Mgeni
 Rasmi katika Mpambano wa Kimataifa wa kuwani Mkanda wa Ubingwa wa Dunia
 wa WBU,kati ya Mabondia Francis Cheka wa Tanzania na Phil Williams wa 
Marekani,Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mh. Dkt. Fenella 
Mukangala (mwenye koti jeupe) akimvisha Mkanda wa Ubingwa huo,Bondia 
Francis Cheka baada ya kumshinda kwa Point Mpinzani wake,katika Mchezo 
uliomalizika usiku huu kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee,Jijini Dar es 
Salaam.Kulia ni Bingwa wa Zamani wa Masumbwi,Fransous Bhotha.
 Bondia
 Francis Cheka wa Tanzania (kushoto) akimrushia makonde makali mpinzani 
wake,Phil Williams kutoka nchini Marekani wakati wa mpambano wao wa 
Kimataifa kuwania Mkanda wa Ubingwa wa Dunia wa WBU,uliofanyika usiku 
huu kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee,Jijini Dar es Salaam.Bondia Francis
 Cheka ameibuka kidedea baada ya kumchapa mpinzani wake huyo kwa Point.
Bondia
 Phil Williams kutoka nchini Marekani (kulia) nae alikuwa akijibu 
mashambulizi kwa mpinzani wake,Francis Cheka.hadi mwisho wa mchezo 
uliokuwa wa raundi 12,Francis Cheka aliweza kuibuka Kidedea kwa kumchapa
 mpinzani wake huyo kwa point na kufanikiwa kumnyang’anya mkanda wa 
Ubingwa wa Dunia wa WBU.
 Chukua hiyoooooo…
 Hapa lazima ukae,mie ndio kisiki cha mpingo:hivyo ndivyo Bondia Francis Cheka alivyoonekana kuifanya kazi yake vilivyo.
 Refa
 wa Mchezo huo akimzuia Bondia Francis Cheka baada ya kumkoleza makonde 
kisawasawa mpinzani wake,yaliyompelekea kwenda chini.
Mpambano ukiendelea.
![]()  | 
| Wanahabari wakipata taswira za mpambano huo. | 







