![Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea Maktaba ya Kirais ya Rais Bush (Bush Presidential Library) sehemu ambayo imejengwa kwa mfano wa Ikulu ya Marekani, White House, hususan katika bustani y a Waziri (Rose Garden) pamoja na ofisi ya Rais wa Marekani, Oval office Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea Maktaba ya Kirais ya Rais Bush (Bush Presidential Library) sehemu ambayo imejengwa kwa mfano wa Ikulu ya Marekani, White House, hususan katika bustani y a Waziri (Rose Garden) pamoja na ofisi ya Rais wa Marekani, Oval office](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhPAGFuCb_nm70s6qkM6evx6QVha_WxtHrp_MFdKcOybQgWpPfrN6fPOd-ZvErVj4CB3te9CTNiUV2bvqQ_oapTskO9aDujahuixhafhGpQ2vkPH7jfFMKgqqErmQJ9Kd1wdxjaU3ZtYwaP/s280/b1.jpg) |
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea Maktaba ya Kirais ya Rais Bush
(Bush Presidential Library) sehemu ambayo imejengwa kwa mfano wa Ikulu
ya Marekani, White House, hususan katika bustani y a Waziri (Rose
Garden) pamoja na ofisi ya Rais wa Marekani, Oval office |
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea Maktaba ya Kirais ya Rais Bush (Bush Presidential Library)
na kujionea nafasi kubwa iliyotolewa kwa Tanzania na zawadi ambazo Rais
Bush alizipata katika ziara yake rasmi ya Tanzania wakati akiwa Rais wa
Marekani. Maktaba hiyo ya kuvutia inaendeshwa kwa teknolojia ya kisasa
kabisa ya habari na mawasiliano.
Rais Kikwete alikuwa amesimama mjini Dallas kwa muda akiwa njiani kutoka Washington D.C., kwenda
Houston, jimbo hilo la Texas kuhudhuria mkutano wa wafanyabiashara
wa mafuta na gesi ambao wanataka kuwekeza katika sekta hiyo hapa
Tanzania.
Rais Kikwete amekuwa Marekani kwa ziara ya
kikazi ya siku tisa, ambako miongoni mwa mambo mengine, amehudhuria
Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Marekani na Afrika uliofikia kilele chake
jana kwa kikao kilichoendeshwa na Rais Barack Obama wa Marekani katika
Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani mjini Washington D.C.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjlUVwZmbRkC4l2xXkOj1DIVGM7w5n9pGAgM6YQEgBjAi97W4-Yk0XUby1tVjCHmQN05Cdsv5KqzwZuacpLkSMJVjYRyCBk9TMZetpDHfPAGgFT1GVhDfhqkK2MJ_bvThAPlkb7hc5Qxzyy/s280/b3.jpg) |
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma
Kikwete wakitembelea na kujionea vitu mbalimbali ambavyo Rais mstaafu
George W. Bush alipewa kama zawadi kutoka Tanzania ambavyo vimehifadhiwa
katika Maktaba ya Kirais ya Rais Bush (Bush Presidential Library) |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgOI9R6cg5cA1VH8fAIvZrvRWM-xca42jR0B345XtAEUAHEpMuUIw0txzrS6tGCH7e52x8M8heLO8PQmxVXyawvutGI1HvwhN_EAP9xkIr5DeI8Dj2-cGmOuA3FZo65iv3VYJ1R_rLceX3r/s280/b5.jpg) |
Rais Jakaya
Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea na kujionea vitu
mbalimbali ambavyo Rais mstaafu George W. Bush alipewa kama zawadi
kutoka Tanzania ambavyo vimehifadhiwa katika Maktaba ya Kirais ya Rais
Bush (Bush Presidential Library) |
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiDLoCkgDf_-WdLIBkEmujZNLz9988B8Yga-hlrfG85pSqIg8nPZNilJfsHWNOiixNZyAf6tf_5Ilc7tMfffrit6R3XvkCdVXlaXeLr2tPkGw5HPRMS6XIbRu9r3Uqnu3Va7Vx58B_X0Z2u/s280/b6.jpg) |
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakitembelea sehemu ya
mfano wa ofisi ya kupangia mikakati ya Ikulu ya Marekani iliyotumika na
Rais MStaafu George W. Bush kwenye Maktaba ya Kirais ya Rais Bush (Bush Presidential Library) |
CHANZO:WAVUTI