Wizara ya usalama ya Marekani 
(Pentagon) imetishia kumpeleka mahakamani mwanajeshi alieandika kitabu 
kuhusu jinsi yeye na wenzake walivyomuua gaidi Osama Bin Laden aliekua 
kiongozi wa Al Qaeda.
Mwanajeshi huyo aliekua kwenye 
kundi la wanajeshi wenye ujuzi wa hali ya juu alikua mtu wa pili kuingia
 chumbani alipokuepo Osama ambapo kwenye kitabu alichoandika anaeleza 
kwamba Osama hakua na silaha yoyote walivoingia chumbani kwake, taarifa 
ambayo inatofautiana na iliyotolewa na Pentagon.
Kanuni zinazoongoza oparesheni 
kama iliyomuua Osama zinawanyima wanajeshi waliohusika kutoa siri au 
kutangaza chochote ndio maana anaonekana kavunja makubaliano.
Sasa hivi vyombo vya habari 
vimeanza kuhusisha hicho kitabu na kampeni za urais jambo ambalo 
mwanajeshi huyo amelikataa na kusisitiza kwamba amekiandika hicho kitabu
 ili kuweka hadharani ukweli bila kulenga chama chochote cha siasa wala 
mgombea.
Matt Bissonnette(36) ambae 
hafurahii uongozi wa rais Obama, alikua hataki kutambuliwa kwenye vyombo
 vya habari lakini tayari jina lake limeshajulikana na limesambaa hivyo 
ilimlazimu kujificha.
