Facebook Comments Box

Saturday, January 12, 2013

MWANAJESHI ALIEPIGA PICHA NA LEMA AFUNGWA MIAKA MINNE

 



MTU aliyepiga picha na Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema akiwa amevalia sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), amehukumiwa kifungo cha miaka minne jela.

Abubakari Kikulu (29), alipiga picha na mbunge huyo Desemba 23 mwaka jana, baada ya Lema kumaliza kuhutubia mkutano wa hadhara eneo la Mererani, ikiwa ni sehemu ya mikutano aliyoifanya kutokana na Mahakama ya Rufani Tanzania kumrejeshea ubunge wake.

Mbali na kupiga picha hiyo na Lema pamoja na Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari, kijana huyo alionekana katika picha hiyo akionyesha vidole viwili, ambayo ni alama ya Chadema.

Hata hivyo, baada ya picha hiyo, JWTZ lilimtilia shaka kijana huyo na kutangaza rasmi kumsaka, ili lijiridhishe kama ni mmoja wa wanajeshi wake.

Baada ya kumsaka kwa takriban siku 12, kijana huyo alikamatwa Januari 13, katika Mji wa Bomang’ombe wilayani Hai na baada ya kupekuliwa alikutwa na sare hizo.

Jana, Kikulu alifikishwa mahakamani mjini Moshi, akiwa chini ya ulinzi wa polisi na kusomewa mashtaka mawili, ambayo yote alikiri kuyafanya kama ilivyodaiwa mahakamani.

Baada ya kukiri kosa hilo Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Kilimanjaro, alimhukumu kifungo cha miaka minne jela, ili iwe fundisho wa wakosaji wengine wa aina hiyo.

Kabla ya hukumu hiyo, Wakili wa Serikali, Ignas Mwinuka alimsomea mshtakiwa huyo mashitaka yake mawili, likiwamo la kujifanya Ofisa wa Jeshi, wakati akijua ni uongo.

Wakili huyo alidai mahakamani kuwa Januari 3, mwaka huu katika eneo la Bomang’ombe wilayani Hai, mtuhumiwa huyo alijitambulisha kama mtumishi wa umma.

Katika shtaka la pili, wakili huyo alidai siku hiyo hiyo katika Mtaa wa Msikitini, eneo hilo la Bomang’ombe, mtuhumiwa alipatikana na sare za JWTZ kinyume cha sheria.

Sare hizo ni pamoja na suruali moja, mashati mawili na kofia mbili, vyote vikiwa na alama za Jeshi la Wananchi wa Tanzania la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Baada ya Hakimu Kobelo kumuuliza mshtakiwa kama ni kweli alitenda makosa anayoshitakiwa, mshtakiwa huyo alikiri makosa yake katika hali ambayo haikutarajiwa.

Kutokana na kukiri kwake makosa hayo, Hakimu Kobelo alimhukumu kifungo cha miaka miwili kwa kosa la kwanza la kujifanya Ofisa wa JWTZ na miaka mingine miwili kwa kosa la pili.

Hata hivyo, Hakimu Kobelo alisema kuwa kwa kuwa adhabu hizo zinakwenda kwa pamoja (concurrent), mshtakiwa huyo atatumikia kifungo cha miaka miwili jela.

Kwa mujibu wa hakimu huyo, kosa alilolifanya mtuhumiwa huyo ni baya na linastahili adhabu kali, ili iwe fundisho kwa watu wengine wanaotumia vibaya sare za majeshi nchini.
 

PROF. ISAIAH IBEH DEVELOPS A DRUG TO 'CURE' HIV/AIDS


Benin - Prof. Isaiah Ibeh of the University of Benin, on Tuesday announced the development of a new drug that can cure HIV and AIDS.

Ibeh, who is the Dean of the School of Basic Medical Sciences of the university, told the News Agency of Nigeria (NAN) in Benin that the herbal drug had undergone ``series of successful tests''. ``We are at the threshold of making history, in the sense that we seem to have with us something that will permanently take care of what over time seems to have defied all solutions.

``We are talking about the latest discovery of an oral drug made from plants extraction in Nigeria for the possible cure of the pandemic, HIV and AIDS virus.’’

According to him, research on the project was started in 2010 and culminated in the development of ``Deconcotion X (DX)–Liquid or Bioclean 11 for the cure of HIV and AIDS''.

 ``The existing retroviral drugs are intervention drugs for the management of AIDS but our new discovery is a possible cure.

``We have tried to look at the product first; its toxicological analysis and discovered that it has a large safety margin. ``This means that if animals or human beings are exposed to it, they will not suffer any serious harm at all from the exposure.

``It also helped us to know the quantity we can conveniently give to animals and will feel secure that nothing untoward will happen.

``We have also done the bacteriological analysis on it, after which we looked at its effect on the virus and the result was quite revealing and refreshing.''

Ibeh also said that the drug had been exposed to series of medical examination both in Nigeria and in the USA. He added that the drug had performed well on patients with the HIV virus and had shown evidence of total restoration of damaged tissues.

``The result showed an increase in the body weight of the individual administered with DX. ``The body weight was statistically significant when compared with the control group.''

He said that further tests were being conducted to determine ``at what point will a patient become negative after being administered the drug?''.

``This verification is necessary because it is what is used to measure whether infection is still there or not. So we need to know the siro-convention time.

 ``But preliminary results showed that of the five latest patients orally administered with the drugs, our findings is that up to seven months , three of them were siro negative while two were sill faintly positive.’’

 Ibeh appealed for support from the Federal Government and relevant bodies to assist the university with relevant equipment to sustain the research.



DOWNLOAD WIMBO WA VANESSA MDEE CLOSER HAPA

 




Friday, January 11, 2013

LISSU: HAKUNA SABABU YA BAADHI YA WATU KUWA JUU YA SHERIA

Mwanasheria wa CHADEMA, Tundu Lissu akiwaeleza waandishi wa habari kuwa Chama chake kimependekeza kuwepo kwa utawala wa majimbo utakaorahisisha shughuli za maendeleo kwa wananchi Picha na Salhim Shao 
Kwa ufupi
“Pia kinga ya Rais inatakiwa kuondolewa ili kuleta nidhamu ya utendaji katika ofisi hii ya umma. Akifanya makosa ya jinai ashtakiwe kama mhalifu mwingine, hakuna sababu ya baadhi ya watu kuwa juu ya sheria, kila mtu awe chini ya sheria,”


MCHAKATO wa ukusanyaji wa maoni ya wananchi yatakayosaidia katika uundwaji wa Katiba Mpya unaendelea na safari hii ni zamu ya makundi maalumu vikiwemo vyama vya siasa ambavyo vimeanza kutoa maoni yao mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Mikutano hiyo kati ya Tume na wawakilishi wa vyama vya siasa inafanyika katika Ofisi Kuu za Tume pamoja na Ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam.
Vyama vyote vimepewa fursa ya  kushiriki katika utoaji maoni na baadhi ya mambo ambayo wameyapendekeza kuwamo katika Katiba Mpya ni pamoja na utawala wa majimbo na kuwapo kwa mgombea binafsi.
Kimsingi hoja hizi zimekuwa zikitolewa maoni mara nyingi na wananchi katika mikutano mbalimbali ya Tume iliyokuwa ikifanyika nchi nzima kuanzia Julai hadi Desemba mwaka jana, tofauti na sasa ni kwamba wanasiasa wamezieleza kwa undani zaidi na kuzifafanua namna gani zinavyoweza kuingia katika Katiba ijayo.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimejikita zaidi katika muundo wa Muungano na utawala wa majimbo, wakati Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimejielekeza kwenye hoja ya mgombea binafsi.
Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu anasema kuwa chama chake kinataka kuona Katiba Mpya inakuja na mfumo mpya ambao utaleta mabadiliko katika nyanja mbalimbali zikiwamo utawala, rasilimali, ulinzi wa mali za umma, haki za binadamu, uwajibikaji serikalini na muundo wa Jamhuri ya Muungano ambao utasaidia kuunusuru usivunjike.
Lissu anasema kuwa kuna kila sababu ya Katiba Mpya kuleta mabadiliko katika muundo wa Muungano ambao Chadema wanapendekeza uwe Muungano wa Shirikisho wa Serikali tatu, yaani Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ndogo ya Jamhuri ya Muungano.
“Hatuwezi kuendelea na mfumo uliopo wa Muungano kwani una upungufu mwingi. Ni fursa nzuri ambayo tumeipata ya kutengeneza Katiba Mpya ya nchi ambayo kimsingi inapaswa kuleta mabadiliko yatakayounusuru au kuuokoa Muungano usivunjike. Tukikosea tunaweza kujikuta tunatengana kama ilivyo kwa Ethiopia na Eritrea, Sudan na Sudan Kusini, Yugoslavia na Czechoslovakia,” anasema Lissu.
Pia anasema kwa kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni wa hiari kunatakiwa kuwe na haki ya kujitoa kwa upande usioridhika kuendelea kuwa kwenye Muungano.
Anasema utaratibu wa kujitoa uwe kwa njia ya kura ya maoni itakayopigwa na wananchi wa upande mmojawapo wa Muungano na ikiwa theluthi mbili ya wananchi wakikubali kujitoa basi iruhusiwe wajitoe kwa sababu Muungano huu haukuwa wa lazima.
Lissu anaongeza kuwa kwenye mambo ya Muungano wamependekeza yawemo mambo saba tu ambayo ni ulinzi na usalama, wizara zisizozidi 18, Bunge lisilozidi wawakilishi 300, mamlaka ya uteuzi ya Rais ambayo yanapaswa kupunguzwa, Rais ashtakiwe akifanya makosa ya jinai, pamoja na kuweka bayana suala la umilikaji wa rasilimali za nchi.
Kuhusu mamlaka ya uteuzi ya Rais anaeleza kuwa ni lazima yapunguzwe ili kuiondoa nchi kwenye mfumo wa urais wa kifalme.


POLISI WAKAMATWA WAKISAFIRISHA DAWA ZA KULEVYA



Picha hii na Maktaba.

ASKARI polisi wawili wa wilayani Bunda, mkoani Mara, wanashikiliwa na jeshi la polisi katika mkoa wa Simiyu, kwa tuhuma ya kusafirisha madawa ya kulevya aina ya mirungi.

Kamanda wa polisi mkoani Simiyu Salum Msangi, amesema kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 7:30 mchana, katika kizuizi cha polisi kilichoko katika eneo la wilaya ya Busega, karibu na mji mdogo wa Lamadi, kwenye barabara kuu ya Mwanza-Musoma.

Kamanda Msangi amewataja asakari polisi hao kuwa ni pamoja na mwenye namba E. 4640 koplo Daniel na E. 6224 Koplo Mwinyihaji, na kwamba walikamatwa wakiwa na mirungi yenye uzito wa kilo 72 iliyokuwa imewekwa kwenye mabegi mawili.

Alisema kuwa askari hao walikuwa na gari binafsi yenye namba T. 168 DWB, aina ya Noah, ambapo pia walikuwa na wanawake wawili, Achien Aoko (30) na Penina Samson (20), ambao wote ni wakazi wa wilayani Tarime.

Aidha, alisema kuwa baada ya askari hao ambao walikuwa wamevaa kiraia kufika katika kizuizi hicho, gari yao ilipekuliwa na askari, na ndipo ikagundulika kwamba kulikuwa na mabegi mawili ya mirungi.

Kamanda Msangi alisema kuwa askari hao tayari wanaendelea na mashitaka ya kijeshi, ambapo wanawake waliokuwa nao jana wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Bariadi ambayo kwa sasa inafanya kazi kama mahakama ya mkoa wa Simiyu.




KESI YA DK. ULIMBOKA: MTUHUMIWA J. MULUNDI AMTAKA BALOZI WA KENYA KORTINI




Dk. Stephen Ulimboka baada ya kipigo kikali kutoka kwa J. Mulundi


Raia wa Kenya, Joshua Mulundi (21) anayekabiliwa na mashitaka ya kumteka na kutaka kumuua Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk Stephen Ulimboka, ameiomba Mahakama kumleta Balozi wa nchi yake mahakamani.

Mulundi alitoa ombi hilo jana mbele ya Hakimu Agnes Mchome wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya upande wa mashitaka kudai kuwa upelelezi wa kesi yake bado haujakamilika. Alihoji kwa nini upelelezi wa kesi hiyo unachelewa kukamilika na kwa nini upande wa mashitaka hawaleti mashahidi mahakamani ili kesi hiyo iishe?

Hakimu Mchome alisema jambo hilo liko nje ya uwezo wa Mahakama hiyo kwa kuwa haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo, isipokuwa Mahakama Kuu.

Mulundi aliiomba Mahakama kushinikiza Balozi wa Kenya aende mahakamani, huku akidai ameshaanza mgomo mahabusu na ataendelea nao. Hakimu Mchome alisema Mahakama hiyo haina uwezo wa kumshinikiza balozi wa nchi yake kufika mahakamani, lakini anaweza kufuata utaratibu kwa yeye kumuandikia Balozi wake barua.

Hata hivyo Mulundi hakuridhika na majibu hayo na kuomba apelekwe kwa Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Ilvin Mugeta ili akawasilishe malalamiko. Alitolewa katika chumba cha Hakimu Mchome na kupelekwa ofisini kwa Hakimu Mugeta ambako alidai upelelezi wa kesi yake unacheleweshwa.

Hata hivyo Hakimu Mugeta alisema Mahakama haina uwezo wa kuharakisha Polisi kukamilisha upelelezi kwa sababu kesi hiyo iko chini ya Polisi.

Hakimu Mchome ameahirisha kesi hiyo hadi Januari 23 mwaka huu itakapotajwa tena. Upande wa mashitaka uliwasilishwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Tumaini Kweka.

Alipotoka mahakamani, Mulundi alikuwa anachechemea hasa mguu wa kushoto kitu ambacho kilisababisha ashuke kwa taabu katika ngazi za Mahakama. Pia alionesha sura ya huzuni, lakini Ofisa Magereza waliokuwa naye walishangaa na kudai alitoka mahabusu akitembea vizuri.

Inadaiwa kuwa, Juni 26 mwaka jana, katika eneo la Leaders Club, Mulundi alimteka Dk Ulimboka. Katika shitaka la pili anadaiwa Juni 26 mwaka jana, akiwa katika eneo la Msitu wa Mabwepande Tegeta, Dar es Salaam, kinyume cha sheria inadaiwa alijaribu kumsababishia kifo Dk Ulimboka. Kwa mara ya kwanza mshitakiwa huyo alipandishwa kizimbani mahakamani hapo Julai 13 mwaka jana.







Thursday, January 10, 2013

HAWA NDIO WANAFUNZI WALIONGOZA (VICHWA ) WALIOMALIZA DARASA LA SABA


Picture
Wanafunzi walioongoza mtihani wa taifa wa darasa la saba wa mwaka 2012, Janeth Kijazi (kushoto) Justina Kalala (katikati)na Kellen Mudogo wakiwa shule ya sekondari ya wasichana, St Marian Bagamoyo, jana, walikoanza kidato cha kwanza. Wanafunzi hao walihitimu elimu ya msingi katika Shule ya Tusiime ya jijini Dar es Salaam. (Picha: Florence Majani)



MGAO WA UMEME HAUPO NA HAUTAKUWEPO - PROF: MUHONGO


Picture


Wednesday, January 9, 2013

SALAMA NA SAJUKI NDANI YA MKASI




CCM WAKANUSHA TUHUMA ZA BAVICHA


 Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Nape Nnauye  
---
 
SIKU moja baada ya Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha), kudai CCM inashirikiana na baadhi ya viongozi wake kukisaliti chama hicho, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amekanusha tuhuma hizo.Nape alisema CCM haihusiki na mgogoro wowote ndani ya chama hicho, hivyo wanapaswa kumtafuta mchawi wao siyo kukilaumu chama chake.

“Mchawi wanaye wenyewe ndani ya chama chao, hatuhusiki na lolote hivyo wanapaswa kujipanga na kuulizana kubaini tatizo linalowasumbua,” alisema.

Aliongeza kuwa CCM haina muda wa kuhujumu chama hicho, ila wana muda wa kutekeleza ilani za chama maeneo mbalimbali nchini.

Nape alisema kutokana na hali hiyo, CCM imejipanga kuhakikisha ahadi zinatekelezwa kwa vitendo, ikiwamo maazimio yaliyotolewa kwenye mkutano mkuu wa chama hicho.Baadhi ya viongozi wa Bavicha wanaodaiwa kushirikiana na CCM kudhooficha Chadema na wengine walifukuzwa uanachama


SAKATA LA BASHE NA MEMBE LAFIKIA PATAMU

Picture
Bernard Membe (Mb, W)

MGOGORO wa makada wawili wa CCM; Benard Membe na Hussein Bashe umechukua sura mpya, baada ya mbunge huyo wa Mtama, kukiomba chama hicho tawala kuingilia kati ili kuupatia suluhu.

Mvutano wa Bashe na Membe ulianza wakati wa kampeni za uchaguzi wa ndani wa CCM hasa uchaguzi wa NEC baada ya Bashe kumtuhumu Membe kwa mambo mbalimbali ikiwamo kukigawa chama.

Kauli hiyo ya Bashe ilimkera Membe ambaye kwa nyakati tofauti amekuwa akisisitiza kuwa atamshughulikia mwanasiasa huyo chipukizi wa CCM ili amtambue.

“Nitashughulika na Bashe ndani ya chama kwa maana ya kumfikisha kwenye kamati zetu, ili ayaeleze vizuri ambayo amenipakazia na kunichafua sana… Lakini mambo mengine ambayo yamekaa kijinai sasa hayo ndiyo nitakayoyapeleka mahakamani,” alisema Membe baada ya taarifa hizo.

Habari zilizopatikana jana zimeeleza kuwa Membe amemwandikia barua Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Phillip Mangula kumwomba amtake Bashe athibitishe kauli zake mbalimbali dhidi yake.

Moja ya mambo Membe anamtaka Bashe ayathibitishe ni kwamba waziri huyo wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kuwahi kusema kuwa akiwa Rais, atawafukuza watu kumi na moja nchini ambao anaamini kuwa siyo Watanzania, “Barua hii ina tuhuma nyingi, lakini kikubwa mheshimiwa huyo (Membe) amekiomba chama kimtake Bashe athibitishe tuhuma zake dhidi yake, ikiwamo hili la kuwafukuza Watanzania 11,” kilidokeza chanzo chetu cha habari ndani ya CCM.

Chanzo hicho kimeeleza kuwa baada ya makamu mwenyekiti huyo kupata barua ya Membe, ameipeleka katika Ofisi ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kwa hatua zaidi. Habari zimeeleza kuwa tayari Kinana ameifanyia kazi barua hiyo kwa kumwandikia barua Bashe ili ajibu tuhuma zinazomkabili ifikapo kesho Januari 10.

Nakala ya barua hiyo ya Kinana imetumwa kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Nzega ambako Bashe anatokea akiwa Mjumbe wa Mkutano Mkuu Taifa kupitia wilaya hiyo, “Tayari Bashe ameandikiwa barua na CCM kumtaka ajibu malalamiko hayo ya mwenzake Membe,” kilieleza chanzo hicho cha habari.

Membe hakupatikana kwa siku tatu mfululizo, ili azungumzie suala hilo baada ya simu yake ya mkononi kutopatikana na taarifa zilizopatikana ofisini kwake, zimeeleza kuwa yuko likizo jimboni kwake Mtama, Lindi.

Bashe hakuthibitisha wala kukanusha kupata barua hiyo ya CCM inayomtaka ajibu madai ya Membe, badala yake akasema: “Membe aliahidi kunishughulikia na mimi ninangoja anishughulikie.”

Mangula alipotafutwa juzi kuzungumzia suala hilo alisema asingeweza kusema chochote kwa kuwa alikuwa hajafika ofisini tangu alipokwenda kwenye mapumziko ya mwisho wa mwaka, “Sijajua chochote kilichoendelea ofisini kwa sababu nilikuwa kijijini kwangu kwa ajili ya Sikukuu ya Krimasi na Mwaka Mpya. Nikiingia ofisini naweza kuwa katika nafasi ya kujua kilichoendelea,” alisema Mangula. Hata hivyo, alipopigiwa simu jana, iliita bila kupokewa na baadaye ikazimwa kabisa.

Kinana naye hakupatikana jana baada ya simu yake pia kuita na kupokelewa na mtu mwingine mara kadhaa ambaye alieleza kuwa alikuwa mkutanoni siku nzima.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alijibu kwa kifupi na kukata simu,” Sijapata wala kuona barua ya malalamiko ya Membe kwa Bashe.”

Novemba 10, mwaka jana Bashe akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma, alimtuhumu Membe akidai kuwa ndiye anayehusika na vipeperushi vya kumhujumu mwenyekiti wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete vilivyokuwa vimetawanywa na watu wasiojulikana siku chache kabla ya uchaguzi wa mwenyekiti na nafasi nyingine kufanyika.


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU