Kampuni ya Apple imesema imeuza simu yake mpya aina ya iPHONE 5 milioni 2 ndani ya masaa 24 baada ya kuizindua duniani kote. Mauzo hayo ni oda zilizotolewa kabla ya simu hiyo kuzinduliwa (pre oder). Vilevile kampuni hiyo imesema haitabadili siku ya kuitoa rasmi kwa wateja wake hao. Imebainisha kuwa itapeleka kwa wateja hao tarehe 21 septemba mwaka huu.