| Kikosi cha Yanga | 
MABINGWA
 watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yana SC wameanza vema 
kampeni za kutetea taji lao, baada ya kuwafumua Ashanti United ‘Watoto 
wa Jiji’ mabao 5-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mabao
 ya Yanga leo yalifungwa na Jerry Tegete dakika za 10 na 57, Simon Msuva
 dakika ya 47, Haruna Niyonzima dakika ya 73 na Nizar Khalfan dakika ya 
90, wakati bao pekee la Ashanti lilifungwa na Shaaban Juma dakika ya 89
Young Africans inayonolewa na kocha mholanzi Ernie Brandts imeanza 
vizuri harakati zake za kutetea Ubingwa kwa kuhakikisha inashinda mchezo
 wa mwanzo na ndivyo vijana wa Jangwani walivyofanya.
Ilimchukua 
dakika 10 Jerson Tegete kuipatia Young Africans la kwanza kwa kumchambua
 mlinda lango wa Ashanti kufuatia pasi nzuri wa winga wa kulia Saimon 
Msuva kuitoka ngome ya Ashanti na kumpasia mfungaji aliyeukwamisha mpira
 wavuni bila ajizi. 
Ashanti walifanya mashambulizi langoni mwa 
Yanga kupitia kwa Hussein Sued lakini ukuta wa Yanga uliokuwa chini ya 
Mbuyu Twite na nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro' ulikuwa kikwazo kwake 
kumfikia mlinda mlango Ally Mustapha 'Barthez'.
Kiungo Athuman Idd
 'Chuji' alitolewa nje dakika ya 18 ya mchezo kuufuaia kuumia na 
kushinda na kuendelea na mchezo na nafasi yake kuchukuliwa na kiungo 
Frank Domayo 'Chumvi' . 
Kutokua makini kwa washambuliji wa Yanga 
Didier Kavumbagu, Saimon Msuva na Jerson Tegete kulizifanya timu kwenda 
mapumziko zikwa 1-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Yanga 
kujipatia bao la pili dakika ya 48 ya mchezo kupitia kwa mshambuliaji 
Saimon Msuva aliyewatoka walinzi wa Ashanti na kuachia shuti kali 
liliokwenda moja kwa moja wavuni.
Jerson Tegete aliipatia Young 
Africans bao tatu dakika ya 58 kwa usatdi wa hali ya juu akimalizia pasi
 safi ya Saimon Msubva aliyewatoka walinzi wa Ashanti United na kujaza 
krosi safi ambayo Tegete aliiweka kifuani kabla ya kumchambua mlinda 
mlango.
Yanga iliendelea kucheza inavyotaka huku ikitawala dimba 
la katikati kupitia kwa viungo wake Haruna Niyonzima, Salum Telela na 
Frank Domayo hali iliyowapelekea wachezaji wa Ashanti kucheza faulo 
nyingi na mwamuzi kuwaadhibu kwa kadi za njano na mmoja wao kutolewa nje
 kwa kadi nyekundu.
Haruna Niyonzima aliipatia Young Africans bao 
la nne dakika ya 74 ya mchezo kwa kichwa, akimalizia mpira wa adhabu 
uliopigwa na mlinzi wa pembeni David Luhende kufuatia Saimon Msuva 
aliyekuwa amechezewa madhambi na walinzi wa Ashanti United.
Dakika
 ya 90 Ashanti United walijipatia bao kupitia kwa Shaban Juma kufuatia 
uzembe wa walinzi wa Yanga waliotegeana kumkaba mfungaji aliyeukokota 
mpira toka nje ya 18 na kuingia nao ndani ya sita na kumfunga mlinda 
mlango Ally Mustapha 'Barthez'.
Huku washabiki na wapenzi wa soka 
wakiwa wanatoka nje wakijua mpira umemalizika, Nizar Khalfani aliipatia 
Young Africans bao la tano na kukamilisha ushindi huo mnono akimalizia 
pasi ya Saimon Msuva ambaye leo alikua mwiba mkali kwa walinzi wa 
Ashanti.
Mpaka dakika 90 za mchezo za mwamuzi Israel Mjuni Nkongo zinamalizika, Young Africans 5 -1 Coastal Union.
Kocha
 mkuu wa Yanga Ernie Brandts amekipongeza kikosi chake na kusema ni 
mwanzo mzuri katika msimu huu, aidha amesema wachezaji wake wangekuwa 
makini basi leo wangeibuka na ushindi mnono zaidi ya hizo bao tano 
walizozipata kutoka kwa wauza mitumba wa Ilala - Ashanti united.
Mara
 baada ya mchezo wa leo wachezaji wote wamepewa mapumziko siku ya kesho 
mpaka siku ya jumatatu watakapoanza mazoezi kujiandaa na mchezo dhidi ya
 Coastal Union ya Tanga siku ya jumatano tarehe 28.08.2013 katika dimba 
la uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Young Africans: 1.Ally
 Mustapha 'Barthez', 2.Juma Abdul, 3.David Luhende, 4.Nadir Haroub 
'Cannavaro', 5.Kelvin Yondani, 6.Athuman Idd 'Chuji'/Frank Domayo, 
7.Saimon Msuva, 8.Salum Telela, 9.Didier Kavumbagu/Hussein Javu, 
10.Jerson Tegete/Nizar Khalfani, 11.Haruna Niyonzima