
Naibu Mstahiki Meya wa Halmashauri ya 
Ilala ambaye pia Diwani wa Kata ya Vingunguti Omary Kumbilamoto ameeleza
 sababu zilizopelekea Zahanati ya Vingunguti kufuzu na kupatiwa cheo cha
 nyota nne na serikali kupitia wakaguzi wake (TRN) na imekuwa miongoni 
mwa Zahanati tano zilizofuzu.
Akizungumza mara baada ya kupokea 
taarifa kutoka kwa Mwenyekiti  wa Kamati ya Zahanati Ibrahim Aeshi 
Nduze, Naibu Meya Kumbilamoto ameeleza kuwa hali ya mara ya kwanza 
katika zahanati hiyo haikuwa shwari lakini kwa jitihada zake na 
kushirikiana na Halmashauri na Serikali alifanikiwa kufanya mambo 
mbalimbali katika maboresho ya zahanati hiyo na hatimae imefanikiwa 
kupewa hadhi ya nyota nne.
Akiyataja mambo waliyoweza kuyafanya 
katika Zahanati hiyo ni pamoja na Ununuzi wa Gari ya Wagonjwa 
(Ambulance), Mashine ya Kufulia,Jenereta, Choo kwa kinamama 
wanaojifungua, utanuzi wa maabara, ufungaji wa feni nne, mashne tatu za 
kupmia uzito kwa watoto,kipimo cha presha na kiti cha kubebea wagonjwa.
Zahanati nyingine zilizoweza kupandishwa
 hadhi Halmashauri ya Ilala ni pamoja na Zahanati ya Tabata, Mongo la 
Ndege, Kinyerezi na Kadlugambwa.
Taarifa kutoka Kamati ya Zahanati 
imeeleza kuwa mwanzo zahanati yetu ilikua na nyota mbili ambapo hizo 
zahanati nyingine zilikua na nyota tatu hivyo vingunguti imepanda nyota 
mbili.
Kamati hiyo imewashukuru wananchi kwa 
mawazo, maoni, na changamoto walizozitoa ambazo zimezifanyiwa kazi na ku
 pelekea zahanati hiyo kupata nyota mbili za ziada, kamati memshukuru 
pia Diwani Omary Said Kumbilamoto kwa kuwaongoza, kuwashauri, na kutoa 
mchango wa hali na mali ii kufikia malengo.

