Habari ifuatayo imetumwa na Abunuwasi Alinacha (email: a...a...@gmail.com):
---
Katibu
Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe. Wilbroad Slaa
majuzi, Ijumaa, kule Sikonge, Tabora amezua na kutunga jipya.
Amedai
kuwa Julai 2, mwaka huu, 2012, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alisafiri kwenda Hong Kong kumwokoa
mtoto wake wa kiume, Ridhiwani Kikwete ambaye anadaiwa kuwa alikuwa
amekamatwa na mihadarati siku moja kabla, yaani Julai Mosi.
Huu ni uongo wa dhahiri kwa sababu ratiba ya Mhe. Rais Kikwete katika siku hizo anazozitaja Slaa iko wazi.
Julai
Mosi, akitumia Ndege ya Rais, alisafiri kwenda Rwanda ambako
alihudhuria Sherehe za Miaka 50 ya nchi hiyo na akalala mjini Kigali.
Julai 2 alisafiri kwenda Bujumbura kuhudhuria Sherehe za Miaka 50 ya
Burundi. Alirejea Dar es Salaam Julai 3 na Julai 4 alikutana na ujumbe
wa Kampuni ya IBM na Mjumbe Maalum kutoka Zimbabwe. Julai 5, alikwenda
Dodoma ambako aliendesha Kikao cha Baraza la Mawaziri na kurejea Dar es
Salaam siku hiyo hiyo. Sasa alikwenda Hong Kong lini? Ama alikuwa
Burundi na Hong Kong siku hiyo hiyo? Slaa anadai pia kuwa alipowasili
Hong Kong, Mheshimiwa Rais Kikwete alipokelewa na Balozi wa Tanzania
nchini China, Mheshimiwa Philip Marmo ambaye alimpeleka kwenye mkutano
na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China Mheshimiwa Hu Jintao. Huu ni uongo
mwingine wa dhahiri na ambayo sijui unamsaidia nini Slaa. Slaa anasema
uongo kuhusu Balozi Marmo kwa sababu ratiba ya Mheshimiwa Marmo kwa siku
sita za mwezi Julai nayo iko wazi na siyo kificho.
Kwanza,
Ubalozi wa Tanzania katika China hauko Hong Kong bali uko mjini Beijing
na Mheshimiwa Marmo hajawahi hata kufika Hong Kong. Taarifa kutoka Hong
Kong amekuwa anazipata kutoka kwa Balozi Mdogo wa heshima wa Tanzania
Mheshimiwa Clement Chan. Hata juzi, Ijumaa, Oktoba 26, Balozi Marmo
alikutana na Bwana Clement Chan. Balozi Marmo anapanga kutembelea Hong
Kong kwa mara ya kwanza mwishoni mwa mwezi ujao, Novemba, 2012. Angalia
ratiba ya Mheshimiwa Marmo katika wiki ya kwanza ya mwezi Julai mwaka
huu:
Julai Mosi, Balozi Mamro alikuwa
ofisini Beijing. Julai 2, Balozi alihudhuria Sherehe za Siku ya Mongolia
mchana na usiku alihudhuria Sherehe za Siku ya Djibouti kwenye Hoteli
ya Lengedane mjini Beijing. Siku nzima ya Julai 3 alishiriki katika
warsha ya Kampuni ya China Chemicals Techonologies Group ambayo inataka
kufungua viwanda cha madawa na mbolea nchini Tanzania. Asubuhi ya Julai
4, Balozi Marmo alikutana na ujumbe wa Kampuni ya Sichaun Honda Group
inayowekeza katika miradi ya Mchuchuma na Liganga na jioni ya siku hiyo
alikutana na ujumbe wa Kampuni ya Mawasiliano ya ZTE. Julai 5, Balozi
alihudhuria Sherehe za Siku ya Venezuala Day na Julai 6 alijiunga na
Mabalozi wa Nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki katika mkutano wa Forum
on Trade na Cooperation na jioni alihudhuria Sherehe za Rwanda Day.
Sasa, Balozi Marmo alikwenda lini Hong Kong kumpokea Mheshimiwa Rais
kama siyo uongo?
Katika
siku zinazotajwa, Bwana Ridhiwan alikuwa Dar es salaam muda wote. Kwa
hakika, Ridhiwan hajapata kufika Hong Kong ama China katika maisha yake
yote. Nchi pekee inayokaribia China ambayo amewahi kuitembelea ni Dubai
kwa sababu hata India hajapata kufika. Ratiba hizi za Mhe. Rais na
Mheshimiwa Marmo na ukweli kuwa Ridhiwan hajapata hata kufika China ama
Hong Kong ni ushahidi usiopingika kuwa Mzee Slaa kwa mara nyingine
ametunga, yeye amekuwa bingwa wa goofing. Huyu ni mtu anayezeeka vibaya.
Tunaamini kuwa ameanza kuchanganyikiwa pengine kwa kuzidiwa na jukumu
ya kulea mtoto-mjukuu na kumtunza mchumba Bi Josephine ambaye wanaishi
kama vimanda kwa sababu huyo mama bado anayo ndoa halali. Pole sana Mzee
Slaa kama Josephine na mwanae amekushinda