Facebook Comments Box

Monday, January 14, 2013

WABABA WA BSS (2012) AKABILIWA NA KESI YA KUTEMBEA NA MWANAFUNZI


 Mapenzi yao yalianza tangu binti akiwa kidaato cha tatu lakini halikuwa penzi lenye mashamu shamu kwa kuwa wabababa alikuwa bado hajamiliki pesa na heshima katika jamii inayomzunguka kama sasa mara tuu baada ya kuchukua kifuta jasho cha bss na vijihela alivyopewa na mapapaa waliokubali kazi aliioifanya bss hivyo kuwa na kiburi kilichomfanya amtie mimba mwananfunz ambae aligundulika kuwa ametoa mimba mara taarifa za mahusiano ya wababa na mwanafunzi huyo kufikishwa kwa mama mzazi wa binti huyo. Wababa aliwekwa ndani kwa muda wa siku mbili na kesi bado ipo mahakamani na wazazi wa binti wameapa kumweka ndani wababa na kumfanya kama Babu Sea huku binti akiwa hajaonekana siku ya 4 sasa na kutokujulikana alipo kwa madai anampenda wababa na wakimfunga tu nae anakunywa sumu.


Sunday, January 13, 2013

SAFARI YA YANGA YA MWAKA 1973 KUZINDUA TOTO AFRICA FC MWANZA ( Part II)

Waliosimama kuanzia kulia Mzee Kwala, Sululu, Chotta, Muhamed Mkweche, Muhamed Yahaya "Tostao" (anaechungulia jina lake halijapatikana) Kassim Manara,Shirsaz Shariff (wawili wa mwisho majina yao hayajapatikana) Waliochuchumaa kuanzia kushoto Abdulrahman, kibonge, Bilal Kabange, Muhamed Rishard Adolph, Muhamed Sengendo, Gordian Mapango, Jaffar Abdulrahman (wawili waliobaki majina yao hayajapatiakana ila kati ya hao wote ambao majina yao hayajapatikana mmoja wao ni Dr Ramadhan Dau)

Baada ya kuona ilivyopatikana timu ya Yanga B na mwaliko wa safari leo tunaendelea kuona safari ilivyokuwa na nini kilitokea.
Safari ilifanyika na ili kuwapa hamasa vijana Yanga ilitoa mchezaji mmoja kutoka timu ya wakubwa ambae alikuwa ni Boi Wiskens ambae alikuwa namba tatu mchezaji huyu alichezea hadi timu ya Taifa. Kutokana na ubovu wa barabara mchezaji wa Yanga B Muhamed Yahaya Tostao aliumia goti. walipofika wakakuta timu zitakazo shiriki ni Toto wenyewe kama wenyeji, Pamba na Cooperation United ya Shinyanga.Kikawaida list ya Yanga huwa inapangwa Dar Es Salaam ila Kocha Victor yeye alikuwa anaruhusu kipa kupanga beki yake na list ilikuwa hii ambayo ilicheza mechi ya kwanza na Pamba na kushinda 3 kwa 1.
1. Bilal Kabange 2. Jafar Abdulrahman 3. Shiraz Sharif 4. Muhamed Mkweche 5. Muhamed Rishard Adolph 6.Muhamed Yahaya Tostao 7 na 8 wamesahaulika 9 Kassim manara. Kipa alipomtaja Tostao kila mtu alikataa na kusema mgonjwa ila usiku wa walipofika Mzee Mangara Tabu Mangara alipiga simu hospitali ya mwanza (Bugando) na Tostao akapewa huduma na akaambiwa mechi ikiisha arudi kwa matibabu zaidi. Kama kawaidamechi zote Yanga walishinda kwa 3 kwa 1 isipokuwa moja tu Cooperation United ambayo walishinda 2 kwa 1 na golini alikaa Juma Pondamali messah. Baada ya mechi na kuchukua ubingwa Yanga walipewa zawadi ya saa ya ukutani kubwa ambayo walirudi na kuikabidhi kwa uongozi pamoja na kombe.
Baada ya kufika Dar Es Salaam Simba B waliomba barua ya kucheza na Yanga B kwenye uwanja wa Karume. Wakati huo Yanga B ikiwa haijafungwa mechi hata moja (watakubali au hawatakubali vipi iliundwa Nyota africa na Pan Africa Ijumaa ijayo itaendelea kwa ajili ya sehemu ya mwisho)

HII NDIO KAMPUNI YA FILAMU INAYOMILIKIWA NA WEMA SEPETU


Kupitia mtandao wa kijamii wa picha wa Instagram, Wema Sepetu ameshare picha za kwanza zinazoonesha logo ya kampuni yake iitwayo Endless Fame Films. “Nawaomba mzidi niombea nifike nnapotaka endless fame ifike… Inshallah,” ameandika mrembo huyo.


PETER WA P SQUARE AKIWA MAREKANI NA MTOTO WAKE


Mwimbaji wa kundi la P Square la Nigeria, Peter Okoye alikua California Marekani kwenda kumsalimia mtoto wake wa kiume ambae amepata na girlfriend wake Lara Omotayo ambae kwa sasa yuko San Francisco Marekani na akiwa huko atajifungua mtoto wake wa pili na Peter Okoye mwishoni mwa january 2013.
Kundi la P Square limekataa kupokea mialiko ya showz za january 2013 ili wapumzike kutokana na mfululizo wa show walizopata siku zilizopita.
.
.
.
.

Peter Okoye na baby mama wake Lola Omo

HAYA NDIO MAPENDEKEZO YA SAED KUBENEA KWENYE KATIBA MPYA


 
Nani anataka nini katika katiba mpya?

Haya ni maoni yaliyowasilishwa na Saed Kubenea wa MwanaHALISI; gazeti lililofungiwa na serikali kwa muda usiojulikana tangu 30 Julai 2012.
 
                                                                      

JUZI (10 Januari 2013) wenye vyombo vya habari na asasi nyingine za habari waliwasilisha kwa Tume ya Katiba Mpya, mapendekezo ya asasi zao na hata kuongeza maoni binafsi kama mwenyekiti wa mkutano wa Katiba, Prof. Mwesiga Baregu alivyoruhusu.

Saed Kubenea, Mkurugenzi Mtendaji wa Hali Halisi Publishers Limited (HHPL), wachapishaji wa magazeti ya MwanaHALISI na MISETO, aliwasilisha maoni yake. Ndimara Tegambwage ameyasoma na kuyafanya moja ya mambo muhimu aliyoona yenye thamani. Anatushirikisha:

Mapendekezo: Katiba Mpya (Na Saed Kubenea)

1. Kuhusu vyombo vya Habari
KATIBA itamke kuwa vyombo vya kutunga sheria (Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; Baraza la Wawakilishi, Bunge la Tanganyika au Bunge la Shirikisho; na vyovyote vile vitakavyokuwepo) visitunge:
a) Sheria inayopingana (inayokinzana), inayokwaza au kuingilia uhuru wa kuwa na maoni (kufikiri)
b) Sheria inayopingana, inayokwaza au kuingilia uhuru wa kujieleza (kutoa kauli)
c) Sheria inayopingana, inayokwaza au kuingilia uhuru wa habari (kupata habari zozote zinazohusu jamii zilizoko mikononi mwa serikali)
d) Sheria inayopingana, inayokwaza au kuingilia uhuru wa vyombo vya habari (kazi za utafutaji, ukusanyaji na usambazaji wa habari inayofanywa na waandishi wa habari na watangazaji)
e) Sheria inayopingana, inayokwaza au kuingilia uhuru wa kujumuika kwa amani (mikutano/maandamano ambavyo kihalisi ni njia za wanajamii kuwasiliana au kupeleka ujumbe kwa wahusika)

2. Kuhusu Mamlaka ya DPP
Katiba itamke kuwa:
a) Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) ateuliwe na chombo huru cha uteuzi (siyo rais wa nchi) na athibitishwe na Bunge
b) DPP awajibike kwa Bunge (Chombo cha kutunga sheria)

3. Mapendekezo mengine
1. Katiba itamke kuwa ARDHI ni mali ya Watanzania. Isiwekwe chini ya rais bali iwe chini ya wananchi wa Tanzania. Serikali itakuwa tu na mamlaka ya kutwaa ardhi kwa ajili ya manufaa ya umma ambayo yameainishwa kama vile ujenzi wa miundombinu, utunzaji wa mazingira na uboreshaji makazi. Serikali isiwe na uwezo wa kutwaa ardhi kwa ajili ya uwekezaji wa mtu binafsi au kampuni kama inavyoelezwa sasa na Sheria ya Ardhi ya Mwaka 1999.

2. Katiba itamke kuwa kila kijiji kitakuwa na serikali ya kijiji ambayo itaongoza kijiji hicho pamoja na uwezo wa kutunga sheria ndogo na kuzipitisha chini ya usimamizi wa mkutano mkuu wa kijiji. Serikali za vijiji ndizo zitakuwa na mamlaka ya kusimamia na kulinda haki za wananchi juu ya umiliki wao wa ardhi ya kijiji na kupanga mipango ya matumizi ya ardhi. Zitakuwa na uwezo wa kutoza kodi na kuendesha miradi ya maendeleo vijijini.

3. Katiba itamke kuwa rasilimali za madini, mafuta, gesi na maliasili, ni mali ya Watanzania na ni lazima zitumike na kuvunwa kwa manufaa ya Watanzania. Serikali haitasaini mikataba bila kibali cha bunge; bali itakuwa na uwezo wa kutoa leseni za utumiwaji wake. Utoaji huo wa leseni lazima pia uwe wa wazi na ambao utaidhinishwa na Bunge.

4. Katiba itamke kwamba migogoro yote ya uwekezaji sharti isuluhishwe kwa mujibu wa sheria za Tanzania na Mahakama za Tanzania. Hili ni takwa la Kanuni ya makubaliano ya Calvo na vilevile Azimio Na. 1803 la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa la Mwaka 1962 na Azimio Na. 3281 la 1974 la Baraza hilo juu ya Haki na Wajibu wa Mataifa juu ya Maliasili.

5. Katiba itamke kuwa rais atachaguliwa kwa kupigiwa kura na kupata zaidi ya asilimia 50 ya kura za watu wanaotakiwa kupiga kura. Yeye na serikali yake ni lazima awajibike kwa bunge na kila uteuzi anaofanya kwa nafasi za juu za uongozi, sharti uidhinishwe na bunge baada ya Bunge kuhojiana nao.
6. Katiba itamke kuwa Bunge lina madaraka na haki ya kumfuta kazi rais kwa kutowajibika au kwa kutumia madaraka yake vibaya.

7. Katiba itamke kuwa rais hatakuwa na haki au uwezo wa kulivunja bunge kwa sababu yoyote ile.

8. Katiba itamke kuwa rais hatakuwa na kinga dhidi ya mashitaka yoyote yale akiwa madarakani na baada ya kutoka madarakani. Mtu yeyote anaweza kufungua kesi dhidi yake binafsi au ofisi yake.

9. Katiba itamke kuwa uteuzi wa majaji wa mahakama kuu na mahakama ya rufaa ufanywe na chombo huru (badala ya rais) na ufuate umahiri na uelewa wa sheria pamoja na uadilifu wa kimaadili na kisheria.

10. Katiba itamke kuwa mhimili wa Mahakama, ukiongozwa na Jaji Mkuu, ndio usimamie na kuwasilisha bajeti yake bungeni (badala ya serikali kama ilivyo sasa).

11. Katiba itamke kuwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na viongozi wengine wakuu wa tume, wateuliwe na chombo huru cha uteuzi baada ya wanaotaka nafasi hiyo kuomba na kufanyiwa usaili. Aidha, maamuzi ya tume, kwa nafasi yoyote ile ya wagombea, yaweze kupingwa na mtu yeyote mahakamani.

12. Katiba itamke kuwa kukosa uadilifu au kutumia madaraka vibaya, kama itakavyothibitishwa na chombo husika, ni kosa la jinai.

13. Katiba itamke kuwa wote wanaojipatia utajiri kwa kuhujumu uchumi au watu wanaojitajirisha kwa kutumia madaraka yao ya umma, lazima washitakiwe kwa kosa la uhaini na mali zao zote, ikiwa ni pamoja na zile za walionufaika kutokana na kosa hilo, zitaifishwe.

14. Cheo cha Makamu wa Rais kiondolewe. Kibaki cha Waziri Mkuu.

15. Katiba itamke kuwa wakuu wa mikoa, wilaya (kama ni lazima kuendelea kuwa nao) wapatikane kwa kupigiwa akura ili w3aweze kuwajibika vema katika maeneo yao. Mameya wa miji na majiji nao wachaguliwe na wananchi moja kwa moja badala ya kuchaguliwa na madiwani.

16. Katiba itamke haki ya kuishi katika mazingira safi na salama lazima.

17. Katiba itamke kuwapo haki ya kufungua kesi za kutetea katiba, haki za binadamu na utawala wa sheria bila gharama zozote zile.

18. Katiba itamke kuwa elimu na afya ni haki kwa Watanzania wote.

19. Katiba itamke haki ya starehe.


Mwisho.


Saturday, January 12, 2013

KAMA TANZANIA HAINA DINI NI HUKO BARA SIYO ZANZIBAR- PROF ABDUL SHERIF

Prof Abdul Sherif

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetahadharishwa isilete hoja ya nchi kutokuwa na dini katika katiba ya nchi kwani Wazanzibari hawatakubali kupokonywa haki zao za kidini kama Mahakama ya Kadhi.

Ushauri huo umetolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Katiba Zanzibar, Professa Abdul Sherif muda mfupi baada ya kutoka kwenye meza ya utoaji wa maoni mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba yaliofanyika juzi katika ukumbi wa Eacrotanal Mjini Unguja ambapo aliwasilisha maoni ya Baraza la Katiba Zanzibar.

Professa Sherif amesema mabadiliko ya katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yanayofanyika yazingatia suala la dini kwani katiba ya Tanzania inazungumzia serikali haina dini lakini katiba ya Zanzibar haina kifungu hicho na hivyo suala la dini waachiwe watu wenyewe badala ya kuingizwa katika katiba.

Alisema huenda kuingizwa kifungu hicho kunaweza kuleta matatizo hasa kwa kuzingatia Zanzibar ina asilimia 99 ya waislamu na hivyo hawawezi kukubali kufutwa mahakama yao ya kadhi ambayo wameikuta tokea miaka kadhaa ya wazazi wao.

“Kuwepo kwa kifungu cha katiba kuhusu dini kunaweza kuchochea suala hata la mahakama ya kadhi nadhani wazanzibari hawatakubali kuambiwa mahakama ya kadhi ifutwe sasa sisi tunashauri suala hili lisiingizwe katiba katiba” alishauri.

Professa Sherif ambaye ni bingwa wa historia na ameshawahi kupokea tunzo mbali mbali duniani kutokana na mchango wake mkubwa katika kuandika vitabu kadhaa vya historia amesema wazanzibari wana haki ya kuwa na mahakama ya kadhi kutokana na kuwa idadi yao ni kubwa na hivyo wana haki ya kujiamulia mfumo wa wanaoutaka katika kuendesha nchi yao.

Aidha alisema miaka kadhaa wazanzibari wameishi bila ya kutokea ugomvi wa aina yoyote kuhusiana na dini na ndio maana hata wakati wa utawala wa Uingereza kuna makanisa makubwa yalijengwa Zanzibar ambapo wakati huo wakristo walikuwa wachache mno lakini kutokana na kuheshimu dini nyengine utawala wa Sultan ambaye ni muislamu alithubutu kutoa kibali cha kujengwa makanisa.

“Miaka yote wazanzibari hawajawahi kugombana kwa habari ya dini wanagombana kwa mambo mengine lakini sio dini wamekuwa na uvumilivu mkubwa na kushirikiana na ndio maana kuna mahekalu, misikini na makanisa lakini watu wake hawagombani” alisema Professa Sherif.

Akizungumzia masuala mengine kwa ujumla alisema bunge la Tanzania halikuwa na haki wala mamlaka ya kupunguza au kuongeza mambo ya muungano ambao yalikubaliwa katika hati ya Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar zilipoungana ambapo awali yalikuwa mambo 11 tu.

Professa Abdul Sherif amesema mambo yaliongezwa yamefanyika kinyume cha sheria na hivyo yalioongezwa yote yamekuwa batili kwa mujibu wa sheria kwa kuwa bunge halikuwa na madaraka hayo.

Katika hatua nyengine Chama Cha Wanasheria Zanzibar (ZLS) kimependekeza katika katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwepo kwa mfumo wa serikali pamoja na kuwepo kwa fursa ya mgombea binafsi kuwania uongozi wa nchi badala ya mfumo uliopo sasa.

Akiwasilisha maoni yake mbele ya tume ya mabadiliko ya katiba jana, Katibu wa chama hicho, Mussa Kombo alisema mfumo wa kuwepo kwa serikali tatu ndio utakaofaa kwa sasa pamoja na kupendekeza kuwepo kwa mgombea binafsi katika kuwania nafasi za urais nchini.

Alisema mfumo wa serikali tatu utasaidia kuondosha manungunuko na malalamiko yasiokwisha kati ya pande mbili hizo ambapo kwa miaka kadhaa sasa serikali imeshindwa kutafanyia kazi mambo ya kero za muungano.

“Sisi kama ZLS tunaona mfumo wa serikali tatu ndio unaofaa kwa sasa kuingizwa katika katiba mpya kuwepo na serikali ya Zanzibar na kuwepo na serikali nyengine jina lolote litakaloitwa na pia kuwepo na serikali ya muungano ambayo hiyo itakuwa ni ndogo itashughulikia masuala ya muungano tu” alisema Mussa nje ya mkutano wa utoaji wa maoni yaliofanyika ukumbi wa Eacrotanal Mjini Unguja.

Kombo alisema katiba mpya ianishe waziwazi hizo serikali tatu na mamlaka zake ili kusiwepo na utata kwani mfumo uliopo sasa haujaelezwa kikamilifu katika katiba na hivyo kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka pande mbili zilizoungana.

Aidha alisema ZLS imeona kuwepo na mgombea binafsi atakayewania nafasi ya urais kwani imani yao ni kwamba anaweza kupatikana kiongozi mzuri atakayetokana nje ya chama cha siasa.

“ZLS tunaamini tunaweza kupata kiongozi nje ya chama” alisema Kombo na kuongeza kwamba mambo mengine waliopendekeza na ZLS kuingizwa katika katiba mpya ni suala la uraia, ulinzi, sarafu, na uhamiaji ambayo yote yawe ni ya muungano na mambo mengine yaliobaki yasiwe na muungano.

Kombo alisema mambo ambayo sio ya muungano yanapaswa kuamuliwa kwa pamoja na kwa ridhaa ya pande mbili zilizoungana huku kila serikali iwe na chombo chake cha maamuzi ambapo walipendekeza kuwepo na bunge la Zanzibar, bunge la bara au vyovyotelitakavyotwa na kuwepo na bunge la pamoja.

Alisema tabia ya serikali ya upande mmoja kujiamulia na serikali ya pili kushindwa kutoa maamuzi haipendezi na hivyo wameshauri jambo lolote liamuliwe kwa pande mbili tena kwa makubaliano.

Akizungumzia suala la haki za binaadamu kuingizwa katika katiba Professa Chris Peter Maina wa Kituo Cha Huduma za Sheria Zanzibar, alisema haki zote za binaadamu ziwekwe katika katiba ikiwa pamoja na haki ya kupata elimu na afya iwe ni ya lazima pamoja na ile haki ya msingi ya kuishi.

Professa Maina alisema katika mpya ianishe haki ya kutumikishwa kwani kumekuwepo na tatizo kubwa la watu kuchukuliwa na kupelekwa nje ya nchi kutumikishwa na hivyo katiba iseme wazi kwamba haki hiyo ni ya msingi, ikiwa pamoja na haki ya kuandamana

Pia alipendekeza katika katiba mpya kuwepo na uhuru wa vyombo vya habari badala ya katiba ya sasa inavyosema uhuru wa kupata habari peke yake.

Mambo mengine aliyotaka yawemo katika katiba ni uhuru wa fikra na maoni iwe ni pake yake na uhuru wa dini na imani huku akipendekeza haki ya kupiga kura kwa watu waliofungwa au waliopo rumande na kulindwa kwa mali iliyopatikana kihalali.

Maoni mengine ya kituo hicho cha huduma za sheria ni pamoja na kuwepo wimbo wa taifa na alama za utaifa, lugha ya taifa, katiba iwe ndio juu ya kila kitu, ulinzi wa katiba na pia katiba ianishe nani mtanzania na aelezwe katika katiba.



KIGOMA; NDEGE YA ATCL YAPASUKA KIOO IKIWA ANGANI

Hii ndio ndege ya kwanza iliyopata ajali Kigoma
 
ZAIDI ya abiria 25 waliokuwa wakisafiri na ndege ya Shirika la ndege nchini ATCL kutoka Kigoma kuelekea Dar es Salaam wamenusurika kifo kutokana na ndege waliyokuwa wakisafiria kupata hitilafu ikiwa angani jambo lililomlazimu rubani wa ndege hiyo kufanya jitihada na kuirudisha kiwanjani.

Hali hiyo imetokana na moja ya vioo vya mbele vya ndege hiyo kupasuaka na hivyo kuruhusu upepo mkali kuingia ndani na hivyo kuwafanya marubani wa ndege hiyo kufanya kazi ya ziada kuhakikisha ndege hiyo inatua salama.

Ndege hiyo ilikuwa ikifanya safari yake ya kwanza mkoani humo ikiwa ni miezi 10 baada ya ndege nyingine ya shirika hilo kuanguka na kuharibika mkoani Kigoma.

Baadhi ya abiria waliokuwemo kwennye ndege hiyo, Athumani Batumwa na Fred Mbassa wamesema ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria 50, ilipata itilafu ya kioo cha mbele kiasi cha dakika 30 baada ya kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Kigoma.

Kaimu meneja wa shirila la ATCL, Kepteni Milton Lazaro amekiri kutokea kwa hitilafu hiyo na amewaondoa hofu wasafiri juu ta tatizo hilo nakwamba ni sehemu ya matatizo yanayoweza kutokea kwa ndege yoyote.



MAHSUSI KWA WATU WA UJIJI



MWANAJESHI ALIEPIGA PICHA NA LEMA AFUNGWA MIAKA MINNE

 



MTU aliyepiga picha na Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema akiwa amevalia sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), amehukumiwa kifungo cha miaka minne jela.

Abubakari Kikulu (29), alipiga picha na mbunge huyo Desemba 23 mwaka jana, baada ya Lema kumaliza kuhutubia mkutano wa hadhara eneo la Mererani, ikiwa ni sehemu ya mikutano aliyoifanya kutokana na Mahakama ya Rufani Tanzania kumrejeshea ubunge wake.

Mbali na kupiga picha hiyo na Lema pamoja na Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari, kijana huyo alionekana katika picha hiyo akionyesha vidole viwili, ambayo ni alama ya Chadema.

Hata hivyo, baada ya picha hiyo, JWTZ lilimtilia shaka kijana huyo na kutangaza rasmi kumsaka, ili lijiridhishe kama ni mmoja wa wanajeshi wake.

Baada ya kumsaka kwa takriban siku 12, kijana huyo alikamatwa Januari 13, katika Mji wa Bomang’ombe wilayani Hai na baada ya kupekuliwa alikutwa na sare hizo.

Jana, Kikulu alifikishwa mahakamani mjini Moshi, akiwa chini ya ulinzi wa polisi na kusomewa mashtaka mawili, ambayo yote alikiri kuyafanya kama ilivyodaiwa mahakamani.

Baada ya kukiri kosa hilo Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Kilimanjaro, alimhukumu kifungo cha miaka minne jela, ili iwe fundisho wa wakosaji wengine wa aina hiyo.

Kabla ya hukumu hiyo, Wakili wa Serikali, Ignas Mwinuka alimsomea mshtakiwa huyo mashitaka yake mawili, likiwamo la kujifanya Ofisa wa Jeshi, wakati akijua ni uongo.

Wakili huyo alidai mahakamani kuwa Januari 3, mwaka huu katika eneo la Bomang’ombe wilayani Hai, mtuhumiwa huyo alijitambulisha kama mtumishi wa umma.

Katika shtaka la pili, wakili huyo alidai siku hiyo hiyo katika Mtaa wa Msikitini, eneo hilo la Bomang’ombe, mtuhumiwa alipatikana na sare za JWTZ kinyume cha sheria.

Sare hizo ni pamoja na suruali moja, mashati mawili na kofia mbili, vyote vikiwa na alama za Jeshi la Wananchi wa Tanzania la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Baada ya Hakimu Kobelo kumuuliza mshtakiwa kama ni kweli alitenda makosa anayoshitakiwa, mshtakiwa huyo alikiri makosa yake katika hali ambayo haikutarajiwa.

Kutokana na kukiri kwake makosa hayo, Hakimu Kobelo alimhukumu kifungo cha miaka miwili kwa kosa la kwanza la kujifanya Ofisa wa JWTZ na miaka mingine miwili kwa kosa la pili.

Hata hivyo, Hakimu Kobelo alisema kuwa kwa kuwa adhabu hizo zinakwenda kwa pamoja (concurrent), mshtakiwa huyo atatumikia kifungo cha miaka miwili jela.

Kwa mujibu wa hakimu huyo, kosa alilolifanya mtuhumiwa huyo ni baya na linastahili adhabu kali, ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaotumia vibaya sare za majeshi nchini.
 

PROF. ISAIAH IBEH DEVELOPS A DRUG TO 'CURE' HIV/AIDS


Benin - Prof. Isaiah Ibeh of the University of Benin, on Tuesday announced the development of a new drug that can cure HIV and AIDS.

Ibeh, who is the Dean of the School of Basic Medical Sciences of the university, told the News Agency of Nigeria (NAN) in Benin that the herbal drug had undergone ``series of successful tests''. ``We are at the threshold of making history, in the sense that we seem to have with us something that will permanently take care of what over time seems to have defied all solutions.

``We are talking about the latest discovery of an oral drug made from plants extraction in Nigeria for the possible cure of the pandemic, HIV and AIDS virus.’’

According to him, research on the project was started in 2010 and culminated in the development of ``Deconcotion X (DX)–Liquid or Bioclean 11 for the cure of HIV and AIDS''.

 ``The existing retroviral drugs are intervention drugs for the management of AIDS but our new discovery is a possible cure.

``We have tried to look at the product first; its toxicological analysis and discovered that it has a large safety margin. ``This means that if animals or human beings are exposed to it, they will not suffer any serious harm at all from the exposure.

``It also helped us to know the quantity we can conveniently give to animals and will feel secure that nothing untoward will happen.

``We have also done the bacteriological analysis on it, after which we looked at its effect on the virus and the result was quite revealing and refreshing.''

Ibeh also said that the drug had been exposed to series of medical examination both in Nigeria and in the USA. He added that the drug had performed well on patients with the HIV virus and had shown evidence of total restoration of damaged tissues.

``The result showed an increase in the body weight of the individual administered with DX. ``The body weight was statistically significant when compared with the control group.''

He said that further tests were being conducted to determine ``at what point will a patient become negative after being administered the drug?''.

``This verification is necessary because it is what is used to measure whether infection is still there or not. So we need to know the siro-convention time.

 ``But preliminary results showed that of the five latest patients orally administered with the drugs, our findings is that up to seven months , three of them were siro negative while two were sill faintly positive.’’

 Ibeh appealed for support from the Federal Government and relevant bodies to assist the university with relevant equipment to sustain the research.



DOWNLOAD WIMBO WA VANESSA MDEE CLOSER HAPA

 




 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU