Pages

Monday, December 15, 2014

BREAKING NEWS: PRUIJM KUREJEA KUINOA YANGA

kocha Mdachi Hans Van Der Pruijm huenda akarejea nchini kuifundisha tena YANGA,kutoka chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya klabu hiyo kinasema kocha huyo wa zamani wa klabu hiyo huenda akawasili usiku wa leo kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya awali.

Mwishoni mwa juma hili kwenye mchezo wa NANI MTANI JEMBE Yanga ilifungwa na mtani wake wa jadi Simba mabao 2-0 huku timu hiyo inayonolewa na Mbrazil Marcio Maximo ikionyesha kiwango cha kawaida kwenye mchezo huo ikilinganishwa na kipindi cha mdachi huyo.
AHSANTE: SHAFFIH DAUDA