Pages

Monday, September 8, 2014

MABASI YA DAR EXPRESS NA SIMBA MTOTO YAGONGANA WAMI

 
Katika hali ambayo haieleweki ajali hizi za mfululizo ambazo zimetokea katika juma moja, ambapo watu walio wengi wanashindwa kuelewa tatizo ni nini magari au madereva? . 
 
Maana ukiacha ajali ya Kijiji cha Sabasaba-Butiama, leo pia imetokea ajali nyingine ambapo ilikuwa saa tano asubuhi Gairo-Morogoro, baada ya Basi la Air Bus kuuwa watu na kabla muda haujapita sana, Mabasi mawili ya Dar express na Simba Mtoto nayo yamegongana kama inavyoonekana pichani hapa chini.

Tatizo ni nini la ajali kutokea mfululizo namna hii?
 

 Abiria wakiwasaidia wenzao kushuka.
Basi la Dar Express lililokuwa linatoka Arusha na basi la Simba Mtoto lililokuwa linaenda Tanga yamegongana uso kwa uso maeneo ya Wami. Majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika hospitali ya Chalinze.