Tuesday, July 23, 2013
OCD: MSIWAPE MAJAMBAZI DAWA ILI WASIKAMATWE WAPENI POLISI DAWA ILI WAWAKAMATE
Inaripotiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Polisi katika wilaya ya Mufindi, PCD
Ambwene Manyasi amewataka waganga wa jadi kuacha mara moja kuwapatia
majambazi dawa za kutokukamatwa na polisi, na badala yake waganga hao
wawapatie askari polisi dawa za kuwaona na kuwakamata wahalifu.
Eliasa Ally wa gazeti la Majira anaripoti kutoka Mufindi kuwa kauli na wito huo umetolewa na OCD huyo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mufindi, wakati akizungumza na waganga wa jadi na tiba asilia kutoka Mudindi.
OCD amesema ni jukumu la kila mwananchi kuuchukia uhalifu na kulisaidia jeshi la polisi kutimiza wajibu wake. Amenukuliwa akisema ifuatavyo:
"Ninyi waganga wa jadi na tiba asili kazi yenu kubwa ni kutubu magonjwa yanayowasibu watu na siyo kutibu mbinu za majambazi ili wasiwe wanakamatwa wanapofanya uhalifu, hapo tutakuwa hatusaidiani, badala ya waganja kuwa wachonganishi, wawe waunganishaji wa wananchi, polisi na jamii. Badala ya kutoa dawa ya sisi polisi tusiwaone wala tusiwamamate majambazi, sasa nyinyi waganja mtoe dawa ya kutuwezesha kuwaona na kuwakamata kiurahisi majambazi wanaofanya uhalifu katika jamii yetu, huo ndiyo ushirikiano na polisi jamii tunayoizungumzia."
Aliwataka waganga hao kuhakikisha kuwa shughuli zao haziwi chanzo cha kutokea kwa maovu, kufumbia macho maovu na kusababisha jamii iwachukie waganga na polisi.
OCD alisema Jeshi la Polisi limejikita katika mambo makubwa matatu ambayo aliyataja kuwa ni polisi jamii, hali ya weledi na hali ya usasa.
Eliasa Ally wa gazeti la Majira anaripoti kutoka Mufindi kuwa kauli na wito huo umetolewa na OCD huyo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mufindi, wakati akizungumza na waganga wa jadi na tiba asilia kutoka Mudindi.
OCD amesema ni jukumu la kila mwananchi kuuchukia uhalifu na kulisaidia jeshi la polisi kutimiza wajibu wake. Amenukuliwa akisema ifuatavyo:
"Ninyi waganga wa jadi na tiba asili kazi yenu kubwa ni kutubu magonjwa yanayowasibu watu na siyo kutibu mbinu za majambazi ili wasiwe wanakamatwa wanapofanya uhalifu, hapo tutakuwa hatusaidiani, badala ya waganja kuwa wachonganishi, wawe waunganishaji wa wananchi, polisi na jamii. Badala ya kutoa dawa ya sisi polisi tusiwaone wala tusiwamamate majambazi, sasa nyinyi waganja mtoe dawa ya kutuwezesha kuwaona na kuwakamata kiurahisi majambazi wanaofanya uhalifu katika jamii yetu, huo ndiyo ushirikiano na polisi jamii tunayoizungumzia."
Aliwataka waganga hao kuhakikisha kuwa shughuli zao haziwi chanzo cha kutokea kwa maovu, kufumbia macho maovu na kusababisha jamii iwachukie waganga na polisi.
OCD alisema Jeshi la Polisi limejikita katika mambo makubwa matatu ambayo aliyataja kuwa ni polisi jamii, hali ya weledi na hali ya usasa.
Sunday, July 21, 2013
Saturday, July 20, 2013
MKUTANO MKUU WA SIMBA WAFANYIKA KWA UTULIVU NA AMANI HUKU RAGE AKIZINDUA MKAKATI MPYA WA MAENDELEO WA SIMBA
| Ibrahim Masoud Maestro na Mwenyekiti wa kamati ya usajili Zakaria Hans Pope |
| Mwenyekiti aliyepita wa Simba Hassan Dalali alikuwa mmoja wa walio hudhuria. |
| Wanachama |
| Katibu Mkuu wa Simba Mtawala |
VIDEO: KIJANA AKUTWA AKITOA HUDUMA ZINAZOTOLEWA NA MADAKTARI BINGWA KWENYE ZAHANATI
CALL FOR INTERVIEW - MINISTRY OF HEALTH AND SOCIAL WELFARE
Ministry of Health and
Social Welfare is hereby announcing the names of applicants who have
been selected to appear for an interview for the post of laboratory
technologist.
The interview will be conducted at National Blood Transfusion Services (NTBS) head office at Ilala-Mchikichini opposite Msimbazi Centre on 27thJuly, 2013 starting from 9.00 am.
The interviewees should appear with all Academic and professional credentials (original certificates). The cost regarding to travel, accommodation and meals should be incurred by the candidates themselves.
The interview will be conducted at National Blood Transfusion Services (NTBS) head office at Ilala-Mchikichini opposite Msimbazi Centre on 27thJuly, 2013 starting from 9.00 am.
The interviewees should appear with all Academic and professional credentials (original certificates). The cost regarding to travel, accommodation and meals should be incurred by the candidates themselves.
| S/NO | NAME | SEX | TELEPHONE NUMBER |
| 1 | MAYALLA WILLIAM | M | TEL 0712 063564/ 0786 015066 |
| 2 | MATHAYO MBUYA | M | TEL 0768 229280/ 0656 264844 |
| 3 | HASSAN O. MBEGA | M | TEL 0756 877175/ 0787 877175 |
| 4 | DAVID ENOCK | M | TEL 0762 742232 |
| 5 | TOGOLANI G. MAYA | F | TEL 0714 640074 |
| 6 | SUZANA D. MBOTO | F | TEL 0787 576771 |
| 7 | SHABANI R. MZIRAY | M | TEL 0754 942946/ 0713 992143 |
| 8 | HUSSEIN ATHUMAN | M | TEL 0655 866606 |
ACTING PERMANENT SECRETARY
MINISTRY OF HEALTH AND SOCIAL WELFARE
P.O.BOX 9083
DAR ES SALAAM
Friday, July 19, 2013
AZAM TV WAINGIA MKATABA WA MILIONI 331 NA SIMBA SPORTS CLUB KWA AJILI YA KURUSHA SIMBA TV
Kutoka kushoto Mwenyekiti wa Simba Aden Rage, Katibu mkuu wa Simba Evodius Mtawala, Meneja wa Azam Said Mohamed na Abubakar Bakhresa baada ya kuweka saini mkataba huo.
KAMPUNI
ya mpya ya Habari nchini, Azam Media Group, leo imeingia Mkataba wa
miaka mitatu wenye thamani ya Sh. Milioni 331 na klabu ya Simba ya Dar
es Salaam kwa ajili ya kurusha kipindi maalum cha klabu hiyo,
kitakachojulikana kama Simba TV kupitia kituo kipya cha Televisheni,
Azam TV.
Mwenyekiti wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage, kwa pamoja na Katibu, Evodius Mtawala na Mjumbe wa Baraza la Wadhamini, Hamisi Kilomoni waliiwakilisha klabu hiyo katika utiaji saini wa Mkataba huo mnono kwenye ukumbi wa Kibo, jengo la PSPF, Dar es Salaam.
Upande wa Azam uliwakilishwa na Mkurugenzi Mkuu, Abubakar Bakhresa, Meneja Mkuu, Said Mohamed na Mwanasheria, Shani Christoms ambao waliikabidhi Simba SC hundi za fedha hizo kwenye hafla hiyo.
Meneja wa Azam Media, Mzee Said alisema kwamba Mkataba huo ni mwanzo tu, lakini kampuni hiyo imejipanga kusaidia zaidi soka ya Tanzania kwa kuingia mikataba mingi yenye manufaa kwa mchezo huo nchini.
Alhaj Rage, pamoja na kuwashukuru Azam Media kwa Mkataba huo mnono, alisema klabu inategemea kujikomboa zaidi kiuchumi kutokana na mikataba ya udhamini kama hiyo na muda si mrefu wataingia mikataba mingine itakayokuza zaidi pato la klabu.
“Nimesikia pia mnataka kununua haki za Televisheni za Ligi Kuu ya Tanzania Bara, mimi nasema karibuni na katika hilo, natoa angalizo, mkinunua haki za TV za Ligi Kuu, naomba mtoe fungu sawa kwa kila klabu, hakuna kubagua eti huyu apate kidogo, yule apate zaidi, hapana,”.
“Lazima mpira wa miguu katika nchi hii maendeleo yafike kila sehemu na tuondoe ubinafsi wa kujifikiria eti sisi Simba ndiyo tupate zaidi, hapana. Hiyo si haki, lazima na zile klabu ndogo pia nazo zinufaike sawa na sisi kwa kuwa tunacheza ligi moja,”alisema Rage ambaye pia ni Mbunge wa Tabora Mjini (CCM).
Mwenyekiti wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage, kwa pamoja na Katibu, Evodius Mtawala na Mjumbe wa Baraza la Wadhamini, Hamisi Kilomoni waliiwakilisha klabu hiyo katika utiaji saini wa Mkataba huo mnono kwenye ukumbi wa Kibo, jengo la PSPF, Dar es Salaam.
Upande wa Azam uliwakilishwa na Mkurugenzi Mkuu, Abubakar Bakhresa, Meneja Mkuu, Said Mohamed na Mwanasheria, Shani Christoms ambao waliikabidhi Simba SC hundi za fedha hizo kwenye hafla hiyo.
Meneja wa Azam Media, Mzee Said alisema kwamba Mkataba huo ni mwanzo tu, lakini kampuni hiyo imejipanga kusaidia zaidi soka ya Tanzania kwa kuingia mikataba mingi yenye manufaa kwa mchezo huo nchini.
Alhaj Rage, pamoja na kuwashukuru Azam Media kwa Mkataba huo mnono, alisema klabu inategemea kujikomboa zaidi kiuchumi kutokana na mikataba ya udhamini kama hiyo na muda si mrefu wataingia mikataba mingine itakayokuza zaidi pato la klabu.
“Nimesikia pia mnataka kununua haki za Televisheni za Ligi Kuu ya Tanzania Bara, mimi nasema karibuni na katika hilo, natoa angalizo, mkinunua haki za TV za Ligi Kuu, naomba mtoe fungu sawa kwa kila klabu, hakuna kubagua eti huyu apate kidogo, yule apate zaidi, hapana,”.
“Lazima mpira wa miguu katika nchi hii maendeleo yafike kila sehemu na tuondoe ubinafsi wa kujifikiria eti sisi Simba ndiyo tupate zaidi, hapana. Hiyo si haki, lazima na zile klabu ndogo pia nazo zinufaike sawa na sisi kwa kuwa tunacheza ligi moja,”alisema Rage ambaye pia ni Mbunge wa Tabora Mjini (CCM).
CHANZO:BIN ZUBEIRY
Subscribe to:
Posts (Atom)


