CHADEMA imesema imelazimika kuratibu maandamano na mkutano wa hadhara 
kama ishara ya kuwapokea wabunge wa upinzani kwa madai ya kuwashitakia 
Wananchi kitendo cha Bunge kuondoa kwa hoja zao binafsi.
Moja
 ya h oja hizo ni hoja binafsi ya Mnyika iliyokuwa ikipendekeza Bunge 
lijadili na kupitisha maazimio ya hatua za haraka za kuboresha 
upatikanaji wa maji safi na ushughulikiaji wa maji taka katika jiji la 
Dar es Salaam, hoja ambayo ilitupiliwa mbali na kuzua mtafaruku bungeni.
Hoja
 nyingine ni ya Mbunge wa Kuteuliwa na Rais, ambaye pia ni mwenyekiti wa
 NCCR-Mageuzi, James Mbatia aliyoitoa bungeni juu ya udhaifu wa mitaala 
ya elimu nchini.
Jeshi la Polisi nchini
 kupitia Kamanda wa Polisi wa mkoa Kipolisi wa Temeke, Engelbert Kiondo 
amesema ni marufuku kwa CHADEMA kuandamana kama walivyokusudia ila, ni 
ruhusa kufanya mkutano.
Amesema sababu 
za kuzuia maandamano hayo ni kutokana na usumbufu utakaojitokeza katika 
maeneo ambayo maandamano hayo yamepangwa kupitia ikiwa ni pamoja na 
kuingilia na pengine kuzuia shughuli za kawaida za maeneo hayo, matumizi
 ya barabara na pengine kuchangia vitendo vya uharibifu wa mali na 
uvunjifu wa amani. Hivyo akasema alikwishakuwasiliana na viongozi wa 
CHADEMA wa Temeke kuhusu suala hilo na kuwataarifu kuwa maandamano 
yoyote yatakayofanyika yatakuwa ni kinyume na sheria na hivyo 
itawalazimu Polisi kuchukua hatua za kisheria pale inapobidi.
Naye
 Kamanda wa CHADEMA anayeratibu maandamano hayo, Benson Kigaila alisema 
maandalizi ya maandamano hayo yanaendelea kama yalivyopangwa kutokana na
 kuwa hajapokea ujumbe wowote kutoka Jeshi la Polisi kama walivyoahidi 
kumpigia simu kwa maelezo zaidi.
Maandamano hayo yamepangwa kufanyika kuanzia TAZARA na kuhitimishwa kwa mkutano wa hadhara wilayani Temeke.
Benson
 alisema mkutano huo ni mwanzo wa mfululizo wa mikutano itakayofanyika 
kwenye kanda 10 zilizotengwa na CHADEMA, kuanzia mwenzi huu.