Picha zifuatazo zinaonesha baadhi ya Taswira za Wilaya mpya ya BUHIGWE, Mkoani Kigoma kama zinavyoonekana hapa chini.
Friday, February 1, 2013
HUU NI MUONEKANO WA MJI WA KIGOMA NA ZIWA TANGANYIKA.
Huu ndiyo muonekano wa Mji wa Kigoma sambamba na Ziwa Tanganyika, na Ghorofa linaloonekana ni la Shirika la Nyumba ambalo linataraji kuzinduliwa rasmi hivi karibuni na Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
PUNGUZO LA GHARAMA ZA KUPIGA SIMU KUANZA KUTUMIKA MWEZI MACHI 2013.
Mamlaka
ya mawasiliano Tanzania TCRA imeyataka makampuni ya simu za mkononi
Tanzania kuhakikisha yanaanza rasmi mpango wa punguzo la bei ya kupiga
simu katika mitandao mingine kutoka bei inayotumika sasa hivi ya
shilingi 113 kwa dakika mpaka shilingi 34 na senti 92 ikiwa ni bei mpya
inayotakiwa kuanza kutumika kuanzia siku ya kwanza ya mwezi March 2013.
Mkurugenzi
Mtendaji wa TCRA Profesa John Nkoma amesema uamuzi wa kufanya hivyo ni
kutokana na kupanda kwa gharama za maisha ambapo makampuni hayo
yanatakiwa kuanza utekelezaji wa agizo hilo na hatua za kisheria
zitachukuliwa kwa kampuni yeyote ambayo itafanya kinyume na hayo
maagizo.
Namkariri
akisema “bei itaendelea kushuka kadri miaka inavyokwenda, tarehe 1
january 2014 bei itatakiwa kuwa sh 32 na senti 40, tarehe 1 january 2015 sh
30 na senti 58, tarehe 1 january 2016 itatakiwa kuwa sh 28 na senti 57,
hizi bei ni za juu kabisa na Kampuni za simu ni ruksa kwao kuzungumza
na wakatumia bei ya chini kabisa”
TUNDA LA STAFELI LAGUNDULIKA KUTIBU SARATANI
Tunda aina la Stafeli.
TUNDA
la stafeli linatibu magonjwa kadhaa, ikiwamo saratani kwa ubora wa
karibu mara 10,000 ya matibabu ya kawaida yanayopatikana kwenye vituo
vya afya, utafiti umebaini.Utafiti
huo uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Dawa cha Purdue nchini Marekani,
umeeleza kuwa mbali na kutibu saratani, tunda hilo pia ni tiba ya
matatizo ya msongo na mfadhaiko.
“Maajabu
ya stafeli ni kwamba lina uwezo wa kuangamiza chembehai zenye saratani
pasipo kusababisha madhara katika mwili kama zinavyofanya dawa nyingine
za ugonjwa huo au mionzi,” imesema sehemu ya utafiti huo uliochapishwa
kwa mara ya kwanza katika Jarida la Kemia na Madawa la nchini Marekani,
mwaka 2010.
Taasisi ya utafiti wa Saratani ya Nchini Uingereza(NIR) ilifanya utafiti wa kwanza kuhusu maajabu ya stafeli mwaka 1976. Katika
utafiti huo ilibainika kuwa majani, mizizi na tunda la stafeli, vina
uwezo wa kutibu saratani, lakini matokeo ya utafiti huo hayakutangazwa
kwa umma kwa hofu ya kuua viwanda vya dawa za saratani.
Inaelezwa
kuwa kirutubisho kilichopo katika stafeli kinatumia jina la kibiashara
la ‘Triamazon’ na kimepigwa marufuku kutumika nchini Uingereza na
Marekani kutokana na uwezo wake mkubwa wa kitiba.Utafiti
mwingine uliofanywa na Chuo Kikuu cha Kikatoliki nchini Korea na
kuchapishwa katika jarida la Bidhaa Asilia ulibaini kuwa stafeli lina
uwezo wa kuponya saratani ya tumbo.
Utafiti
wa chuo hicho ulienda mbali na kusema kuwa tunda hilo linaweza kulenga
seli za saratani tu, bila kushambulia seli muhimu za mwili kama ambavyo
tiba ya mionzi ifanyavyo.
Tunda la
Stafeli lina kirutubisho muhimu kiitwacho Annona Muricata, ambacho
ndicho chenye uwezo wa kupigana na maradhi ya saratani. Imeelezwa kuwa stafeli lina uwezo wa kutibu aina 12 za saratani ikiwemo ya matiti, kongosho, mapafu na ya kibofu cha mkojo.
Pamoja na
kutibu saratani, kirutubisho hicho kilichopo katika tunda hilo pia
huweza kutibu vimelea, shinikizo la damu, msongo wa mawazo, matatizo ya
mfumo wa fahamu na sukari.Utafiti
huo unaonyesha kuwa kirutubisho kimegwacho katika tunda hilo kinaweza
kwa asilimia kubwa kupambana na saratani bila kumuacha mgonjwa na
madhara kama kusikia kichefuchefu, kutapika, kupungua uzito na
kunyonyoka nywele.
Thursday, January 31, 2013
WANAFUNZI WAPATAO 1580 KUNUFAIKA NA MPANGO WA UFUNDISHWAJI WA LUGHA YA KINGEREZA KWA NJIA YA TEKNOLOJIA
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa,Addo Mapund akitiliana saini na Bi Anne Devilliers,Mratibu wa Mradi wa mpango wa ufundishwaji wa Lugha ya Kingereza kwa njia ya teknorojia ya kisasa (Techonoroji Enhanced Edcation) TEE-TZ chini ya ufadhili wa kampuni ya Pan African Energy,inayojishughulisha na kazi ya uchimbaji,usambazaji na uuzaji wa gesi asilia ya Songosongo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa,Addo Mapunda akibadilishana hati na Bi Anne Devilliers,Mratibu wa Mradi wa mpango wa ufundishwaji wa Lugha ya Kingereza kwa njia ya teknorojia ya kisasa (Techonoroji Enhanced Edcation) TEE-TZ chini ya ufadhili wa kampuni ya Pan African Energy,inayojishughulisha na kazi ya uchimbaji,usambazaji na uuzaji wa gesi asilia ya Songosongo.
Mkuu wa Wilaya ya Kilwa,Abdallah Ulega akizungumza machache mara baada ya kushuhudia utiaji saini wa mkataba huo wa miaka mitatu.
WANAFUNZI wapatao 1,580 wanaosoma Shule tisa za Sekondari,wilayani Kilwa, mkoani Lindi,watanufaika na mpango wa ufundishwaji wa Lugha ya Kingereza kwa njia ya teknolojia ya kisasa TEE-TZ chini ya ufadhili wa kampuni ya Pan African Energy,inayojishughulisha na kazi ya
uchimbaji,usambazaji na uuzaji wa gesi asilia ya Songosongo. Mradi huo wa miaka mitatu,utagharimu jumla ya Sh, ya Sh,144,945,218/-zitakazotumika kujenga misingi bora ya Lugha ya kingereza kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza kuanzia mwaka 2013. Hayo yameelezwa na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya hiyo, Addo Mapunda,alipokuwa akitoa taarifa katika hafla fupi ya kutiliana na saini ya utekelezaji wa mpango huo.
Mapunda alisema mpango huo,utakaochukuwa takribani muda wa kipindi cha miaka mitatu,umeanza rasmi mwezi huu kwa wanafunzi wapatao 1,580 wa kidato cha kwanza kutoka Shule tisa za Sekondari zilizopo katika wilaya hiyo. Amezitaja Sekondari zitakazonufaika na mpango huo kuwa ni,Kilwa day iliyopo mji mdogo wa masoko, Mtanga, Songosongo, Mbuyuni, Kinjumbi,Miteja,Mingumbi,Kikanda na Sekondari ya wasichana ya Ilulu. Mkurugenzi Mapunda alisema mafunzo hayo kwa kuanzia yatakuwa ni ya wiki sita,yameanza rasmi hivi karibuni na kwamba walimu wapatao 30 wakiwemo (12) wa kigeni (Volunteers) wakiwemo na walimu wazawa (18). “Hizi Shule tisa kila moja italazimika kutoa walimu wawiliwatakaopatiwa mafunzo kwa ajili ya kuendesha mpango huu katika Shule zote hizo”Alisema Mapunda. Aidha, Mapunda alisema kupitia ufadhili wa mpango huo wa mafunzo ya kingereza,Halmashauri ya wilaya itaendesha semina/warsha kutoa stadi za kufundishia masomo hayo kwa Sekondari hizo tisa zenye walimu wapatao (71).
Mapunda alisema mafunzo hayo ni nyongeza kwa walimu wote waliopo katika Shule hizo tisa za mafunzo ya kingereza ya aina mbili,TEE-TZ itakayoendeshwa kwa ufadhili wa ubalozi wa Marekani,(RELO-Regional
English Language Office kwa Sh,24,158,480/-.Katika ufadhili wa mafunzo hayo ya TEE-TZ na RELO jumla ya Sh,169,103,698/-ndizo zitakazotumika kwa ajili ya utekelezaji wake. Mratibu wa mradi huo,kutoka kampuni hiyo ya Pan African Energy,Anne Devilliers,amesema lengo la mpango huo ni,kutaka kuwawezesha wanafunzi waelewe masomo yao kwa elimu ya Sekondari na kuongeza viwango vya
ufaulu katika mitihani yao ya kidato cha nne.Devilliers akasema imebainika kwamba wapo wanafunzi waliowengi wamekuwa hawafanyi vizuri katika masomo na mitihani yao,kutokana nakutoielewa vyema Lugha ya Kingereza. Mkuu wa wilaya hiyo ya Kilwa, Abdallah Ulega, ameipongeza kampuni ya
Pan African Energy,na akasema kwamba kwa kiasi furani itasaidiakuboresha kiwango cha elimu ndani ya wilaya hiyo,mkoa na Taifa kwa ujumla. Mpango huo,ulianza kwa majaribio katika wilaya ya Mafia mkoani
Pwani,mwaka 2010 na 2011,baada ya kuona mafanikio yake,ndipo uongoziwa wilaya ya Kilwa,ukaamua mpango huo kupelekwa ndani ya wilaya yao.
DKT. ASHA ROSE MIGIRO AWAASA WANANCHI WA BUHIGWE KUWA NA MSHIKAMANO
Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Nyangamba iliopo kwenye Kijiji cha Janda,Wilayani Buhigwe,Kigoma wakati alipoitembelea shule hiyo na kuangalia maendeleo ya Wanafunzi wa shule hiyo,alipokuwa kwenye ziara ya kukutana na wananchi wa Wilaya hiyo jana.
Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Muhinda kilichopo kwenye Wilaya Mpya ya Buhigwe,Mkoani Kigoma wakati akiendelea na Ziara yake ya kutembelea Kata zote zilizopo wilayani humo.Dkt. Asha-Rose Migiro amewataka wananchi wa kijiji hicho kuwa na mshikamano ili kuweja kunyanyua maendeleo ya kijiji na wilaya kwa ujumla.
Katibu wa NEC,Siasa na Uhusiano wa Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro akipokelewa kwa shangwe na wananchi wa kijiji cha Viongozi mbali mbali wa CCM katika Kijiji cha Mnanila,Wilayani Buhigwe.
Viongozi wa kijiji wakitambulishwa.
KOCHA KIM POULSEN ATEUA WACHEZAJI 21 WA KUIVAA CAMEROON
KOCHA WA STARZ KIM POULSEN
Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametaja kikosi cha wachezaji 21 kitakachoingia kambini Jumapili (Februari 3 mwaka huu) kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Cameroon (Indomitable Lions).
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Dar es Salaam leo (Januari 31 mwaka huu), Kim amesema mechi dhidi ya Cameroon itakuwa kipimo kizuri kwake kwa sababu ni sehemu ya maandalizi kabla ya kucheza mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Morocco itakayofanyika Machi mwaka huu.
“Itakuwa mechi ngumu na kipimo sahihi kwetu. Tuko tayari, tutacheza kwa staili yetu kwa sababu ni sehemu ya maandalizi kabla ya mechi dhidi ya Morocco. Ni mechi nzuri kwa sababu wachezaji wameonyesha wako tayari.
“Tumetoka kucheza dhidi ya Zambia na Ethiopia. Lengo ni Taifa Stars kucheza fainali za AFCON 2015, kwa hiyo mechi dhidi ya Cameroon ni sehemu ya mipango yetu kuhakikisha tunafika huko,” amesema Kim ambaye amerejea nchini juzi kutoka Afrika Kusini kuzifuatilia timu za Morocco na Ivory Coast zilizo kundi moja na Tanzania katika mechi za mchujo za Kombe la Dunia.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itacheza na Morocco, Machi 24 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Stars inashika nafasi ya pili katika kundi lake nyuma ya Ivory Coast inayoongoza. Timu nyingine katika kundi hilo ni Gambia.
Wachezaji aliowaita kwenye kikosi chake ni makipa Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ali (Azam) na Aishi Manula (Azam). Mabeki ni Erasto Nyoni (Azam), Nassoro Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Kelvin Yondani (Yanga), Shomari Kapombe (Simba) na Issa Rashid (Mtibwa Sugar).
Viungo ni Amri Kiemba (Simba), Simon Msuva (Yanga), Frank Domayo (Yanga), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Salum Abubakar (Azam), Khamis Mcha (Azam), Athuman Idd (Yanga) na Mwinyi Kazimoto (Simba). Washambuliaji ni Mrisho Ngasa (Simba), na Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).
Wednesday, January 30, 2013
KIWANDA CHA CHEMICOTEX KIMEWAKA MOTO
Kiwanda
cha ChemiCotex kilichopo huko Africana njia ya Tegeta jijini Dar es
Salaam kimeungua moto jioni ya leo tar 30/01/2013.
IGP MWEMA APATA AJALI MBAYA MOROGORO
IGP SAID MWEMA
Jinamizi
la ajali limeendelea kuwaandama viongozi wa juu serikali na vyama
baada ya juzi waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa kunusurika kifo katika
ajali iliyotokea eneo la Bwawani mkoani Morogoro ,Mkuu wa jeshi la
polisi nchini (IGP ) Said Mwema leo amenusurika kifo baada ya gari
lake alilokuwa akisafiria kupinduka.
Ajali
hiyo imetokea majira ya mchana katika eneo Mkundi Manispaa ya
Morogoro wakati kiongozi huyo akitokea jijini Dar es Salaam kwenda
mkoani Dodoma.
Hata
hivyo katika ajali hiyo hakuna madhara makubwa kwa binadamu zaidi ya
gari kuharibika kiasi na msafara wa IGP kuendelea na safari ya
Dodoma kwa kutumia usafiri mwingine .
Tuesday, January 29, 2013
MAFURIKO YALETA BALAA MORO JIONI YA LEO
Mvua
kubwa iliyonyesha morogoro jioni ya leo imesababisha mafuriko katika
mtaa wa morogoro.Mvua hiyo iliyoanza kunyesha kuanzia saa tisa alasiri
imenyesha takribani kwa masaaa mawili imesababisha mafuriko katika
barabara ya msamvu kuingia katikati ya mji hali iliyosababisha msongamano
mkubwa wa magari.
Maji yakiwa yamejaa eneo la mtawala baada ya mvua kubwa kunyesha jioni hii mkoani morogoro
Mafuriko
hayo yaliingia katika makazi ya watu na hapa ni mashine za kukoboa
mpunga wakiwa wamesimamisha kazi zao baada ya maji kuingia ndani.
VILIO VYATAWALA BAADA YA LULU KUACHIWA LEO KWA DHAMANA
Lulu
na mama yake mzazi wakilia baada ya kukutana nje ya Mahakama, Lulu
amechiwa huru na Mahakama leo january 29 2013 mchana, pembeni ni
mwigizaji Dr. Cheni ambae amekua karibu na familia ya Lulu kwa muda
mrefu sana.
Ama kwa hakika nnje ya mahaka pamegeuka kilio mara muigizaji elizabeth
michael kuachiwa kwa dhamana leo tarehe 29 lulu amepewa dhama kutokana
na kesi inayomkabili ya kumuuwa bila kukusudia aliyekuwa star wa bongo
movie marehemu steven kanumba.
Mara baada ya lulu kumuona mama yake wamejikuta wakiangua kilio hadi
watu wakaribu wakawa wanashangaa.kazi ilikuwa kwa muigizaji dk cheni
ambaye kiukweli katika watu wakupongezwa katika hili anachukuwa nafasi
ya kwanza kwa binadamu ,cheni amekuwa mstari wa mbele kumsimamia lulu
hadi amepata dhamana.
| Lulu akiingia kwenye gari huku akisaidiwa na Dk cheni kwa nyuma yake |
Mama yake lulu aliwahi kukaririwa akisema kwa sasa anamuona cheni ni
zaidi ya binadamu wa kawaida kwani bila yeye hajui kama ataweza
kumuokowa mwanae mama huyo amejikuta akilia kwa furaha baada ya kumuona
tena mwanae huyo.
Dk chen amezungumza na thesuperstarstz na kutuambia anashukuru mungu
kwakumpa moyo wa ujasiri wa kumsaidia binti huyo kwani wengi walimsusa
lakini tukumbuke mungu ndiye mlipaji wa yote hatupaswi kumuhukumu mtu
kwani hata mahakama bado haijamuhukumu lulu sasa sikuona sababu ya
baadhi ya wasanii kujitenga na lulu na ndio maana nikajitolea kumsaidia
hadi nijue mwisho wake.
| Lulu akilia kwa furaha na kushindwa hata kuongea chochote alipokuwa anahojiwa jambo lililofanya cheni amuongelee |
Cheni ambaye ni mmoja kati ya wadhamini waliotoa milioni 20 za
kitanzania cheni amekuwa masaada mkubwa sana kwa lulu jambO ambalo
limefanya lulu kumuona cheni ni zaidi ya baba yake kwa sasa na ndio
maana mara nyingi hata kabla ya tukio la lulu na kanumba kutokea bado
lulu alikuwa anamuita cheni baba japo haikujulikana kwanini na cheni
katika familia ya kina lulu anaheshimika sana na ndio maana haikuwa
rahisi kwake kutojitolea kwa hilo.
Subscribe to:
Posts (Atom)





















