![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjxJaDXj319sUlpQmcFEVOfwifZJ9Ayt_sM7bEH4dFW7kufkE0GCxtYddlhT9POudNuVBgsXilyjxCWD5TEU43yy-v6Y8JIW7TPU7D8rw1IiLqabXNTuH0TnnRdnsyNuMDajO749MPXjyQa/s280/Sheikh-Ponda1.jpg) |
Sheikh Ponda Issa Ponda |
Habari zilizotufikia zinasema kuwa Sheikh Ponda Issa Ponda kapigwa risasi mkoani morogoro leo. Inasemkana sheikh Ponda alipigwa risasi baada ya kushuka kwenye tax kwa ajili ya kuhutubia mhadhara katika eneo la kiwanja cha ndege. Chanzo cha habari kinasema risasi hizo zimempiga bega la kushoto naa sheikh ni mzima ila chanzo kingine cha habari kinasema amepigwa risasi nyingi na huenda mauti yamemkuta. (Inna lillah wa inna illayhi rajiuun)
RPC, Faustine Shilogile, anasema hali ni shwari
ila Ponda hajui hali yake Maana polisi walizuia gari la Ponda wamkamate,
lakini wananchi wakaanza kushambulia polisi ndipo wakarusha risasi
hewani kutawanya watu, lakini wananchi wakamtorosha. Anasema taarifa ni
nyingi za uongo, hakuna watu polisi wala hospitali waliozingira na
anaomba anayejua alipo atoe taarifa.