- Inawezekana kuwa imetekwa nyara
- Au Haitambui majukumu yake. 
Wale wanaofahamu dhana nzima ya kuanzishwa Kamati ya Maridhiano 
Zanzibar umefika wakati wa kujiuliza IKo wapi kamati ya Maridhiano?
Amma kwa wale wasiofahamu dhana na chimbuko la kuanzishwa kamati ya maridhiano wao watasema kamati hii ipo.
Ni vyema kufahamu chimbuko la dhana ya Kuweko Kamati ya Maridhiano. 
Baada ya miongo ya misuguano ya kisiasa Zanzibar juhudi kadhaa 
zilichukuliwa kurudisha imani miongoni mwa Wazanzibar ili kuendeleza 
siasa chini ya misingi ya demokrasia, haki, usawa, pamoja na kutii 
sheria za nchi huku tukidumisha usalama, umoja na amani.
Juhudi zilizaa matunda mwaka 2009, baada ya maridhiano yaliyofikiwa 
baina ya vyama vya CCM na CUF na kuamua kufuta uhasama yaliyosimamiwa na
 wajumbe kutoka pande zote mbili. Mwanzoni yalikuwa mazungumzo 
yaliyoendeshwa kwa siri kubwa hadi pale ilipofika time ya kuyatangaza, 
viongozi wakuu wawili waliyabariki, kuyakubali na kuyaridhia.
Kilichofuata ilikuwa ni “Road map” kuelekea dhamira thabiti ya 
maridhiano haya ikiwa ni pamoja na kuliomba Baraza la Wawakilishi 
kujadili dhana nzima, pale itakapoonekana    inawafiki maridhiano haya 
yasimamiwe kikatiba. Halkadhalika maamuzi yote lazima yasimamiwe na 
wananchi wenyewe kwa kupiga kura ya maoni kukubali au kukataa.
Hivyo basi, Kamati ile iliyoasisi maridhiano ilikabidhisha mamlaka 
yake kwa Baraza la Wawakilishi. Wakati wa mjadala, Baraza la Wawakilishi
 liliunda kamati, ambayo ndio iliyosimamia hadi kuhitimisha maridhiano 
na kuikaribisha Serikali  ya Umoja wa Kitaifa.
Hapo utaona hadi kukamilika kwa maridhiano kulitokana na kamati 
mbili; i) kamati ya kuasisi maridhiano na (ii) kamati ya kusimamia 
maridhiano.
Hapa ndio dhana ya kuendelea kuwa na Kamati ya Mridhiano ilipoanzia. 
Kuona kwamba ili Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar iweze kudumu na 
kutatua vikwazo vitakavyojitokeza lazima kuwe na upande mwengine (third 
party). Upande huu utakuwa suluhishi wa mizozo pindi ikijitokeza. 
Vilevile utakuwa ndi muelekeo (dira) kuielekeza serikali pamoja na kuwa 
kunganishi kwa wananchi.
Kwa vile haya ni maridhiano bila ya shaka kulikuwa na uhasama, hivyo 
suala la usuluhishi na kusameheana lilipaswa lipewe nafasi yake. 
Kuorodheshwa na sera za kitaifa na kutengwa zile sera za kivyama ilikuwa
 ndio uti mgongo wa Kamati ya Maridhiano.
Haya yote yalitakiwa kufanywa na ile kamati iliyoundwa na Baraza la 
Wawakilishi kwani imetokana na chombo cha kutunga sheria, imechaguliwana
 wananchi pia inajumuisha wajumbe kutoka vyama vyote viwili (CCM  na 
CUF).
Kinyume chake ile kamati ya Waasisi ndio iliyojichukulia na 
kujitwisha kama ndio Kamati ya Maridhiano. Hili limepelekea kukosa 
utendaji na kupoteza muelekeo wa dhana nzima ya kuwa na Kamati ya 
Maridhiano.
Kuna haja ya kufikiria kuundwa upya wa Kamati ya Maridhiano ili iweze
 kufikia lengo la kuweko kwake. Zanzibar inahitaji sera za kitaifa, 
umoja, suluhu (reconciliation),   nani mwengine kama sio uimara wa 
Kamati ya Maridhiano.
SOURSE: MZALENDO NET