Rais
 Jakaya Kikwete akiwahutubia wananchi katika maadhimisho ya siku ya 
Ukimwi Duniani yaliyofanyika kwenye uwanja wa Ilulu Mjini Lindi, huku 
wadau mbalimbali wa masuala ya mapambano ya ukimwi wakishiriki kwa 
kufanya maonyesho na kutoa elimu na maelezo mbalimbali yanayohusu 
mapambano ya ukimwi, Rais Pia ameshuhudia utiwaji saini wa msaada wa 
Dola za Kimarekani Milioni 308 kutoka mfuko wa Global Fund uliosainiwa 
kati ya Katibu katibu wa Ofisi ya rais Paniel Lyimo na Ramadhan 
Kijahkati Kabu Mkuu Wizara ya Fedha huku Mfuko wa Global Fund 
ukiwakilishwa na Christoph Benn Mkurugenzi wa mfuko huo. 
Christoph
 Benn Mkurugenzi wa mfuko Global Fund akizungumza wakati wa maadhimisho 
ya siku ya Ukimwi Duniani iliyofanyika kwenye uwanja wa Ilulu mjini 
Lindi.
Rais
 Jakaya Kikwete akipokea maandamano ya wananchi wa mkoa wa Lindi wakati 
wa maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani iliyofanyika mjini Lindi leo . 
kutoka kulia ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete, Mkurugenzi wa Tume ya 
kudhibiti Ukimwi TACAIDS Fatuma Mrisho na kushoto ni mkuu wa mkoa wa 
Lindi Ludovick Mwananzila
Rais
 Jakaya Kikwete akipokea maandamano ya wananchi wa mkoa wa Lindi wakati 
wa maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani iliyofanyika mjini Lindi leo . 
kutoka kulia ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Hussein Mwinyi, Mke wa
 Rais Mama Salma Kikwete, Mkurugenzi wa Tume ya kudhibiti Ukimwi 
TACAIDS,Fatuma Mrisho. 
Rais
 Jakaya Kikwete akishuhudia Utiwaji wa Saini wa msaada wa dola za 
Kimarekani milioni 308 kwa ajili ya mapambano ya Ukimwi nchini, mkataba 
huo umesainiwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Paniel Lyimo kushoto na 
Ramadhan Kijah katikati, kulia ni Christoph Benn mkurugenzi wa Mfuko wa 
Global Fund, waliosimama nyuma kushoto ni Mkewa Rasi Mama Salma Kikwete,
 Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi na kulia ni Ursula
 Muller Mjumbe wa bodi ya The Global Fund,
Rais
 Jakaya Kikwete akiongozana na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiingia kwenye
 uwanja wa Ilulu mjini Lindi tayari kwa kushiriki katika maadhimisho ya 
siku ya ukimwi Duniani ambayo yamefanyika mkoani Lindi kitaifa.kutoka 
kushoto ni Mkurugenzi wa TACAIDS Fatma Mrisho na Mkuu wa Mkoa wa Lindi 
Ludovick Mwananzila
Rais
 Jakaya Kikwete akimuonyesha jambo Mkurugenzi wa tume ya kudhibiti 
Ukimwi Fatma Mrisho wakati alipotembelea mabanda mbalimbali katika 
maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani mjini Lindi leo.
Rais
 Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Bw.Rajab Mwenda afisa masoko 
wa Mpango wa damu Salama wakati alipotembelea katika banda hilo kwenye 
maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani mjini Lindi leo.
Baadhi
 ya viongozi wa Dini na waalikwa mbalimbali waliohudhuria katika 
maadhimisho hayo wakifuatilia kwa karibu matukio yaliyokuwa yakiendelea 
katika maadhimisho hayo.
Waheshimiwa viongozi wa serikali na baadhi ya wabunge wakiwa katika maadhimisho hayo kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi.
Mwakilishi
 wa mfuko wa bima ya Afya ya Jamii mjini Lindi NHIF Bi. Fortunata 
Raymond wa tatu kutoka kulia akiongoza maandamano ya wafanyakazi wa 
mfuko huo katika maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani.
Kikundi cha matarumbeta kikiongoza maandamano hayo yaliyokuwa yakipita mbele ya Rais kwenye uwanja wa Ilulu leo mjini Lindi.




















