WATU watatu akiwemo aliyekuwa Polisi, Edna Kadogo wamehukumumiwa kifungo
cha miaka saba jela katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es
Salaam baada ya kupatikana na hatia ya kula njama na kuiba Sh milioni
330 mali ya Jeshi la Polisi.
Hakimu Gene Dudu alitoa hukumu hiyo baada ya kuridhika na ushahidi pamoja na vielelezo vilivyowasilishwa na upande wa mashitaka.
Washitakiwa
hao walikuwa wanakabiliwa na mashitaka matatu ya kula njama, kughushi
na wizi wa kiasi hicho cha fedha kwenye akaunti namba 2011000015
inayoitwa Police Retention Collection kwenye benki ya NMB Meatu.
Akisoma
hukumu hiyo , Hakimu Dudu alisema upande wa mashitaka umethibitisha
bila kuacha shaka mashitaka mawili dhidi ya washitakiwa watatu na
mahakama imewaona wana hatia.
Alisema katika mashitaka ya kula
njama watatumikia kifungo cha miaka miwili jela na wizi wa Sh milioni
330 watatumikia kifungo cha miaka mitano jela.
Adhabu hizo
zitakwenda pamoja ambayo ni sawa na kifungo cha miaka mitano. Mbali na
Kadogo, washitakiwa wengine waliotiwa hatiani ni mfanyabiashara Joshua
Aseno na Mfanyakazi wa Benki, Adelina Lwekoramu.
Baada ya kutoa
hukumu hiyo, Hakimu Dudu alimuaru, Aseno arudishe Sh milioni 30 na
nyingine zilizoingizwa kwenye akaunti yake kutoka katika akaunti ya
polisi na Kadogo anatakiwa kurudishwa milioni 10.
Aidha mahakama
imewaachia huru washitakiwa Vedastus Mafuru, Kennedy Achayo, Luciana
Limbu, Agnes Maro, Mkika Nyasebwa, Amos Hangaya. kwa kuwa upande wa
mashitaka umeshindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yao.
Kesi hiyo
ilikuwa ikikabili washitakiwa 11 lakini Fortunatus Biseko na Deogratias
Lumato waliachiwa huru baada ya kuonekana hawana kesi ya kujibu na hivyo
wakabaki tisa