Facebook Comments Box

Friday, February 22, 2013

PSPF WAONESHA NYUMBA ZAO ZA MKOPO ZILIZOPO BUYUNI - CHANIKA




Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) umekamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wa nyumba 641 katika mikoa mitano ambazo zilianza kuuzwa tangu Novemba mwaka 2012. Mradi huo unalenga kutatua tatizo la makazi kwa wanachama wake na jamii kwa ujumla.

Mikoa iliyojengwa nyumba hizo na idadi ya nyumba katika mabano ni Dar es salaam – Buyuni (491), Morogoro – Lukobe (25), Shinyanga – Ibadakuli (50), Tabora – Usule (25) na Mkoa wa Mtwara – Mang’amba (50).

Aidha kwa Mujibu wa maelezo ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSPF, Bwana Adam Mayingu amewaambia wanandishi wa habari na viongozi mbalimbali waliotembelea eneo la mradi huo Mkoa wa Dar es Salaam kuwa Shirika lake limejenga nyumba za aina nne ambazo ni za nyumba viwili, Vyumba vitatu, Nyumba za vyumba vitatu kimoja ikiwa ni Master na Nyumba ya vymba vine kimoja kikiwa ni Master.

Gharama ya ununuzi wa nyumba hizo ambazo zinauzwa kwa wanachama wa Mfuko huo ni kati ya Shilingi Milioni 64 hadi milioni 94 gharama zikijumlishwa na Kodi ya ongezejo la Thamani.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) Adam Mayingu (katikati) akiwaonesha maofisa wa Jeshi la Polisi moja ya nyumba 491 zilizopo katika mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu ambazo zitkopeshwa kwa wanachgama wa mfuko huo. Nyumba hizo zipo katika eneo la Kigezi Kata ya Majohe wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF) Adam Mayingu (kushoto) akifafanua jambo wakati wa ziara hiyo ya kuakagua makazi hayo. Kulia ni  Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Hery Mohamed Kessy Nyumba hizo zipo katika eneo la Kigezi Kata ya Majohe wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.
 Wadau mbalimbali wakitembelea nyumba hizo hii leo.

 Ziara ikiendelea katika nyumba hizo zipatazo 491




MALKIA WA NYUKI AMLIPA ALIYEKUWA KOCHA WA TIMU YA SIMBA MILOVAN CIRKOVIC


Ushahidi wa cheki aliyopewa Milovan Cirkovic na Malkia wa Nyuki kulipa deni alilokuwa akiidai Simba.


Thursday, February 21, 2013

TANZANIA BREWERIES YAKABIDHI BASI JIPYA KWA TIMU YA TAIFA




Mkurugenzi Mtendaji wa Kampauni ya Bia Tanzania (TBL) Robin Goetzsche (wa tatu kushoto) akikabidhi funguo kama ishara ya kukabidhi basi la Taifa Stars kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Leodgar Tenga (wan ne kushoto) wakati Kilimanjaro Premium Lager ilipokabidhii basi hilo makao makuu ya TBL Jijini Dar es Salaam leo. Wengine kutoka kushoto ni Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kaviske, Mkurugenzi wa Masoko wa TBL Kushilla Thomas, Kocha wa Taifa Stars, Kim Poulsen, Mchezaji wa Taifa Stars aliyewawakilisha wenzake, Erasto Nyoni, Katibu Mkuu wa TFF Angetile Osiah, Ofisa Mwandamizi wa Baraza la Michezo Tanzania, Chalukulu John na Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF Sunday Kayuni.




Kocha wa Timu ya Taifa Kim Poulsen akishuka kutoka kwenye basi jipya la Taifa Stars lililolabidhiwa na Kilimanjaro Premium Lager.











MUHIMBILI WAKANUSHA KUVAMIA OFISI YA MKURUGENZI


 
Gazeti la Mwananchi ISSN-0856-7573 Na.4621 la tarehe 20 Februari 2013
lilichapisha habari katika ukurasa wake wa pili iliyokuwa na kichwa cha habari “Muhimbili Wavamia Ofisi ya Mkurugenzi”. Awali ya yote tunapenda ieleweke kuwa  wafanyakazi hawakuvamia ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kwa kuwa kulikuwa na mawasiliano na wafanyakazi waliotaka kumuona kupitia kwa Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi TUGHE Tawi la Muhimbili na alikuwa amekubaliana na ombi la kukutana nao.

Pili, tunapenda kutoa ufafanuzi kwamba wafanyakazi hawa hawakuvamia kama gazeti linavyodai. Aidha, tunakanusha sababu zilizotolewa na Gazeti la Mwananchi kwamba wafanyakazi walivamia ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wakishinikiza kulipwa mishahara ambayo kwa mujibu wa taarifa za gazeti hili ni kuwa haijalipwa kwa muda wa miezi mitatu tangu mwaka jana mwezi wa 11.

Tunapenda kuueleza umma kwamba taarifa hizi ni upotoshaji wa hali halisi ya ulipaji wa mishahara kwa wafanyakazi na taarifa hizi hazijatafitiwa kutoka mamlaka za Hospitali kuthibisha ukweli wake. Habari hizi siyo za kweli kwa kuwa Hospitali haijawahi kukosa mishahara ya wafanyakazi, hususan katika kipindi kinachodaiwa wafanyakazi hawakupata mishahara. Tumebaini pia gazeti hili limetumia majina ya watu likidai ni wafanyakazi wa Hospitali hii wakati siyo kweli kwa nia ya kuufanya umma uamini kwamba habari hizi ni halali na za kweli wakati ni kinyume chake. Watu wenye majina Anna Msigwa alitajwa kama Muuguzi na Anthony Semukasi siyo miongoni mwa wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili hivyo ni majina bandia. Kwa hiyo habari hii ni ya uzushi usio na ukweli wowote. Ni mtu mmoja tu aliyetajwa kwa jina la Ndg. Faustine Fidelis, ndiye tunamtambua kuwa mfanyakazi katika Hospitali hii na Katibu wa tawi la TUGHE Muhimbili.

Tunapenda umma uelewe kwamba kama kuna mfanyakazi hapati mshahara basi atakuwa ni mfanyakazi mpya ambaye taratibu za kupata mshahara wake kutoka serikalini zinafanyika. Wafanyakazi wa aina hii ni wachache na tunaamini kwamba hawakulengwa na taarifa hizi ambazo zilitaka umma uamini kwamba wafanyakazi wote wa Hospitali ya Taifa Muhimbili hawajapata mishahara tangu Novemba 2012 hadi sasa.

Tunapenda kutoa ufafanuzi kwamba wafanyakazi walienda kwenye ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kudai motisha iliyotokana na mapato kupitia huduma iliyotolewa kwa wagonjwa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Taifa (NHIF) ambayo iliahidiwa kulipwa na Uongozi wa Hospitali. Malipo haya siyo sehemu ya mishahara bali ni motisha kwa wafanyakazi yenye lengo la kuongeza tija. Malipo haya yalichelewa kulipwa kwa baadhi ya wafanyakazi lakini yalikuwa katika hatua za mwisho za maandalizi ya kulipwa. Wafanyakazi walielezwa hili na walielewa na kuendelea na kazi.

Hospitali ya Taifa Muhimbili iko tayari kutoa ushirikiano kwa vyombo vya habari kuviwezesha kutoa taarifa sahihi kwa umma. Tunawasihi waandishi wa habari kupata ufafanuzi wa taarifa zozote wanazopata kuhusu Hospitali kabla ya kuandika na kupotosha umma.


Imetolewa na Ofisi ya Uhusiano
Februari 21, 2013



Wednesday, February 20, 2013

ANGALIA VIBONZO HIVI VINAVYOHUSU MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

Uzuri wa wachora vibonzo ni utumiaji wao wa mchoro kuwakilisha maada ambayo kwa mtu mwingine angehitaji kurasa nyingi za karatasi ili kueleweka. Angalia vibonzo hivi viwili ambavyo vinatosha kabisa kukupa taswira ya elimu hapa Tanzania




Tuesday, February 19, 2013

MWENYEKITI WA KIJIJI ALIEUZA MLIMA ATIMULIWA MADARAKANI NA WANANCHI

WANANCHI wa Kijiji cha Zuzu Kata hiyo mkoani Dodoma, Wameiangusha Serikali ya Kijiji hicho iliyokuwa ikiongozwa na aliyekuwa Mwenyekiti Peter Mtawale (49) wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambaye ameamua kuiacha Ofisi yake kwa kosa la kuuza Mlima wa Widete.

Mtawale aliyezaliwa 1963 alikubali kujiuzulu kwa kuutangazia Mkutano wa Hadhara karibuni mwaka huu baada ya kubanwa na tuhuma nyingi ikiwemo ya kuuza Mlima huo kwa Mwekezaji ambaye alikiri Serikali yake ilimruhusu uchimbaji wa Rupia bila kuwaarifu wananchi.

Mbali ya Tuhuma za kuuza Mlima bila kuwataarifu wananchi na Uongozi wa Kata, nyingine ni pamoja na mauzo ya Changarawe (Kifusi), Maji, Mchanga,  Ufujaji  wa Fedha ya Malambo Mbgani, Ushuru wa Magari, kuingia kwa wageni bila taarifa, Kutoitishwa kwa Vikao na kusoma Mapato na Mtumizi, Milio ya Milipuko, na Viongozi kufunga Maji bila Mita.

“Kuna Uchochezi ninaofanyiwa na Diwani wa Kata Awadhi Abdalah (CCM), Mwenyekiti wa Changu (CCM) Omari Kagusi na Katibu Mwenezi Solo (CCM) ambapo 14.1.2012 walifanya kikao cha Siri kunijadili bila kunitaarifu,”alisema Mtawale alipohojiwa na kuonekana anafanya kazi zake kwa kuongozwa na Kigogo mmoja wa Kata anayempotosha.

Alipoulizwa kwa nini Serikali yake haikuwaarifu wananchi juu ya kuuzwa kwa Mlima huo hadi wakapatana Mwekezaji akipata anachochimba Mwekezaji atachukua asilimia 60% na Kijiji asilimia 40% alisema, kwa kuwa vikao vinakaa mara tatu kwa mwaka ilikuwa wawaarifu Machi, 2013.

Pamoja na kukiri kuingia mkataba huo mwezi Desemba 2012 alikubali walifanya makosa ya kutowaarifu wananchi na Uonozi wa Kata, lakini akasema Katibu Tarafa Joyce Malare ametumwa kutatua mgogoro huo lakini walishindwa kukaa hadi 21.1.2013 kutokana na koramu (akidi) kutokutimia.

Diwani Abdalah alipoulizwa alikiri kuwepo kwa Mgogoro huo na kusema yeye ametoa Taarifa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ambaye amesema analifanyia Kazi, lakini alishangaa Katibu Tarafa kuanza kumuingilia akifanya Kazi za Kisiasa ili kumgonganisha na Wananchi Jambo alilosema hawezi kuvumilia na kukubali wananchi wadhulumiwe haki yao.

Aidha Katibu Tarafa Malare alipoulizwa na mwandishi amefikia wapi katika utatuzi wa mgogoro huo, hakuonesha ushirikiano na kuanza kumponda Mwandishi, “…nani kakwambia umbeya huo? ...Kwa utaratibu nikifanya kazi nampelekea mkubwa wagu siyo wewe!!”

Alimwagika maneno yasiyo na staha bila kujua Mwandishi alimhoji Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Lephy Benjamini juu ya mgogoro na kujibiwa anaushughulikia Malare.



HUYU NDIO AFISA MTENDAJI MKUU MPYA WA TTCL


 Picture
Bodi ya Wakurugenzi ya TTCL imemteua Dkt. Kamugisha Kazaura kuwa Ofisa mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo.

Dkt. Kazaura amechukua nafasi ya aliyekuwa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu Bw. Said Amir Said ambaye amestaafu hivi karibuni kwa mujibu wa sheria. Kabla ya uteuzi huo Dkt. Kazaura alikuwa ni Afisa mkuu wa ufundi (CTO)wa TTCL.

Bodi ya wakurugenzi ya TTCL imewaomba wafanyakazi na menejimenti kumpa afisa Mtendaji mkuu mpya ushirikiano wa kutosha ili kuwa na mshikamamo wa pamoja ili kuleta ufanisi katika utendaji wa kazi.

Kwa kusisitiza Bodi imesema, “Tufanye kazi na tusonge mbele pamoja, kama timu ililyoshikamana pamoja na iliyodhamiria kuinua utawala bora.”

Dkt. Kamugisha Kazaura alitunukiwa shahada ya Uzamili (Masters) na Uzamivu (PhD)katika fani ya Habari na mawasiliano ya simu katika chuo kikuu cha Waseda kilichopo Tokyo, Japan.


KIPANYA: BUNGE LISIPORUSHWA LIVE



OLD BAGAMOYO ROAD KUITWA MWAI KIBAKI ROAD KUANZIA KESHO

Hapa ni Msasani Kwa Warioba katika barabara ya Old Bagamoyo Road ambayo kuanzia kesho itaitwa Barabara ya Mwai Kibaki Road kwa heshima aliyotunukiwa kiongozi huyo wa Kenya na Hlmashauri ya Wilaya ya Kinondoni kufuatia ziara yake ya kitaifa ya siku mbili itayoanza kesho jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadik, barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 10.1 ni kuaniza kwenye mataa ya Moroccco karibu na makao makuu ya Airtel hadi mzunguko wa kuelekea Africana kule Mbezi Beach, mkabara na uwanja wa kulenga shabaha wa JWTZ.

Akiongea usiku huu, Mkuu huyo wa Mkoa amesema Rais Kibaki anatarajiwa kuwasili kesho saa 9 alasiri na kupkewa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete, ambapo usiku atamwandalia dhifa ya kitaifa Ikulu.  Keshokutwa. Alhamisi, Rais Kibaki ataongea na wazee wa Dar es salaam katika ukumbi wa PTA ulioko viwanja vya SabaSaba barabara ya Kilwa Road. Pia atatembelea sehemu mbalimbali atazopangiwa katika ziara yake hiyo ambayo pia ataitumia kuwaaga Watanzania kwani muhula wake wa uongozi utafikia kikomo baadaye mwaka huu.


HII NDIO HISTORIA YA CLOUDS ILIPOTOKEA NA ILIPO SASA




JERRY MURO KUENDELEA KUWA HURU

UPANDE wa Mashitaka katika rufaa ya kupinga kuachiwa huru kwa Aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji (TBC) Jerry Murro aliyekuwa anakabiliwa na mashitaka ya kuomba rushwa ya Sh milioni 10 umeiomba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es salaam kuamuru kesi hiyo isikilizwe upya.


Mawakili wa wa Serikali walidai hayo jana mbele ya Jaji Fauz Twaib kwa kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilikosea kisheria katika kuweka kumbukumbu ya Mwenendo wa
kesi hiyo jambo lililosababisha kutoa uamuzi usio wa haki.

Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk Eliezer Feleshi alikata rufaa kupinga hukumu iliyotolewa Novemba 30 mwaka juzi na Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Frank Moshi, ambayo ilimuachilia huru Murro, Deogratius Mgasa na Edmund Kapama waliokuwa wanakabiliwa na mashitaka hayo.

Katika rufaa hiyo, Wakili wa Serikali Awamu Mbagwa alidai kuwa mahakama haikuandika vizuri kumbukumbu za ushahidi na vielelezo  katika Mwenendo wa kesi ambapo kuna baadhi ya
ushahidi haueleweki unamaanisha nini jambo lililosababisha Hakimu kufikia uamuzi usio wa haki.

Aidha alidai kuwa kuna baadhi ya vielelezo na ushahidi haupo kwenye mwenendo wa kesi,  ikiwemo maelezo ya onyo yaliyotolewa na Murro katika kituo cha polisi na kitabu cha wageni waliofika katika hoteli ya Sea Cliff ambayo wajibu rufaa wanadaiwa kuomba rushwa.

Aliieleza mahakama kuwa, kitabu cha wageni kilikataliwa kupokelewa mahakamani kama kielelezo lakini katika Mwenendo wa kesi haijaandikwa na hata uamuzi wa pingamizi la kielelezo hicho haukutolewa na kudai kuwa kukosekana kwa uamuzi huo kumesababisha Hakimu kutofikia uamuzi wa haki.

Aidha katika mwenendo wa kesi hakuna kumbukumbu za wao kuwasilisha Mkanda wa kamera inayonasa matukio (CCTV) ulioonesha wajibu rufaa walipokwenda kufanya
makubaliano ya kupokea rushwa, lakini walishindwa kuuangalia na  baadaye wakaamua kutumia picha za kawaida.

Aliongeza kuwa kesi hiyo awali ilikuwa inasilizwa na Hakimu Gabriel Mirunde lakini Hakimu Frank Moshi ndiye aliyetoa hukumu hivyo kutokana na kuandikwa vibaya kwa mwenendo wa kesi hiyo Hakimu Moshi alishindwa kuelewa ushahidi na utoa uamuzi usio wa haki.

Akijibu hoja wakili wa Murro, Richard Rweyongeza aliiomba mahakama kutupilia mbali hoja hiyo kwa uwa haina  misingi kisheria pia wakata rufaa hawajaeleza ni vipi kukosewa kwa mwenendo wa kesi hiyo kumesababisha kufikia uamuzi usi sahihi.

Naye Wakili wa wajibu rufaa wengine, Majura Magafu alidai kuwa wakata rufaa hawajalalamika kuhusu hukumu iliyotolewa bali maandishi katika mwenendo wa kesi  na katika hukumu hiyo hakuna sehemu ambayo Hakimu alilalamika kuwa alipata shida kusoma mwenendo wa kesi hiyo.

Alidai endapo mahakama itamua kesi hiyo isikilizwe upya itakuwa ni sawa na kufanyabiashara ya kuchagua mahakimu kuwa kama wameshindwa kwa hakimu huyo wajaribu kwa mwingine jambo ambalo haliruhusiwi kisheria.

Warufani walikuwa na sababu nne lakini imesikilizwa sababu moja ambapo baada ya kusikiliza hoja hizo Jaji Twaib aliahirisha shauri hilo hadi Aprili 29 mwaka huu atakapotoa uamuzi.

Washitakiwa wanadaiwa kuwa waliomba rushwa kutoka kwa aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Michael Wage kwa lengo la kuzuia kutangazwa kwenye
televisheni habari za tuhuma za ubadhirifu wa fedha za umma akiwa mhasibu wa halmashauri hiyo.

Katika madai hayo, Muro na wenzake wanadaiwa Januari 28 mwaka jana jijini Dar es Salaam, walikula njama ya kutenda kosa hilo na Januari 29 mwaka jana katika Hoteli ya
Sea Cliff Dar es Salaam waliomba rushwa ya Sh milioni 10 kutoka kwa Wage.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU