Pages

Tuesday, December 18, 2012

AKAMATWA NA UCHAWI MAHAKAMANI KISUTU

Kijana ambae ni mganga kutoka katika mkoa wa Tanga wilaya ya Muheza eneo la Kerege amekamatwa na vifaa ambavyo vinadaiwa kuwa vya kichawi ambavyo alikuwa akiingia navyo mahakamani ili kumfanyia uganga mmoja ya watu wanaokabiliwa na kesi katika mahakama hiyo. Polisi waliweza kugundua kupitia vifaa maalumu ambavyo vimefungwa mahakamani hapo. Picha hapo juu ni mganga huyo akiwa chini ya ulinzi wa polisi