Sunday, July 21, 2013
Saturday, July 20, 2013
MKUTANO MKUU WA SIMBA WAFANYIKA KWA UTULIVU NA AMANI HUKU RAGE AKIZINDUA MKAKATI MPYA WA MAENDELEO WA SIMBA
| Ibrahim Masoud Maestro na Mwenyekiti wa kamati ya usajili Zakaria Hans Pope |
| Mwenyekiti aliyepita wa Simba Hassan Dalali alikuwa mmoja wa walio hudhuria. |
| Wanachama |
| Katibu Mkuu wa Simba Mtawala |
VIDEO: KIJANA AKUTWA AKITOA HUDUMA ZINAZOTOLEWA NA MADAKTARI BINGWA KWENYE ZAHANATI
CALL FOR INTERVIEW - MINISTRY OF HEALTH AND SOCIAL WELFARE
Ministry of Health and
Social Welfare is hereby announcing the names of applicants who have
been selected to appear for an interview for the post of laboratory
technologist.
The interview will be conducted at National Blood Transfusion Services (NTBS) head office at Ilala-Mchikichini opposite Msimbazi Centre on 27thJuly, 2013 starting from 9.00 am.
The interviewees should appear with all Academic and professional credentials (original certificates). The cost regarding to travel, accommodation and meals should be incurred by the candidates themselves.
The interview will be conducted at National Blood Transfusion Services (NTBS) head office at Ilala-Mchikichini opposite Msimbazi Centre on 27thJuly, 2013 starting from 9.00 am.
The interviewees should appear with all Academic and professional credentials (original certificates). The cost regarding to travel, accommodation and meals should be incurred by the candidates themselves.
| S/NO | NAME | SEX | TELEPHONE NUMBER |
| 1 | MAYALLA WILLIAM | M | TEL 0712 063564/ 0786 015066 |
| 2 | MATHAYO MBUYA | M | TEL 0768 229280/ 0656 264844 |
| 3 | HASSAN O. MBEGA | M | TEL 0756 877175/ 0787 877175 |
| 4 | DAVID ENOCK | M | TEL 0762 742232 |
| 5 | TOGOLANI G. MAYA | F | TEL 0714 640074 |
| 6 | SUZANA D. MBOTO | F | TEL 0787 576771 |
| 7 | SHABANI R. MZIRAY | M | TEL 0754 942946/ 0713 992143 |
| 8 | HUSSEIN ATHUMAN | M | TEL 0655 866606 |
ACTING PERMANENT SECRETARY
MINISTRY OF HEALTH AND SOCIAL WELFARE
P.O.BOX 9083
DAR ES SALAAM
Friday, July 19, 2013
AZAM TV WAINGIA MKATABA WA MILIONI 331 NA SIMBA SPORTS CLUB KWA AJILI YA KURUSHA SIMBA TV
Kutoka kushoto Mwenyekiti wa Simba Aden Rage, Katibu mkuu wa Simba Evodius Mtawala, Meneja wa Azam Said Mohamed na Abubakar Bakhresa baada ya kuweka saini mkataba huo.
KAMPUNI
ya mpya ya Habari nchini, Azam Media Group, leo imeingia Mkataba wa
miaka mitatu wenye thamani ya Sh. Milioni 331 na klabu ya Simba ya Dar
es Salaam kwa ajili ya kurusha kipindi maalum cha klabu hiyo,
kitakachojulikana kama Simba TV kupitia kituo kipya cha Televisheni,
Azam TV.
Mwenyekiti wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage, kwa pamoja na Katibu, Evodius Mtawala na Mjumbe wa Baraza la Wadhamini, Hamisi Kilomoni waliiwakilisha klabu hiyo katika utiaji saini wa Mkataba huo mnono kwenye ukumbi wa Kibo, jengo la PSPF, Dar es Salaam.
Upande wa Azam uliwakilishwa na Mkurugenzi Mkuu, Abubakar Bakhresa, Meneja Mkuu, Said Mohamed na Mwanasheria, Shani Christoms ambao waliikabidhi Simba SC hundi za fedha hizo kwenye hafla hiyo.
Meneja wa Azam Media, Mzee Said alisema kwamba Mkataba huo ni mwanzo tu, lakini kampuni hiyo imejipanga kusaidia zaidi soka ya Tanzania kwa kuingia mikataba mingi yenye manufaa kwa mchezo huo nchini.
Alhaj Rage, pamoja na kuwashukuru Azam Media kwa Mkataba huo mnono, alisema klabu inategemea kujikomboa zaidi kiuchumi kutokana na mikataba ya udhamini kama hiyo na muda si mrefu wataingia mikataba mingine itakayokuza zaidi pato la klabu.
“Nimesikia pia mnataka kununua haki za Televisheni za Ligi Kuu ya Tanzania Bara, mimi nasema karibuni na katika hilo, natoa angalizo, mkinunua haki za TV za Ligi Kuu, naomba mtoe fungu sawa kwa kila klabu, hakuna kubagua eti huyu apate kidogo, yule apate zaidi, hapana,”.
“Lazima mpira wa miguu katika nchi hii maendeleo yafike kila sehemu na tuondoe ubinafsi wa kujifikiria eti sisi Simba ndiyo tupate zaidi, hapana. Hiyo si haki, lazima na zile klabu ndogo pia nazo zinufaike sawa na sisi kwa kuwa tunacheza ligi moja,”alisema Rage ambaye pia ni Mbunge wa Tabora Mjini (CCM).
Mwenyekiti wa Simba SC, Alhaj Ismail Aden Rage, kwa pamoja na Katibu, Evodius Mtawala na Mjumbe wa Baraza la Wadhamini, Hamisi Kilomoni waliiwakilisha klabu hiyo katika utiaji saini wa Mkataba huo mnono kwenye ukumbi wa Kibo, jengo la PSPF, Dar es Salaam.
Upande wa Azam uliwakilishwa na Mkurugenzi Mkuu, Abubakar Bakhresa, Meneja Mkuu, Said Mohamed na Mwanasheria, Shani Christoms ambao waliikabidhi Simba SC hundi za fedha hizo kwenye hafla hiyo.
Meneja wa Azam Media, Mzee Said alisema kwamba Mkataba huo ni mwanzo tu, lakini kampuni hiyo imejipanga kusaidia zaidi soka ya Tanzania kwa kuingia mikataba mingi yenye manufaa kwa mchezo huo nchini.
Alhaj Rage, pamoja na kuwashukuru Azam Media kwa Mkataba huo mnono, alisema klabu inategemea kujikomboa zaidi kiuchumi kutokana na mikataba ya udhamini kama hiyo na muda si mrefu wataingia mikataba mingine itakayokuza zaidi pato la klabu.
“Nimesikia pia mnataka kununua haki za Televisheni za Ligi Kuu ya Tanzania Bara, mimi nasema karibuni na katika hilo, natoa angalizo, mkinunua haki za TV za Ligi Kuu, naomba mtoe fungu sawa kwa kila klabu, hakuna kubagua eti huyu apate kidogo, yule apate zaidi, hapana,”.
“Lazima mpira wa miguu katika nchi hii maendeleo yafike kila sehemu na tuondoe ubinafsi wa kujifikiria eti sisi Simba ndiyo tupate zaidi, hapana. Hiyo si haki, lazima na zile klabu ndogo pia nazo zinufaike sawa na sisi kwa kuwa tunacheza ligi moja,”alisema Rage ambaye pia ni Mbunge wa Tabora Mjini (CCM).
CHANZO:BIN ZUBEIRY
Thursday, July 18, 2013
BENEDICT CHARLES LUKUMAY WA MASAI CLUB AFARIKI DUNIA
![]() |
| Marehemu Benedict (Kulia) |
Habari
nilizozipata muda mchache uliopita na kuthibitishwa na ndugu na jamaa wa
karibu zinasema Benedict Chalres Lukumay amefariki kwa ajali ya gari
eneo la Mikumi mkoani Morogoro usiku huu.
Chanzo cha kifo chake kimeelezwa kuwa ni ajili ya gari iliyotokea eneo la Mikumi mkoani Morogoro majira ya saa mbili usiku.
Meneja mkuu wa Meridian Hotel LTD Mzee Mponda amethibitisha juu ya kifo hicho, huku akinieleza kuwa ilitokana na ajali ya gari.
"Wakiwa na mwenzake aliyefahamika kwa jina la Adrian na gari binafsi wakielekea mkoani Iringa gari aliyokuwamo marehemu iligonga nyuma roli lililokuwa limesimama njiani." alisema Mzee Mponda.
Adrian ambaye ndiye aliyekuwa anaendesha gari alinusurika kwenye ajali hiyo.
Benedict alikuwa ni mmoja kati ya Wakugenzi watendaji wa kampuni ya Meridian Hotel LTD inayomiliki na kuendesha kumbi za burudani zikiwemo Masai Kinondoni, Masai Ilala na Masai Galapo Ilala.
Kifo chake kimeacha pengo kubwa si tu kwa familia bali hata wapenda burudani, akifahamika kimchango katika kusimamia na kuendeleza burudani na yakiwemo maonyesho mbalimbali ya wanamuziki wa bongo fleva na fani nyinginezo.
Chanzo cha kifo chake kimeelezwa kuwa ni ajili ya gari iliyotokea eneo la Mikumi mkoani Morogoro majira ya saa mbili usiku.
Meneja mkuu wa Meridian Hotel LTD Mzee Mponda amethibitisha juu ya kifo hicho, huku akinieleza kuwa ilitokana na ajali ya gari.
"Wakiwa na mwenzake aliyefahamika kwa jina la Adrian na gari binafsi wakielekea mkoani Iringa gari aliyokuwamo marehemu iligonga nyuma roli lililokuwa limesimama njiani." alisema Mzee Mponda.
Adrian ambaye ndiye aliyekuwa anaendesha gari alinusurika kwenye ajali hiyo.
Benedict alikuwa ni mmoja kati ya Wakugenzi watendaji wa kampuni ya Meridian Hotel LTD inayomiliki na kuendesha kumbi za burudani zikiwemo Masai Kinondoni, Masai Ilala na Masai Galapo Ilala.
Kifo chake kimeacha pengo kubwa si tu kwa familia bali hata wapenda burudani, akifahamika kimchango katika kusimamia na kuendeleza burudani na yakiwemo maonyesho mbalimbali ya wanamuziki wa bongo fleva na fani nyinginezo.
BARAZA KUU LA USALAMA LAJADILI USALAMA WA WAANDISHI WA HABARI
Bwa. Mustafa Haji Abdinur
mwandishi kutoka Somalia anayeandikia AFP akizungumza mbele ya Baraza
Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, wakati Baraza hilo siku ya Jumatano
lilipojadili usalama wa waandishi wa habari katika maeneo yenye
migogoro, Bw. Abdinur ambaye amejifundisha mwenyewe uandishi wa
habari alieleza kwamba pale alipo ni kama maiti inayotembea na kwamba ni
suala la muda tu yeye kuuawa kutokana na ukweli kwamba waandishi
wenzake wengi wamekwisha kuuawa nchini Somalia. Hii ili kuwa ni mara ya
kwanza kwa waandishi wa kimataifa kuzungumza ndani ya Baraza hilo.
Imeandikwa na Mwandishi Maalum, NY -- Baraza
Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa, jana jumatano liliendesha
majadiliano ya wazi kuhusu usalama wa waandishi wa habari katika maeneo
yenye migogoro.
Majadiliano hayo yaliratibiwa na Marekani ambaye ni Rais wa Baraza hilo kwa mwezi huu wa Julai, na kuhudhuriwa na waandishi wanne wa kimataifa ambao walipata fursa ya kuelezea masahibu wanayokumbana nayo wakati wa kitekeleza majukumu yao.
Majadiliano kuhusu suala la usalama wa waandishi wa habari katika maeneo yenye migogoro ni ya kwanza kufanyika ndani ya Baraza hilo, tangu lilipopitisha Azimio namba 1738 mwaka 2006 lililokuwa likizungumzia suala hilo. Aidha hii pia ni mara ya kwanza kwa waandishi wa kimataifa kuzungumza ndani ya Baraza Kuu la Usalama.
“Hapa nilipo mimi ni maiti anayetembea, ninatembea pasi kujua nani anaweza kuondoa uhai wangu,wakati wowote naweza kupotea maisha. naweza kuuawa hata na kijana mdogo ilimradi ana silaha”
Kauli hiyo ilikuwa ni ya Bw. Mustafa Haji Abdinur anayeandikisha AFP akitoka Somalia. Na kuongeza kwamba rafiki zake wengi ambao ni waandishi wenziye tayari wameshapotea maisha na kwamba kwa yeye
Majadiliano hayo yaliratibiwa na Marekani ambaye ni Rais wa Baraza hilo kwa mwezi huu wa Julai, na kuhudhuriwa na waandishi wanne wa kimataifa ambao walipata fursa ya kuelezea masahibu wanayokumbana nayo wakati wa kitekeleza majukumu yao.
Majadiliano kuhusu suala la usalama wa waandishi wa habari katika maeneo yenye migogoro ni ya kwanza kufanyika ndani ya Baraza hilo, tangu lilipopitisha Azimio namba 1738 mwaka 2006 lililokuwa likizungumzia suala hilo. Aidha hii pia ni mara ya kwanza kwa waandishi wa kimataifa kuzungumza ndani ya Baraza Kuu la Usalama.
“Hapa nilipo mimi ni maiti anayetembea, ninatembea pasi kujua nani anaweza kuondoa uhai wangu,wakati wowote naweza kupotea maisha. naweza kuuawa hata na kijana mdogo ilimradi ana silaha”
Kauli hiyo ilikuwa ni ya Bw. Mustafa Haji Abdinur anayeandikisha AFP akitoka Somalia. Na kuongeza kwamba rafiki zake wengi ambao ni waandishi wenziye tayari wameshapotea maisha na kwamba kwa yeye
Bwa. Richard Engel kutoka NBC
News mmoja kati ya waandishi wanne walioalikwa na Baraza Kuu la Umoja
wa Mataifa kueelezea uzoefu wao na mikimikiki wanayokumbana nayo
wanapotekeza majukumu yao ya kiuandishi. Bw. Engel ambaye amesema
amewahi kutekwa, alilitaka Baraza Kuu la Usalama linapojadilia kuhusu
dhana nzima ya usalama wa waandishi, kujadili pia ni nani hasa
mwandishi wa habari anaye stahili ulinzi na akahoji kama wanaharakati
ambao nao wanachukua picha za matukio mbalimbali na kuzipost kwenye
mablog kama nao ni waandishi wa habari. pembeni yake ni Bi. Kathleen
Carroll, ambaye ni mhariri mtendaji wa Associated Press na Makamu
mwenyekiti wa Bodi ya Kamati ya Kulinda Waandishi ( CPJ) yeye katika
mchango wake alisema licha ya kwamba waandishi wengi wanapoteza maisha
wakati wakitafuta habari kwenye maeneo yenye migogoro lakini waandishi
watano kati ya sita wanauawa ndani ya nchi zao wakati wakitimiza
majukumu yao.
kuwa hai mpaka sasa ni kama bahati lakini ni suala la wakati tu.
Naye Bi. Cathleen Carrol ambaye ni Mhariri Mtendaji wa Associated Press na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Kamati ya Kuwalinda Waandishi ( CPJ) pamoja na kuelezea kwa uchungu mkubwa matukio ya mauaji yaliyowakumbua waandishi wenzake katika maeneo mbalimbali duniani anasema, katika shirika lao kuna eneo ambalo limetengwa maalum kwaajili ya kuwaenzi waandishi wote ambao wamepoteza maisha katika utekelezaji wa majukumu yao.
Kwa upande wake, mwandishi Richard Engel wa NBC news, yeyé pamoja na kuelezea mikasa mbalimbali ambayo amekwisha kumbana nayo yakiwamo ya kutekwa wakati akiripoti matukio ya migogoro, yeyé alikwenda mbalia zaidi kwa kuuliza ni nani hasa mwandishi wa habari.
Bw, Engel alieza kwamba ulinzi wa waandishi wa habari hivi sasa unakuwa mgumu sana tofauti na miaka ya nyuma kutokana na kile alichosema kuibuka kwa makundi mengi yanayofanya kazi za waadishi wa habari.
“ Wakati tukijadili hoja hii ya usalama wa waandishi wa habari, pengine pia ni muhimu tukajiuliza hivi ni nani hasa mwandishi wa habari, je mwanaharakati anaye shika video au kamera na kalamu je naye ni mwandishi, au je na yule mwanamgambo mwenye silaha lakini naye ameshika kamera na kupiga picha je naye ni mwandishi” akahoji Bw, Engel
Anasema kwamba ni jambo la kawaida hivi unapokwenda kwenye tukio fulani kukutana na makundi ya watu kila mmoja akiwa ameshika kamera yake akichukua matukio, na katika mazingira kama haya, ni vigumu kwa vyombo vya ulinzi na usalama kutofautisha nani hasa ni mwadishi aliyesomea na kubobea kwenye fani hiyo na yupi mwanarakati.
Kwa maoni yake anasema pamoja na hamu ya kila mtu kutaka kutaka kukukusanya habari na kuzisambaza kupitia mitandao ya kijamii, ni vime kujiuliza nani anastahili na anapwashwa kupewa ulinzi anapotimiza majukumu yake na kwa vyovyote vile anasema kama ilivyo kwa wanadiplomasia ambao wanakinga vilevile waandishi waliosomea na wenye weledi na taaluma yao wanatakiwa kupewa ulinzi.
Majadiliano hayo yalifunguliwa na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Jan Eliasson, na yalikuwa na mvuto wa ina yake hasa kutoka na kauli zilizokuwa zikitolewa na baadhi ya wachangiaji.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu alieleza kwamba hujuma dhidi ya waandishi wa habari ni jambo lisilokubalika kwa kile alichosema ni kubinya uhuru wa upatikanaji na utoaji wa habari, lakini pia ni ukiukwaji wa uhuru wa kujieleza. Akalipongeza Baraza kwa kuitisha mjadala huo
Akasema karne iliyopita waandishi wa habari wapatao 600 walipoteza maisha katika matukio mbalimbali na wengine wakiishia magerezani, huku asilimia 90 ya matukio hayo hakuna hatua zozote za kisheria zilizochukuliwa.
Pamoja na wachangiaji wengi kukiri kwamba mazingira ya ufanyaji kazi kwa waandishi wa habari yamezidi kuwa magumu na hatari, walielezea pia kwamba mazingira hatarishi hayapo tu katika maeneo yenye vita bali hata katika nchi wazofanyia kazi. Ambapo takwimu kutoka CPJ zinaonyesha katika kila waandishi watano kati ya sita wanauliwa wakiwa ndani ya nchi zao.
Wengi wa wazungumzaji walieleza kwamba baadhi ya waandishi ama wamekuwa wakitishiwa maisha yao na familia zao au hata kupoteza maisha kwa kuandika na kuchapicha habari zinazofichua vitendo vya rushwa , vitendo vya jinai au kashfa zinazohusu makundi mbalimbali ya jamii na vilevile kuandika habari za uchochezi kati ya kundi moja na jingine..
Wengine wakaenda mbali kwa kusema wakati mwingine waandishi wenyewe wanajiweka katika mazingira ya hatari kwa kukiuka misingi ya kazi zao, kwa kuandika habari zinazopendelea upande mmoja, au kufanya kazi kinyume cha matakwa na matarajio ya yule anayemfanyia kazi.
Wazungumzaji hao wakatoa wito kwa Baraza kuu la Usalama kuangalia namna bora ya kuboresha ulinzi wa waandishi wa habari katika mazingira hatarishi kama vile vita na migogoro na pia wakatoa wito wito kwa waandishi wa habari kuzingatia misingi ya taaluma zao na kuepuka kujingiza katika mitengo isiyo ya lazima.
Suala lingine lililozungumwa kwa kina ni lile la kutofikishwa mbele ya mkono wa sheria watu wanaotuhumiwa kuwahujumu waandishi wa habari.
Naye Bi. Cathleen Carrol ambaye ni Mhariri Mtendaji wa Associated Press na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Kamati ya Kuwalinda Waandishi ( CPJ) pamoja na kuelezea kwa uchungu mkubwa matukio ya mauaji yaliyowakumbua waandishi wenzake katika maeneo mbalimbali duniani anasema, katika shirika lao kuna eneo ambalo limetengwa maalum kwaajili ya kuwaenzi waandishi wote ambao wamepoteza maisha katika utekelezaji wa majukumu yao.
Kwa upande wake, mwandishi Richard Engel wa NBC news, yeyé pamoja na kuelezea mikasa mbalimbali ambayo amekwisha kumbana nayo yakiwamo ya kutekwa wakati akiripoti matukio ya migogoro, yeyé alikwenda mbalia zaidi kwa kuuliza ni nani hasa mwandishi wa habari.
Bw, Engel alieza kwamba ulinzi wa waandishi wa habari hivi sasa unakuwa mgumu sana tofauti na miaka ya nyuma kutokana na kile alichosema kuibuka kwa makundi mengi yanayofanya kazi za waadishi wa habari.
“ Wakati tukijadili hoja hii ya usalama wa waandishi wa habari, pengine pia ni muhimu tukajiuliza hivi ni nani hasa mwandishi wa habari, je mwanaharakati anaye shika video au kamera na kalamu je naye ni mwandishi, au je na yule mwanamgambo mwenye silaha lakini naye ameshika kamera na kupiga picha je naye ni mwandishi” akahoji Bw, Engel
Anasema kwamba ni jambo la kawaida hivi unapokwenda kwenye tukio fulani kukutana na makundi ya watu kila mmoja akiwa ameshika kamera yake akichukua matukio, na katika mazingira kama haya, ni vigumu kwa vyombo vya ulinzi na usalama kutofautisha nani hasa ni mwadishi aliyesomea na kubobea kwenye fani hiyo na yupi mwanarakati.
Kwa maoni yake anasema pamoja na hamu ya kila mtu kutaka kutaka kukukusanya habari na kuzisambaza kupitia mitandao ya kijamii, ni vime kujiuliza nani anastahili na anapwashwa kupewa ulinzi anapotimiza majukumu yake na kwa vyovyote vile anasema kama ilivyo kwa wanadiplomasia ambao wanakinga vilevile waandishi waliosomea na wenye weledi na taaluma yao wanatakiwa kupewa ulinzi.
Majadiliano hayo yalifunguliwa na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Jan Eliasson, na yalikuwa na mvuto wa ina yake hasa kutoka na kauli zilizokuwa zikitolewa na baadhi ya wachangiaji.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu alieleza kwamba hujuma dhidi ya waandishi wa habari ni jambo lisilokubalika kwa kile alichosema ni kubinya uhuru wa upatikanaji na utoaji wa habari, lakini pia ni ukiukwaji wa uhuru wa kujieleza. Akalipongeza Baraza kwa kuitisha mjadala huo
Akasema karne iliyopita waandishi wa habari wapatao 600 walipoteza maisha katika matukio mbalimbali na wengine wakiishia magerezani, huku asilimia 90 ya matukio hayo hakuna hatua zozote za kisheria zilizochukuliwa.
Pamoja na wachangiaji wengi kukiri kwamba mazingira ya ufanyaji kazi kwa waandishi wa habari yamezidi kuwa magumu na hatari, walielezea pia kwamba mazingira hatarishi hayapo tu katika maeneo yenye vita bali hata katika nchi wazofanyia kazi. Ambapo takwimu kutoka CPJ zinaonyesha katika kila waandishi watano kati ya sita wanauliwa wakiwa ndani ya nchi zao.
Wengi wa wazungumzaji walieleza kwamba baadhi ya waandishi ama wamekuwa wakitishiwa maisha yao na familia zao au hata kupoteza maisha kwa kuandika na kuchapicha habari zinazofichua vitendo vya rushwa , vitendo vya jinai au kashfa zinazohusu makundi mbalimbali ya jamii na vilevile kuandika habari za uchochezi kati ya kundi moja na jingine..
Wengine wakaenda mbali kwa kusema wakati mwingine waandishi wenyewe wanajiweka katika mazingira ya hatari kwa kukiuka misingi ya kazi zao, kwa kuandika habari zinazopendelea upande mmoja, au kufanya kazi kinyume cha matakwa na matarajio ya yule anayemfanyia kazi.
Wazungumzaji hao wakatoa wito kwa Baraza kuu la Usalama kuangalia namna bora ya kuboresha ulinzi wa waandishi wa habari katika mazingira hatarishi kama vile vita na migogoro na pia wakatoa wito wito kwa waandishi wa habari kuzingatia misingi ya taaluma zao na kuepuka kujingiza katika mitengo isiyo ya lazima.
Suala lingine lililozungumwa kwa kina ni lile la kutofikishwa mbele ya mkono wa sheria watu wanaotuhumiwa kuwahujumu waandishi wa habari.
Wednesday, July 17, 2013
PICHA: MAJENGO YA SCHOOL OF LAW YAKABIDHIWA KWA SERIKALI
Kaimu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bibi Christina Sonyi akitia
saini hati ya makabidhiano ya majengo ya Law School of Tanzania wakati
wa shughuli ya makabidhiano ya majengo hayo iliyofanyika jana Julai
16,2013 jijini Dar Es Salaam. Wanaoshuhudia ni Bw. Emmanuel Mayeji
kutoka Wizara ya Katiba na Sheria (wa kwanza kulia), Mh. Jaji Gerald
Ndika Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (wa pili
kulia), na wa kwanza kushoto ni Bw. Aloyse P. Mushi Mkurugenzi Mtendaji
kutoka Co-architecture.
Kaimu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bibi Christina Sonyi amepokea
hati ya makabidhiano pamoja na funguo za majengo ya Taasisi ya Mafunzo
ya Uanasheria kwa Vitendo kutoka kwa Naibu Meneja wa Kampuni ya Beijing
Construction Engineering Group, Bw. Zhang Chengwei iliyokuwa ikijenga
majengo hayo na kukamikika.
Makabidhiano hayo yalifanyika jana, siku ya Jumanne, Julai 16, 2013 jijini Dar es Salaam.
Anayeshuhudia katikati ni Bw. Aloyse P. Mushi, Mkurugenzi Mtendaji wa Co-Architecture.
Picha, maelezo: Farida Khalfan
Makabidhiano hayo yalifanyika jana, siku ya Jumanne, Julai 16, 2013 jijini Dar es Salaam.
Anayeshuhudia katikati ni Bw. Aloyse P. Mushi, Mkurugenzi Mtendaji wa Co-Architecture.
Picha, maelezo: Farida Khalfan
Subscribe to:
Posts (Atom)



