Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Simba Mussa Hassan Mgosi amejiunga rasmi na klabu ya Mtibwa Sugar ya Manungu Morogoro.
Mgosi ambaye msimu uliopita alikuwa akiitumikia klabu ya JKT Ruvu amejiunga na Mtibwa kwa mkataba wa mwaka mmoja.
Akiongea na mtandao huu, kocha wa Mtibwa Sugar Mecky Mexime amethibitisha kwamba klabu yake imemsajili mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba, "Mgosi anakidhi vigezo vya mshambuliaji tunayemhitaji baada ya kuondoka wa Javu aliyejiunga na Yanga. Ameshaini mkataba wa mwaka mmoja na atajiunga na kambi ya maandalizi ya msimu mpya hivi karibuni
Mgosi ambaye msimu uliopita alikuwa akiitumikia klabu ya JKT Ruvu amejiunga na Mtibwa kwa mkataba wa mwaka mmoja.
Akiongea na mtandao huu, kocha wa Mtibwa Sugar Mecky Mexime amethibitisha kwamba klabu yake imemsajili mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba, "Mgosi anakidhi vigezo vya mshambuliaji tunayemhitaji baada ya kuondoka wa Javu aliyejiunga na Yanga. Ameshaini mkataba wa mwaka mmoja na atajiunga na kambi ya maandalizi ya msimu mpya hivi karibuni

Klabu
 ya Coastal Union imekamilisha usajili wa mshambuliaji wa kiuganda Yayo 
Lutimba kutoka timu ya mamlaka ya mapato ya Uganda URA. 
Aliyefanikisha
 zoezi hilo ni meneja wa Wagosi, Akida Machai ambaye amepanda ndege 
mpaka jijini Kampala kunasa saini ya kijana mdogo mwenye miaka 19, Yayo 
Lutimba Kato kutoka timu ya mamlaka ya mapato Uganda (URA).
Nassor
 Ahmed ‘Binslum’, ambaye ni mkurugenzi wa ufundi amesimamia kwa kiasi 
kikubwa kufanikisha usajili wa wachezaji takriban tisa ukijumlisha na 
Kato amezungumza na blog hii usiku wa leo baada ya Meneja Machai kuenda 
kumtambulisha Kato kwa Binslum na kuweka wazi kuwa tatizo la ukame wa 
mabao litaisha kwa wana Mangush.
Itakumbukwa
 kocha Mkuu wa Coastal Union, Hemed Morocco wiki chache zilizopita 
wakati wa kujiandaa na mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya URA, 
aliweka wazi bado kikosi chake kina matatizo ya umaliziaji.
Alibainisha
 kikosi hicho kipo vizuri kila idara kuanzia golikipa, mabeki na viungo 
ila hakuna mtu mwenye uchu wa mabao hivyo kuahidi kuwatumia wachezaji 
haohao kuwafundisha namna ya kuadhiri magolikipa wa timu pinzani.
Ndiyo
 maana winga Danny Lyanga alikuwa akichezeshwa namba kumi ili 
kumuangalia uwezo wake wa kupachika mabao lakini hakuonekana kucheza 
vema kwenye mechi ya URA.
Kwa
 usajili wa miaka miwili kuitumikia Coastal Union kinda huyu atakuwa na 
nafasi nzuri sana kujitengenezea jina nchini Tanzania hasa baaada ya 
kuwa na rekodi nzuri ya kuwafunga Simba na Yanga mabao mawili mawili 
katika mechi walizokutana nazo kwa vipindi tofauti.
Zipo
 taarifa kuwa Yanga nao walikuwa mbioni kumnyakua kinda huyu lakini 
Meneja Akida Machai amewazidi akili kwa kumfuata hukohuko kwao Uganda. 
Na hizi ni mbinu za ‘kimafia’ zinazotumiwa na timu kubwa duniani kote 
kunasa wachezaji mahiri.
Mungu
 akipenda kesho Kato ataungana na wachezaji wenzake katika kambi iliyopo
 pembezoni mwa bahari ya hindi Raskazone Hotel, jijini Tanga.
Wagosi
 wameanza vizuri mechi zao mbili za majaribio ambapo mechi ya kwanza 
walishinda bao 1-0 dhidi ya URA na siku tatu baadaye wakashuka dimbani 
dhidi ya Simba SC ambao nao walichapwa 1-0. Zipo taarifa za kucheza 
mechi ya kirafiki siku ya Eid pili uwanja wa Mkwakwani lakini 
zikishathibitishwa na timu tutakayocheza nayo tutawahabarisha.