DPP wa Serikali Ibrahim Mzee asema hajaona ushahidi ambao ungemuwezesha kumshitaki kijana Omari alituhumiwa kwa mauwaji ya Padri Mushi.
Na kwa upande wa Mahakama pia umelitaka Jeshi la Polisi kumfikisha mtuhumiwa huyo Mahakamani siku ya Jumatatu na waeleze vielelezo tosha kwanini wamemchelewesha kumpeleka mahakamani wakati wanajua kuwa mtuhumiwa hupaswa kukaa kituo cha Polisi kwa muda wa masaa 24 tu na baadae kufikishwa mahakamani.