Taarifa rasmi kutoka kwenye klabu hiyo iliyotolewa muda mfupi uliopita inasema kwamba Guardiola atachukua majukumu yake ya kuwa manager mpya wa timu hiyo baada ya msimu wa 2012-2013 kuisha, na amesaini mkataba wa miaka mitatu wa kuifundisha timu hiyo inayoongoza ligi ya Bundesliga.
Wednesday, January 16, 2013
PEP GUARDIOLA KUWA KOCHA MPYA WA BAYERN MUNICH
Taarifa rasmi kutoka kwenye klabu hiyo iliyotolewa muda mfupi uliopita inasema kwamba Guardiola atachukua majukumu yake ya kuwa manager mpya wa timu hiyo baada ya msimu wa 2012-2013 kuisha, na amesaini mkataba wa miaka mitatu wa kuifundisha timu hiyo inayoongoza ligi ya Bundesliga.
NYUMBA YA KAPTENI WA NDEGE YA RAIS YABOMOLEWA
Nyumba iliyokuwa katika mtaa wa Ohio kitalu namba 15 inayoripotiwa kwua ilikuwa inamilikiwa na Kapteni Msataafu wa Ndege ya Rais, Bw. Felix Kileo imevunjwa chini ya usimamizi wa Kampuni ya udalali ya Rhino Auction Mart, kwa madai kuwa kampuni hiyo imepewa kazi hiyo ya kubomoa na tassisi ya Benki ya Wakulima, TIB.
Kwa mujibu wa maelezo ya wabomoaji hao, TIB wanataka kujenga jengo la orofa kwenye eneo hilo, baada ya nyumba hiyo kupewa na serikali na mtumishi wa serikali aliyekuwa anaishi kwenye nyumba hiyo kupewa nyumba nyingine.
Mtoa maelezo hayo amesema, mtumishi huyo wa Serikali alikaidi kutoka katika nyumba hiyo ndiyo maana kampuni hiyo ilipewa kazi ya kuingia kwa kuvamia nakuanza kuvunja.
Ndugu wakaribu wa Kapteni huyo ambae mwenyewe hakuwepo kwa muda huo eneo la tukio wamelalamikia kitendo anachofanyiwa ndugu yao.
“Huyu mimi ni nduguyangu amekuwa mtumishi wa serikali za awamu zote, amestaafu mwaka jana kama rubani wa ndege ya Rais lakini anachofanyiwa ni udhalilishaji, na vitendo hivi si vya kistaraabu hata kidogo. Ni ufisadi tu huu. Pesa zitatoa roho ya mtu!” alisikika akisema mmoja wa kaka wa Kapteni huyo.
Kwa mujibu wa ndugu hao kesi ya msingi iko mahakamani na kesho kutwa inasikilizwa lakini wameshangazwa kitendo cha kuwavamia bila hata barua ya mahakama ya kuvunja nyumba hiyo.
Baada ya kufunguliwa kesi, upande wa serikali ulishinda, lakini Kapteni huyo kupitia mawakili wake walikata rufaa iliyotaka zoezi la kuendeleza kiwanja hicho kusimama.
Kwa mujibu wa maelezo ya wabomoaji hao, TIB wanataka kujenga jengo la orofa kwenye eneo hilo, baada ya nyumba hiyo kupewa na serikali na mtumishi wa serikali aliyekuwa anaishi kwenye nyumba hiyo kupewa nyumba nyingine.
Mtoa maelezo hayo amesema, mtumishi huyo wa Serikali alikaidi kutoka katika nyumba hiyo ndiyo maana kampuni hiyo ilipewa kazi ya kuingia kwa kuvamia nakuanza kuvunja.
Ndugu wakaribu wa Kapteni huyo ambae mwenyewe hakuwepo kwa muda huo eneo la tukio wamelalamikia kitendo anachofanyiwa ndugu yao.
“Huyu mimi ni nduguyangu amekuwa mtumishi wa serikali za awamu zote, amestaafu mwaka jana kama rubani wa ndege ya Rais lakini anachofanyiwa ni udhalilishaji, na vitendo hivi si vya kistaraabu hata kidogo. Ni ufisadi tu huu. Pesa zitatoa roho ya mtu!” alisikika akisema mmoja wa kaka wa Kapteni huyo.
Kwa mujibu wa ndugu hao kesi ya msingi iko mahakamani na kesho kutwa inasikilizwa lakini wameshangazwa kitendo cha kuwavamia bila hata barua ya mahakama ya kuvunja nyumba hiyo.
Baada ya kufunguliwa kesi, upande wa serikali ulishinda, lakini Kapteni huyo kupitia mawakili wake walikata rufaa iliyotaka zoezi la kuendeleza kiwanja hicho kusimama.
Tuesday, January 15, 2013
SUNZU AUZWA READING KWA BILLION 7 - AENDA KUFANYA VIPIMO VYA AFYA
Sunzu ambaye anachezea klabu ya TP Mazembe ya DRC ambayo imeandika kwenye mtandao wake kwamba ada ya uhamisho ya $4.8million imeshakubaliwa na kilichobakia ni mchezaji kukamilisha vipimo vya afya.
Mfungaji huyo wa penati ya ushindi ya Zambia dhidi ya Ivory Coast katika AFCON 2012, anatarajia kurudi Afrika ya kusini January 19, siku mbili kabla ya mabingwa watetezi kuchuana na Ethiopia katika mechi ya ufunguzi.
HATIMAE SIMBA WAMUUZA OKWI

Kwa taarifa za ndani kutoka ndani ya klabu ya Simba ni kwamba timu hiyo imefikia maamuzi ya kumuuza mshambuliaji huyo kwenda Etoile du Sahel ya Tunisia kwa ada ya uhamisho itakayovunja rekodi ya uhamisho hapa nchini ya $300,000.
Mwenyekiti wa klabu hiyo ya Simba Mh. Aden Rage kwa sasa yupo nchini Tunisia akisimamia taratibu zote za uuzwaji wa Okwi ambaye alisaini mkataba mpya wa kuitumikia Simba hivi karibuni.
"Ni kweli Mwenyekiti yupo Tunisia akishughulikia uuzwaji wa Okwi kwa klabu ya Etoile du Sahel. Ada ya uhamisho ni dola laki tatu na muda mchache ujao dili litakamilika na Okwi atapewa ruhusa ya kuzungumza maslahi binafsi na klabu yake mpya." - kilisema chanzo cha habari kutoka ndani ya Simba.
Etoile du Sahel ni klabu mojawapo yenye mafanikio makubwa barani Afrika, ikiwa inashikilia rekodi ya kuwa klabu pekee barani afrika kushinda kila kombe linaloandaliwa na CAF.
Monday, January 14, 2013
POLISI YAKAMATA VIROBA 202 VYA MADAWA YA KULEVYA LEO
TENGA KUTOGOMBEA TENA UONGOZI TFF
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amesema hatagombea tena wadhifa huo katika uchaguzi uliopangwa kufanyika Februari 24 mwaka huu.
Akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye ofisi za TFF leo, Rais Tenga amesema wakati anaingia kwenye uongozi mwaka 2004 ajenda ilikuwa na kuijenga TFF kama taasisi kwa kuweka mifumo ya uendeshaji ikiwemo kutengeneza katiba na kanuni, jambo ambalo limefanyika.
“Wajumbe wamekuwa wakiniuliza Rais vipi? Mimi hapana. Nilishafika pale pa kufika. Tulipoanza wakati ule ilikuwa ni kujenga taasisi. Na kazi hiyo tumeifanya. Tulipoingia mwaka 2004 hiyo ndiyo ilikuwa ajenda,” amesema Rais Tenga.
Amesema walitengeneza Katiba, vyombo huru vya kufanya uamuzi, kuongeza wigo wa wapiga kura ambapo hivi sasa kwenye mpira wa miguu hakuwezi kutokea migogoro, hata ikitokea kuna mfumo wa kuidhibiti.
Rais Tenga ameishukuru Sekretarieti ya TFF, Kamati ya Uchaguzi ya TFF, kamati za uchaguzi za wanachama wa TFF na vyama wanachama wa TFF kwa hatua iliyofikiwa katika uchaguzi ambapo mikoa yote imekamilisha uchaguzi na kubaki vyama shiriki pekee.
Ametoa mwito kwa wadau kujitokeza kugombea uongozi TFF, kwani baada ya kujenga taasisi ajenda iliyobaki ni mpira wa miguu wenyewe ikiwemo nini kifanyika ili mpira uchezwe katika maeneo mbalimbali.
“Tumeshatengeza mfumo, sasa ni kuangalia jinsi ya kuendeleza mpira. Changamoto ni tufanye nini ili mpira uendelee. Tunataka watu wengine wabebe hiyo ajenda ili tuangalie tunakwendaje mbele,” amesema.
Pia amesema ushirikiano ambao amepata kwa wapenzi na wadau wa mpira wa miguu ni wa ajabu. Vilevile ameishukuru vyombo vya habari, Serikali, klabu, wadhamini na wafadhili kwa mchango wao katika uendeshaji wa mpira wa miguu nchini.
ANGALIA PICHA ZA MAANDAMANO YA WANAFUNZI WA IFM LEO
| Ulinzi ukiwa umeimarishwa wizarani kufuatia kadhia hiyo ya wanafunzi wa chuo cha usimamizi wa fedha |
| Hapa wanafunzi wakiwa safarini kwenda kumuona kamanda kova |
| Kamanda Kova akimsikiliza Rais wa wanafunzi wa Chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) akimuelezea kadhia nzima. Baadae Kamanda Kova aliamuru wanafunzi hao waende wote Kigamboni kushughulikia kadhia hiyo |
| Kamanda Kova akitoa taarifa kwa waandishi wa habari |
| Hapa wanafunzi wakiimba "tunavuka bure , tunavuka bure" huku wakielekea kwenye kivuko |
| Hapa wanafunzi wakigoma kushuka kwenye kivuko ilichukua saa zima ndio wakashuka na kuruhusu kivuko kiendelee na shughuli zake kama kawaida |
| Wakati wengine wakikataa kushuka wengine walikuwa wakiongezeka |
Subscribe to:
Posts (Atom)

