Facebook Comments Box

Friday, March 1, 2013

SIRI YA MTUNGI; SEHEMU YA SABA (EPISODE 7)




POLISI WANATUHUMIWA KUMPIGA RISASI MWALIMU HUYU


PictureMwalimu mmoja wa Shule ya Sekondari Kitulo wilayani Makete aliyefahamika kwa jina la Casto Sote Kawamba ameuawa kwa kupigwa risasi na askari wa Jeshi la Polisi, Makete

Mkuu wa polisi wa wilaya ya Makete, SP Peter Kaiza akizungumza na FrancisGodwin blog kuhusu tukio hilo lililotokea katika eneo la benki ya NMB tawi la Makete juzi majira ya saa moja na robo alisema  kuwa mwalimu huyo alikuwa anakwenda kupata huduma za kibenki kupitia mashine ya  kutolea  pesa ya ATM akiwa na pikipiki, na kuamriwa na askari mmoja aitwaye Jose Msukuma, kuvaa kofia.

Inadaiwa  kuwa kisa cha mauwaji yake ni madai ya kutokuvaa kofia na baada ya kuitwa na askari hao alikaidi amri na kutaka kumgonga askari huyo aliye kuwa lindoni.

Hata  hivyo  mmoja kati ya  askari ambaye   jina lake halikufahamika mara  moja alisikika  akidai kuwa  chanzo cha mtu huyo kupigwa  risasi  ilikuwa akihisiwa  kuwa ni jambazi baada ya  kufika kwa usafiri wa pikipiki (bodaboda) na kuhisiwa kuwa amefika  kwa ajili ya kuora katika benki hiyo na hivyo askari katika hali ya  kujihami alimpiga risasi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Makete, Idd Nganya ambaye ndie mwajiri wa marehemu amesema kuwa mwili wa marehemu bado umehifadhiwa katika Hospitali ya wilaya ya Makete wakati utaratibu wakusafirisha mwili huo kwenda kwao Mbeya kwa ajili ya mazishi ukiendelea.

Mganga mkuu mfawidhi ambaye ni msemaji wa hospitali ya wilaya ya makete Dr Michael Gulaka amesema kuwa wao walipokea mwili wa marehemu na sio majeruhi.
kwa habari zaidi na picha ingia FrancisGodwin blog


RUFAA YA JOHN MNYIKA DHIDI YA UENDESHAJI MBOVU WA BUNGE WA JOB NDUGAI

RUFAA DHIDI YA UENDESHAJI WA BUNGE USIOKUWA WA HAKI NA UKIUKAJI WA KANUNI WA NAIBU SPIKA JOB NDUGAI KATIKA KUONDOA HOJA BINAFSI YA MAJI

Tarehe 28 Februari 2013 nimewasilisha rasmi rufaa kwa mujibu wa Kanuni ya 5 (4) dhidi ya uendeshaji wa Bunge usiokuwa wa haki wa Naibu Spika Job Ndugai kwa kukiuka kanuni ya 58 (5) kwa kulihoji bunge kinyume na kanuni kufanya uamuzi badili wa kuondoa hoja binafsi kuhusu hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa majisafi na ushughulikiaji wa majitaka katika Jiji la Dar es salaam.

Nimefanya hivyo baada ya kupata kumbukumbu rasmi ya Bunge (Hansard) za kikao cha tano cha tarehe 4 Februari 2013 cha mkutano wa kumi wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Katika Mkutano huo Naibu Spika Job Ndugai alisema na kufanya maamuzi kwamba: “Sasa ninahoji wanaoafiki kwamba hoja hii iondolewe waseme ndiyo…..hoja imeondolewa. Walioafiki Wameshinda”; wakati mtoa hoja sikuwa nimeomba idhini yoyote ya hoja yangu kuondolewa.

Maamuzi hayo ni kinyume na Kanuni ya 58 Fasili 5 ambayo inaelekeza kwamba “Endapo hoja imefikishwa Bungeni, mtoa hoja anaweza tu kuiondoa hoja yake kwa kusimama mahali pake na kusema ‘Ninaomba ruhusa kuondoa hoja’ na papo hapo Spika ataliuliza Bunge kama linaafiki hoja hiyo kuondolewa na inapotokea Wabunge walio wengi watakubali, Spika atasema ‘hoja hiyo inaondolewa kwa idhini ya Bunge’ na hoja hiyo itakuwa imeondolewa na Bunge litaendelea na shughuli inayofuata”.

Ushahidi wa Kumbukumbu Rasmi za Bunge (Hansard) za kikao tajwa unathibitisha ukiukwaji huo wa kanuni kama ifuatavyo:

“…WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuwa hoja iliyo mbele ya Bunge lako Tukufu ni kuitaka Serikali kuboresha upatikanaji wa huduma ya majisafi na uondoaji wa majitaka Jijini Dar es Salaam, ambalo tayari linatekelezwa na mpango maalumu uliotengewa fedha nyingi na Serikali, hivyo naomba kutoa hoja kwamba hoja hii iondolewe. Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja…

MBUNGE FULANI: Waziri amesema uongo, amedanganya!

NAIBU SPIKA: Sasa ninahoji wanaoafiki kwamba hoja hii iondolewe waseme ndiyo.

WABUNGE FULANI: Sasa utaihoji vipi wakati tuna majadiliano?

WABUNGE FULANI: Ndiyooooooooo!

NAIBU SPIKA: Wanaokataa waseme siyo.

WABUNGE FULANI: Siyooo!

NAIBU SPIKA: Hoja imeondolewa. Walioafiki wameshinda.

(Hoja ilitolewa iamuliwe)
(Hoja iliamuliwa na Kuafikiwa)
(Hoja Binafsi ya Mheshimiwa John Mnyika iliondolewa na Bunge)

MHE. TUNDU M. LISSU: Aaaaaa! Aaaaaaaaaaah! Aibu!

NAIBU SPIKA: Hoja imeondolewa na Bunge linaahirishwa hadi kesho saa tatu kamili asubuhi…”

Hivyo, pamoja na kuwa Kanuni ya 8 inataka Spika kuendesha shughuli za Bunge na kutoa maamuzi kwa haki, uadilifu na bila chuki wala upendeleo wowote kwa kuongozwa na Katiba ya Nchi na Kanuni za Bunge, Naibu Spika wa Bunge alifanya maamuzi yenye kukiuka kanuni ya 58 Fasili ya 5 kwa kuruhusu hoja yangu kuondolewa kwa hoja iliyowasilishwa na Waziri wa Maji.

Kufuatia rufaa hii Spika atataarifiwa kwa mujibu wa kanuni ya 5 (4) na kuitisha kikao cha kamati ya kanuni kwa mujibu wa kanuni ya 5 (5) ya kanuni za Kudumu za Bunge na kulijulisha bunge kuhusu uamuzi utakaotolewa.

Wenu katika uwakilishi wa wananchi,
John Mnyika (Mb)



Thursday, February 28, 2013

HUYU NDIO MKURUGENZI MPYA WA BENKI YA NBC

NATIONAL BANK OF COMMERCE
PRESS RELEASE


The National Bank of Commerce (NBC) has today announced the appointment of Mizinga Melu as its new Managing Director, subject to regulatory approval. The appointment is with effect from 20th May 2013.

Mizinga is joining NBC from Standard Chartered Bank Zambia where until now she has been Managing Director since 2007. She takes over from Lawrence Mafuru, who left the bank in December, 2012.

Mizinga has previously served in senior roles at Standard Chartered, including as Global Head of Development Organisations in the United Kingdom where she was responsible for strategy development and implementation as well as Africa Regional Head of Financial Institutions in Kenya and South Africa where she led formulation of Standard Chartered’s FI business strategy in Africa. Prior, she served as Head of Treasury at Standard Chartered Bank Tanzania between 2000 and 2003.

Mizinga holds a Masters in Business Administration (MBA) from Henley Management College (UK) and is an Associate of the Chartered Institute of Bankers (A.C.I.B). She holds numerous other banking qualifications.

Commenting on the appointment, Barclays Africa Chief Executive Officer and Head of Africa Group Strategy, Kennedy Bungane said: “The appointment of Mizinga reiterates the importance of NBC to our ‘One Africa Strategy’ and we are excited that she is joining us at a time we are making steady progress towards our goal of becoming the go-to bank in Africa.”

Dr. Mussa Juma Assad, Chairman of NBC commented: “The board welcomes Mizinga to NBC and looks forward to working with her in maintaining the position of NBC as a leading bank in Tanzania.”

Commenting on her appointment, Mizinga said: “NBC has over the years proven to be an important financial services provider in Tanzania. I am privileged to have the opportunity to lead this great bank at this important moment and I am looking forward to working with every colleague in NBC as we continue on our journey of transforming the bank in the market.”

Mizinga will report directly to Kennedy Bungane, Barclays Africa Chief Executive Officer and will be a member of the Barclays Africa Executive Committee.


WAKILI: MAHAKAMA IMUONE PONDA HANA KESI YA KUJIBU



UPANDE wa Jamhuri katika kesi ya uchochezi na wizi wa malighafi ya Sh. milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislam, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake 49 wameiomba  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imuone Ponda na wenzake wanakesi ya kujibu kwa sababu umeweza kujenga kesi yao.

Kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya upande wa Jamhuri unaowakilishwa na wakili Mwandamizi wa Serikali Tumaini Kweka na Inspekta wa Polisi,  Hamisi Said na upande wa utetezi unaowakilishwa na Juma Nassor na Njama kuwasilisha majumuisho yao kwa njia ya mdomo ya kuomba mahakama iwaone washitakiwa wanakesi ya kujibu au la.

Kweka ambaye alitumia dakika kumi tu kuwasilisha majumuisho alidai upande wa Jamhuri umeweza kujenga kesi yake kupitia mashahidi wake 16 na vielelezo 13 walivyovileta mahakamani ambapo waamini kisheria vitawafanya washitakiwa wapande kizimbani kujitetea.

Wakili wa utetezi Nassor Juma akiwasilisha majumuisho yake, aliomba mahakama iwaone washitakiwa hawana kesi ya kujibu na waachiliwe huru kwa sababu upande wa Jamhuri umeshindwa kujenga kesi yao.

Nassor alidai wanachokiona katika kesi hiyo ni kuwa kuna mgogoro wa ardhi ambao ulitakiwa ukatatuliwa kwanza na Mahakama ya Ardhi kwa mujibu wa kifungu cha 167 cha Sheria ya Ardhi Na.4 ya mwaka 1999, “Sisi upande wa utetezi tunaiomba mahakama hii iwaachilie huru washitakiwa wote na iwaone hawana kesi ya kujibu kwas ababu kesi hii imefunguliwa kwa jazba na polisi na upande wa Jamhuri umeshindwa kuleta ushahidi ambao utaweza kuishawishi Mahakama iwaone washitakiwa wote wana kesi ya kujibu,” alidai wakili Nassor.

Hakimu Nongwa aliarisha kesi hiyo hadi Machi 4 mwaka huu, ambapo atakuja kutoa uamuzi wa ama kuwaona washitakiwa wana kesi ya kujibu au la na kuamuru Ponda na Mkadamu warudishwe rumande kwa sababu bado Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk Eliezer Feleshi hajaondoa hati yake ya kuwafungia dhamana.



KUFELI KIDATO CHA NNE:LAWAMA ZINAPO MFIKIA NYERERE

Picture

UNAAMBIWA HII NDIO HOTELI NDEFU KULIKO ZOTE DUNIANI: ANGALIA NA MANDHARI YAKE

Hivi ndivyo jengo hoteli hiyo inavyo onekana

Hii ni sehemu ya kupumzika na kupata chakula kwenye hoteli hiyo



Hata hapa chakula kinalika






Hoteli hii imefunguliwa Dubai Tarehe 26 baada ya kupata hadhi ya Hoteli ndefu kuliko zote duniani kutoka kwa Guinness World Records ambao ni watunza kumbukumbu wa matukio wa dunia.
Hoteli hii ina mita 355 ambazo ni sawa na futi 1,099. Jengo refu kuliko yote duniani lina mita 828 ambazo ni sawa na mita 2,717

 

 

 

 

 



KESI YA MAUAJI YA MWANGOSI ASKARI WAWAZUIA WANAHABARI


SAKATA la mtuhumiwa wa mauwaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha Chanel Ten mkoani Iringa marehemu Daudi Mwangosi askari wa FFU mwenye namba G2573 Pasificus Cleophace Simoni (23), limeendelea kuchukua sura mpya baada ya wanahabari kunusurika kupigwa na askari polisi ambao walikuwa wakiwazuia kusogea katika chumba cha mahakama kusikiliza kesi hiyo. Askari polisi hao wakiwa zaidi ya 10 walitumia nguvu za ziada katika kuwadhibiti wanahabari wa vyombo mbalimbali waliofika kusikiliza na kuripoti mwenendo wa kesi hiyo namba 1 ya mwaka 2012 ya mauwaji ya mwanahabari mwenzao, Mwangosi aliyeuwawa Septemba 2 mwaka 2012 katika kijiji cha Nyololo wilaya ya Mufindi wakati wa polisi walipokuwa wakitumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) aliokuwa katika shughuli za ufunguzi wa matawi ya chama hicho. Hata hivyo moja kati ya mbinu waliyopata kuitumia leo wakati mtuhumiwa huyo akifikishwa mahakamani hapo ni kuwafukuza waandishi wa habari eneo hilo la mahakama na kumtoa mtuhumiwa huyo kwa kificho cha hali ya juu kwa kumweka katikati ya watuhumiwa wa makosa mingine zaidi ya 8 huku mtuhumiwa akijificha sura yake kukwepa kamera za waandishi na baadhi ya askari wakimkinga ili kukwepa kupigwa picha. Tukio hilo lilitokea muda wa saa 6.10 mchana wakati mtuhumiwa huyo askari alipokuwa akitolewa na watuhumiwa wengine kutoka chumba cha mahabusu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Iringa na kumpeleka katika chumba cha Mahakama ya wazi kwa ajili ya kesi hiyo kutajwa tena. Hivyo katika hali ya kushangaza ni pale askari hao kuwataka wanahabari hao kusongea umbali wa meta 700 kutoka eneo la Mahakama hiyo wakati mtuhumiwa huyo akiingizwa katika chumba cha Mahakama ya wazi mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa Iringa, Gladys Barthy ili kesi hiyo iweze kutajwa kwa zaidi ya mara ya tano sasa bila upelelezi kukamilika. Uamuzi wa askari hao uliwashangaza hata baadhi ya wananchi waliofika kusikiliza kesi na kuwawekea dhamana ndugu zao na kulazimika kuungana na wanahabari kupinga uamuzi huo na kusababisha askari kuwafukuza pia wananchi hao na kuwataka waungane na wanahabari kuondoka eneo hilo la chumba cha mahakama. Hakimu mkazi mkoa wa mkoa wa Iringa mheshimiwa Barthy alisema kuwa kitendo kilichofanywa na polisi hao kuwazuia wanahabari si maagizo ya Mahakama na kuwa wanahabari hao walikuwa huru kuingia kusikiliza kesi hiyo na kuhabarisha umma kwani hakukiwa na siri wala hakuna maagizo ya mahakama ya kuwataka polisi kuwafukuza wanahabari mahakamani hapo. “Kwanza nawapa pore sana kwa misukosuko mlioipata ....ila mimi nilikuwa ndani ya mahakamani sikujua kinachoendelea huko nje ya mahakama ila nawahakikishieni kuwa kesi hii ilikuwa ikisikilizwa katika mahakama ya wazi na mlikuwa huru kusikiliza,” alisema hakimu huyo akiakimhoji mmoja kati ya viongozi wa polisi kuhusu polisi hao kunyanyasa wanahabari na kuwataka kutorudia kufanya hivyo tena. Mwendesha mashitaka wa serikali Blandina Manyanda aliiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo na kuwa upelelezi bado haujakamilika na mahakama hiyo kupanga tarehe 14 machi ambapo kesi hiyo itafikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa.

SOURCE: WAVUTI



BAADA YA KUJAZWA MAHELA MILOVAN AONDOKA BONGO


ALIYEKUWA kocha wa Simba Milovan Cirkovic ameondoka nchini jana alfajili na shirika la ndege ya Uturuki baada ya kufanikiwa kulipwa fedha zake dola 32 alizokuwa anaidai klabu hiyo.

Kocha huyo ambaye alikuja nchini mapema mwezi huu kwa ajili ya kudai fedha zake baada ya kudanganywa na uongozi wa Simba kuwa wanamtamlipa fedha zake bila mafanikio yoyote ndipo aliamua kuja kudai mwenyewe.

Hata hivyo baada ya kusota muda mrefu huku viongozi wakiwa wanampa ahadi kila siku hatimaye jana alfajiri alifanikiwa kuondoka baada ya kulipwa deni lake la Dola 32 kutoka kwa Malkia wa nyuki Rahma Al Kharoos ambaye ni mjumbe wa kamati ya fedha na mfadhili wa klabu hiyo.

Kocha huyo ameondoka na rekodi ya ubingwa Simba ikiwa ni pamoja na rekodi kubwa ya ushindi ‘mnene’ wa mabao 5-0 dhidi ya watani wao Yanga, msimu uliopita.
 
Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage amesema kuwa uongozi wake haupaswi kulaumiwa kwa kusajili wachezaji wasio kuwa na uwezo bali anayetakiwa kulaumiwa ni aliyekuwa kocha wao Mserbia Milovan Cirkovic.

Rage alisema kuwa wachezaji wote waliowasajili msimu huu ni pendekezo la kocha huyo ambaye alitimuliwa raundi ya kwanza baada ya timu kutofanya vizuri katika michezo yake ya mwisho.

Alisema awali waliwaleta wachezaji wawili kutoka Cameroon lakini kocha aliwakataa na kuwasajili wachezaji wake ambao aliwataka yeye.

Aliongeza kuwa haoni sababu ya wao kulaumiwa kwa sababu wao ni uongozi na sio wachezaji na kuongeza kuwa kama watu wanawalaumu wao wanacheza namba ngapi uwanjani.

Rage akiwa anatoa kauli hiyo tayari kocha Milovan kwa upande wake alikwisha sema kuwa katika wachezaji ambao alitaka wasajiliwe aliyesajiliwa ni Mrisho Ngassa pekee na wengine uongozi ulishindwa.

Msimu huu simba iliweza kusajili beki Lino Musombo, Kanu Mbiyavanga (Congo), Patrick Ochierg (Kenya) na Komabil Keita (Mali).

Lakini baadaye waliwaacha wachezaji watatu na kumbakiza mmoja Keita kwa madai ya kushindwa kuonyesha uwezo mzuri katika timu yao.


DOLA 337,000 ZATUMIKA KUNUNUA iPAD BUNGENI

 

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.


BUNGE nchini Uganda limetumia zaidi ya  dola 377,000 kununa kompyuta aina ya iPad kwa ajili ya wabunge wote .
Maofisa wa bunge hilo walisema kuwa mbali na kuwaweka wabunge hao karibu na  ulimwengu wa teknolojia, wanatarajia kuwasaidia kupunguza gharama za fedha zinazotokana na matumizi ya uchapishaji wa nyaraka mbalimbali.
Kamishna wa bunge hilo Elijah Okupa alisema kuwa kompyuta hizo ni bora na zinafaa kwa matumizi hivyo ni vyema zikatumiwa vizuri.
Alisema  iPad hizo zitakuwa ni mali ya wabunge lakini kama mtu atatumia kwa muda wa miaka mitano asitegemee itakuwa na ubora uleule wa kumwezesha mwingine atumie kwa miaka hiyo alisema Okupa
Kwa mujibu wa takwimu kutoka katika bunge hilo zilionyesha Serikali imekuwa ikitumia zaidi ya dola 12 katika miaka miwili sasa kwa ajili ya mahitaji ya kama kompyuta, uchapishaji wa nyaraka, mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha mawasiliano kuwa bora katika bunge.
Kwa mujibu wa mbunge kutoka mashariki, Medard Segona alisema kuwa kutokana na uwepo wa ipad hizo wanategemea kupunguza matumizi ya fedha zilizokuwa zikipotea hapo awali.
‘’Vifaa hivyo vitapunguza sana matumizi ya fedha kwa kuwa hapo awali wizara ya fedha ilikuwa ikichapisha zaidi ya nyaraka 400 kwa kila mbunge na maofisa wengine waliopo ndani ya bunge hilo’’alisema
Aliongeza kuwa komputa hizo ni muhimu kwa utendaji kazi hasa katika kipindi hicho cha kuendeleza matumizi ya teknolojia.
Hata hivyo taarifa zilisema kuwa wabunge hao bado hawana uelewa mzuri juu ya matumizi hayo licha ya kuwa kampuni imeahidi kutoa  mkataba wa mafunzo ambayo pia yatasaidia kupunguza gharama za matumizi.


Wednesday, February 27, 2013

KIWANDA CHA NGUO CHA MAZAVA CHANUSURIKA KUUNGUA KWA MOTO


Picture
Suma na Asha wakiwa hoi baada ya kufikishwa wodi namba 3 hospitali ya mkoa wa Morogoro (picha: Dunstan Shekidele)
Imeripotiwa kuwa Kiwanda cha nguo cha Mazava kinachomilikiwa na wawekezaji kutonga  nje ya nchi, kilichopo Msamvu mkoani Morogoro kimepata hitilafu ya umeme majira ya saa nne wafanyakazi wakiwa ndani wakishona nguo.

Hali ya hewa iliyobadilika kutokana na moshi ndani ya jengo hilo imesababisha baadhi ya wafanyakazi wanaokadiriwa kuwa 30, kuanguka na wengine kupoteza fahamu  na hivyo kupelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu zaidi.

Waandishi wa habari, Wafanyakazi wa shirika la umeme - TANESCO na Wafanyakazi wa zima-moto waliofika hapo kwa ajili ya kusaidia uokozi na kupata raarifa, walizuiwa kuingia ndani ya kiwanda hicho na wamiliki ambao ni raia wa China wakidai hakuna tukio lolote kubwa linalohitaji huduma ya uokozi hadi kuingia ndani.
Mwandishi wa habari Dunstan Shekidele anasema kumbukumbu za matukio zinaonyesha kuwa  hili ni tukio la tatu.

Akiwahoji baadhi ya wafanyakazi wa kituo hicho, amefahamishwa kwamba hali hiyo huenda hali hiyo inatokana na hujuma za baadhi ya wafanyazi wanaolalamika kufanya kazi kwa saa 12 na kulipwa mashahara ya shilingi elfu 80/=.
Picture
(picha: Dunstan Shekidele)
Picture
Bi, Subira Juma Athumani [kushoto] akiwa na majeruhi wenzake. (picha: Dunstan Shekidele)



 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU