (sita kwa KO) alipigwa mara tatu zote kwa KO alitoka sare mara moja tangu 2004. Mkubwa ni Ally ambaye ni marehemu, anafuatiwa na Rashid Matumla aliyewahi kuwa bingwa wa dunia mara mbili, bingwa wa mabara, Afrika mara moja na ndiye anaaminika kuwa bondia mkali zaidi ya wengine. Anafuatia Hassan, Mbwana ambaye anaelezwa ‘kudakwa’ Ulaya, Kareem na Mkwanda.
--- Habari kwa mujibu wa magazeti ya MWANANCHI na GPL
YANGA imemponza mwamuzi, Martin Saanya wa Morogoro aliyechezesha mechi yao na Coastal Union ambaye amefungiwa mwaka mmoja kwa kuchezesha mchezo huo chini ya kiwango.
Saanya amepewa adhabu hiyo ya kutochezesha mechi yoyote ya soka ndani ya kipindi hicho sawa na mshika kibendera namba moja wa mechi hiyo, Jesse Erasmo ambaye alishindwa kutoa uamuzi sahihi wa adhabu ya penalti waliyopewa Coastal ndani ya dakika za nyongeza kabla ya mpira kumalizika na kusababisha sare ya bao 1-1.
Penalti hiyo ndiyo ilisababisha vurugu ambazo zilifanywa na mashabiki wa Yanga ambao , walimshambulia mwamuzi kwa chupa za maji na kuvunja kioo cha basi la wachezaji wa Coastal na kumjeruhi kichwani beki wa timu hiyo, Hamis Hamad aliyelazimika kuwahishwa hospitali.
Adhabu hizo zimekuja baada ya Bodi ya Ligi kupitia taarifa ya kamishna wa mechi hiyo, Omary Walii kutoka Arusha.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Silas Mwakibinga aliliambia Mwanaspoti kuwa: “Saanya na Erasmo wamefungiwa mwaka mmoja kuchezesha mechi za ligi baada ya bodi kupitia ripoti ya kamishina wa mchezo huo.
Saanya ameadhibiwa kwa kuchezesha chini ya kiwango na alitoa adhabu ya penalti iliyofungwa na Coastal akiwa mbali na tukio,” alisema Mwakibinga na kufafanua kuwa posho za waamuzi wa mechi kwa sasa ni Sh 250,000 mbali na nauli na teksi tofauti na zamani walipokuwa wanalipwa shilingi 170,000.
“Kwa upande wa Erasmo ndiye alikuwa eneo la tukio ilipotokea penalti, lakini alishindwa kumsaidia mwamuzi wa kati na kubaki ameduwaa kama asiye na uhakika.”
Mwakibinga alisema mbali na adhabu hizo kwa waamuzi, Kamati imemfungia kocha wa makipa wa Coastal Union, Juma Pondamali muda wa miezi mitatu na faini ya Sh1 milioni kwa kutoa lugha ya matusi kwa mashabiki wanaodaiwa ni wa Simba.
Katika hatua nyingine, Coastal imetozwa faini ya Sh100,000 kwa kuchelewa kikao cha maandalizi ya mechi asubuhi kwa dakika 23 huku Yanga ikitozwa faini ya Sh1 milioni kwa mashabiki wake kurusha chupa uwanjani na pia kumvamia mwamuzi huku viongozi wakishindwa kuwadhibiti.
Kuhusu basi la Coastal hakukuwa na taarifa kwani tukio lilitokea nje ya uwanja.
SOURCE> MWANASPOTI
