Chama tawala nchini Uganda cha National Resisitance Movement-NRM- 
kimewafukuza baadhi ya wanachama wake wanne, wote wakiwa ni wabunge, kwa
 kile kilichoitwa utovu wa nidhamu.
Mbunge mwingine yeye amesimamishwa kwa muda wa miezi mitatu kwa sababu za ulevi.
Katibu
 mkuu wa chama hicho Amama Mbabazi anasema hii kwa tafsiri yake 
inamaanisha kuwa wabunge hao wamepoteza viti vyao, jambo ambalo wahusika
 wanapinga.
Katibu 
mkuu wa chama tawala cha NRM na wakati huo waziri Mkuu wa Uganda, Amama 
Mbabazi, ametangaza maamuuzi ya kamati kuu ya chama hicho kuhusu 
majaliwa ya wabunge wanne waliopewa jina la ‘wabunge waasi’ kutokana na 
misimamo yao dhidi ya masuala mbalimbali katika chama hicho.
Mbabazi
 alitoa kauli hiyo na kusema, “Muhammad Nsereko afukuzwe kutoka NRM;kuwa
 Theodor Sekikubo afukuzwe kutoka NRM; kuwa Barnabas Tinkasimire 
afukuzwe kutoka NRM; kuwa Wilfred Nuwagaba wamefukuzwe kutoka NRM; na 
kuwa Vicent Kyamadidi Muzuni asimamishwe uana chama wa NRM kwa muda wa 
miezi mitatu.”
Wabunge
 wanne waliofukuzwa kutoka chama: Nsereko; Sekikubo; Tinkasimire pamoja 
na Niwagaba wamekuwa wakipinga na kukosoa saana uongozi wa sasa wa chama
 hususan kutokana na madai ya ufisadi dhidi ya vigogo wa chama.
Na
 wanasema hatua hii ni ya kuwaandama kisiasa kwa kusema ukweli dhidi ya 
wanachoita uongozi mbaya. Hatua ya kuwafukuza wanachama hao , inasekena 
ni kutokana na utovu wa nidhamu.
Wabunge hao walishtakiwa katika 
kamati ya nidhamu ya chama na kukabiliwa mashataka saba: kuwapigia debe 
wagombea wa vyama vya upinzani katika uchaguzi mdogo; kupaka matope 
wagombea rasmi wa chama cha NRM wakati wa uchaguzi mdogo; kutoa madai ya
 uongo kwa vombo vya habari dhidi ya chama cha NRM; kutumia majukwaa 
haramu, kama vile vyombo vya habari na mikutano ya hadhara ya vyama vya 
upinzani kuzungumzia masuala yanayowakera;kujihusisha katika uundaji wa 
genge ndani mwa NRM; matumizi ya lugha chafu;na mwisho kukaidi kamati ya
 nidhamu ya chama.Wote licha ya kuwaita kufika mbele ya kamati hiyo 
kujieleza walipinga.
Hii ndiyo mara ya kwanza tangu mfumo wa vyama vingi kuanza tena mwaka wa 2006, chama cha NRM kufukuza wanachama wake.
Na
 hii imezusha tafsiri tofauti kwa wabunge wanaofukuzwa chama.Katibu mkuu
 wa NRM anasema kuwa hii inamaanisha kuwa wamepoteza viti vyao vya 
ubunge.
Mbabazi 
aliongeza kusema kuwa ''Kulingana na sheria za Uganda, hususan kifungu 
83 cha katiba ya taifa ni kuwa mtu anaweza kuwa mbunge pindi tu ikiwa 
amechaguliwa kama mbunge wa kujitegemea,au ikiwa amechaguliwa baada ya 
kuungwa mkono na chama Fulani,au ni waziri,au kama mwanajeshi.''
Hakuna
 njia nyingje ile. Wabunge hao wanasema kuwa katiba haikubali mbunge 
yeyote kubadili chama bungeni.Ikiwa mtu atapoteza uungwaji mkono wa 
chama chake hii ina maana kuwa amepoteza kiti chake.
Lakini hilo limepingwa na mbunge muathiriwa na tena wakili, Wilfred Niwagaba.
Niwagaba
 alisema ''Ikiwa anadhani kwa kutusimamisha au kutufukuza uanachama ina 
maana kuwa tunapoteza viti vyetu,nasikitika sikubaliani na tafsiri 
hiyo.Hakuna hata mmoja wetu ameondoka kutoka chama kwa hiari.''Hata 
hivyo mwenzao Vincent Kyamadidi amesimamishwa uanachama kwa muda 
kutokana na madai kuwa alilewa na kujaribu kupigana hadharani jambo 
ambalo linakwenda kinyume na maadili ya chama.
Aidha yeye alipoita kujieleza alifika mbele ya kamati hiyo.
Bado kuna vuta ni kuvute kuhusu majaliwa ya wabunge wanne, ikisemekana wamekwenda mahakani kupinga kufukuzwa kwao.