KENYA-- Padri  wa kanisa Katoliki amekutwa amekufa baada ya kujiua leo 
asubuhi katika eneo la Turkana siku moja baada ya kufikishwa katika 
mahakama ya Lodwar kwa madai ya kumlawiti mwanafunzi wa kidato cha tatu.
Mwili
 wa John Manzi ulipatikana ukining’inia katika makazi ya mapadri 
dayosisi ya Lodwar Jumatano, siku moja baada ya kuachiliwa kwa dhamana 
ya KSh100,000 na kaimu hakimu mwandamizi Harrison Barasa.
Afisa
 mkuu wa polisi Turkana Kati  John Onditi,  alisema maiti ya kasisi huyo
 ilipatikana ikining’inia nyumbani kwake Jumatano asubuhi.
Upande
 wa mashitaka ulikuwa umedai kuwa padri huyo alimshawishi mvulana huyo 
mwenye umri wa miaka 18 nyumbani kwake Ijumaa usiku ambapo walipata 
vileo kabla ya kutekeleza kitendo hicho mwathiriwa akiwa amelewa.
Mwanafunzi
 huyo aliamka asubuhi na kugundua kuwa padri huyo alikuwa amemlawiti 
kabla ya kupiga ripoti polisi akiwa ameandamana na mzazi wake.
Marehemu
 kisha alijisalimisha mwenyewe kwa kituo cha polisi cha Lodwar baada ya 
kudokezewa kuwa mvulana huyo amepiga ripoti polisi.
Kuachiliwa
Tukio
 hilo liliibua maswali miongoni mwa waumini wa kanisa hilo na makasisi 
wengine waliojazana katika kituo hicho cha polisi wakimtaka padri huyo 
awachiliwe.
Daktari aliyemchunguza 
mwathiriwa alithibitisha kuwa matokeo yake yanaambatana na madai ya 
mvulana huyo ya kulawitiwa. Vile vile, madaktari walisema kuwa mvulana 
huyo anapokea ushauri hasa baada ya kutatizwa sana na tukio hilo.