Facebook Comments Box

Tuesday, July 9, 2013

NYATI MWEUPE AZUA TAFRANI NGORONGORO


WAHIFADHI watafiti na wataalamu kadhaa, wako katika harakati za kumsaka Nyati wa ajabu anayedaiwa kuwa na rangi ya maziwa, ambaye hivi karibuni ameonekana katika mwambao wa bonde kuu la Ngorongoro (Kreta) na kusababisha tafrani kubwa.
Kwa mujibu wa mtalaam wa ikolojia katika mamlaka hiyo, Patrice Mattay, uwepo wa nyati (mbogo) huyo wa aina yake hifadhini hapo, kumeibua suala jipya katika utafiti wa wanyama pori, kwani hakujawahi kuwepo Nyati mwenye rangi nyeupe popote duniani. Kwa kawaida Nyati huwa anangozi yenye rangi nyeusi.
Nyati huyo mweupe aligundulika kwa mara ya kwanza na maafisa wa polisi wanaofanya kazi katika kituo cha polisi kilichopo ndani ya hifadhi hiyo, ambao wanasema mnyama huyo hupita katika maeneo ya kituo hicho majira ya asubuhi akiwa miongoni mwa mbogo wengine takribani 20. Ngorongoro ina nyati wapatao 350.


“Ni kweli hata mimi binafsi nimemshuhudia Nyati huyo mweupe akikatiza katika sehemu mbalimbali za hifadhi ya Ngorongoro majira ya asubuhi akiwa katika kundi la mbogo wengine,” alisema mkuu wa kituo cha Ngorongoro Afisa wa Polisi, JJ Paul.

Hadi sasa ni maaskari wanaofanya doria katika maeneo ya hifadhi hiyo, hususan nyakati za asubuhi, ndio wanaothibitisha kwa kiwango kikubwa kumuona Nyati huyo wa ajabu ambaye sasa anatarajiwa kuwa atakuwa kivutio kipya cha utalii nchini.

Meneja Uhifadhi katika mamlaka ya Ngorongoro, Amiyo T. Amiyo amesema tayari shirika lake limekwisha tuma askari wake kadhaa kumsaka Nyati huyo wa ajabu, ili kubaini eneo ambalo anapatikana kwa ajili ya kuwezesha utafiti zaidi.

“Na kwa mtu yeyote mwenye kutuletea taarifa kuhusu Nyati huyo mweupe zitakazotuwezesha kumpata mnyama huyo, basi naye pia atazawadiwa ipasavyo,” alisema Amiyo.

Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro ndiyo inayoongoza kwa kupata watalii wengi nchini na kwa mujibu wa Ofisa Utalii wa Shirika hilo, Asantaeli Melita, zaidi ya wageni 585,000 hutembelea eneo hilo, na hasa Kreta, kila mwaka.

Idadi ya wanyamapori walioko Ngorongoro kwa sasa inafikia 300,000 wengi wao wakiwa ndani ya bonde lenyewe huku baadhi na hasa twiga wakiishi nje ya Kreta.

Mbali na Mbogo wa jabu aliyegunduliwa hivi karibuni, eneo la Ngorongoro pia lina maajabu mengine kadhaa, ukiwemo kilima cha mchanga unaotembea bila kusambaratika, idadi kubwa ya Kakakuona, mnyama anayedaiwa kuwa na uwezo wa kutabiri, pamoja na idadi kubwa ya wanyama adimu kama Mbwa-mwitu na Faru.


TAARIFA YA MWEZI WA RAMADHAAN


Assalaamu 'alaykum wa Rahmatullaahi wa Barakaatuh,
Tumefuatilizia sana kila pahali taarifa za mwezi, na hatujapata taarifa zozote za mwezi kuonekana popote duniani jana Jumatatu 29 Sha'baan 1434H (8 Julai 2013M). Hivyo, leo Jumanne tunakamilisha siku thalathini za Sha'abaan  In shaa Allaah, na Jumatano (10 Julai 2013M) itakuwa ni siku ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhaan.
KITONGONI inawaombea Ramadhaan ya kheri na baraka nyingi, mchume thawabu tele, Swawm zikubaliwe, dhambi zighufuriwe, na Allaah Atutakabalie 'amali zetu.  Tusiache kuwaombea du’aa ndugu zetu Waislam popote walipo ulimwenguni walio katika dhiki za ukandamizwaji,
vita, njaa na machafuko. Na pia tukumbukane kwa du’aa kwani Mtume Swalla-Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam amesema katika Hadiyth kutoka kwa Ummu Dardaa (Radhiya-Allaahu ‘anhaa): ((Atakayemuombea ndugu yake kwa siri Malaika aliyewakilishwa kwake husema: “Aamiyn nawe pia upate mfano wake)) (wa kama unayomuombea) [Muslim]
Kwa Munaasabah wa kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhaan, Alhidaaya imewaekea tayari  mafundisho mbalimbali yenye manufaa katika kuongeza elimu na kuimarisha 'ibaadah zenu ili muweze kuchuma mema mengi na muweze kufikia kuipata taqwaa ambayo ndio lengo kuu la Swawm.

Monday, July 8, 2013

MWANAFUNZI WA VETA DODOMA AJICHOMA MOTO KISA WIVU WA MAPENZI


MWANAFUNZI wa Chuo cha Ufundi (VETA), mkoani Dodoma, Taliki Juma (22), amefariki dunia baada ya kujilipua kwa mafuta ya petroli. Mbali na mwanafunzi huyo kufariki, watu wengine wanane waliokuwa karibu na moto huo nao walijeruhiwa vibaya.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma na kusainiwa na Kamanda wa Polisi wa mkoa, David Misime, tukio hilo lilitokea juzi saa 12.30 jioni katika Kitongoji cha Machaka, Kata ya Nzughuni.

Kamanda Misime alisema, katika tukio hilo marehemu alinunua mafuta ya petroli lita tano katika kituo cha mafuta cha Nanenane na kisha kujilipua.

“Juma ambaye ni mwanafunzi wa fani ya ufundi wa magari, alimwaga petroli hiyo ndani ya saluni ya Irene Mapunda na kujilipua.

“Watu waliokuwa karibu naye walijaribu kumsihi asijilipue lakini hawakufanikiwa, kwani aliwasha kibiriti ndani ya saluni hiyo na kusababisha moto mkubwa kulipuka ambao uliwaunguza wengine waliokuwa karibu naye pamoja na mali zote zilizokuwa ndani ya Saluni hiyo.

“Uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi, hata hivyo Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linaendelea na uchunguzi wa kina juu ya tukio hili,” ilieleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo waliojeruhiwa ni Mugina Hessein (32), Benson Mushi (11) Japhet Japhet (18), Meshack John (18), Swaibu Kassim (20),Ester Silau (30), Shaban Pili (20) na Fedrick Gabriel (21).

Majeruhi wote wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma (General) na tathimini ya hasara iliyosababishwa na moto huo bado haijafahamika.


LIVERPOOL REJECT £ 30 M ARSENAL BID FOR SUAREZ


Luis Suarez Liverpool have turned down a £30m bid from Arsenal for 26-year-old Uruguayan striker Luis Suarez. Suarez has been at the centre of transfer speculation since saying in May that it would be a "good moment for a change", and admitted it would be "difficult to say no" to Real Madrid. Liverpool refused to comment on reports of Arsenal's move and have previously insisted Suarez is not for sale. However, it is understood an approach was made and instantly rejected. Chelsea have also been linked with a move for Suarez and it remains to be seen if Arsenal take their interest further as manager Arsene Wenger continues to finalise a deal for Real Madrid's Gonzalo Higuain. Real are expected to emerge as the most serious test of Liverpool's resolve not to sell Suarez unless they receive an offer in the region of the £50m which saw Fernando Torres move to Chelsea in January 2011. Liverpool manager Brendan Rodgers remains relaxed about Suarez's situation and the striker has yet to indicate to the club that he wishes to leave. The Merseyside club's stance has always been that they have no desire to part with Suarez - and even if Liverpool's hand is forced by the player's own discontent they will not be pushed into a deal and will hold out for the maximum price.


MLIPUKO WA KIPINDUPINDU MBEYA: MIKUSANYIKO YAPIGWA MARUFUKU

UGONJWA wa kipindupindu, umeingia katika wilaya ya Kyela na kuua watu wawili na 39 wakiwa wamelazwa.

Taarifa zinasema ugonjwa huo umeibuka wilayani humo wiki iliyopita ukisadikika kuanzia katika Kijiji cha Ngonga na kisha kusambaa hadi Kilwa.

Kutokana na hofu ya kupata maambukizi kwa wananchi wengine, serikali imepiga marufuku mikusanyiko ikiwemo ya harusi, kipaimara, ngoma, michezo na sikukuu inayosherehekewa kila mwaka ya wakulima. 


--- taarifa via Kalulunga blog



SABABU ZA ZITTO KABWE KUTOSHIRIKI TAMASHA LA MATUMAINI

Kupitia account yake ya facebook Mh. Zitto Kabwe amepost hotuba hii akielezea kushindwa kwake kufika katika tamasha la siku ya matumaini.
POST YAKE AMEANZA KWA KUANDIKA HIVI.

Global Publishers leo 7.7.2013 waliandaa Tamasha la Matumaini. Bahati mbaya sana sikuweza kuwahi kutokana na safari nilizonazo. Hii ni hotuba niliyopanga kuitoa na kuwatumia waandaaji.

TAMASHA LA MATUMAINI

Leo nilikuwa niwe nanyi kwa ajili ya siku hii muhimu sana kwa nchi yetu, siku ya matumaini kama inavyoandaliwa na Kampuni ya Global Publishers. Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa ndugu yangu Erick Shigongo kwa kuandaa tamasha hili kila mwaka. Nasikitika kuwa sitaweza kufanya pambano la ngumi na ndugu Ray na pia kuchezea timu yangu ya Wabunge wa Simba dhidi ya watani zetu Yanga. Hata hivyo naamini kuwa tamasha litakuwa na mafanikio makubwa na nipo nanyi japo sipo Dar es Salaam.

Ilikuwa niwepo Dar es Salaam leo, lakini nimeshindwa kuondoka Marekani kwa sababu Spika wa Bunge Mama Anna Makinda ameniagiza kwenye safari nyingine ndefu kwenda visiwa vya Cayman na baadaye Namibia kwa shughuli za Umoja wa Wabunge wa Jumuiya ya Madola. Sikuweza kukwepa jukumu hili la kitaifa maana limekuja ghafla na mimi nipo huku jirani na maeneo hayo. Naomba radhi sana kwamba sipo nanyi leo.

Nawaomba muiombee amani nchi yetu na msimamie haki kwa wananchi wote bila kubagua dini zao, rangi zao, hali yao kimaisha na ufuasi wa vyama vya siasa. Mwaka huu tumeshuhudia matukio ambayo yanatikisa msingi wa Taifa letu – Umoja. Hivi sasa msingi wetu una nyufa ambazo kwa kweli hatujajua bado nini kinacholeteleza mambo haya kama kulipua makanisa, kulipua mikutano ya vyama vya siasa na kuua viongozi wa dini.

Matukio haya yanatuelekeza kuwa makini sana na kauli zetu kwani baadala ya kuunganisha wananchi tunawezajikuta tunawagawa zaidi Watanzania na hivyo kuwa na mzunguko wa machafuko (vicious circle of violence). Ni wajibu wa viongozi wa kisiasa na wananchi kuepuka kabisa kuanza kurushiana maneno na lawama kuhusu matukio haya, kwani inawezekana lawama na maneno yetu yakawa yanampa nguvu adui wetu ambayo hatujamjua bado.

Napenda niwakumbushe kwamba ni rahisi sana kusambaza chuki na ni vigumu sana kuondoa chuki miongoni mwa wananchi. Viongozi hatari kama Hitler walitumia sana mbinu ya kueneza chuki dhidi ya jamii ya Jews na matokeo yake yalikuwa ni vita vikuu vya pili vya dunia na zaidi ya watu milioni 6 wasio na hatia kupoteza maisha. Sisi sote tuna jukumu moja la kuhakikisha tunajenga Taifa lenye kujali HAKI na lenye mshikamano mkubwa miongoni mwa raia. Kwa nia hii tu ndio tutaweza kuwa na Taifa imara lenye heshima mbele ya mataifa mengine duniani. Ni kwa njia hiyo tu ndio tutaweza kutokomeza umasikini uliokithiri mijini na vijijini hapa nchini kwa kuongeza uzalishaji na kupanua ajira. Ikumbukwe bila HAKI hakuna AMANI na bila UWAJIBIKAJI hakuna UTULIVU.

Tukiegemea siasa za CHUKI. Tukashindwa kuwa na mahusiano ya kawaida miongoni mwa viongozi kuhusu masuala ya msingi ya nchi. Tukashindwa kujadiliana kwa hoja kuhusu sera zetu. Tutapata viongozi aina ya Hitler nchini mwetu. Wote tukatae. Sisi ni Watanzania. Muwe na Tamasha jema la Matumaini.

Zitto Kabwe
7.7.2013, Aspen Colorado, USA.


Sunday, July 7, 2013

PICHA ZA PAMBANO LA WABUNGE WASHABIKI WA YANGA NA WABUNGE WASHABIKI WA SIMBA

Rais Kikwete akielekea kukagua timu.
Rais Kikwete akisaini mpira utakaotumika.
...Akiwakagua…
Rais Kikwete akielekea kukagua timu.
Rais Kikwete akisaini mpira utakaotumika.
...Akiwakagua Yanga.picha zote na GPL


KOCHA WA AZAM ASEMA HAMTAKI KASEJA: MAKIPA ALIO NAO WANATOSHA

KOCHA Mkuu wa Azam FC, Muingereza Stewart Hall amekiri Juma Kaseja ni bonge la kipa, lakini amesema kwamba sasa anataka Aishi Manula na Mwadini Ally wapambane kuwania nafasi ya kipa wa kwanza wa timu na hana mpango wa kusajili kipa mwingine.
Muingereza huyo amesema kipa wake mwingine, Jackson Wandwi anampeleka kucheza kwa mkopo Ashanti United ya Ilala iliyopanda Ligi Kuu msimu huu, ili kukusanya uzoefu baadaye arejee kushindana na Mwadini na Aishi.
Hatumuhitaji Kaseja; Stewart Hall kulia akiwa na Msaidizi wake, Kali Ongala

“Najua Kaseja ameachwa Simba SC, na nasikia watu wanamzungumzia sana wakimhusisha na Azam. Mimi nakubali yule ni kipa mzuri na ana uzoefu. Ila mimi nina makipa wazuri wawili, Aishi na Mwadini. Nataka hawa wagombee kuwa kipa wa kwanza wa timu,”alisema.
Hall amesema kwamba bado Azam ina makipa wengine wazuri wa timu za vijana, ambao watakuwa wakipewa nafasi ya kujifua na kikosi cha kwanza msimu ujao.
“Kama nitakuwa na Aishi na Mwadini kama makipa wawili imara wa timu ya kwanza, maana yake Wandwi ataendelea kuua kiwango chake. Nimeona bora nimpeleke Ashanti ili akakusanye uzoefu, baadaye arejee kwenye timu akiwa imara,”alisema.
Azam wakiwa mazoezini ufukwe wa Coco Dar es Salaam jana. Wandwi (katikati) anapelekwa kwa mkopo Ashanti United.

Aidha, kuhusu maandalizi ya msimu mpya, Hall amesema kwamba kwa sasa Azam ambayo itaiwakilisha Tanzania kwa mara ya pili mfululizo kwenye Kombe la Shirikisho Afrika mwakani, iko katika mazoezi.
“Tunaendelea na mazoezi ya msimu mpya. Kwa sasa tupo katika programu ya ufukweni na gym. Baada ya hapo tutaanza programu rasmi ya uwanjani. Lakini wiki mbili za mwanzo za Agosti tutakwenda Afrika Kusini kuweka kambi,”.
“Tukiwa huko tutafanya mazoezi katika Uwanja mzuri na kupata mechi nne za kujipima nguvu dhidi ya timu kama Orlando Pirates, Kaizer Chiefs, Mamelodi Sundwons na nyingine,”alisema

Endelea kusoma hapa 

Saturday, July 6, 2013

HUYU NDIO MZEE ABDULLAH AL RUWEIHY ALIETEMBEA KWA MIGUU KUTOKA DAR HADI TANGA



Mwarabu aliyetembea kwa Miguu Dar es salaam mpaka Tanga.
Baba yake alitembea kutoka Dar es salaam mpaka  Kigoma
Yafuatayo ni mahojiano yaliyofanyika kati ya mwandishi  na mzee Abdullah Mohammed Alruweihy mwaka 2007 katika kijiji cha Saadani eneo la Tongoni wakati  wa uhai wake.Alifariki mwaka 2009/2010.Mwenyezi Mungu amrehemu.
Swali:Sisi pale jijini Tanga tunakufahamu zaidi kwa jina la mzee Ruwehi.Jina lako kwa ukamilifu ni nan?.
Jibu:Mimi jina langu ni Abdullah bin Muhammad bin Habiib bin Salim bin Ally bin Suleiman bin Salim Al Rawaahy.
Swali:Umezaliwa wapi?.
Jibu:Nimezaliwa kijiji cha Ndono kwa Mwana Kurwa  Tabora.
Swali:Tupe historia ya wazazi wako kwa kifupi.
Jibu:Mama yangu  alikuwa akiitwa  Zuhura kutoka kabila la Manyema.Baba yangu alikuwa ni mmoja ya wafanyaji wa biashara aliyetoka kutoka nchi ya Oman.Alikuja mpaka Zanzibar.Akaona Zanzibar hapamfai akaondoka kuelekea sehemu za bara.Akafika sehemu moja inaitwa Tabora kama nilikutajia.
Sasa baada ya kufika hapo.Huyu bwana alikuwa anafanza kazi za biashara.Wakati huo walimchunuka Majarumani.Na ikawa wanatumia vitu vingi  katika dukani kwake.
Sasa  ilipokuwa imetokea ile vita wak
awa majarumani wanashambuliwa na waiengereza.
Swali:Ni vita gani hiyo?
Jibu:Ni vita ya 1914
Swali:Jee ndiyo ile vita ya mwanzo ya dunia?.
Jibu:Hapana,haikuwa vita ya mwanzo ya dunia.Ile vita ya maji maji ni vita mbali ile.Hii ilikuwa ni vita ya pili.
Swali:Ilikuwa ni mwaka gani?.
Jibu:Ilikuwa ni  1914.
Swali:Wewe ulizaliwa mwaka gani hasa?.
Jibu:Mimi nilizaliwa tarehe 10/02/1908
Swali:Tuendelee na historia ya wazazi wako.
Jibu:Mzazi  wangu mbali na kufanza utaratibu akawa na mlahaka na wale wajarumani mpaka ilipoingia vita.
Vita iliendelea mpaka baadae akaja mmoja anaitwa bwana Robert Fonreto. Akamwambia Muhammed una habari?.Vita inaendelea vikali na sisi hapa tulipo hatukukaa vizuri.Akamwambia sasa tutafanza nini?.Akamwambia risasi imekuwa kidogo na baruti  kidogo lakini askari wapo wa kuweza kuendesha kazi.Sasa tutafanza mashauri  gani?.
Akamwambia kama shauri ya risasi na baruti mimi nitafanza taratibu ya kuweza kutafuta na maarif mengine.Akamwambia unaweza  kweli,akajibu ndio.Akamwambia haya ondoka nenda.
Akaondoka moja kwa moja mpaka akafika Dar es salaam.Wakati ule wajarumani wenyewe ndio wameikamata Dar es salaam.Akatoka Dar es salaam moja kwa moja mpaka akafika kwenye nchi ya Mukkalla,Yemen.Akatoka Mukalla akenda juu,akapata risasi na baruti jumla debe thamanini na nne (84).
Ikawa chini akaweka risasi na madebe mengine akaweka baruti,lakini juu akaweka tende.Akaajiri jahazi moja lakini mimi wakati ule bado mdogo.Lakini ile historia walivyokuwa  wananieleza wale waliiokuwa wenziwe.
Akasikilizana na nahodha kuwa hii ni tende nipelekee Dar es salaam.Nahodha akaondoka mpaka akafika Unguja.Wakati ule Unguja ilikuwa ndani ya mikono ya waarabu wenyewe.Unguja ana nduguze.Mmoja anaitwa sheikh Suleiman bin Said Alruwahiy.Anakaa sehemu moja kule Unguja panaitwa Michungwa miwili.
Walipofika kule wakamwambia habari gani uliyonayo Mohammed?.Aliwaambia sina habari yoyote.Nimekuja tu kuwasalimia.Hakuwaambia ile siri yake.
 Ile jahazi baada ya pale akamwambia chukua hii mizigo kateremshe Dari salaam.Mimi nipo kidogo hapa halafu nakuja.Nahodha akaendesha jahazi hadi Dari salaam.Wakati ule ilipofika ile jahazi Dari salaam haipo tena ndani ya mikono ya Wajarumani.Imo ndani ya mikono ya Muiengereza.Kashatawala muiengereza.     
ITAENDELEA... 

SOURSE:  ISLAMICTIDES

PICHA ZA HARUSI YA DIDA WA TIMES FM

HONGERA SANA DIDA NA MUMEO MPYA, NDOA HALALI YA KIISLAM..


VIDEO: KWA WALE WAPENZI WA WEMA SEPETU HII NDIO REALITY SHOW YAKE

Wema Sepetu alitangaza kwamba anaandaa reality show yake chini ya kampuni anayoimiliki “Endless Fame”. Muda umefika wa kuanza kuonyesha hiyo show yenyewe na Wema ameshatoa teaser au kionjo cha reality show hiyo ambayo inaonyesha baadhi ya vitu vinavyohusika kwenye show hiyo. Kwenye hii teaser inamuonyesha Wema anazungumzia kazi, mahusiano na katajwa Diamond humo,ziara za Wema na maisha ya nyumbani. 
 


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU