Facebook Comments Box

Saturday, November 10, 2012

HATIMAYE LORD EYEZ AZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI

Embedded image permalink

Embedded image permalink 
Tukio zima limefanyika double view hotel, sinza. Lord amewataka watu wasimhukumu na tuwe na subira hadi mahakama itakapoamua 
Pia kasema anaandaa mchakato wa kuwachukulia hatua wote waliopotosha habari kwakuwa alishinikizwa kuonekana ameiba


WALTER CHILAMBO NDIO MSHINDI WA EBSS



BONGO STAR SEARCH

                                                   Salama katokelezeaaaaaa
                                                  Madam ritha tayari kwa shindano
                                              Zantel's Director of Communications, Awaichi Mawalla


AZAM WAMFUKUZA MCHEZAJI MWINGINE TENA

BEKI wa Azam FC, Aggrey Morris Ambroce amefukuzwa kwenye kambi ya timu hiyo leo mjini Tanga, baada ya kuthibitika naye alipokea rushwa kutoka klabu ya Simba ili kuihujumu timu hiyo katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Aggrey ameondolewa kambini leo, siku moja tu baada ya kipa Deo Munishi ‘Dida’ na mabeki Said Mourad na Erasto Nyoni nao kusimamishwa kwa tuhuma hizo.
Azam ilifungwa na Simba mabao 3-1 Oktoba 27, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mechi za Ligi Kuu na baada ya hapo ikamfukuza kocha wake Mserbia, Boris Bunjak na kumrejesha Muingereza, Stewart Hall.
Habari kutoka ndani ya Azam zimesema kwamba baada ya kupata taarifa hizo, uongozi ulizifanyia kazi taratibu na kujiridhisha kabisa wachezaji hao watatu walikula njama za kuihujumu timu katika mechi hiyo.
Kwa sababu hiyo, uongozi kwanza umewasimamisha wachezaji hao na hatua zaidi zitafuatia baadaye.
Hata hivyo, Dida hakucheza mechi hiyo, kwani Oktoba 27, kikosi cha Azam kilikuwa; Mwadini Ali, Ibrahim Shikanda, Samir Hajji Nuhu, Said Mourad, Aggrey Morris, Abdulhalim Humud, Jabir Aziz aliyempisha Abdi Kassim, Himid Mao aliyempisha Kipre Balou, John Bocco ‘Adebayor’ aliyempisha Khamis Mcha ‘Vialli’, Kipre Herman Tcheche na Salum Abubakar.
Siku hiyo, Azam walitangulia kufunga dakika ya nne, kupitia kwa Adebayor ambaye alimtoka beki Mkenya Paschal Ochieng na kumchambua Juma Kaseja, kabla ya Felix Mumba Sunzu Jr., kuisawazishia Simba dakika mbili baadaye, akiunganisha kwa kichwa krosi maridadi ya Mrisho Khalfan Ngassa kutoka wingi ya kulia.
Okwi aliifungia Simba bao la pili dakika ya 40, baada ya kutokea kizaazaa langoni mwa Azam kufuatia mpira uliopigwa langoni mwa timu hiyo na Mwinyi Kazimoto na dakika tano tu tangu kuanza kipindi cha pili, Mganda huyo tena akawainua vitini mashabiki wa Simba, akifumua shuti la umbali wa mita 19, baada ya kuwatoka mabeki wa Azam.
Habari zaidi zinasema kwamba, uchunguzi unaendelea kufanywa juu ya wachezaji wengine wanaotuhumiwa kuwa katika mkumbo huo wa kuihujumu timu na ikithibitika ni ukweli, watachukuliwa hatua pia bila kujali majina yao.
Azam tayari iko Tanga tangu jana saa 8:00 mchana wa kwa ajili yao ya mchezo wao wa mwisho wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kesho dhidi ya Mgambo JKT, Uwanja wa Mkwakwani.

KAMATI YA SAIDIA SERENGETI ISHINDE RIDHIWANI KIKWETE NDANI

Ridhiwani
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania limeteua wadau 10 kwa ajili ya kusaidia timu ya taifa ya vijana walio na umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys itakayopambana na Congo (Brazaville) katika mechi ya raundi ya tatu ya michuano ya awali ya Mataifa ya Afrika.Uteuzi huo umefanywa na Rais wa TFF, Leodegar Tenga baada ya Kamati ya Vijana ya TFF kufanya kikao chake kujadili kwa umakini ushiriki wa timu hiyo na kupeleka mapendekezo yake kwa rais huyo wa shirikisho.
Kutokana na umuhimu wa mechi hiyo itakayoamua timu itakayofuzu kucheza fainali za Mataifa ya Afrika, TFF imeona umuhimu wa kuwa na kamati ambayo itakuwa na majukumu mawili makubwa ambayo ni:

1. Kuhamasisha vijana waone umuhimu na kuwa na ari ya kushinda mechi hiyo

2. Kuhamasisha umma uone umuhimu wa mechi hiyo na hivyo kuisaidia iweze kufuzu.

Walioteuliwa kuunda kamati hiyo ni:
1. Ridhiwani Kikwete                                    Mwenyekiti
2. Ahmed Seif (Magari)                                 Mjumbe
3. Nassoro Bin Slum                                      Mjumbe
4. Henry Tandau                                            Katibu
5. Ahmed Mgoyi                                            Mjumbe
6. Aboubakar Bakhresa                                 Mjumbe
7. Angetile Osiah                                           Mjumbe
8. Kassim Dewji                                             Mjumbe
9. Abdallah Bin Kleb                                     Mjumbe
10. Salim Said                                                Mjumbe

Baada ya kuvuka raundi mbili za kwanza bila ya kucheza mechi kutokana na wapinzani wake kujitoa, timu ya Serengeti Boys inahitaji kufanya kila iwezalo kuweza kuiondoa Congo kwenye mashindano hayo na kuweka rekodi ya kufuzu kucheza fainali hizo za Afrika ambazo pia zitatoa wawakilishi wa Afrika kwenye mashindano ya Kombe la Dunia.

Mechi za kwanza za raundi ya tatu zitachezwa kati ya Novemba 16 na 18, 2012 na mechi za marudiano zitachezwa kuanzia Novemba 30, 2012 hadi Desemba 2, 2012.


BASI LA YANGA LAPASULIWA KIOO NA MTU ALIOVAA NGUO NYEKUNDU

Basi la Yanga

BASI la Yanga limefanyiwa fujo na watu wasiojulikana, wanaosadikiwa kuwa ni mashabiki wa Simba, eneo la Kabuku, wakiwa njiani kuelekea Tanga.
Baraka Kizuguto, Ofisa tovuti wa Yanga aliye katika msafara wa timu ameiambia kitongoni mida hii kwamba, jamaa aliyerushwa jiwe alikuwa juu ya mti na limepasua kioo, ila halijajeruhi mtu.
Amesema wametoa ripoti Polisi, ingawa hawakufanikiwa kumkamata mtu kwa sababu wahusika walikuwa wamekwishakimbia baada ya tukio.
Yanga iliyoondoka leo alfajiri Dar es Salaam tayari ipo Tanga , imefikia katika hoteli ya Central City, barabara ya Nane na jioni itafanya mazoezi kwenye Uwanja wa Gymkhana.
Yanga iko Tanga kwa ajili mchezo wao wa mwisho wa mzunguko wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya wenyeji Coastal Union kwenye Uwanja wa Mkwakwani, Tanga Jumapili.
Yanga imepania kushinda mechi hiyo ili kujiweka katika mazingira mazuri katika msimamo wa Ligi Kuu, ambayo mzunguko wake wa pili utarejea Januari mwakani.
Yanga ilifanya mazoezi yake ya mwisho kwenye Uwanja wa sekondari ya Loyola, Mabibo, Dar es Salaam jana na wachezaji wake wote wapo vizuri, chini ya kocha wake Mholanzi, Ernie Brandts.
Wchezaji wa Yanga wamepania kuvunja rekodi ya Coastal Union kutofungwa kwenye Uwanja wao wa nyumbani, Mkwakwani, Tanga katika mechi hiyo.
Akizungumza na kitongoni kwa niaba ya wenzake mapema wiki hii, Nahodha Msaidizi wa Yanga, Nadir Haroub Ally ‘Cannavaro’ alisema kwamba wanataka kustawisha uongozi wao katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa kuwafunga Coastal Jumamosi.
Alisema wanajua Coastal ni timu nzuri na wanatarajiwa upinzani katika mechi hiyo, ila ameonya Yanga ya sasa ni tishio na wachezaji wako vizuri ‘ile mbaya’.
“Kwa kweli mimi na wachezaji wenzangu tunamshukuru mwalimu mpya (Ernie Brandts) kwa kutupa vitu vipya na muhimu. Timu yetu imebadilika na kila mtu anaona sasa. Wale Coastal si hawafungwi kwao wale, sasa sisi tutaenda kuwafunga pale pale, tena kipigo kikali,”alisema.
Lakini pia habari za ndani kutoka Yanga zinasema kwamba tayari wachezaji wameahidiwa donge nono iwapo watashinda mechi hiyo.
Wachezaji hao, walizawadiwa Sh. Milioni 15 kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Azam FC mwishoni mwa wiki katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo, uliifanya Yanga iongoze Ligi Kuu kwa kufikisha pointi 26, ikiwa imebakiza mechi moja ya mzunguko wa kwanza dhidi ya Caostal Union mjini Tanga, ikifuatiwa na Simba SC yenye pointi 23, ambayo juzi imefungwa 2-0 na Mtibwa Sugar mjini Morogoro.

Thursday, November 8, 2012

AZAM YASIMAMISHA WACHEZAJI BAADA YA KIPIGO CHA SIMBA

Azam imeonekana kuingia katika mgogoro na wachezaji wake mahiri kwa madai kuwa walipewa pesa ili kuihujumu timu yao ili ifungwe na simba. Timu hiyo ilifungwa 3 kwa 1 na simba. Wachezaji walio simamishwa ili kupisha uchunguzi ni 1. Erasto Nyoni 2. Said Moradi 3. Deograatius Munishi a.k.a Dida

MAHAKAMA KUU YATOA UAMUZI KESI YA LEMA

IMG-20121108-WA0007
IMG-20121108-WA0006
Baadhi ya wananchi, wapenzi wa Chadema wakimlaki Mh Lema mara baada ya kuwasili katika viwanja vya mahakama.
IMG-20121108-WA0004
Jopo la Majaji likiwa tayari kuanza kazi
IMG-20121108-WA0003Kutoka kushoto, Henry Kileo, Nuru Ndosi na Mh Godbless Lema
IMG-20121108-WA0002Henry Kileo akiwa ndani ya ukumbi wa Mahakama Kuu, Dar es Salaam
IMG-20121108-WA0005Katibu wa Chadema Kanda ya Kinondoni, Henry Kileo (kushoto) akibadilishana mawazo na mdau wa Chadema mara baada ya kuwasili viwanja vya Mahakama Kuu
IMG-20121108-WA0008
IMG-20121108-WA0009
Wananchi na viongozi wakiingia kuandikisha chumba cha mapokezi katika Ofisi ya Chadema Kinondoni, Dar es Salaam.
IMG-20121108-WA0010Picha tatu za mwisho, baada ya shauri kuamuliwa, Mh Lema akiwashukuru wananchi waliojitokeza katika ya ofisi ya Chadema  Kinondoni Jijini Dar es Salaam.
Pingamizi lililowekwa na upande wa wajibu rufani kupitia Wakili wao Alute Mughwai  ili rufaa ya Lema kupinga kuvuliwa ubunge isisikilizwe limetupiliwa mbali na Mahakama ya Rufaa baada ya kuridhika kwamba kosoro zilizolalamikiwa zilikuwa kwa upande wa Mahakama.
Pia kifungu kilichomhukumu Lema kina makosa hivyo kesi itatajwa tena baada ya siku 14 kwa ajili ya kuendelea kusikiliza hoja za walio kata rufaa.



Wadaiwa kwenye shauri hilo ni wanachama watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mussa Mkanga, Agness Mollel na Happy Kivuyo, waliofungua shauri lililotengua ubunge wa Lema wakidai kuwa wakati wa kampeni alimdhalilisha mgombea wa CCM, Dk. Batilda Burian kwa kutumia lugha za matu
Lema anawakilishwa na Wakili Method Kimomogoro, anayesaidiana na Tindu Lissu.


HATIMAYE DIRECTOR WA FILAMU YA KUMKASHIFU MTUME AHUKUMIWA

.
The man behind an anti-Muslim film that led to violence in the Middle East has been sentenced to one year in prison.
Mark Basseley Youssef, 55, was sentenced on Wednesday for violating probation stemming from a 2010 bank fraud conviction.
US District Court Judge Christina Snyder handed down the sentence after Youssef admitted four of eight alleged violations including obtaining a fraudulent California driver’s licence.
Youssef served most of a 21-month prison term in the bank fraud case. Federal authorities wanted Youssef to serve two years for the violations.
After he was released from prison, Youssef was barred from using computers or the Internet for five years without approval from his probation officer.
None of the violations had to do with the content of “Innocence of Muslims,” a film that depicts Mohammad as a religious fraud, pedophile and a womaniser.
The movie sparked violence in Libya and other parts of the Middle East, killing dozens. Enraged Muslims had demanded severe punishment for him, with a Pakistani cabinet minister even offering $100,000 to anyone who kills him.
Federal authorities have said they believe Youssef is responsible for the film, but they have not said whether he was the person who posted it online.
He also was not supposed to use any name other than his true legal name without the prior written approval of his probation officer.
At least three names have been associated with Youssef since the film trailer surfaced – Sam Bacile, Nakoula Basseley Nakoula and Youssef. Bacile was the name attached to the YouTube account that posted the video.
Court documents show Youssef legally changed his name from Nakoula in 2002, though when he was tried, he identified himself as Nakoula. He wanted the name change because he believed Nakoula sounded like a girl’s name, according to court documents.

Tuesday, November 6, 2012

HII NDIO SIRI NDANI YA SIMBA



Kipa wa Simba,Juma Kaseja.

KOCHA MKUU wa Simba, Milovan Cirkovic ameapa kuendelea kumtumia kipa Juma Kaseja mechi zote huku bosi wa makipa, James Kisaka naye akiweka wazi hali ya mambo na kilichotokea Simba ikaondoka kileleni mwa Ligi Kuu Bara.

Milovan ametamka hivi: "Sijui kitu gani tumekutana nacho maana tunarekebisha makosa kwenye mazoezi wakiingia uwanjani kwenye mechi wanarudia tena, nashindwa kuelewa."

Lakini Kocha wa Makipa, Kisaka amesema bao alilofungwa, Juma Kaseja na Hussein Javu wa Mtibwa Sugar na timu yake kulala mabao 2-0 juzi Jumapili ni makosa yake na sasa kazi aliyonayo ni kurudisha imani kwa mashabiki wake ingawa amesisitiza hajashuka kiwango na kuwataka mashabiki wakumbuke fadhila.

Milovan amesema ataendelea kumtumia kwenye kikosi chake kwa sababu anaamini ndiye kipa bora zaidi ya wote. Kisaka amesema kutokana na uzoefu wake na idadi ya mabao 10, Kaseja aliyofungwa katika mechi za Ligi Kuu Bara ni uzembe wa mabeki na makosa ya kawaida.

"Wanaposema, Kaseja ameshuka kiwango siyo kweli kwa sababu aina ya mabao aliyofungwa si makosa yake ni safu nzima ya ulinzi. Kwanza Simba ilikuwa na tatizo la beki, mabao yaliyofungwa yalikuwa yanasababishwa na beki. Pili, kumekuwa na makosa ya kutoelewana kwa safu nzima ya ulinzi," alisema Kisaka.

"Lakini hili la pili tulilofungwa na Mtibwa linaweza kuwa ni makosa yake kwa sababu alienda kucheza mpira kwa kupiga chenga na adui akatumia udhaifu mwanya huo kumnyang'anya na kufunga.

"Unajua mashabiki wamekuwa wakisubiri kuona ubaya tu wazungumze na hawakumbuki fadhila ambazo Kaseja alizifanya kwa kipindi chote cha ushindi. Kaseja alifanya juhudi binafsi tukashinda beki ilikuwa haieleweki lakini hilo hawajui na kuangalia kosa hili la leo na kumpa wakati mgumu kufanya kazi ya ziada ili kurudisha imani kwa mashabiki wake.

"Naamini, Kaseja ndiye kipa bora zaidi ya wote kikosini ndiyo maana nampa nafasi ya kudaka mechi zote, makosa yanatokea ni hali ya kawaida hata hivyo nitaendelea kumtumia kwenye mechi zangu," aliongeza Milovan.
Hata hivyo, Kaseja aliyekuwa katika wakati mgumu na huzuni, aligoma kuzungumza lolote.

Matokeo hayo ambayo yaliipa Yanga mwanya wa kuongoza ligi yalimtoa machozi Kaseja haswa baada ya mashabiki kuonyesha kutokuwa na imani naye na kumuimbia nyimbo za kumdhihaki.

Hali halisi
Kwa mujibu wa duru za ndani ya Simba, uwezekano wa Milovan kukaa benchi la ufundi kwenye mzunguko wa pili wa ligi ni mdogo kwa kuwa hajatimiza malengo ambayo uongozi ulimtaka kushinda mechi zote nne dhidi Azam, Polisi Morogoro, Mtibwa na Toto African.

Aliishinda Azam mabao 3-1, akatoa suluhu na Polisi kabla ya kufungwa mabao 2-0 na Mtibwa juzi Jumapili na Jumapili ana kibarua cha Toto jijini Dar es Salaam.

Msimu uliopita Moses Basena alitimuliwa Simba baada ya kumaliza mzunguko wa kwanza akiwa na pointi 28 wakati Milovan akishinda mechi ya mwisho atamaliza na 26.

Habari zinapasha kuwa viongozi wa juu wa Simba jana Jumatatu walijadiliana hali ya mambo ingawa hawakutaka kutoa ufafanuzi wowote.

Hali ya kutoaminiana na pia kutopendana kwa baadhi ya wachezaji, chokochoko za ndani ya uongozi imedaiwa kuwa ni chanzo cha matokeo hayo ingawa wachambuzi wa mambo wanaeleza sare za Simba ni kutokana na uchakavu wa viwanja na morali ndogo ya timu.

Simba imetoka suluhu mechi mbili za Tanga dhidi ya Coastal Union na JKT Mgambo, kabla ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu dhaifu na inayochukia kushinda mechi ya Polisi Morogoro na juzi juzi huko huko Morogoro ikapigwa mabao 2-0 na Mtibwa.

Habari za ndani zinadai baadhi ya wachezaji wamekuwa wakiogopana kwa imani za kishirikina na wengine hawaongei kabisa wala kupeana pasi uwanjani.

Habari zinadai pia hata kucheza mechi nyingi kwa Kaseja peke yake hakuwafurahishi baadhi ya wachezaji ambao wanadai amechoka ndiyo maana inafika wakati anafungwa magoli laini ambayo Wilbert Mweta asingefungwa.

Suala la Kaseja limeonekana gumu kwani viongozi pamoja na makocha wanamkubali mno na wala hawana mpango wa kumweka benchi licha ya kelele za wanachama.

Jingine kubwa ni kwamba baadhi ya wachezaji wanadai kocha Milovan anaingiliwa na baadhi ya viongozi ambao wanamlalamikia kwa kutotoa nafasi kwa wachezaji wengi vijana na badala yake kuendelea kung'ang'ania walewale.


KATIBU WA MUFTI ZANZIBAR AMWAGIWA TINDIKALI

Watu mbalimbali wakiaangalia Katibu wa mufti Zanzibar Fadhili Soraga akipelekwa Hospitali baada ya kumwagiwa Tindikali na watu wasiojulika. Katibu alikuwa akifanya mazoezi kwenye viwanja vya mwanakwerekwe

Hapa akipelekwa kwenye chumba cha huduma ya kwanza hospitali ya mwanakwerekwe

Hapa akipandishwa kwenye gari ili awahishwe Muhimbili Hospital dar es Salaam


 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU