Facebook Comments Box

Thursday, February 28, 2013

KESI YA MAUAJI YA MWANGOSI ASKARI WAWAZUIA WANAHABARI


SAKATA la mtuhumiwa wa mauwaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo cha Chanel Ten mkoani Iringa marehemu Daudi Mwangosi askari wa FFU mwenye namba G2573 Pasificus Cleophace Simoni (23), limeendelea kuchukua sura mpya baada ya wanahabari kunusurika kupigwa na askari polisi ambao walikuwa wakiwazuia kusogea katika chumba cha mahakama kusikiliza kesi hiyo. Askari polisi hao wakiwa zaidi ya 10 walitumia nguvu za ziada katika kuwadhibiti wanahabari wa vyombo mbalimbali waliofika kusikiliza na kuripoti mwenendo wa kesi hiyo namba 1 ya mwaka 2012 ya mauwaji ya mwanahabari mwenzao, Mwangosi aliyeuwawa Septemba 2 mwaka 2012 katika kijiji cha Nyololo wilaya ya Mufindi wakati wa polisi walipokuwa wakitumia nguvu kuwatawanya wafuasi wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) aliokuwa katika shughuli za ufunguzi wa matawi ya chama hicho. Hata hivyo moja kati ya mbinu waliyopata kuitumia leo wakati mtuhumiwa huyo akifikishwa mahakamani hapo ni kuwafukuza waandishi wa habari eneo hilo la mahakama na kumtoa mtuhumiwa huyo kwa kificho cha hali ya juu kwa kumweka katikati ya watuhumiwa wa makosa mingine zaidi ya 8 huku mtuhumiwa akijificha sura yake kukwepa kamera za waandishi na baadhi ya askari wakimkinga ili kukwepa kupigwa picha. Tukio hilo lilitokea muda wa saa 6.10 mchana wakati mtuhumiwa huyo askari alipokuwa akitolewa na watuhumiwa wengine kutoka chumba cha mahabusu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Iringa na kumpeleka katika chumba cha Mahakama ya wazi kwa ajili ya kesi hiyo kutajwa tena. Hivyo katika hali ya kushangaza ni pale askari hao kuwataka wanahabari hao kusongea umbali wa meta 700 kutoka eneo la Mahakama hiyo wakati mtuhumiwa huyo akiingizwa katika chumba cha Mahakama ya wazi mbele ya hakimu mkazi wa mahakama ya mkoa wa Iringa, Gladys Barthy ili kesi hiyo iweze kutajwa kwa zaidi ya mara ya tano sasa bila upelelezi kukamilika. Uamuzi wa askari hao uliwashangaza hata baadhi ya wananchi waliofika kusikiliza kesi na kuwawekea dhamana ndugu zao na kulazimika kuungana na wanahabari kupinga uamuzi huo na kusababisha askari kuwafukuza pia wananchi hao na kuwataka waungane na wanahabari kuondoka eneo hilo la chumba cha mahakama. Hakimu mkazi mkoa wa mkoa wa Iringa mheshimiwa Barthy alisema kuwa kitendo kilichofanywa na polisi hao kuwazuia wanahabari si maagizo ya Mahakama na kuwa wanahabari hao walikuwa huru kuingia kusikiliza kesi hiyo na kuhabarisha umma kwani hakukiwa na siri wala hakuna maagizo ya mahakama ya kuwataka polisi kuwafukuza wanahabari mahakamani hapo. “Kwanza nawapa pore sana kwa misukosuko mlioipata ....ila mimi nilikuwa ndani ya mahakamani sikujua kinachoendelea huko nje ya mahakama ila nawahakikishieni kuwa kesi hii ilikuwa ikisikilizwa katika mahakama ya wazi na mlikuwa huru kusikiliza,” alisema hakimu huyo akiakimhoji mmoja kati ya viongozi wa polisi kuhusu polisi hao kunyanyasa wanahabari na kuwataka kutorudia kufanya hivyo tena. Mwendesha mashitaka wa serikali Blandina Manyanda aliiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo na kuwa upelelezi bado haujakamilika na mahakama hiyo kupanga tarehe 14 machi ambapo kesi hiyo itafikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa.

SOURCE: WAVUTI



BAADA YA KUJAZWA MAHELA MILOVAN AONDOKA BONGO


ALIYEKUWA kocha wa Simba Milovan Cirkovic ameondoka nchini jana alfajili na shirika la ndege ya Uturuki baada ya kufanikiwa kulipwa fedha zake dola 32 alizokuwa anaidai klabu hiyo.

Kocha huyo ambaye alikuja nchini mapema mwezi huu kwa ajili ya kudai fedha zake baada ya kudanganywa na uongozi wa Simba kuwa wanamtamlipa fedha zake bila mafanikio yoyote ndipo aliamua kuja kudai mwenyewe.

Hata hivyo baada ya kusota muda mrefu huku viongozi wakiwa wanampa ahadi kila siku hatimaye jana alfajiri alifanikiwa kuondoka baada ya kulipwa deni lake la Dola 32 kutoka kwa Malkia wa nyuki Rahma Al Kharoos ambaye ni mjumbe wa kamati ya fedha na mfadhili wa klabu hiyo.

Kocha huyo ameondoka na rekodi ya ubingwa Simba ikiwa ni pamoja na rekodi kubwa ya ushindi ‘mnene’ wa mabao 5-0 dhidi ya watani wao Yanga, msimu uliopita.
 
Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa Simba Ismail Aden Rage amesema kuwa uongozi wake haupaswi kulaumiwa kwa kusajili wachezaji wasio kuwa na uwezo bali anayetakiwa kulaumiwa ni aliyekuwa kocha wao Mserbia Milovan Cirkovic.

Rage alisema kuwa wachezaji wote waliowasajili msimu huu ni pendekezo la kocha huyo ambaye alitimuliwa raundi ya kwanza baada ya timu kutofanya vizuri katika michezo yake ya mwisho.

Alisema awali waliwaleta wachezaji wawili kutoka Cameroon lakini kocha aliwakataa na kuwasajili wachezaji wake ambao aliwataka yeye.

Aliongeza kuwa haoni sababu ya wao kulaumiwa kwa sababu wao ni uongozi na sio wachezaji na kuongeza kuwa kama watu wanawalaumu wao wanacheza namba ngapi uwanjani.

Rage akiwa anatoa kauli hiyo tayari kocha Milovan kwa upande wake alikwisha sema kuwa katika wachezaji ambao alitaka wasajiliwe aliyesajiliwa ni Mrisho Ngassa pekee na wengine uongozi ulishindwa.

Msimu huu simba iliweza kusajili beki Lino Musombo, Kanu Mbiyavanga (Congo), Patrick Ochierg (Kenya) na Komabil Keita (Mali).

Lakini baadaye waliwaacha wachezaji watatu na kumbakiza mmoja Keita kwa madai ya kushindwa kuonyesha uwezo mzuri katika timu yao.


DOLA 337,000 ZATUMIKA KUNUNUA iPAD BUNGENI

 

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.


BUNGE nchini Uganda limetumia zaidi ya  dola 377,000 kununa kompyuta aina ya iPad kwa ajili ya wabunge wote .
Maofisa wa bunge hilo walisema kuwa mbali na kuwaweka wabunge hao karibu na  ulimwengu wa teknolojia, wanatarajia kuwasaidia kupunguza gharama za fedha zinazotokana na matumizi ya uchapishaji wa nyaraka mbalimbali.
Kamishna wa bunge hilo Elijah Okupa alisema kuwa kompyuta hizo ni bora na zinafaa kwa matumizi hivyo ni vyema zikatumiwa vizuri.
Alisema  iPad hizo zitakuwa ni mali ya wabunge lakini kama mtu atatumia kwa muda wa miaka mitano asitegemee itakuwa na ubora uleule wa kumwezesha mwingine atumie kwa miaka hiyo alisema Okupa
Kwa mujibu wa takwimu kutoka katika bunge hilo zilionyesha Serikali imekuwa ikitumia zaidi ya dola 12 katika miaka miwili sasa kwa ajili ya mahitaji ya kama kompyuta, uchapishaji wa nyaraka, mbalimbali kwa ajili ya kuwezesha mawasiliano kuwa bora katika bunge.
Kwa mujibu wa mbunge kutoka mashariki, Medard Segona alisema kuwa kutokana na uwepo wa ipad hizo wanategemea kupunguza matumizi ya fedha zilizokuwa zikipotea hapo awali.
‘’Vifaa hivyo vitapunguza sana matumizi ya fedha kwa kuwa hapo awali wizara ya fedha ilikuwa ikichapisha zaidi ya nyaraka 400 kwa kila mbunge na maofisa wengine waliopo ndani ya bunge hilo’’alisema
Aliongeza kuwa komputa hizo ni muhimu kwa utendaji kazi hasa katika kipindi hicho cha kuendeleza matumizi ya teknolojia.
Hata hivyo taarifa zilisema kuwa wabunge hao bado hawana uelewa mzuri juu ya matumizi hayo licha ya kuwa kampuni imeahidi kutoa  mkataba wa mafunzo ambayo pia yatasaidia kupunguza gharama za matumizi.


Wednesday, February 27, 2013

KIWANDA CHA NGUO CHA MAZAVA CHANUSURIKA KUUNGUA KWA MOTO


Picture
Suma na Asha wakiwa hoi baada ya kufikishwa wodi namba 3 hospitali ya mkoa wa Morogoro (picha: Dunstan Shekidele)
Imeripotiwa kuwa Kiwanda cha nguo cha Mazava kinachomilikiwa na wawekezaji kutonga  nje ya nchi, kilichopo Msamvu mkoani Morogoro kimepata hitilafu ya umeme majira ya saa nne wafanyakazi wakiwa ndani wakishona nguo.

Hali ya hewa iliyobadilika kutokana na moshi ndani ya jengo hilo imesababisha baadhi ya wafanyakazi wanaokadiriwa kuwa 30, kuanguka na wengine kupoteza fahamu  na hivyo kupelekwa hospitalini kwa ajili ya matibabu zaidi.

Waandishi wa habari, Wafanyakazi wa shirika la umeme - TANESCO na Wafanyakazi wa zima-moto waliofika hapo kwa ajili ya kusaidia uokozi na kupata raarifa, walizuiwa kuingia ndani ya kiwanda hicho na wamiliki ambao ni raia wa China wakidai hakuna tukio lolote kubwa linalohitaji huduma ya uokozi hadi kuingia ndani.
Mwandishi wa habari Dunstan Shekidele anasema kumbukumbu za matukio zinaonyesha kuwa  hili ni tukio la tatu.

Akiwahoji baadhi ya wafanyakazi wa kituo hicho, amefahamishwa kwamba hali hiyo huenda hali hiyo inatokana na hujuma za baadhi ya wafanyazi wanaolalamika kufanya kazi kwa saa 12 na kulipwa mashahara ya shilingi elfu 80/=.
Picture
(picha: Dunstan Shekidele)
Picture
Bi, Subira Juma Athumani [kushoto] akiwa na majeruhi wenzake. (picha: Dunstan Shekidele)



MUFT SIMBA ATENGUA NAFASI YA SHEIKH MKUU SEMWALI WA MOROGORO


  Sheikh Mkuu na Tanzania, Mufti Issa bin Shaaban Simba, ametengua nafasi ya Shekhe Mkuu mkoani Morogoro, Yahya Semwali akidaiwa kushindwa kusimamia maendeleo ya Waislamu mkoani humo.

Katika barua yake kwa Shekhe Semwali yenye namba MK/BR/UL/03/04/79 ya Februari 19 mwaka huu, Mufti Simba alisema uamuzi huo umefikiwa kwenye kikao cha Baraza la Ulamaa Taifa hivyo anatakiwa kukabidhi ofisi.

Kutokana na uamuzi wa baraza hilo, Mufti Simba amemteua Shekhe wa Mkoa wa Dodoma, Mustafa Shaaban kukaimu nafasi hiyo kwa barua yenye namba MK/BR/UL/03/04/81 ya Februari 20 mwaka huu na kusisitiza kuwa, nafsi hiyo inapaswa kujazwa ndani ya siku 90 kwa kufanya uchaguzi mwingine.

“Waumini wa Kiislamu mkoani Morogoro wapewe fursa ya kuchagua Sheikh mwingine wa Mkoa,” ilisema barua hiyo.

Uamuzi huo umepokelewa kwa hisia tofauti na viongozi mbalimbali wa BAKWATA mkoani humo akiwemo Sheikh
Semwali aliyeondolewa madrakani ambaye alisema madai yaliyotolewa dhidi yake si sahihi na yameegemea upande
mmoja yakisukumwa na hisia zaidi.

Alisema kuondolewa kwake katika nafasi hiyo kunatokana na hisia za kuunga mkono msimamo wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Issa Ponda jambo ambalohalina ukweli.

Sheikh Semwali alisema:
Hisia nyingine zilizojionesha ni kitendo cha mimi kwenda ibada ya Hijja kupitia taasisi nyingine tofauti na Baraza la Waislamu nchini (BAKWATA), pamoja na uamuzi wangu wa kutengua uchaguzi wa baraza hili ngazi ya kata, wilayani Gairo.

Uchaguzi huu ulifanyika kinyime na utaratibu bila ya ngazi husika kama BAKWATA Wilaya na Mkoa kuwa na taarifa, hili ndio lililomsukuma Mufti Simba kufikia maamuzi haya japo baraza hili Mkoa lina taarifa za ukikukwaji husika lakini bado aliendelea kukaa kimya.
Kuhusu madai ya kushindwa kusimamia maendeleo ya Waislamu, Sheikh Semwali alisema hivi sasa katika Wilaya zote kuna miradi ya maendeleo kama ule wa Wilaya ya Ulanga ambako kuna ujenzi wa vyumba vya maduka 14.

Pia kuna mchakato wa upatikanaji ekari 20 kwa ajili ya upandaji miti ya matunda ambapo hivi sasa walikuwa kwenye hatua za mwisho kupata ekari nyingine 600.

Alisema Wilaya ya Morogoro Vijijini kuna vyumba vitano vya maduka, Mvomero vyumba vinne vya madrasa na Kilombero vyumba vitano vya biashara ambapo maendeleo hayo  yametokana na juhudi zake.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti wa Baraza la Masheikh mkoani humo, ambalo lilikaa hivi karibuni kupitia maamuzi hayo, Sheikh Shaaban Nyoni, alisema uamuzi wa Mufti Simba amekiuka Katiba ya BAKWATA.
Shekhe Semwali alichaguliwa hakuteuliwa hivuyo kama alikuwa na tatizo, wao kama baraza ndio waliopaswa kuwasilisha tatizo lao kwa Mufti Simba si vinginevyo.

Halmashauri ya BAKWATA Mkoa inatarajia kukutana kesho (leo), ili kujadili uamuzi huu na baadaye kikao cha Mashekhe wote wa Wilaya na Mkoa, watakaa kujadili na kutoa msimamo.
Imam wa Msikiti wa Al Aqswaa wa Mazimbu, mkoani humo, Sheikh Mohamed Msoma ambaye ni mjumbe wa Baraza la Masheikh, alisema si sahihi Mufti Simba kumuondoa Sheikh Semwali katika nafasi yake.



KAGERA SUGAR WAPELEKWA PUTA MPAKA WAOMBA POO KWA YANGA: WAMEPIGWA KAMOJA TU

Niyonzima akiwapungia mikono mashabiki baada ya mechi

Na Mahmoud Zubeiry
KWA mara ya pili mfululizo, kiungo Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima leo tena amekuwa shujaa wa timu yake, Yanga SC baada ya kuifungia bao pekee la ushindi katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Niyonzima alijikuta akituzwa fedha na mashabiki wa timu yake baada ya mechi hiyo, iliyokuwa ngumu kwa Wana Jangwani, kutokana na kuibeba timu hiyo mara mbili mfululizo kwa kufunga mabao ya juhudi binafsi, ikiwemo mechi iliyopita dhidi ya Azam FC. 
Didier Kavumbangu akipiga shuti langoni mwa Kagera mbele ya mabeki wa Kagera
Ushindi huo unaifanya Yanga ifikishe pointi 42, baada ya kucheza mechi 18, hivyo kujitanua kileleni mwa Ligi Kuu, ikiizidi Azam FC kwa pointi sita, ambayo inashika nafasi ya pili kwa pointi zake 36, wakati mabingwa watetezi, Simba SC wanashika nafasi ya tatu kwa pointi zao 31.
Kagera inabaki na pointi zake 28 katika nafasi ya tano, baada ya kucheza mechi 19, chini ya Coastal Union ya Tanga inayoshika nafasi ya nne kwa pointi zake 30.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Simon Mberwa kutoka Pwani, aliyesaidiwa na Milambo Tshikungu wa Mbeya na Said Tibabimale kutoka Mwanza, hadi mapumziko, hakuna timu iliyofanikiwa kuona lango la mwenzake.
Hata hivyo, mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Didier Kavumbangu aliikosesha timu yake bao, baada ya kupiga juu ya lango mkwaju wake wa penalti dakika ya 44.
Refa Mberwa, alitoa penalti hiyo baada ya Kavumbangu mwenyewe kudakwa miguu kwenye eneo la hatari na kipa wa Kagera, Mganda Hannington Kalyesebula.
Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko, Yanga inayofundishwa na Mholanzi, Ernie Brandts ikiwatoa Kavumbangu na Bahanuzi na kuwaingiza Jerry Tegete na Mganda Hamisi Kiiza, wakati Kagera inayofundishwa na mzalendo, Abdallah Kibadeni, iliwatoa Mnigeria Darlington Enyinna na Julius Mrope na kuwaingiza Paul Ngway na Themi Felix.
Mabadiliko hayo yaliongeza uhai kwa kila upande na kuongeza kasi na ladha ya mchezo, lakini bahati hii leo ilikuwa kwa wana Jangwani, kutokana na kupata bao pekee la ushindi lililofungwa na kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Niyonzima.   
Niyonzima alifunga bao hilo dakika ya 65, baada ya kumhadaa kiungo wa Kagera, George Kavilla na kufumua shuti kali akiwa umbali wa mita 25, lililomshinda kipa wa Kagera, Kalyesebula.
Halikuwa na tofauti sana na bao pekee la ushindi alilofunga kwenye mchezo uliopita wa timu yake dhidi ya Azam FC, Uwanja huo huo wa Taifa, Jumamosi iliyopita.   
Mshambuliaji wa zamani wa Simba, Shijja Mkinna alikosa bao la wazi dakika ya 89, baada ya kupewa pasi nzuri na Paul Ngway, lakini akapiga juu ya lango.
Hiyo ilikuwa nafasi pekee ya kujutia kwa Kagera ambao leo iliitoa jasho Yanga.  Jerry Tegete naye alikosa bao la wazi dakika ya 87, akishindwa kuunganisha krosi ya Simon Msuva. 
Kwa ushindi huo, Yanga imelipa kisasi cha kufungwa 1-0 na Kagera katika mchezo wa kwanza wa ligi hiyo, mwishoni mwa mwaka jana mjini Bukoba.
Katika mchezo huo, kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Frank Domayo, Didier Kavumbangu/Hamisi Kiiza dk67, Said Bahanuzi/Jerry Tegete dk 67 na Haruna Niyonzima.
Kagera Sugar; Hannington Kalyesebula, Benjamin Asukile, Martin Muganyizi, Malegesi Mwangwa, Amandus Nesta, Gaorge Kavilla, Julius Mrope/Paul Ngway dk 62, Juma Nade, Darlington Enyinna/Themi Felix dk 69, Shijja Mkinna na Daudi Jumanne.    

SOURCE: BIN ZUBEIRY

ALIYEKUWA MWENYEKITI WA TUME YA UCHAGUZI KENYA SAMWEL KIVUITU AMEAGA DUNIA


336544_319369068086667_163569676999941_1031123_336563521_o

Wakili aliyekuwa mwenyekiti  wa tume ya uchaguzi ya Kenya,  ECK ndugu Samuel Kivuitu ameaga dunia
Taarifa zilizotolewa na familia ya Kivuitu zinasema kuwa marehemu aliaga dunia jana usiku mwendo wa saa nne katika hospitali ya MP Shah iliyopo jijini Nairobi, alikokuwa amelazwa kwa matibabu ya saratani.
Kivuitu alikuwa akisumbuliwa na saratani ya  koo ambapo alikuwa akipelekwa katika hospitali hiyo mara kwa mara kwa muda wa miaka miwili.

Marehemu Kivuitu alivuma sana mwaka 2007 baada ya matokeo ya uchaguzi wa Rais nchini Kenya yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya wakati huo ECK yeye akiwa Mwenyekiti, matokeo ambayo yalipokelewa kwa hisia tofauti na kuwa sababu hasa ya kuchochea machafuko makubwa kuwahi kushuhudiwa katika historia ya Kenya ambapo watu 1,133 waliuawa na wengine laki sita na nusu kuachwa bila ya makazi.


Monday, February 25, 2013

ANGALIA LIVE HAPA MDAHALO WA MWISHO WA WAGOMBEA URAIS WA KENYA

Live Video streaming by Ustream

MDAHALO WA MWISHO WA WAGOMBEA URAIS KENYA UMEANZA



Mdahalo wa mwisho wa wagombea wa uchaguzi nchini Kwenya unafanyika jioni ya leo.
Awali kulikuwa na taarifa kuwa mgombea wa Urais Uhuru Kenyatta alikuwa amesusia mdahalo huo akidai kuwa mdahalo wa kwanza waliokuwa wanauendesha mjadala wenyewe waliangazia sana swala la ICC na kuwafanya wagombea wengine kumlemea.
Duru zilisema kuwa Uhuru alisitisha kampeini zake leo ili kuweza kujiandaa vilivyo kwa mjadala huo.
Wagombea wengine akiwemo waziri mkuu Raila Odinga wanajiandaa kwa mjadala huo ambaop hii leo utalipa kipao mbele mbele swala la ardhi, sera za kigeni, na uchumi.
Kura za maoni zinaonyesha kuwa asilimia tisini ya wapiga kura wanaona mjadala huu una manufaa kwa wakenya. Asilimia themanini na tano walisema wako trayari kutazama mjadala huo.
Asilimia robaini ya wapiga kura waliohojiwa punde baada ya mjadala wa kwanza walisema wangempigia kura Uhuru Kenyatta wakati asilimia 33 walisema wangempigia kura Raila Odinga.Wawili hao ndio wagombea wakuu katika uchaguzi huu.



RAGE AKATAA KUJIUZURU ILA ASEMA MAAMUZI YATAKAYOFUATA NI MAGUMU

Mh Aden Rage akiwa amependeza katika rangi za kijani na njano
Na Dina Ismail
KAMATI ya utendaji ya klabu ya Simba inatarajiwa kutoa uamuzi mgumu kuhusiana na mwenendo mbaya ulionayo timu hiyo katika ligi kuu ya Vodacom.
Aidha, Rage amekanusha taarifa za kujiuzulu kwake kufuatia mwenendo mbaya wa timu hiyo kwenye ligi hiyo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, mwenyekiti wa Simba Alhaj Ismail Aden Rage alisema kwamba kamati ya utendaji ya Simba ilitarajiwa kukutana jana kwa ajili ya kujadili mustakabali wa timu yao.
Alisema kikao hicho kitajadili kwa kina hali iliyopo sasa ambayo imesabababisha timu yao kupoteza hata matumaini ya kutetea ubingwa wao.
“Tutakuna baadaye leo na kujadili hali hii maana tukiiacha hivi hivi inaweza kutuletea madhara makubwa sana…pia tutatoa maamuzi mazito baada ya kikao chetu,”alisema.
Kuhusu na taarifa za kujiuzulu kwake, Rage alisema anashangazwa na taarifa hizo zinapotoka kwani kama atafikia uamuzi huo ataitisha mkutano na waandishi wa habari na kuzungumzia hatua hiyo.
“Mimi sijasema nitajiuzulu jamani hata hiyo taarifa yenyewe ukiisoma haileweki, hivyo nawaomba wanasimba kutulia kuona kipi kitakachofuata,”aliongeza Rage
Simba imeonekana kusuasua sua katika ligi hiyo baada ya kutokuwa na matokeo ya kuridhisha sambamba na kuamulia vipigo katika mechi zake.
Hali hiyo ilianza kujitokeza tangu mwishoni mwa mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo ambao ulipelekea kutoka kileleni hadi kushika nafasi ya tatu.
Aidha, tangu kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi hiyo, Simba imeshinda mechi mbili dhidi ya African Lyon 3-1 na Tanzania Prisons 1-0, huku ikitoka sare mbili dhidi ya JKT Ruvu na JKT Oljoro kwa bao 1-1 kabla ya kufungwa bao 1-0 na Mtibwa Sugar juzi. 

SOURCE:  BIN ZUBEIRY 

SERIKALI YAITOA KATIBA YA TFF YA MWAKA 2012 YAAGIZA UCHAGUZI UTUMIE KATIBA YA 2006

Serikali imeingilia kati sakata la uchaguzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kuamuru kufutwa kwa katiba ya sasa ya shirikisho hilo na badala yake kuamuru itumike katiba ya zamani (mwaka 2006) baada ya kubaini kuwa iliyopo ina kasoro nyingi.

Katika taarifa yake kwa waandishi wa habari leo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo imeeleza kuwa katiba ya sasa ya TFF si halali. Imeelezwa vilevile kuwa msajili wa vyama vya michezo aliyedaiwa kuipitisha katiba hiyo ameondolewa.

Mchakato wa uchaguzi mkuu wa TFF umesimamishwa kutokana na mgogoro mzito uliotokana na kuenguliwa kiutata kwa wagombea kadhaa, wakiwamo Jamal Malinzi anayewania urais na Michael Wambura anayetaka kugombea nafasi ya makamu wa rais.

Kamati ya rufani ya TFF inayoongozwa na Iddi Mtiginjola ndiyo iliyozua balaa lote la sasa baada ya kuwaengua kina Malinzi na mwishowe kumuacha makamu wa sasa wa rais, Athumani Nyamlani abaki kuwa mgombea pekee.


Hata hivyo, tayari mchakato wa uchaguzi huo uliozua mabishano makali umeshasimamishwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) na maafisa wa chombo hicho cha juu cha mchezo wa soka duniani wameshaanza kuwasili kufuatilia kinachotokea nchini.

Uamuzi wa serikali wa kufuta katiba ya sasa na kutaka itumike ya 2006 unampa ahueni kubwa Wambura ambaye alishasema hadharani kuwa  ataiburuza TFF mahakamani kama isipoachana na katiba mpya na kufuata ya zamani; huku akitoa sababu kadhaa za kupinga matumizi ya katiba mpya, mojawapo ikiwa ni kupitishwa kwake kwa njia ya waraka wa barua pepe (e-mail) kwenda kwa wajumbe badala ya kufuata maelekezo ya katiba yanayotaka mabadiliko kufanywa na wajumbe kupitia mkutano mkuu.

Hata hivyo, kwa mujibu wa taratibu za FIFA, ni marufuku kwa shughuli za soka kuingiliwa na serikali au mahakama na nchi yoyote inayokwenda kinyume na taratibu hizo hujikuta ikifungiwa kama ilivyowahi kutokea nchini Kenya.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU