Kikosi cha Yanga
Kikosi cha Coast Union
Picha Maktaba: 
  
Katika kile kilichodaiwa kuwa ni maandalizi ya Ligi kuu ya Tanzania Bara ambayo inataraji kuanza hapo mwezi ujao wa Tisa ilitokea hali ya kushangaza pale timu mbili ambazo pia zinajiandaa na ligi hiyo YANGA
 na COASTAL  Ziligongana Pemba jana. 
Baada ya timu ya Yanga kutua kisiwani kwa 
mafungu (juzi)siku ya Jumatatu na timu ya Coastal union nayo ilitua kwa mafungu kisiwani humo jana (siku ya Jumanne). 
Hali
 hiyo ilileta mkanganyiko wa nani atautumia uwanja wa Gombani kabla ya 
kukubaliana kuwa timu zote zitakuwa na vipindi viwili vya kufanya maoezi uwanjani hapo ambapo Coastal ndiyo wanaanza saa 12 asubuhi mpaka saa 2 mbili asubuhi na Yanga wanaanza 
saa 2 asubuhi mpaka saa 4, na wanarudi tena saa 8 mchana mpaka saa 10 
jioni, ndiyo Coastal wanaingia tena kumalizia awamu yao ya pili.
 Awali
 iliarifiwa kuwa ziara ya wana jangwani hao ilipangwa kuanza tarehe za 
mwanzoni mwa mwezi huu hivyo kufikia tarehe 17 hadi 18 ndiyo wangekuwa 
wanaondoka, lakini kwa kuwa jambo hilo limewekwa sawa ratiba ndiyo 
itakuwa hiyo, kufatia timu 2 hizo za bara kugongana kisiwani humo na 
wekundu wa msimbazi kuwa Unguja wadau wanahoji kuna ni visiwani??
 Chanzo: kitongoni(Pemba)

