Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Raphael Muhuga 
aliyemwakilisha Mkuu wa Majeshi ya Tanzania katika sherehe za 
maadhimisho ya miaka 67 ya Umoja wa Mataifa tangu kuzaliwa kwake.
Mgeni rasmi Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta 
akiwasili katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo katika 
Kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Umoja wa Mataifa Tanzania kusheherekea
 miaka 67 tangu uanzishwe.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou akimlaki na
 Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta kwenye 
viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaa leo.
Pichani Juu na Chini ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. 
Alberic Kacou (katikati) akimtambulisha Mh. Samwel Sitta kwa baadhi ya 
Wakurugenzi wa Mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa hapa nchini.
Waziri wa Afrika Mashariki Mh. Samuel Sitta akipokea heshima ya wimbo 
wa Taifa baada ya kuwasili katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es 
Salaam leo kuhudhuria kilele cha maadhimisho ya wiki ya Umoja wa Mataifa
 baada ya kutimiza miaka 67 ya UN tangu kuanzishwa.
Mh. Samuel Sitta akikagua gwaride maalum katika kilele cha wiki ya maadhimisho ya Umoja wa Mataifa.
Waziri wa Afrika Mashariki akishuhudia upandishwaji wa bendera ya Umoja
 wa Mataifa ikiwa ni ishara ya kusheherekea miaka 67 ya Umoja huo katika
 viwanja vya Karimjee jijini Dar leo.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou, Mgeni 
rasmi Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta na Mkuu
 wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meha Jenerali Raphael Muhuga wakiwa 
Meza kuu.
Pichani Juu na Chini ni viongozi wa Madhehebu ya Dini nchini wakiomba 
Dua kwa ajili ya kubariki sherehe za kutimiza miaka 67 ya Umoja wa 
Mataifa tangu kuanzishwa.
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samwel Sitta akizungumza 
katika sherehe za kutimiza miaka 67 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa 
Mataifa (UN) katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, Sitta 
aliipongeza Umoja wa Mataifa kwa kuisaidia Tanzania katika nyanja 
mbalimbali za maendeleo ili kutokomeza umaskini.Waziri Sitta alisisitiza
 kwamba bado Umoja wa Mataifa unakabiliwa na changamoto nchini kama vile
 amani na usalama, tatizo la njaa, mabadiliko ya tabia nchi na uwepo wa 
silaha za maangamizi.Mh. Sitta alifafanua katika kilele cha sherehe hizo
 umuhimu wa kupitia na kusaidia nchi zinazoendelea kufikia malengo ya 
millennia.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. Alberic Kacou akitoa 
nasaha zake wakati wa maadhimisho ya umoja huo katika viwanja vya 
Karimjee alisema matatizo ya njaa, kupanda kwa bei za mafuta na 
mtikisiko wa uchumi duniani ni kati ya changamoto kubwa ambazo Umoja wa 
Mataifa inakabiliana navyo katika dunia ya leo. Dtk Kacou pia 
aliipongeza Tanzania katika juhudi zake za kupunguza vifo vya wakinamama
 wakati wa kujifungua na watoto ili waweze kufikia malengo ya millennia 
itakapofika 2015.Mratibu Mkazi wa UN alisema Tanzania imepunguza kwa 
kiasi kikubwa maambukizi mapya ya ugonjwa wa Ukimwi.
Katibu wa UNA Tanzania Fancy Nkuhi akizungumza kwenye hafla hiyo 
alisema umoja wa mataifa imefanya kazi kubwa katika kuwaunganisha vijana
 wa bara la Afrika. Nkuhi alisema kupitia YUNA walitoa elimu ya afya ya 
uzazi na ugonjwa wa Ukimwi kwa vijana katika mikoa kumi hapa nchini 
Tanzania katika harakati ya kuelimisha vijana madhara ya ugonjwa huo na 
afya ya uzazi kwa vijana.
Wanafunzi kutoka shule ya mchepuo wa kiingereza ya Heritage (Heritage 
English Medium Schools) ambao walikuwa kivutio wakati wa maadhimisho ya 
miaka 67 ya wiki ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania wakiwa katika 
gwaride maalum kupamba sherehe hiyo.
Meza kuu ikifurahia jambo wakati wa gwaride la watoto wa shule ya 
Heritage baada ya kuonyesha mbwembwe katika kupamba sherehe hiyo.
Wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Azania wakitoa burudani ya Wimbo maalum wa kuipongeza UN kutimiza miaka 67 ya kuzaliwa.
Wanafunzi kutoka shule ya mchepuo wa kiingereza ya Heritage (Heritage 
English Medium Schools) wakiimba wimbo maalum uliobeba ujumbe wa 
kuhimiza utunzaji wa amani miongoni mwa mataifa wakati wa maadhimisho ya
 miaka 67 ya Umoja wa Mataifa.
Pichani Juu na Chini ni baadhi ya Mabalozi, Wakurugenzi wa Mashirika ya
 Umoja wa Mataifa na Wafanyakazi wa UN na wageni mbalimbali 
waliohudhuria sherehe hizo.
Pichani ni baadhi ya maafisa wa Jeshi waliohudhuria sherehe hizo.
Waziri Sitta akiwa ameambatana na Mwenyeji wake Mratibu Mkazi wa UN 
Tanzania Dkt. Alberic Kacou (kushoto) wakisikiliza maelezo kutoka kwa 
Afisa wa Kitengo cha maafa UN Bw. Mdathiru Abubakar (wa pili kushoto) 
akielezea namna ya shirika la Umoja wa Mataifa linavyoshiriki pindi 
inapotokea maafa nchini. Kulia ni Judith Bihondwa wa UNICEF.
Afisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania Hoyce Temu (kulia) 
akifafanua utendaji wa kazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa kupitia 
mashirika yake 21 yanavyofanya kazi kwa ukaribu na Serikali ya Tanzania 
kwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samuel Sitta (wa pili 
kushoto) aliyeambata na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dkt. 
Alberic Kacou.
Mwenyekiti wa Shirikisho la vijana la Umoja wa Mataifa nchini (YUNA) 
Bw. Lwidiko Edward akisalimiana na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika 
Mashariki Mh. Samwel Sitta kwenye banda la maonyesho la Umoja wa Mataifa
 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar.
Waziri Sitta katika banda la maonyesho la shirika linalohudumia 
wakimbizi nchini (UNHCR). Katikati ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa 
nchini Dkt. Alberic Kacou na kushoto ni Afisa Habari kutoka kitengo cha 
habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Stella Vuzo.
Afisa Itifaki na Uhusiano wa Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha 
(AICC) Bw. Rodney Thadeus akimweleza Waziri Sitta jinsi ya kituo cha 
Kimataifa cha Mikutano Arusha (AICC) kinavyojipambanua kwa kupokea 
wageni mbalimbali wanaofanya mikutano katika kituo hicho na kutmia 
mwanya huo kutangaza Utalii na vivutio vya nchi.
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mh. Samwel Sitta na Mratibu 
Mkazi wa Umoja wa Mataifa Dkt. Alberic Kacou katika picha ya pamoja na 
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwenye
 banda la maonyesho katika wiki ya Umoja wa Mataifa.




























