Lady Jay Dee
East African popular musician Lady Jay Dee ameamua kuwapa modongo
Clouds fm kupitia Twitter kutokana na wimbo wake mpya uliotoka
hivi karibuni Joto hasira kutopigwa katika radio hiyo. Jay dee
ameandika kuwa radio ya watu isiyopiga nyimbo za wasanii wa watu ila
wasanii wao tu. Angalia tweet za Queen of Bongofleva huyo.
"Radio ya watu isiopiga nyimbo za wasanii wa watu ila za wasanii wao tu, wasiopendwa na watu.
"Anaedai kuianzisha bongoflava aliapa kuiua bongo flava. Sasa hata wasioijua Hiphop nao wana beef na Bongo flava! Damn !!"
Jay Dee pia anaonekana kujizatiti na kujiamini kuonyesha kuwa yupo kwa
lolote yeye kama Komandoo Binti Machozi aliandika tena "Kill me if u
can. Am on Fire, siogopi ng'oooooo Jipangeni, Ni kweli nimelamba sumu,
lakini hainidhuru. Nakunywa maziwa daily, I will survive".
"Hee! Kuna watu wanadhani nili tweet nikiwa nimelewa, nilimaanisha
na msimamo ni huo. Sitasema oooh kuna mtu ka hack ac yangu nooo its
me"
" Kuna DJ flani alikuwa akipiga nyimbo nilizoshirikishwa akifika
sehemu nilioimba mimi anakata verse yangu nimtaje?? Sa hivi anakat ya
Prof J"
Hata hivyo si Jay Dee pekee kuanza kulaumu kwani wapo wanamuziki wengine wanaolaumu nyimbo zao kutokupigwa.
SOURCE:JAMII FORUM