Facebook Comments Box

Sunday, February 10, 2013

CHADEMA WAFUKUZA WENGINE MOROGORO


Ndugu Amani Mwaipaja


Chama cha Demokrasia na maendeleo chadema mkoa wa morogoro kimemfukuza uanachama aliyekuwa mgombea Ubunge wa jimbo la morogoro mjini na mwanasheria wa chama hicho mkoa wa morogoro Amani Mwaipaja  wakimtuhuni kutumika kukivuruga chama hicho wakati huu wa vuguvugu la Kuimarisha  vyama vya siasa kuelekea uchaguzi wa viongozi wa serikaliza mitaa na vijiji mwaka 2014 na uchaguzi mkuu wa Rais Wabunge na Madiwani mwaka 2015.

CHANJO YA UKIMWI YAPATIKANA NCHINI


 


JOPO la Madaktari wa Chuo wa Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), limekamilisha utafiti wa chanjo mpya ya virusi vya Ukimwi, ambao umethibitisha kuwa chanjo ya DNA -MVA ilikuwa salama na yenye uwezo wa kufanya mwili utengeneze kinga dhidi ya virusi vya Ukimwi (VVU).
Utafiti huo ulifanyika nchini kati ya mwaka 2007-2010 na 2008-2012.
Utafiti wa awali uliofanyika kati ya mwaka 2007 hadi 2010, ambao ulijulikana kama HIVIS-03, ulihusisha askari 60 polisi na magereza wa jijini Dar es Salaam, ambao walipewa chanjo hiyo na baadaye kuachwa wakiishi maisha yao ya kawaida kwa muda wa miaka mitano.
Akizungumza na Mwananchi Jumapili, Profesa Muhammad Bakari, aliyeongoza jopo la madaktari waliofanya utafiti huo alisema kuwa umezaa matunda na kuthibitisha kwamba chanjo ya DNA –MVA waliyopewa askari hao, ilikuwa salama na yenye uwezo wa kufanya mwili utengeneze kinga dhidi ya virusi vya Ukimwi (VVU).
“Chanjo hiyo inaweza kutengeneza vichocheo vya kinga dhidi ya VVU kwa asilimia 100 kwa washiriki waliopatiwa chanjo zote tano. Haya ni matokeo mazuri sana kupita hata matarajio watafiti, pia ni ya muhimu katika harakati za kutafuta chanjo dhidi ya VVU,” alisema.
Profesa Bakari, ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mafunzo wa MUHAS, alisema kwamba hakuna mshiriki aliyekufa, wala kupata athari za moja kwa moja kwa na kupatiwa chanjo kutokana na tafiti hizo.
Alisema kuwa askari walioshiriki utafiti huo walifanya hivyo kwa hiari yao hadi kukamilisha utafiti huo.
Alibainisha kwamba jopo la madaktari bado liliendelea na utafiti zaidi, ulioanza mwaka 2008 hadi 2012, ili kupata chanjo sahihi ya VVU kwa aina ya pili ya chanjo ijulikanayo kama TAMOVAC-01(Tanzania and Mozambique HIV Vaccine Program), iliyohusisha pia nchi ya Msumbiji.
“Hatukuishi hapo, utafiti wa pili (TAMOVAC-01), ulifanyika kati ya mwaka 2008 na mwaka 2012. Utafiti huu ulijumuisha pia nchi ya Msumbiji.
Profesa Bakari alisema kuwa utafiti nchini Tanzania ulihusisha washiriki 120, kati yao 60 wakiwa ni kutoka jijini Dar es Salaam.
Alibainisha kwamba kwa mara nyingine washiriki hao walitoka katika Jeshi la Polisi, Magereza na raia wa kawaida, huku wengine 60 wakiwa raia wa kawaida kutoka jijini Mbeya.
Mtaalamu huyo alieleza kwamba utafiti huo pia ulionyesha kuwa mchanganyiko wa chanjo ya DNA-MVA ulikuwa salama.


MAANDAMANO YA CHADEMA YAPIGWA MARUFUKU

CHADEMA imesema imelazimika kuratibu maandamano na mkutano wa hadhara kama ishara ya kuwapokea wabunge wa upinzani kwa madai ya kuwashitakia Wananchi kitendo cha Bunge kuondoa kwa hoja zao binafsi.

Moja ya h oja hizo ni hoja binafsi ya Mnyika iliyokuwa ikipendekeza Bunge lijadili na kupitisha maazimio ya hatua za haraka za kuboresha upatikanaji wa maji safi na ushughulikiaji wa maji taka katika jiji la Dar es Salaam, hoja ambayo ilitupiliwa mbali na kuzua mtafaruku bungeni.

Hoja nyingine ni ya Mbunge wa Kuteuliwa na Rais, ambaye pia ni mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia aliyoitoa bungeni juu ya udhaifu wa mitaala ya elimu nchini.

Jeshi la Polisi nchini kupitia Kamanda wa Polisi wa mkoa Kipolisi wa Temeke, Engelbert Kiondo amesema ni marufuku kwa CHADEMA kuandamana kama walivyokusudia ila, ni ruhusa kufanya mkutano.

Amesema sababu za kuzuia maandamano hayo ni kutokana na usumbufu utakaojitokeza katika maeneo ambayo maandamano hayo yamepangwa kupitia ikiwa ni pamoja na kuingilia na pengine kuzuia shughuli za kawaida za maeneo hayo, matumizi ya barabara na pengine kuchangia vitendo vya uharibifu wa mali na uvunjifu wa amani. Hivyo akasema alikwishakuwasiliana na viongozi wa CHADEMA wa Temeke kuhusu suala hilo na kuwataarifu kuwa maandamano yoyote yatakayofanyika yatakuwa ni kinyume na sheria na hivyo itawalazimu Polisi kuchukua hatua za kisheria pale inapobidi.

Naye Kamanda wa CHADEMA anayeratibu maandamano hayo, Benson Kigaila alisema maandalizi ya maandamano hayo yanaendelea kama yalivyopangwa kutokana na kuwa hajapokea ujumbe wowote kutoka Jeshi la Polisi kama walivyoahidi kumpigia simu kwa maelezo zaidi.

Maandamano hayo yamepangwa kufanyika kuanzia TAZARA na kuhitimishwa kwa mkutano wa hadhara wilayani Temeke.

Benson alisema mkutano huo ni mwanzo wa mfululizo wa mikutano itakayofanyika kwenye kanda 10 zilizotengwa na CHADEMA, kuanzia mwenzi huu.



ZITTO KABWE ALALAMIKIA MH SPIKA KUVUNJA KAMATI YAKE

.
Katika mkutano wa Kumi wa Bunge la Kumi la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Spika wa Bunge ndugu Anna Makinda alitangaza mabadiliko kadhaa ya muundo wa Bunge katika Kamati mbalimbali za Bunge. Moja ya maamuzi ya Spika yalikuwa ni kufutwa kwa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma ambayo inajulikana kifupi kama POAC.
Maamuzi haya yameleta sintofahamu kwa wananchi wengi na wafuatiliaji wa masuala ya Bunge na Uwajibikaji katika nchi yetu. Ni muhimu tufahamu uundwaji wa POAC ulitokana na misingi gani na kwamba Uamuzi wa Spika unarudisha nyuma maendeleo makubwa ya kujenga Bunge imara na lenye meno. Maamuzi ya Spika ni kinyume cha kanuni za Bunge, sheria ya Ukaguzi na Katiba ya nchi. Maamuzi ya Spika yanavuruga Bunge,ni ya hovyo na yanapaswa kupingwa na kila mdau wa Uwajibikaji nchini.
Baada ya Tanzania kuingia kwenye zoezi la Ubinafsishaji, mashirika mengi ya Umma yaliuzwa na mengine kufa kabisa. Wakati huo kulikuwa na chombo kinaitwa SCOPO (Standing Committee on Parastatal Organisations) kwa madhumuni ya kusimamia uendeshaji wa Mashirika ya Umma. Bunge lilikuwa na Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma na kamati hiyo ilifutwa mwaka 1997 kufuatia hatua za ubanifsishaji na ukweli kwamba Mashirika ya Umma hayatakuwapo na hivyo hapakuwa na haja ya kuwapo kwa kamati hiyo. Mwenyekiti wa mwisho wa Kamati hiyo alikuwa ni Mzee William Shellukindo wakati huo akiwa Mbunge wa Jimbo la Bumbuli wilayani Lushoto mkoani Tanga.
Mwaka 2007, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali alifanya mkutano wa Uwajibikaji na kueleza Taifa kuwa kimsingi Mashirika ya Umma bado yapo na mahesabu yao, kwa kuwa hayaangaliwi, ni mabaya sana nafedha za umma zinapotea. Pia alieleza kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 143(5) inamtaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kutoa taarifa za Ukaguzi za Mashirika ya Umma (Public Authorities and Other Bodies). Hivyo aliomba Bunge liunde Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma ili liweze kupokea, kujadili na kutoa maelekezo kuhusu mahesabu ya Mashirika ya Umma na kusimamia ufanisi wa Mashirika ya Umma. Vile vile alishauri Kamati hiyo isimamie sera ya Ubinafsishaji wa Mashirika ya Umma. Spika wa Bunge wa wakati huo, kupitia Kamati aliyoiunda chini ya Job Ndugai (wajumbe wengine walikuwa dkt Willibrod Slaa, Beatrice Shelukindo, Hamad Rashid Mohammed na Nimrod Mkono) wakaunda Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma kwa mujibu wa Kanuni za Bunge za Mwaka 2007. Kamati ya POAC iliundwa rasmi mwaka 2008 mwezi Februari. Nilipewa dhamana ya kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Kamati hii. Sababu za kuanzishwa kwa kamati ya POAC bado zipo na kimsingi sababu hizo ni za maana sana sasa kuliko ilivyokuwa kabla.
Majukumu ya POAC yaliainishwa na sehemu ya tatu ya nyongeza ya nane ya Kanuni za Bunge toleo la mwaka 2007, kanuni ya 115 (13)(a-e). Majukumu hayo ni pamoja na kushughulikia mahesabu yaliyokaguliwa ya Mashirika ya Umma, kuainisha maeneo sugu ya matumizi mabaya ya fedha za Umma, kutathmini ufanisi wa Mashirika ya Umma na kufuatilia utekelezwaji wa sera ya ubinafsishaji wa mashirika ya Umma. Kuanzia mwaka 2008 Mdhibiti na Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali amekuwa akitoa taarifa za mahesabu ya mashirika kama Katiba ya nchi inavyomtaka na sheria ya ukaguzi ya mwaka 2008. Sheria hii imeitaja kamati ya POAC kama moja ya kamati zenye majukumu ya kuwasilisha Bungeni taarifa ya mwaka ya mahesabu ya Mashirika ya Umma.
Katika kipindi cha miaka mitano POAC imekuwa ikitekeleza majukumu yake kwa umahiri na kwa kweli kwa uwazi sana kuliko kamati nyingine zote za Bunge. Taarifa ya mwisho ya POAC katika Bunge iliyowasilishwa katika mkutano wa saba wa Bunge, mwezi Aprili mwaka 2012 ulipelekea kutolewa kwa hoja ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu ambayo ilisababisha mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri. Hatua hii ilikuwa ni hatua muhimu sana katika kuweka mizizi ya utamaduni wa uwajibikaji nchini kwetu. Wakati Kamati inajiandaa na Taarifa yake ya Mwaka 2012 kwenye Mkutano wa Kumi na Moja, Spika ameivunja. Ikumbukwe maagizo ya mwisho ya Kamati ya POAC yalikuwa ni kuzuia mifuko ya hifadhi ya jamii kutoa mikopo kwa Serikali bila ya kuwapo kwa mikataba. Hivi sasa Serikali imekopa zaidi ya shilingi 1.2 trilioni kutoka mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa ajili ya miradi mbalimbali, mikopo hiyo ya fedha za wafanyakazi haina mikataba yeyote na POAC iliona hatari ya fedha za wafanyakazi kupotea na kuleta madhara makubwa kwa wastaafu nchini.
Katika maelezo yake Spika amesema nchi nyingine duniani hazina kamati kama ya POAC. Nadhani waliomshauri Spika waliamua kumdanganya na yeye akadanganyika. Nchi zote za Afrika Mashariki zina Kamati ya kusimamia Mashirika ya Umma. Kenya inaitwa Public Investments Committee, Uganda inaitwa State Corporations Committee na hata nchi nyingine kama India ambazo zinafuata utamaduni wa kibunge kama wetu wanayo na wanaita Public undertakings Committee. Nchini Afrika Kusini sio tu kuna Kamati ya Mashirika ya Umma bali pia kuna Wizara inayosimamia Mashirika ya Umma (Ministry of Public Entreprises). Kimsingi Kamati ya POAC ilipaswa kuongezewa nguvu zaidi ili kufikia uwezekaji wa Serikali kwenye makampuni binafsi badala ya kuifuta. Uwezekaji wa Serikali kwenye makampuni kama BP, AirTel, Kilombero Sugar, SonGas nk hauna uangalizi wowote.
Uamuzi wa Spika wa Bunge kuifuta Kamati ya POAC ni uamuzi unaorudisha nyuma juhudi za nchi kujenga asasi za uwajibikaji, ni kinyume cha sheria ya ukaguzi wa umma inayotaja Kamati tatu za Bunge za kusimamia fedha za Umma na ni kinyume cha Katiba ya nchi. Spika wa Bunge anasema kazi za Kamati ya POAC zitafanywa na Kamati ya PAC; Tanzania ina jumla ya Mashirika ya Umma 258 yenye thamani ya shilingi trilioni 10.2 mpaka mwezi Juni mwaka 2012, hata kamati ya POAC ilikuwa haiwezi kushughulikia Mashirika yote ya Umma katika mwaka mmoja, PAC itawezaje kusimamia Wizara za Serikali, Mikoa na wakala za Serikali na wakati huo huo Mashirika ya Umma 258? Kwa vyovyote vile Taifa linarudi miaka ya kabla ya 2008 ambapo Mashirika ya Umma yalikuwa kichaka cha kuiba fedha za Umma. Hivi karibuni Kamati ya POAC iligundua mtindo wa Wizara za Serikali kupeleka fedha Serikali kwenye Mashirika na kutumia kifisadi ili kukwepa ukaguzi kwenye Wizara (Wizara ya Utalii ilipeleka zaidi ya shilingi 600 milioni Bodi ya Utalii mwaka 2010/2011). Ikumbukwe pia wizi wa EPA, MEREMETA na hata uuzaji holela wa baadhi ya mali za Serikali kupitia ubinafsishaji ulifanyika nyakati ambazo Bunge halina kamati inayosimamia Mashirika ya Umma.
Kwa vyovyote vile Spika wa Bunge amedhihirisha namna ambavyo anafanya maamuzi bila kuzingatia maslahi ya nchi wala kuzingatia historia ya uwajibikaji katika nchi. Namna mijadala ya Bunge inavyoendeshwa, namna anavyobeba ajenda za Serikali katika kujenga Bunge kibogoyo na namna anavyofanya maamuzi kwa kukurupuka, inahitaji hatua za kuokoa misingi ya uwajibikaji wa nchi. Ni lazima Spika wa Bunge adhibitiwe kwa kuondolewa katika nafasi hiyo haraka iwezekanavyo. Spika lazima ajue kwamba Mamlaka yapo kwa wananchi na yeye ni msimamizi tu wa vikao vya Baraza la wananchi liitwalo Bunge. Anna Makinda lazima adhibitiwe, vinginevyo nchi yetu itaumia.



KCMC STUDENTS RAISED 2.7 MILLION TO SPONSER 23 CHILDREN

This years education sponsoring campaign from Kilimanjaro Christian Medical University College (KCMUCo) students and Kilimanjaro Christian Medical Centre(KCMC) staffs raised a total of 2,755,000 Tshillings enabling us to sponsor 23 children at the msamaria center for street children .On behalf of SAL (Shine A Light) i would like to thank everyone who in one way or the other contributed in making this campaign a success.
 joining hands touching hearts

















 


Saturday, February 9, 2013

LIVE MATCH CENTRE:FULL TIME SIMBA SC 1 - 1 JKT OLJORO



Mpira umemalizika Simba 1-1 JKT Oljoro

Mpira unaweza isha muda wowote na matokeo bado 1kwa1.Zimeongezwa dk 2


Dk ya 42 kipindi cha pili simba wanapoteza nafasi ya kupata bao la ushindi


Dk 37 kipindi cha pili Jkt oljoro wanakosa goli la wazi.

Dk ya 28 kipindi cha pili, simba wanafanya mabadiliko Edward christopher anaingia na anatoka MudeJkt oljoro wanakosa goli la wazi na wanafanya mabadiliko kwa kumtoa Esau.

Ngasa ameingia kuchukua nafasi ya Rashid

Jkt wanasawazisha bao kufuatia uzembe wa beki ya simba.

JKT OLJORO wanakosa goli la wazi na wanafanya mabadiko ya mchezaji.

Mchezaji wa JKT anapewa kadi ya njano kwa kumkwatua Kazimoto.

Kipindi cha pili kimeanza hakuna mabadiliko yoyote.

Mashabiki wanaodhaniwa wa simba wanawashambulia watu waliovaa nguo zinazodhaniwa za CCM.

Dk 38 Oljoro wanalishambulia sana lango la Simba kwani wanaonyesha kuwakamata vilivyo

Hadi dk ya 34 simba wanaongoza goli moja lililofungwa na Kazimoto kwa shuti kali umbali wa mita 30

Paul Ngalema ameumia vibaya na kutolewa uwanjani ameshindwa kuendelea na mchezo

Dk ya 29 JKT OLJORO wanakosa goli la wazi ktk shambulizi baada ya mpira kumtoka mikononi na JKT wakazubaa.

Kikosi cha Simba kinachoanza leo dhidi ya JKT Oljoro


KASEJA, CHOLLO, NGALEMA, KAPOMBE, KEITA, JONAS, KIEMBA, MUDDE, RASHID ISMAIL, KAZIMOTO na Haruni CHANONGO.


TAARIFA YA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA CCM



Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi itafanya Mkutano wake wa kawaida kuanzia tarehe 10 -11 /02/2013. Kikao hicho kitaongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.   
Wajumbe wa NEC wanatarajiwa kufika Mjini Dodoma leo tarehe 9/02/2013,kwa ajili ya kikao hicho.   
Pamoja na mambo mengine kikao hichi kitatanguliwa na Semina ya siku mbili kwa Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa.   
 Lengo la Semina hii ni kuwaongezea Wajumbe uelewa kuhusu masuala ya Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake hasa ikizingatiwa kwamba wengi wa Wajumbe ni wapya kufuatia Uchaguzi Mkuu wa CCM wa mwaka 2012.   
Mada zitakazowasilishwa kwenye Semina ni pamoja na;
 
1. Nafasi na Wajibu wa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa

2. Umuhimu wa Maadili kwa Viongozi na Watendaji wa Chama Cha Mapinduzi.

3. Mikakati ya kutekeleza maazimio ya Mkutano Mkuu wa Taifa wa nane wa CCM.

4. Mkakati wa kukuza ajira nchini.
 
Semina hii itafuatiwa na Mkutano rasmi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ambao pamoja na mambo mengine utafanya Uchaguzi wa Wajumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi.

Imetolewa:​

Nape Moses Nnauye

KATIBU WA NEC – ITIKADI NA UENEZI

CHAMA CHA MAPINDUZI



AJALI MBAYA KIBAMBA DARAJANI







 Mwili wa Marehemu Dereva kwa Mbele ukiwa Umekandamizwa na Lori lililo beba Mbao izo
 Huu ni Mguu wa Dereva ambaye amekandamizwa na Gari hilo



 Hivi Ndivyo Gari hili lililo beba Mbao limeanguka

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE YANAPATIKANA KWENYE TOVUTI HIZI





Baraza la mitahani la taifa leo limetoa tovuti rasmi kwa ajili ya kuangalizia matokeo pindi yatakavyo tangazwa. Tovuti hizo ni www.necta.go.tz na www.matokeo.necta.go.tz. vilevile wamesema kwamba tovuti ya wizara ya elimu www.moe.go.tz haitatumika kwasasa kwasababu haipo hewani.


WABUNGE WATAKAO KATAA KUHOJIWA NA KAMATI WATAKAMATWA NA POLISI

Bunge limesema wabunge watakaokataa kuhojiwa na Kamati ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge, watakamatwa na polisi na  kufikisha kwenye kikao cha kamati hiyo.

Juiz, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia  na Maendeleo (CHADEMA), Dk Wilbroad Slaa aliwakataza wabunge wake kuitika wito wa kuhojiwa na kamati hiyo hadi Spika atakapojibu  baadhi ya madai ya chama hicho.

Akizungumza na NIPASHE jana, Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge, John Joel, alisema  mbunge anayehitajika kuhojiwa na kamati hiyo hupelekewa barua ya kuitwa na endapo akikataa kufika atakamatwa na  polisi.
“Mbona jambo hili lipo wazi kwa kila mbunge kwa kuwa sheria zinajieleza kuwa ukikataa wito utafuatwa na askari ambaye atakuleta kwa lazima katika kamati hii.
Dk Slaa alikataa wabunge kuhojiwa baada ya  Spika wa Bunge, Anne Makinda, kuitaka  Kamati ya Maadili  kuchunguza vurugu zilizojitokeza  wiki wakati wabunge walipokuwa wakijadili hoja binafsi ya Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), iliyohusu upatikanaji wa majisafi na uondoshaji wa majitaka  Dar es Salaam.


HERI YA KUZALIWA MDAU

Kitongoni inachukua fursa hii adhim kumtakia heri ya kuzaliwa mmoja wa wadau wake ndugu Hassan Bilal Kabange ( Abu Khayrat Hassan Kabange)

 





 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU