Facebook Comments Box

Thursday, October 4, 2012

BAADA YA RAFU MBAYA YA BOBAN, YONDANI AANZA MATIBABU MUHIMBILI (MOI)



Mlinzi wa kati ya timu ya Young Africans, Kelvin Yondani
























Mlinzi wa kati wa kutumainiwa wa klabu ya Young Africans na timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Kelvin Yondani anaendelea vizuri mara baada ya kuanza kupata matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kitengo cha mifupa MOI jijini Dar es salaam.
Daktari wa timu ya Young Africans Dokta Suphian Juma, amesema Yondani alipata mshtuko katika mfupa wake mkubwa, baada ya kuchezewa vibaya na kiungo wa timu ya Simba Haruna Moshi 'Boban'.
Dr Suphian anatoa wasi wasi wapenzi na washabiki wa Young Africans, kwamba Yondani anaendelea vzuri na anatazamiwa kurudi dimbani baada ya wiki mbili. 'Unajua Yondani baada ya kukanygwa na Boban alipata mshituko katika mfupa wake mkubwa mguuni, hivyo anapata matibabu ya kumrejesha katika hali yake ya kawaida.
Katika hali ya kushangaza mwamuzi wa mchezo huo wa watani wa jadi, Mathew Akrama alishindwa kumonyesha kadi nyekundu Boban kwa mchezo mbaya uliopelekea Yondani kutolewa nje na kushidwa kuendelea na mchezo.
Mechi hiyo ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyowakutanisha watani wa jadi wakongwe Afrika Mashariki iliishia kwa sare ya mabao 1-1, mabao yaliyofungwa na Amri Kiemba Simba dakika ya 4 na Said Bahanunzi aliyesawazisha kwa upande wa Young Africans dakika ya 67.
Young Africans leo imeendelea na mazoezi katik uwanja wa shule ya sekeondari ya Loyola kujiandaa na mchezo unaofuata dhidi ya timu ya Kagera Sugar, mchezo utakaofanyika siku ya jumapili katika uwanja wa kaitaba mjini Bukoba.

RAFU MBAYA YA BOBAN YAMPELEKA YONDANI HOSPITALI


Yondan wa pili kutoka kulia waliosimama katika kikosi cha Yanga jana
BEKI Kevin Yondan wa Yanga hajaamka mazoezini leo, kutokana na kuumizwa vibaya na kiungo wa Simba, Haruna Moshi ‘Boban’ katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga wapo Uwanja wa sekondari ya Loyola, Mabibo hivi sasa wakifanya mazoezi, lakini Yondan anajiandaa kwenda hospitali kufanyiwa uchunguzi wa maumivu yake.
Habari kutoka Yanga, zimesema kwamba tangu jana beki huyo anasikia maumivu makali na hatima yake itajulikana baada ya vipimo hivyo.
Yanga jana ilitoka nyuma na kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na wapinzani wao wa jadi, Simba SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, uliopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, kuanzia saa 1:02 usiku.
Habari kutoka ndani ya Simba, zimesema kwamba wachezaji waliahidiwa asilimia ya 60 ya mgawo wa timu kutokana na mapato ya milangoni na asilimia 20 ya kiwango hicho kuongezwa na Friends of Simba, lakini kwa sare hiyo, ahadi hiyo imeota mbawa.
Hata hivyo, uongozi wa Simba unafikiria kuwapa ‘kifuta jasho’ wachezaji wake kwa angalau kulinda hadhi ya klabu kwa kutokubali kufungwa na wapinzani wao hao wa jadi jana.
Yanga ambao walimaliza mechi hiyo wakiwa pungufu baada ya Simon Msuva kutolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 77 kwa kumrudishia rafu Juma Nyosso, ndio waliohaha kusawazisha bao, baada ya kutanguliwa kwa bao la mapema la kiungo Amri Kiemba.  
Hadi mapumziko Simba walikuwa tayari mbele kwa bao 1-0, lililotiwa kimiani na kiungo Amri Kiemba dakika ya pili.
Simba walicheza vizuri kipindi chote cha kwanza wakigongeana pasi za uhakika na kuwazidi kasi uwanjani wapinzani wao, wakati Yanga pamoja na kuzinduka baada ya kufungwa bao, lakini makosa yalikuwa mengi.
Pasi zao zilikuwa nyingi hazifiki, walikuwa wanapokonyeka mipira kirahisi, wanazidiwa nguvu na wapinzani wao katika kugombea mipira na hata mashambulizi yao hayakuwa ya mpangilio, zaidi ya kuonekana kubahatisha zaidi.
Katika kubahatisha huko, Mbuyu Twite alifumua shuti zuri dakika ya 38 kutoka wingi ya kulia, ambalo lilitoka nje sentimita chache.    
Kabla hata ya dakika 45 za kipindi cha kwanza kumalizika, kocha Mholanzi Ernie Brandts alimtoa Hamisi Kiiza na kumuingiza Frank Domayo ili kuimarisha safu ya kiungo, ambayo ilionekana kuzidiwa na Simba inayofundishwa na Mserbia, Milovan Cirkovick.
Kipindi cha pili, Yanga walianza na mabadiliko, kocha Ernie Brandts akimtoa kiungo Nizar Khalfan na kumuingiza mshambuliaji Didier Kavumbangu, ambaye alikwenda kuongeza nguvu ya safu ya ushambuliaji ya timu hiyo.
Angalau, kipindi cha pili Yanga walionekana kucheza vizuri na kupeleka mashambulizi yenye uhai langoni mwa Simba, ingawa safu imara ya ulinzi ya Wekundu wa Msimbazi ilikuwa kikwazo.
Katika dakika ya 63, beki Paul Ngalema aliunawa mpira katika harakati za kuokoa na refa Mathew Akrama akaamuru penalti, ambayo ilikwamisha kimiani kiufundi na Said Bahanuzi ‘Spider Man’.
Katika dakika ya 77 Mathew Amkrama alimtoa nje kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja Simon Msuva, baada ya kumkita Juma Nyosso, aliyemkanyaga ‘kwa bahati mbaya’. Msuva alichezewa rafu na Nyosso na tayari refa alikwishapuliza filimbi na kumpa kadi ya njano beki huyo wa Simba, lakini kiungo huyo wa Yanga akaponzwa na hasira za kitoto.
Pamoja na Yanga kubaki pungufu, waliendelea kucheza vema na mashambulizi yalikuwa ya pande zote mbili. Refa Akrama alishindwa kuumudu mchezo na maamuzi yake mengi yalikuwa chungu kwa Yanga, mfano Haruna Moshi ‘Boban’ alipomchezea rafu mbaya beki Kevin Yondan hadi akashindwa kuendelea na mchezo, na nafasi yake ikachukuliwa na Juma Abdul alimpoza kwa kadi ya njano.
Hakumchukulia hatua yoyote kipa Juma Kaseja aliyeonekana kupoteza muda tangu mwanzo, na alimpa onyo tu zaidi ya mara tatu.
Alipingia Abdul alikwenda kucheza beki ya kulia na Mbuyu Twite akahamia katikati kucheza na Nadir Haroub ‘Cannavaro’.
Baada ya mchezo huo, kocha wa Simba, Milovan alisema kwamba ulikuwa mchezo mzuri na Yanga walicheza vizuri, lakini timu yake ilicheza vizuri na anajivunia. Alisema Yanga imeimarika tofauti na ilivyokuwa awali na kwamba hizo ni dalili Ligi Kuu msimu huu itakuwa ngumu.
Kwa upande wake, kocha wa Yanga, mwanzoni hawakucheza vizuri, lakini baadaye walitulia na kucheza vizuri. “Hii ni mechi ya kweli ya upinzani, unaweza kuona rafu na kadi nyingi,”alisema Brandts.
Kwa matokeo hayo, Simba imefikisha pointi 13, ndani ya mechi tano na kuendelea kuongoza Ligi Kuu, wakati Yanga imefikisha pointi nane na kubaki nafasi ya tano, kwani Coastal Union imetoa sare ya 2-2 na JKT Oljoro mjini Arusha na kufikisha pointi tisa.   
SIMBA: Juma Kaseja, Nassor Chollo, Paul Ngalema, Juma Nyosso, Shomary Kapombe, Jonas Mkude/Haruna Moshi, Amri Kiemba, Mwinyi Kazimoto, Felix Sunzu, Edward Christopher/Daniel Akuffo na Mrisho Ngassa.
YANGA: Yaw Berko, Mbuyu Twite, Stefano Mwasyika, Nadir Cannavaro, Kevin Yondan/Juma Abdul, Athumani Iddi, Simon  Msuva, Haruna Niyonzima, Said Bahanuzi, Hamisi Kiiza/Frank Domayo na Nizar Khalfan/Didier Kavumbangu.


KIBONZO CHA LEO




HUU NDIO UDHAIFU MWINGINE WA TFF

Pichani ni sehemu ya paa la chumba cha habari cha chama cha mpira wa miguu Tanzania (TFF),ambacho kinatumika kukutana na Wanahabari wa vyombo mbalimbali kuhusiana tasnia ya michezo kwa madhumuni ya kuihabarisha jamii.Kwa wanahabari za Michezo naamini kabisa mtakubaliana na mimi kuhusiana na hali iliyopo ndani ya ofisi hiyo,ambayo kimsingi nayo una umuhimu wake mkubwa,lakini imetelekezwa kama hivyo.
Chombo cha kutoa ubaridi ambacho kiliwekwa angalau kupunguza joto la Daslam ofisini humo,lakini kwa sasa ndege wamepata mahala pa kujipumzikia na kuzaliana,lakini sio ishu.
Taa nazo ziko hoi zinaning'inia tu, jambo ambalo ni hatari kwa usalama wa watu.
Baadhi ya Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakisubiri wahusika wa TFF, kukutana na Wanahabari hao kwa ajili ya kuwapa taarifa mbalimbali za michezo, ili jamii ihabarishwe.
Dude la kuwekea Maji ya Kunywa ambalo sijui kwa mara ya mwisho lilitumika lini,kwani limejaa vumbi, haliangaliwi tena.



HII NDIO MBINU MPYA YA KUTOROSHA MADINI

WIZARA ya Nishati na Madini imegundua ‘madudu’ katika sekta ya madini, ikiwamo utoroshaji wa madini ya tanzanite kwa punda na ukwepaji mkubwa wa kodi unaofanywa na kampuni za migodi nchini.

Kutokana na hilo, imefanya marekebisho ya mifumo ya ulipaji kodi iliyowezesha kulipwa kwa baadhi ya madeni na imetangaza Mtanzania yeyote, ikiwamo mfanyakazi wa mgodi atakayetoa taarifa za utoroshaji wa madini, atapewa asilimia 30 ya thamani ya mzigo utakaokuwa umetoroshwa.

Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Masele alisema hayo jana Dar es Salaam alipozungumza katika uzinduzi wa Kitabu cha Ripoti inayohusu Haki za Binadamu katika Kazi, Biashara, Mazingira, Ardhi, Ulinzi na Haki ya Mlaji.

Hafla hiyo iliandaliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na yeye alikuwa mgeni rasmi.

Akizungumza kabla ya uzinduzi wa ripoti hiyo iliyoelezea ukiukwaji mkubwa wa haki za wafanyakazi katika kampuni za madini nchini na uharibifu wa mazingira uliobainika, Masele alikubaliana nayo na kueleza jinsi Serikali ilivyojipanga kukabiliana na kadhia hiyo.

“Kuna ‘madudu’ mengi na makubwa yanafanyika, rasilimali za nchi hii zinatoroshwa na kuyeyuka, tumegundua kule Manyara madini pekee yanayopatikana Tanzania tu ulimwenguni kote-tanzanite yanatoroshwa kwa punda, hii haiwezekani kukaa kimya, wezi wa mali zetu ni Watanzania wenyewe, tubadilike,” alisema Masele na kuongeza: “Kuna watu wanapewa asilimia 10 ya madini yanayotoroshwa, tumegundua hilo pia sasa tumesema mwananchi au mfanyakazi atakayegundua utoroshaji na kutoa taarifa kwetu, tutampa asilimia 30 ya fedha ambayo ni thamani ya mali aliyookoa”.

Akisisitiza ukwepaji kodi, alisema: “Tena nitoe onyo kwa kampuni zinazokwepa kodi na kukiuka haki za binadamu hasa katika sekta inayosimamiwa na wizara yetu, waache mara moja maana kuna mapinduzi makubwa yanafanyika sasa na hatutasita kuyafutia leseni mara moja”.

Masele alisema walibaini kampuni zote za madini nchini zikikwepa baadhi ya kodi kupitia uandikaji wa nyaraka zao na sasa wamezibaini na kuanza kulipa madeni hayo.

Alitoa mfano kampuni ya Barrick katika ukokotoaji wa hesabu, ilibainika kuwa na deni la zaidi ya Sh bilioni 5.6 na hadi sasa imelipa Sh bilioni 2.3; nyingine ni TanzaniteOne inayodaiwa zaidi ya dola za Marekani milioni 2.5.

“Kampuni ya Geita Gold Mine (GGM) ilikuwa inadaiwa zaidi ya dola milioni 1.4 ambazo sasa imeanza kuilipa Halmashauri ya Geita, niseme tu kuna mapinduzi makubwa na tunaamini Watanzania wako nyuma yetu hatuogopi,” alisema Masele.

Kuhusu TanzaniteOne, alisema leseni yake imekwisha tangu Agosti na Serikali imesitisha kuipa leseni nyingine mpaka mpango wa kurejesha asilimia 50 ya hisa serikalini ili kuondoa umiliki binafsi uliopo sasa na masuala mengine ya utendaji vitakapokaa vizuri.

Alisema katika kuhakikisha kuna usimamizi mzuri wa kodi na rasilimali za madini, mafuta na gesi nchini, Wizara inafanya mapinduzi makubwa katika taasisi zake kwa kufumua Bodi, kupanga mifumo na kuongeza nguvu ya kiutendaji ya rasilimali watu.

Masele alisema miongoni mwa Bodi zitakazofumuliwa ni pamoja na ya Shirika la Madini la Taifa (Stamico) ili kuongeza usimamizi katika sekta ya madini, pia itafanya marekebisho makubwa ya utendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na Shirika la Maendeleo ya Mafuta (TPDC).

Alisema lengo la wizara ni kutekeleza malengo ya kiuchumi ya mwaka 2020 hadi 2025 ya nchi kuwa katika uchumi wa kati kwa kutumia rasilimali zake hasa madini, gesi na mafuta na kusisitiza kuwa hawataacha kuwachukulia hatua wezi wa rasilimali, waharibifu wa mazingira na ardhi.

Alitumia fursa hiyo kuwahakikishia wanaharakati wa haki za binadamu, kwamba Serikali inawatambua na haipingi kukosolewa, lakini kwenye pongezi ipewe, huku akiwahakikishia kuwa utafiti wao ni moja ya zana za kuendeleza utendaji unaoendelea hivi sasa katika sekta mbalimbali.

Mkurugenzi wa LHRC, Dk Hellen Kijo-Bisimba aliishukuru Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini kwa kuonesha matumaini mapya kwa wananchi, hasa usalama wao katika maeneo ya kazi kwenye migodi na kampuni za uwekezaji.

Kuhusu ripoti ya utafiti, Kijo- Bisimba alisema utafiti ulifanyika nchi nzima na kugundua ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu kwa wafanyakazi wa migodini, ujira mdogo na usalama kazini, uharibifu wa mazingira na ardhi.

“Ilizoeleka katika nchi nyingi, kwamba walaumiwa wa ukiukaji wa haki za binadamu ni Dola, lakini sasa hali hiyo imebadilika, sekta binafsi inashiriki katika ukiukaji wa haki za binadamu kupitia mifumo yao ya utendaji na kukwepa kulipa kodi,” alisema Dk Kijo-Bisimba.

Akitoa takwimu, Wakili na Mratibu wa Uwajibikaji wa Kampuni na Mazingira wa LHRC, Flaviana Charles alisema wafanyakazi asilimia 15.77 waliohojiwa walikiri kuwapo na ukiukwaji wa haki za binadamu migodini na ujira mdogo, hakuna haki ya kujumuika (kuwa na vyama vya wafanyakazi).

“Pia asilimia 28.22 ya kampuni hazina sera ya kuzuia ajira kwa watoto na asilimia 4.62 ya kampuni hazishirikishi wananchi kuchukua ardhi ya uwekezaji, pia watu hawajui haki zao wanapouziwa bidhaa bandia,” alisema Charles.

LHRC waliiomba Serikali kuhakikisha pia kuwa familia 20 zinazoishi katika mahema Geita zilizopisha mradi wa GGM, zinajengewa nyumba. Naibu Waziri Masele alisema tayari GGM imekubali kujenga nyumba hizo.

Kwa mujibu wa LHRC, utafiti huo ni wa kwanza wao kuufanya nchini kuhusu masuala ya haki za wafanyakazi, mlaji, ardhi, mazingira na ulinzi.



PINI JIPYA LA LINNAH




VODACOM WAZINDUA HUDUMA YA BIMA KWA NJIA YA SIMU

.
.
.
.
Taarifa kwa vyombo vya habari.
Watanzania sasa kupata Bima kupitia huduma ya M–Pesa.
  • Ni ushirikiano kati ya Vodacom na Heritage Tanzania kuzindua bima ya Faraja, Bima ya mazishi na ajali.
  • Wateja kununua na kulipia Bima kupitia M-Pesa.
  • Huduma ya bure kutolewa kwa wateja watakaolipia huduma mara kumi kwa Mwezi.
Dar-es salaam, Octoba 3, 2012 … Huduma ya Vodacom ya M-Pesa imezidi kupiga hatua baada ya kuwawezesha Watanzania kufanya malipo yao ya bima kupitia huduma hiyo.
Hii inafuatia ushirikiano kati ya Vodacom Tanzania na Heritage Tanzania kuzindua Bima ya Faraja, ambayo ni Bima ya mazishi ambayo inamuwezesha mlengwa kulipwa fedha taslim za mazishi kwa muhusika mwenye bima. Bidhaa mbalimbali ziko katika mpango huo ili kukidhi mahitaji ya wateja na bajeti ya malipo ya kila mwezi kuanzia shilingi 20000/= fadi 9800/= kwa Mwezi.
Mteja ana chaguo la kuongeza malipo kwa kuongeza huduma ya vifo vinavyotokana na ajali kulingana na faida na sera zao. Ongezeko hili la ziada litaongeza kiasi cha faida mara tatu kwa ongezeko dogo la malipo.
Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania, Rene Meza, amesema wateja wa Vodacom wanaotumia M-Pesa, wataweza kujipatia bima ya bure kwa mwezi.
“Wateja wetu wote ambao watafanikiwa kutuma pesa walau mara 10 kwa Mwezi watapata  bima ya bure ya kiasi cha Shilingi laki mbili kwa mwezi unaofuata,” amesema Meza.
Suala la kipekee katika huduma hii ni kwamba hakuna haja ya kujaza fomu ili kujiunga na bima hii. Mteja atajiunga kwa njia rahisi kwa kupiga *150*00# na kuchagua kipengele cha bima. Vodacom inahakikisha kuwa wateja wote wa M-pesa wanaweza kupata huduma hii ili kuwa na amani ndani ya familia zao.
 “Ni muhimu kuthibitisha kuwa taarifa zako ni sahihi, na kuthibitisha kuwa unaelewa vigezo na masharti. Taarifa zako zitatumwa moja kwa moja kwenda Heritage Tanzania,” alisema Meza na kuongeza kuwa, “Unaweza kuchagua aina ya bima ambayo inakidhi mahitaji na bajeti yako,”
Bima hii ya Faraja pia itawawezesha kila mmoja kubadili au kuongeza kiwango chake kwa ile yenye faida zaidi kulingana na mahitaji yao na mabadiliko ya bajeti katika maisha yao.
Kwa taarifa zaidi kuhusiana na huduma mteja atapiga 0764 300001 bure au vipeperushi kutoka kwa wakala wa M-Pesa nchini.

Wednesday, October 3, 2012

MASAA MAWILI KABLA YA MECHI YA YANGA NA SIMBA HALI NDIO HII

Basi la Simba likiwa limepaki makao makuu ya Trafiki, kusubiri ulinzi kwa ajili ya kwenda kuipokea timu Bandarini, ikitokea Zanzibar


Basi la Simba likiwa limepaki makao makuu ya Trafiki, kusubiri ulinzi kwa ajili ya kwenda kuipokea timu Bandarini, ikitokea Zanzibar

Eeneo la Gerezani, karibu na BP kama unaenda Kurasini

Eneo la Gerezani, karibu na BP kama unaenda Kurasini

Jamaa amenunua na kuvaa hapo hapo jezi ya Yanga

Biashara ye jezi

Add caption

Mashabiki wa Simba wanaelekea uwanjani

Daudi Chalamila na Simba mwenzie


Barua ya Wazi kwa Waziri husika - Yah: Kudorora kwa huduma za TTCL 03/10/2012 0 Comments BARUA YA WAZI KWA WAZIRI WA MAWASILIANO NA UCHUKUZI KUHUSU KUDORORA KWA TTCL Kwa mara nyingine tena najitokeza kuweza kutoa kero ambazo zina tupata Sisi Wananchi tunao tumia huduma za TTCL Katika Mabadiliko ambayo Serikali ina himiza Wananchi katika kuingia katika Soko la Afrika Mashariki na ya Kati ni kujiendeleza kielimu lakini kuhizwa huko hakuko kwa TTCL wao bado na mfumo wa kizamani, Kwenye Umeme angalao serekari ime gundua kitu fulani kwa nini shirika hili naslo lisi chunguzwe kujua kama kuna masilahi ya watu au kukwama kwao kuna tokana na Elimu au ni watu wana kwamisha :?. Watanzania tulio kuwepo katika Utawala wa Mwalimu Nyerere tuna usemi wa kusema usiache Mbachao kwa Msala upitao. Methali hii inatubana kuitelekeza TTCL. katika Mitandao ambayo inaweza kumsaidia Mwananchi asiye na kipato ni TTCL lakini Shirika limekuwa na kiburi hata kama wateja wakilalamika Shirika la TTCL halisikii malalamiko ya wananchi. Katika kutumia huduma za Internet .wateja wanalazimika kulipa kwenye mtandao wa TTCL Shilingi 30,000 kwa Mwezi au 7000 kwa Bando na hata Shilingi 500 ili waweze kupata huduma. Cha kushangaza baada ya kulipa kwenye mtandao wa TTCL ili upate huduma unakuwa kama vile umepoteza fedha zako unaweza kuwa na kazi yhati inawezekana ika shindika kutuma yenye MB25 ukianza asubuhi ukiwa na bahati ita enda saa kumi jioni kama huna bahati ndiyo basi Kama Una Attach file MB 25 unaweza kujanza Attachment Saa 2 Asubuhi ukafanikisha saa 9:00 Alasiri au ikakata. Ukiingia kwenye Mtandao mwingine Attachment hiyohiyo unachukua dakika 2 – mpaka dakika 5. Je! TTCL ina Wataalamu waliobobea ni vipi ishindwe kuweka Mazingira mazuri kwa wateja wao. Wafanya kazi wa TTCL ambao hawakutaka Majina yao yatajwe wamedai wameweza kutoa Taarifa ya Malalamiko ya Wananchi hakuna kiongozi wa juu anaye tilia maanani malalamiko hayo. Cha msingi kinachoonekana kwa TTCL badala ya kuboresha huduma wao wanawaza kuuza mali za TTCL kama walivyo fanya wilaya ya Tunduru Mkoa wa Ruvuma , Mimi ni Mteja wa TTCL toka ilipoanza . Namba yangu ya Simu 0252602425. Naishi Songea. Ningeomba Watanzania, Wananchi wanaotegemea sana Mtandao wa TTCL, endapo hali ikiendelea namna hii basi Wale wote wanao ihujumu TTCL Serikari ingeweza kuwawajibisha. Haiwezekani Mitandao mingine ifanye kazi lakini mtandao wa Serikari uhindwe kufanya kazi. By Adam Mzuza Nindi, Songea. web: Songea Habari Add Comment Mhe. Mwanjelwa na Dereva wake wapelekwa Dar es Salaam kwa tiba zaidi 03/10/2012 0 Comments Imeelezwa kuwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Viti Maalum CCM, Dkt. Mary Mwanjelwa anasafirishwa kwenda jijini Dar es Salaam kwa ajili ya huduma zaidi za kiafya baada ya kunurusika ajalini jana. Dkt. Mwanjelwa alikuwa amelazwa katika hospitali teule ya Ifisi tangu jana. Ameweza kuzungumza kwa ufasaha na kuwatambua watu aliokuwa wanaingia na kutoka kumjulia hali. Alisema, "Hali yangu ni nzuri, najisikia maumivu sehemu za kiunoni na kwenye mbavu, lakini najisikia vizuri". Nje ya wodi alimokuwa amelazwa walikuwepo baadhi ya viongozi wa CCM pamoja na wananchi waliokwenda kumjulia hali. --- picha na maelezo via Mkwinda blog na MbeyaYetu blog Dkt. Mwanjelwa akiwa hospitalini Ifisi asubuhi ya leo. (picha: Mkwinda) Mwenyekiti wa UWT Mbeya bi. Blorence Kyendesya akitoka hospitalini kumjulia hali Dkt. Mwanyelwa (picha: Mkwinda) Bi. Hilda Ngoye (CCM Viti Maalum, mkoa wa Mbeya), akiwafariji ndugu na jamaa wa Dkt. Mwanjelwa baada ya kumwona wodini (picha: Mkwinda) Dereva wa Mhe. Mwanjelwa akisubiri kusafirishwa Add Comment Posta ya Tanzania, Dar es Salaam: Mara tatu ilitosha, si hii ya nne. Hapana! 03/10/2012 2 Comments UPDATE: Ninashukuru sana kwa ushirikiano na msaada mkubwa wa kushughulikia suala hili ambao nimeupata hadi sasa kutoka kwa Niliyemtumia parcel. Anafuata kila 'step' inayotakikana. Baba, Sabato Tarimo kwa kuwasiliana na mhusika wa Bodi ambaye alifanikisha kupatikana mzigo nilioutuma ukapotea mara ya tatu. Dad, you have always been there for me in good and bad times. I will never be able to say enough THANK YOUs. Zitto Kabwe (Mb) kwa kunisikiliza niki-vent off kuhusu mkasa huu na kunipa ushauri pamoja na kuahidi kufuatilia atakavyoweza. January Makamba (Mb, Naibu Waziri) kwa kuzungumza nami na kunipa maelekezo ya nini cha kufanya na ahadi ya kufuatilia kwa kuwa tayari ilikuwa katika mipango, kwa bahati nzuri kuna na mwananchi mwingine aliwasilisha tatizo linalofahanana na la kwangu, kwa hivyo ni kama nimeongeza uzito wa kuonesha umuhimu wa kushughulikia kadhia hii. Marafiki wote wa facebook na twitter mnaonipa moyo na kuniunga mkono katika kupiga vita udokozi na huduma mbovu katika Shirika letu la Posta Tanzania, hasa mkoa wa Dar es Salaam. Ifike mahali upuuzi huu ufe! Posta ya Tanzania, here I come! Kero ya Posta Tanzania. Nimetuma parcel Tanzania (na hii si mara ya kwanza), kwa njia ya USPS Express Mail, 3-5 days delivery na mara zote ninaowatumia wanapokea kati ya siku ya 5 - 7. Hii niliyotuma tarehe 17 Septemba, 2012 aliyetumiwa hakupigiwa simu wala kutaarifiwa kwa namna yoyote kuwa parcel imefika. Baada ya zaidi ya siku 7 kupita, akaanza kufuatilia. Akipiga simu anaambiwa hatuuoni, bado haujafika. Akaamua kwenda kuwaona ana kwa ana jana, akapewa majibu yale yale. Nikamfahamisha kuwa waliwahi kunipotezea mizigo hawa kwa kauli hizo hizo, na baadaye walipopigiwa simu na "Mkubwa" wao, mzigo ulijulikana uliko ndani ya saa chache siku ile ile. Nikamfahamisha aombe kuonana na Meneja, akafanikiwa. Wakatizama parcel, computer zao (huko kwa Mameneja) zikaonesha parcel ilifika tangu tarehe 23. Meneja akaagiza watizame vifurushi ili wampatie. Kwa kuwa ilikuwa imekaribia muda wa kufunga ofisi, wakamwambia arudi kesho (yaani leo) kuuchukua, lakini kwanza apige simu asubuhi au wao watampigia utakapokuwa tayari. Akawapigia simu asubuhi, wakamwambia bado, apige saa nne. Akapiga simu saa nne, anapewa maelezo tofauti na ya jana, Meneja anamwambia kifurushi hakijapokelewa na maelezo mengine ya kuwa maelezo ya jana haikumaanisha hivyo bali vingine. Amepiga simu kutaka kutoa maelezo mwa Mkubwa wa Posta, anajibiwa kuwa hawezi kuzungumza naye suala hilo, amwambie tu aliyetuma ajaze hayo makaratasi ya USPS ya refund alipwe fidia. Nilipoandika juzi pale wavuti.com kuwa baadhi ya Wafanyakazi wa Posta ni wadokozi na waache udokozi, ni kwa sababu nimeshapata usumbufu mara tatu na sasa ni mara ya nne katika Shirika la Posta la Tanzania, EMS, mkoa wa Dar es Salaam. Mara mbili kati ya hizo parcel nilizotuma kwa njia ya kawaida hazikufika. Mara moja nilipotuma kwa njia ya USPS Express Mail waliupoteza lakini walipigiwa simu na Mr. Mndeme na ndani ya saa chache maelezo yote na ulipo mzigo vilipatikana. Hii mara ya nne, inakuwa ni mara ya pili kutuma kwa USPS Express Mail parcel inapotea na maelezo ya kufuatilia kujua ulipo ninayopewa ni hayo niliyoeleza hapo juu. Nimetaka ku-vent off kwa sasa, ila kazi ndiyo (isiyo ya lazima) ndiyo imeanza tena. Kwa bahati mbaya (au nzuri) kazi ndiyo imeanza rasmi. Posta, nina nyie, mpaka kieleweke kwangu kwa lugha yangu! YOU WILL COUGH UP TO THE LAST DIME!!! This I promise you! Here I come... 2 Comments How to disable/turn off Gmail automatic image display from senders 03/10/2012 0 Comments When you receive an email that contains externally linked images, Gmail usually doesn’t display the images automatically. This behavior is designed to help protect your privacy; if Gmail displayed the images automatically, it could potentially allow the sender of the email to track and see that the images are being fetched, and therefore know when you’ve read their message. But, if someone you've sent email at least twice sends you a message with images in it, you’ll see the image by default (because the people in this group are likely people you know and trust). Gmail will only show images in messages that are authenticated, so you won't have to worry about seeing images in messages where the sender's name or address is spoofed. If you’d like, though, you can change your settings so that images from these senders won’t be shown by default either. Here’s how: ALTERNATIVE I While signed on in your Gmail account, Click the gear icon (see the circle in the scree-shot below) in the upper right, then from the drop down menu, select Settings. In the External content section, select Ask before displaying external content. Click Save Changes. Picture ALTERNATIVE II While signed on in your Gmail account, Click on the down facing arrow on the left, just after the the senders' name (see the red circle in the screen-shot below). A small window opens, look at the bottom to see highlighted words reading, “Don’t display image from now on.” and click on them (see the words in ellipsis illustrated in the screen-shot below). Picture You are done. There is nothing more into it, really. You can reverse and display the images in the future by following above steps, this time clicking to re-enable image display. Add Comment WaHasira: Infakti, hawa si wanangu, lakini... 03/10/2012 0 Comments Picture sidymic.blogspot.com Add Comment “Sisubiri ruhusa ya mtu yeyote, nani asiyejua kuwa Chenge ni mtuhumiwa?” 03/10/2012 1 Comment Uchaguzi unaoendelea ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) umeelezwa kuwa utabiri mwema kwa chama hicho kuelekea Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 kutokana na kuingiza sura mpya huku vigogo wakibwagwa. Aidha, baadhi ya waliong’ara katika uchaguzi huo wametabiriwa neema kushika nafasi za juu katika Serikali ukiwamo urais mwaka 2015 ikiwa watakuwa tayari kusafisha madoa waliyonayo. Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala, Dk Benson Bana aliliambia gazeti hili jana kuwa CCM imedhihirisha ni chama dume, chenye demokrasia na ukomavu kisiasa. Akifafanua, alisema: "Uchaguzi unadhihirisha wazi kuwa CCM bado inadunda na dhana ya kujivua gamba inatekelezwa, watu zaidi ya 5,000 walipitishwa Dodoma huku sura mpya zikijitokeza, miongoni mwao ni vijana, wazee hata wakulima". Dk Bana alisema hatua hiyo imedhihirisha mianya ya rushwa kudhibitiwa ndani ya chama hicho, baada ya kuona magwiji wa siasa akiwamo Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye, wakiangushwa, jambo linaloashiria hakubaliki kuwania urais. "Hakuna asiyejua mbio za Sumaye kutaka urais, sasa kama jimbo la Hanang watu wachache wamekukataa, si rahisi Watanzania wakupe urais, namshauri sasa arejee kutumika katika nafasi yake ya siasa kama Waziri Mkuu mstaafu, maana Watanzania wameamua kufanya mabadiliko," alisisitiza Dk Bana. Kuhusu madai hayo, alipoulizwa Sumaye jana, alisema, "najua unataka habari ya uchaguzi, sasa hivi sisemi lolote ila nitakuja Dar es Salaam kati ya siku mbili au tatu hivi, utaniuliza na hilo swali lako nitakapozungumza nanyi waandishi wa habari." Akizungumzia harakati za urais mwaka 2015 kutokana na uchaguzi huo wa CCM, Dk Bana alisema CCM itang’ara katika uchaguzi ujao ikisimamia mweleko wa sasa, lakini hatima yake imesimama katika mambo mawili; Katiba mpya na uteuzi wa atakayepeperusha bendera kuwania urais. "Uchaguzi 2015 tutarajie mambo makuu mawili; Katiba mpya ndio pekee itatoa mwelekeo wa kitakachotokea, lakini pia CCM inateua nani kuwania urais wakati huo, hii itabadili mtizamo wa siasa, wakiteua vizuri, watawafunika wapinzani," alisisitiza Dk Bana. Dk Bana alivunja ukimya na kueleza wazi kuwa, hivi sasa ndani ya CCM kuna mtu anayenukia urais, ila bado ana madoa anayopaswa kuyasafisha ili akubalike. Alimtaja mtu huyo kuwa ni Waziri Mkuu wa zamani ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa. Hata hivyo, Dk Bana aliitaka CCM iwaadabishe baadhi ya wanachama, baadhi ni viongozi wa nchi akiwamo Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mbunge wa Urambo Mashariki, Samuel Sitta na Peter Kisumo (Mdhamini wa CCM) kwa alichodai, wanazungumza bila kufuata utaratibu. "Hawa wana kambi zao ndani ya chama, wanataka kumvuruga Katibu Mkuu Mukama (Wilson) kwa kauli zao, wasipewe nafasi waadabishwe kurejesha nidhamu," alihimiza Dk Bana aliyekuwa akitoa maoni yake kuhusu uchaguzi unaoendelea CCM. Akijibu tuhuma hizo jana, Sitta alisema: "Nimezoea, kauli zangu hazijawahi kuwafurahisha hata siku moja mafisadi, nataka wajue hivi; nitazungumza mpaka tone la mwisho la pumzi yangu, nimefundishwa kukemea maovu na Baba wa Taifa (Mwalimu Julius Nyerere)". Sitta alijigamba kuwa, alijiunga na TANU Oktoba 3, 1960 akiwa kidato cha tatu na sasa ni miaka 52 ndani ya chama, hajavunja utaratibu wowote katika kukemea maovu na wanaotaka anyamaze, anawakera kwa kuwa amewagusa. "Sitachoka kusema mafisadi, maana wanaharibu nchi yetu, hata Ilani ya chama inanilinda nikemee maovu, sisubiri ruhusa ya mtu yeyote, nani asiyejua kuwa Chenge (Andrew-Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM) ni mtuhumiwa, haiingii akilini eti amepita bila kupingwa Bariadi, watu 11 waliochukua fomu wamefutikia wapi?" Alihoji Sitta. Sitta, Spika mstaafu alipotakiwa kufafanua hoja hiyo, alisisitiza kuwa inajulikana wazi ndani ya chama na wachache wenye ujasiri kama yeye, ndio wana uwezo wa kusema na kusisitiza kwamba hatanyamaza mpaka pumzi yake ya mwisho. Hata hivyo, alikiri kuwa uchaguzi wa CCM umekwenda vizuri ila hivi sasa yapo baadhi ya maeneo bado rushwa inatumika kupindisha matokeo na kusisitiza kwamba ikiwa rushwa itakemewa ndani ya chama na viongozi halali wakapatikana, hata dawa hospitalini zitapatikana na ndilo tamanio la wapenda maendeleo. Dk Bana aliendela kumshauri Rais Jakaya Kikwete kutumia muda mwingi kuzungumza na wanachama katika ngazi za wilaya, kwa kuwa anakubalika kwa zaidi ya asilimia 60 hadi 70 na nguvu ya chama ni mwenyekiti. "Hakuna chama bila mwenyekiti, kitayumba, Kikwete anakubalika, binafsi afanye ziara kuzungumza na wanachama, asisubiri kuonekana wakati wa uchaguzi bali afanye ziara kuimarisha chama," alishauri Dk Bana. Alisema mpaka sasa zaidi ya asilimia 51 ya wagombea wa uchaguzi unaoendelea ni wasomi kuanzia Stashahada na Shahada mbalimbali, kinachogomba upinzani ni watu wachache wanaopiga kelele na kusahau kujenga vyama vyao. "Tatizo la Upinzani ni kwamba, wamegeuka kuwa wanaharakati wa kuitisha maandamano ya mpaka kieleweke, nini kieleweke? Tena wachache ndio wanapiga kelele, wanapaswa kurudi kuwa wanasiasa na si wanaharakati, wawaache Tamwa (Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake) na wengine," alikazia Dk Bana. Alisema ni kwa misingi hiyo, anarejea kauli yake kuwa bado ni ndoto kwa upinzani kushika Dola kwa kuwa wamekuwa na kazi ya kuishambulia Serikali kwa kutumia watu wachache machachari na kusahau kuimarisha ndani na kufanya uchaguzi wao usiwe na mvuto wala vuguvugu kutokana na ufinyu wa demokrasia. "Watu hawataacha kusema kuhusu uchaguzi katika upinzani kuwa watu wanapeana vyeo, kwa sababu ya ushemeji, hili litafutika ikiwa demokrasia ya kweli itaachwa ifanye kazi ndani, wasipige kelele nje wakati ndani hakujakaa sawa," alishauri Dk Bana. Alishauri wapinzani kuiga demokrasia iliyotumika ndani ya CCM na kuhakikisha kuwa mikakati yao kupitia M4C (Chadema) na V4C (CUF), zinazaa matunda ya kuimarisha vyama vyao. Katika hatua nyingine, Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Method Kilaini ametoa maoni yake kuhusu uchaguzi huo wa CCM na kukipongeza chama hicho akidai kimeonesha ukomavu wa kisiasa. "Wale walioshindwa hawapaswi kupiga kelele na kama wakipiga sana, watu watahoji walikuwa si washindani bali kuna kitu walikuwa wanatafuta. Mshindani siku zote anakubali kushindwa," alishauri Kilaini. Wilayani Bariadi Juliana Mahongo alitetea nafasi yake ya Mwenyekiti huku Andrew Chenge akipita bila kupingwa katika nafasi ya ujumbe wa NEC na Masunga Yabuyeze akitetea nafasi yake ya Katibu Mwenezi. Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Erasto Sima aishinda ujumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa na wajumbe wengine Tina Chenge, Gasper Mjuna, Rachael Subanda na Masanja Kidogosa. Pia wilaya ya Itilima ilipata Mwenyekiti wa CCM ambapo Mabula Mohamed alichaguliwa huku ujumbe wa NEC ukienda kwa Daud Njalu ’Nsagali’, na John Nkululu alichaguliwa kuwa Katibu wa Uchumi na ukatibu mwenezi ukienda kwa Mang’ombe Gwalugwa. Katika wilaya ya Busega aliyechaguliwa kushika nafasi ya Mwenyekiti ni Mshoni George, huku uNEC ukienda kwa Raphael Chegeni na Katibu Mwenezi akichaguliwa Raphael Babasha. Mkuu wa Wilaya ya Busega, Paul Mzindakaya, alichaguliwa ujumbe wa Mkutano Mkuu Taifa na wajumbe wengine wakiwa ni Hamis Haule, Josia Mgemu, John Mkale na Mikinesi Mahela. Wilayani Maswa Mwenyekiti wa Wilaya Peter Bunyongoli alichaguliwa tena kuendelea na wadhifa wake na Aron Mboje akachaguliwa kuwa mjumbe wa NEC. Wajumbe watano wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa ni Masanja Mpiga, Pili Kidosela, Amina Almasi, Thobias Kadome na Mercia Emmanuel. --- Habari via Ziro&Tina blog 1 Comment America's Delta Airlines opens office in Dar es Salaam to start direct flights 03/10/2012 0 Comments Picture Picture (photo: blog.delta.com) US-based Delta Airlines has opened office in Dar es Salaam a move the company says is geared towards strengthening the business and economic links that already exist between Tanzania and the US particularly in the tourism sector. Robert Bryan, Delta’s Director Commercial Manager for East Africa and West Africa made the announcement last week during the launching of the new Office. “As US Investors, we are excited to invest in the East African market and we are here because we realize the potential in this country and surrounding the EAC region…” explained the director. With an extensive domestic an international route network Delta in partnership with Kenya Airways and KLM has now opened a direct airline from US to Tanzania and given the market then start the reverse route, from the US to Tanzania Delta Airlines has already opened other sales office in Nairobi and Kampala and the commercial director says they are confident that these new services will attract more US travelers to visit Tanzania. According to Bryan, although Delta does not currently operate direct services to Tanzania, customers traveling to the United States on Delta can book flights via Europe operated by Delta’s joint venture partner KLM or Sky Team partner and Kenya Airways. Additionally, customers can opt to fly via Johannesburg, Lagos or Dubai to Delta’s hub in Atlanta which offers onward connections to more than 150 destinations throughout the U.S and beyond. Delta is investing more than USD 3bn through 2013 in airport facilities and global products, services and technology to enhance the customer experience in air and on the ground. Delta launched its first services between Africa and the United States in December 2006, and right now the airline operates services to the US from five cities in Africa including Accra-Ghana, Lagos- Nigeria, Dakar- Senegal, Johannesburg-South Africa, and Monrovia-Liberia. Delta serves more than 160million customers each year and just in the past year, Delta was named America’s domestic Airline of the Year by Travel Weekly Magazine and it was also named the top Tech-friendly US Airline by PCworld magazine for its innovation in technology and on top of that the company won the Business leading edge awards for US Airlines. Delta headquartered in Atlanta and so far it employs 80,000, employees worldwide and operates a mainline fleet of more than 700 aircraft. With an industry leading global network, Delta and Delta connection carriers offer service to nearly 320 destinations in 60 countries on six continents. --- via The Guardian Add Comment Nyerere Day Oktoba 14, 2012: Unakaribishwa! 03/10/2012 0 Comments Picture Add Comment Ripoti ya MCT ya mauaji ya Daudi Mwangosi kuwekwa hadharani Oktoba 9, 2012 03/10/2012 0 Comments Ripoti ya uchunguzi wa mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa habari mwakilishi wa kituo cha televisheni ya Channel Ten, mkoani Iringa, marehemu Daudi Mwangosi, uliofanywa na timu ya waandishi wa habari watatu kutoka Baraza la Habari (MCT) na Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), itawekwa hadharani Oktoba 9, mwaka huu. Azma hiyo ilitangazwa jana Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga, baada ya timu hiyo kukamilisha uchunguzi wake hivi karibuni. Mukajanga alitangaza azma hiyo alipotakiwa na gazeti la NIPASHE kueleza lini ripoti hiyo itatangazwa. Akijibu swali hilo kwa njia ya maandishi, Mukajanga alisema kwa kifupi: “Jumanne Oktoba 9, 2012 Inshallah.” Awali, NIPASHE ilizungumza na Katibu Mtendaji wa TEF, Neville Meena, ambaye alisema uchunguzi wa timu hiyo umeshakamilika na kwamba, ripoti yake imekabidhiwa kwa Bodi ya MCT. Timu ya waandishi hao iliyoundwa Septemba 4, mwaka huu, iliongozwa na Meneja wa Utafiti na Machapisho wa MCT, John Mirenyi, wajumbe wakiwa ni Mhariri wa masuala ya siasa wa gazeti la Mwananchi, Hawra Shamte na Mkufunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini, Kitivo cha Uandishi wa Habari na Mawasiliano ya Umma, Simon Berege. Timu hiyo ilipewa siku nane na ilianza kazi yake Septemba 6, mwaka huu, kubaini ukweli wa tukio hilo na kuweka kumbukumbu sahihi ya tukio hilo. Wakati huo huo, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Advera Senso, alikataa kuzungumzia timu ya jeshi hilo iliyoongozwa na Mkuu wake, Inspekta Jenerali (IGP), Said Mwema, umekwisha au nini kinaendelea, akisema hawaruhusiwi kufanya hivyo kwa kuwa liko mahakamani kisheria. “…Waziri wa Mambo ya Ndani alishalisemea,” alisema Senso. Mwangosi, ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (IPC), aliuawa kwa kupigwa na bomu lililosambaratisha mwili wake wakati polisi wakiwatawanya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuwazuia kufungua tawi la chama hicho, katika Kijiji cha Nyololo, Wilaya ya Mufindi, mkoani humo, Septemba 3, mwaka huu. Tayari askari polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), mwenye namba G2573, Pasificus Cleophace Simon (23), amefikishwa mahakamani akituhumiwa kwa mauaji ya Mwangosi. -- via Nipashe Add Comment New York’s Mayor Bloomberg aims to save mothers, children in Tanzania


 
Picture
A short video on the work of Bloomberg Philanthropies in Tanzania is playing in the background. (photo by Tagie Daisy Mwakawago)
Picture
President Kikwete answering few questions from the reporters (not in the photo). (photo: Tagie Daisy Mwakawago)
Picture
Tanzania Delegation which consisted of Chief Secretary H.E. Ambassador Ombeni Y. Sefue (5th left), Ambassador Liberata Mulamula, Senior Advisor to President Kikwete, Ambassador Mwanaidi Sinare Maajar (3rd left), Ambassador of the United Republic of Tanzania to the United States of America, H.E. Ambassador Tuvako Manongi (left), Permanent Representative of Tanzaia to the United Nations. Others are Deputy Ambassador Ramadhan Muombwa Mwinyi (4th left), Deputy Permanent Representative of the United Republic of Tanzania to the United Nations, Mr. Prosper Mbena (6th left), Assistant to President Kikwete and Mr. Salva Rweyemamu, Director of Communications to the Tanzania State House. (photo: Tagie Daisy Mwakawago)
Picture
H.E. Jakaya Mrisho Kikwete (3rd right), President of the United Republic of Tanzania in a press conference held today in New York to unveil results of Innovative Maternal Health Program in Tanzaina. Others are the United Nations Secretary General Ban Ki-moon (2nd left), New York City Mayor Bloomberg (left) and Ms. Helen Agerup 2nd right) of the H&B Agerup Foundation in the Dag Hammarskjöld Library at the United Nations Headquarter in New York, USA. (photo by Tagie Daisy Mwakawago)
UNITED NATIONS (Reuters) - New York City Mayor Michael Bloomberg said on Tuesday he is funding the expansion of a pilot maternal health program in Tanzania that is predicted to help 50,000 mothers and their children during the next three years.

A woman dies every two minutes of pregnancy-related problems with 99 percent of such deaths in poor countries, according to the U.N. Population Fund. Common causes are bleeding after childbirth, high blood pressure, infections and unsafe abortions.

"No one should have to die giving birth," Bloomberg told a news conference at the United Nations with Tanzanian President Jakaya Kikwete. "Too many women die due to complications in childbirth because of inaccessible and inadequate care."

The Bloomberg Philanthropies initiative trains assistant medical officers and midwives in remote areas to perform life-saving procedures including caesarean sections and upgrades isolated health centers.

"If you can build a model that you can show works in remote areas where the doctor to patient ratio is 1 to 50,000 then you can start attracting capital from an awful lot of other foundations and perhaps governments," said Bloomberg, founder of Bloomberg LP who has so far donated more than $2.4 billion to charity.

While U.N. data shows maternal deaths globally halved between 1990 and 2010 to 287,000 annually, many states in sub-Saharan Africa are forecast to fail to reach a U.N. target of reducing maternal deaths between 1990 and 2015 by 75 percent.

Tanzania is not on track to meet the U.N. target and has the eighth highest number of maternal deaths in the world - a woman dies almost every hour. Kikwete said that more money was needed to tackle the problem.

"We need to scale up efforts because still too many mothers and children continue to die," Kikwete told reporters.

The Bloomberg Philanthropies maternal health program began in Tanzania in 2006. Bloomberg has now joined forces with Geneva-based H&B Agerup Foundation to spend $8 million to expand the program over the next three years, taking the total spent since the initiative started to $15.5 million.

Bloomberg's third term as New York City mayor finishes at the end of next year and he has said he will then dedicate himself to philanthropy. He hit No. 10 on Forbes latest ranking of the richest people in the United States with an estimated fortune of $25 billion.

In 2011 Bloomberg Philanthropies spent $330 million and Bloomberg has signed up to the Giving Pledge, a philanthropic campaign by two of the world's richest men - Warren Buffett and Bill Gates - that required him to announce he would give away at least half his wealth during his lifetime or after his death.

(Reporting by Michelle Nichols; editing by Andrew Hay)

---
Yahaoo! News
Picture
H.E. Jakaya Mrisho Kikwete (left), President of the United Republic of Tanzania listens Mr. Ban Ki-Moon, Secretary General of the United Nations prior to the press conference of the Maternal Health Program in Tanzania funded by Bloomberg Philanthropies. Second right is Mr. Michael Bloomberg, Mayor of the New York City and Ms. Helen Agerup (2nd left), President of H&B Agerup Foundation. (Photo by Tagie Daisy Mwakawago of the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation)
Picture
President Kikwete explains the much needed training for non-physician clincians in health facilities throughout the regions in Tanzania. (Photo by Tagie Daisy Mwakawago of the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation)
Picture
Ban Ki-moon listens to Mayor Bloomberg prior to press conference of Maternal Health Program in Tanzania funded by Bloomberg Philanthropies held today in Dag Hammarskjöld Library at Nations Headquarters in New York, USA. (Photo by Tagie Daisy Mwakawago)
Picture
H.E. Jakaya Mrisho Kikwete (left), President of the United Republic of Tanzania discusses briefly with New York City Mayor Michael Bloomberg (right) about his country's gratitude towards the Bloomberg Philanthropies initiative which resulted in an increase of over 1,000 delivery health facilities in Kigoma, Morogoro and Pwani Regions in Tanzania. Others in the photo are Ambassador Tuvako Manongi (2nd left), Permanent Representative of the United REpublic of Tanzania to the United Nations and Ms. Helen Agerup (2nd right), President of H&B Agerup Foundation. (Photo by Tagie Daisy Mwakawago of the Ministry of Foreign Affairs and International Co-operation) 


Wednesday, September 26, 2012

TOVUTI ZA SIMBA NA YANGA ZAFUNGWA
















Katika hali ya kusikitisha na kushangaza zile tovuti za klabu kubwa za mpira hapa Tanzania za Yanga na Simba leo zimekuwa hazipo hewani. Watu mbalimbali ambao wamekuwa wakizitafuta kupata habari za klabu zao hizo kongwe. Wamekuwa wakikuta ujumbe unosema "This account has been suspended"
Baadhi ya wataalamu wa mambo ya mawasiliano wanasema hali hiyo itakuwa inatokana na kushindwa kulipia gharama za tovuti hizo kuwepo hewani. Tovuti ya yanga ni www.youngafricans.co.tz na ile ya watani wao wa jadi ni www.simba.co.tz
Juhudi bado zinafanyika kujua nini sababu ya tovuti hizo kutokuwepo hewani zote kwa pamoja kwa wakati mmoja. Ikumbukwe klabu hizi mbili ndio zinaongoza kwa kuingiza mapato na pia zina udhamini mnono.

OKWI KUIKOSA MECHI YA YANGA

Taarifa nilizozipata usiku huu kamati ya ligi iliyokutana leo imemfungia mshambuliaji wa Simba,Emmanuel Okwi michezo mitatu pamoja faini ya tsh 500,000 kutokana na kadi nyekundu aliyopewa kwenye mchezo dhidi ya JKT RUVU kwa kosa la kumpiga kiwiko Kessy Mapande.
Kutokana na adhabu hiyo Emmanuel Okwi ataukosa mchezo dhidi ya Yanga. 

 HIVI NDIVYO ALIVYOPATA KADI NYEKUNDU






 

USISAHAU KU LIKE PAGE YETU