Facebook Comments Box

Monday, June 17, 2013

VIDEO YA KUOMBOLEZA KIFO CHA LANGA




TAMKO LA CHADEMA KUHUSU YANAYO ENDELEA ARUSHA

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinatoa taarifa za Hujuma zinazoendelea katika chaguzi za marudio kwa kata mbalimbali hapa nchini.

Kwa masikitiko makubwa CHADEMA kinatoa taarifa ya matukio ya kusikitisha yanayoendelea katika chaguzi hizi, kama ifuatavyo;

1. KATA YA IYELA,MBEYA.
Katika kata hii Gari la Chama Cha Mapinduzi lenye Usajili namba T 704 BEU,likiwa na watu wawili wanaotambulika kwa majina ya Moris na Nosy,waliwateka vijana wa CHADEMA na mmoja wao kuchomwa kisu,aliechomwa kisu anaitwa Meshack Bernard.Vijana wa CCM waliokamatwa wameachiwa huru na jeshi la polisi na sasa wanatumia gari nyingine yenye rangi nyekundu Toyata Surf namba T-173 ANE,wakiendelea kufanya vitendo hivo viovu.

Na katika kituo cha kupigia kura cha SIDO ,vituo 3 vimelundikwa sehemu moja na eneo hilo kuna Karakana ambayo inawafanya watu kuingia na kutoka kinyume na sheria za uchaguzi.

2. KATA YA MBALAMAZIWA ,MUFINDI KASKAZINI.
Watu sita wamepigwa kwa marungu na visu na kuumizwa vibaya muda huu.Idadi ya vitisho katika kata hii ni kubwa mno hali iliyopelekea idadi ndogo ya watu kujitokeza kupiga kura.

4. NYAMPU LUKANO, SENGEREMA 

Viongozi na makada wa CCM waligawa mapanga kwa vijana wao na kukata watu.Vijana 3 wa CHADEMA wamechomwa kisu na kujeruhiwa vibaya sana.

5:KATA YA MINEPA,MOROGORO.
Tukio lililotokea huko ni kuchomwa moto PIKIPIKI mali ya Chama(M4C) na vijana wa CCM(greenguard). Vile vile Katibu wa Chama wilaya ndugu Lucas Daniel amepigwa na kuumizwa na mwenzake amekatwa vidole.

3.KATA YA MANCHIRA,SERENGETI-MARA
Tumepokea taarifa kuwa Mkuu wa Wilaya kujihusisha na vitendo vya utoaji rushwa kwa wapiga kura,kwa lengo la kuwezesha CCM kushinda. Vijana wetu ni mashuhuda wa tukio hilo na wako tayari kutoa ushahidi juu ya hili piai wameshuhudia vijana wa CCM wakiwa na Bastola na baadhi yao kukamatwa na vijana wa CHADEMA na kupelekwa polisi

Hali kadhalika Jeshi la Polisi limekamata vijana wetu kuanzia jana jioni hadi leo hii na wamekuwa wakitumia mabomu na hivyo kuwajeruhi.Kuna vijana ambao wametekwa na hawajulikani walipo na majina yao na wanakotoka ni kama ifuatavyo
-Barena Maro-Bwitengi
-Samson Ogao-Rwamchanga
-Adam Samson-Bwitengi
-Emmanuel Eliya-Bwitengi
-Onyango Otaro-Miseke
-Manginare Samson-Miseke
-Elija Wilson-Miseke
-Banage Nanai-Rwamchanga
-Matororo saina-Rwamchanga
-Pikipiki Simba-Rwamchanga
John Oninga-Rwamchanga

Na baadhi ya gari zifuatazo zilikua zikishiriki opereshani ya kuwateka wafuasi wa CHADEMA magari hayo ni yenye namba zifuatazo za usajili T286 BFB, T545BFE zote Landcruiser za CCM na T352 AHD.
Diwani wa CHADEMA kata ya MUGUMU Mh.Marwa Waryoba amekamatwa na polisi yupo kituoni ili kumyima fursa ya kukugua zoezi la upigaji kura kama sheria inavyomtaka.

3. KATA YA MIANZINI,DAR ES SALAAM.
Tukio lililotokea huko ni kutekwa kwa wanachama na kiongozi wa Chama. Watu hawa walitekwa na kufungwa vitambaa vyeusi machoni,kisha kupigwa na kuumizwa vibaya. Mmoja kati ya vijana hao ni Katibu wa Vijana CHADEMA tawi la machinjioni anaeitwa Julius Vedastua na mpaka sasa yuko hospital.
Tukio lingine linaloendelea katika kata hii ni vitendo vya Rushwa,makada wa CCM wamekuwa wakivuta watu kutoka kwenye mistari na kuwapatia pesa.
Hali kadhalika kwa baadhi ya maeneo katika kata hii ni kuwa na wasimamizi wengi katika kituo kimoja,na wasimamizi hao wamekuwa wakiwaongoza watu kupiga kura mpaka kwenye ile sehemu ya kupigia kura na kuwapa maelezo juu ya nani wa kumchagua,kitendo ambacho ni kinyume na Sheria.

KATA YA STESHENI, NACHINGEA,LINDI.
Taarifa tulizonazo zinasema kuwa Magari ya CCM yamekuwa yakisomba wapiga kura na kati ya magari yanayotumika ni gari lenye usajili namba T670 DEU.

KATA YA DONGOBESH,MANYARA.
Katika kata hiyo,makada wa CCM wanawavamia katika vilabu vya pombe na kuwanunulia wananchi pombe kama hongo ya kutaka kupigiwa kura,na baada ya kuwanunulia pombe wamekuwa wakiwasomba kwa magari na kuwapeleka katika vituo vyao vya kupigia kura,kitendo hichi ambacho ni kinyume na sheria.

KATA YA GENGE,TANGA.
Matukio yaliyotokea huko ni vijana wa CCM kuwakamata vijana wetu wa Red Brigade na kuwapiga na kuwaumiza. Tukio hili limesharipotiwa polisi.

KATA YA MAKUYUNI,ARUSHA.
Vijana wa Kimasai ambao wamekodiwa na Chama cha Mapinduzi wamekuwa wakivamia wanachama na viongozi wetu na kuwapiga,katika kata hii ndio tukio la kumpiga na kumjeruhi Mh Mbunge Joshua Nasari limefanyika.

Aidha kuhusu mauaji ya Arusha Mwenyekiti wa Chama Taifa,Mh Freeman Mbowe ameshatoa

msimamo wa chama juu ya tukio hilo.

Imetolewa na :
Erasto Tumbo
Afisa Mwandamizi Uenezi



KIBONZO: MABOMU YA ARUSHA

Picture

Sunday, June 16, 2013

WACHEZAJI WAISLAM WA NEWCASTLE WAGOMA KUVAA JEZI ZENYE NEMBO MPYA

imageimage 
Siku chache baada ya mshambuliaji wa kimataifa wa Senegal Pappis Demba Cisse kutoa kauli yakugoma kuvaa nembo ya kampuni ya Wonga ambayo hutoa mikopo yenye riba , mchezaji wa pili ametoka na kuungana na Cisse kwenye msimamo huo wa kutovaa logo ya Wonga kwa kuwa kampuni hiyo inafanya biashara ambayo kwa mujibu wa misingi ya dini ya kiislamu ni Haramu.
Kiungo wa Ivory Coast ambaye atakuwepo uwanjani siku ya jumapili kucheza dhidi ya Taifa Stars Ismael Cheikh Tiote amesema kuwa atazungmza na wanasheria wake kuangalia  wa kutoivaa nembo hiyo . Tiotte kama ilivyo kwa Cisse ni muislamu anayefuata misingi yote ya dini hiyo na kwa mujibu wa sheria za dini yake riba kwenye mkopo unaotolewa kwa mtu mwingine ni haramu.
Newcastle United imesaini mkataba wa miaka minne na kampuni ya Wonga mkataba ambao umeifanya klabu hiyo kuingia kwenye utata na wachezaji wenye imani ya dini ya kiislamu . Newcastle United ina wachezaji wasiopungua watano ambao wamezungmzia kutokuwa tayari kuvaa nembo ya Wonga jambo linaweza kusababisha klabu hiyo kulazimika kuwauza wachezaji kama Pappis Cisse , Tiotte na wenzao kwani hawako tayari kutumiwa kwenye kampeni za matangazo ya kampuni hiyo.


BAADA YA TUKIO LA BOMU UCHAGUZI WA AHIRISHWA ARUSHA


Kufuatia tukio la mlipuko jana jumamosi Arusha, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeahirisha chaguzi za madiwani katika kata zote nne (4) jijini arusha hadi jumapili ya tar 30/6/2013.

 Tume ya taifa ya Uchaguzi imesimamisha kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa udiwani ktk kata nne jijini Arusha. Akizungumza kwa njia ya simu na Radio TBC FM,kutoka Zanzibari mwenyekiti huyo wa tume ya uchaguzi alisema kua wameamua kusimamisha uchaguzi huo ili kuwapa nafasi vyombo vya usalama kuchunguza swala hilo.
Alisema kua sheria inawapa mamlaka kufanya hivyo pale wanapogundua kuwa hakutakua na uhuru wa mpiga kura kwenda kupiga kura. Alisema haiwezekani uchaguzi ufanyike ktk hali kama hiyo huku kukiwa na wasiwasi.


ANGALIA HIGHLIGHT YA MECHI YA BRAZIL 3 - 0 JAPAN


Brazil vs Japan 3:0 MATCH HIGHLIGHTS by footballdaily1

Saturday, June 15, 2013

HUYU NDIO RAIS MPYA WA IRAN

Picture
Hassan Rouhani, Rais Mpya wa Iran
Kiongozi mwenye msimamo wa kati kutoka kwenye chama cha Wahafidhina nchini Iran, Hassan Rouhani, ametangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais nchini humo.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iran imesema, Rouhani ameshinda za zaidi ya kura millioni kumi na nane, ambayo ni zaidi ya asilimia hamsini ya kura zote zilizopigwa.

Wizara hiyo imesema kuwa, idadi kubwa ya raia wa nchi hiyo walijitokeza kupiga kura kiwango ambacho kinakadiriwa kuwa asilimia sabini na tatu ya watu waliosajiliwa.

Mayor wa mji wa Tehran, Mohamad Baqar Qalibaf, alimaliza katika nafasi ya pili


BOMU LALIPUKA KWENYE MKUTANO WA CHADEMA ARUSHA

Watu wawili wanahofiwa kupoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa kutokana na mlipuko wa bomu lililolipuka kwenye mkutano wa CHADEMA katika eneo la Soweto, kata ya Kaloleni jijini Arusha, wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi wa madiwani katika maeneo ya jiji hilo.

Waliojeruhiwa wamekimbizwa katika hospitali za Seliani na Mount Meru ambapo baadhi ya watu wamejitolea vyombo binafsi vya usafiri na wengine wanashirikiana na Madaktari na Wauguzi wa hospitali hizo kutoa huduma ya kwanza.

Kamanda wa polisi mkoani humo, Liberatus Sabas yupo katika moja ya hospitali hizo.

Bomu hilo linaelezwa kuwa lilipuka kwenye mkusanyiko wa watu meta chache kutoka jukwa kuu, mwendo wa saa kumi na mbili na robo jioni wakati mkutano huo ulipokuwa umekwisha na shughuli ya kukusanya michango ikiendelea.

Viongozi wa juu wa CHADEMA, Freeman Mbowe na Godbless Lema walikuwepo na wameendelea kuwepo kwenye eneo hilo.

Polisi wapo katika eneo hilo wakijitahidi kutuliza ghasia lakini inasemekana upo upinzani mkubwa kutoka kwa wananchi wanaojaribu kuwafukuza, hali iliyowalazimu kupiga mabomu ya machozi na kukamata watu kadhaa wakiwemo viongozi wa CHADEMA. Mwandishi mmoja wa habari anaripotiwa kunyang’anywa kamera yake baada kwa kupiga picha, hata baada ya kujitambulisha.

Watu wenye hasira wanaripotiwa kuyashambulia na kuyaharibu baadhi ya magari ya kutoa huduma ya kwanza (ambulance) kwa kuwa yalichelewa kufika kuwaokoa majeruhi.

ILANI: Baadhi ya picha zilizopachikwa hapo huenda zikagusa  hisia ya mtizamaji, tafadhali ikiwa huwezi kuvumilia kuona damu usibofye kitufye cha kuelekea mbele



SIKILIZA MAHOJIANO YA MAREHEMU LANGA KILEO NA DR. ISAAC MARO WA CLOUDS FM

www.kitongoni.blogspot.com
Langa Kileo



KIBONZO: JINSI YA KUKUMBUKA NENO LA SIRI




ANGALIA VIDEO ZA SHOW YA LADY JAY DEE NA MWANA FA ILI UJUE NANI KAMFUNIKA MWENZAKE



Komando Jide akifanya vitu vyake jukwaani



Hapa Fa akiongea



Hapa Fa akiimba unanitega



Hapa Fa akiimba yalaiti

 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU