Young Africans imetoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu ya Coastal Union
 kutoka mkoani Tanga kufuatia bao la kusawazisha la penati ya utata 
dakika ya 90 ya mchezo la kiungo Jerry Santo baada ya Didier Kavumbagu 
kuifungia Yanga bao la kwanza.
Coastal Union ambayo katika mchezo wake wa awali dhidi ya JKT Oljoro 
ilipata  ushindi wa bao 2-0, ilicheza mchezo mbovu tangu mwanzo mwa 
mchezo hali iliyopelekea mwamuzi Martin Sanya ashindwe kulimudu pambano.
Yanga
 iliuanza mchezo kwa kasi kwa lengo la kusaka bao la mapema lakini 
kutokua makini kwa washambuliaji wake Jerson Tegete, Didier Kaumbagu na 
Simon Msuva kuliifanya ishindwe kupata bao kwa dakika 45 za kipindi cha 
kwanza.
Haruna Moshi 'Boban'  na Said Nyosso walionyeshwa kadi za 
njano katika kipindi cha kwanza kufuatia kuwachezea ndivyo sivyo 
wachezaji wa Yanga, ambapo wachezaji hao wa Coastal walishindwa 
kuonyesha soka la uungwana.
Kipindi cha pili cha mchezo kilianza 
kwa Yanga kufanya mabadiliko kwa kuwaingiza Hussein Javu na Hamis Thabit
 waliochukua nafasi za Jerson Tegete na Salum Telela aliyeumia katika 
kipindi cha kwanza.
Mabadiliko hayo yaliongeza uhai kwa timu ya 
Yanga kwani katika dakika ya 69 mshambuliaji Didier Kavumbagu aliipatia 
Young Africans bao la kwanza akimalizia pasi safi ya mlinzi wa pembeni 
David Luhende aliyewazidi uwezo walinzi wa Coastal Union na kumpasia 
mfungaji.
Baada ya kupata bao 
hilo Yanga waliendelea kufanya mashambulizi kupitia kwa washambuliaji 
wake Hussein Javu na Didier Kavumbagu lakini walinzi wa waliendelea 
kucheza ndivyo sivyo kwa wachezaji wa Yanga kana kwamba wanacheza mchezo
 wa mateke na ngumi.
Katika hali iliyowastaabisha wengi 
mwamuzi alimpatia kadi nyekundu Saimon Msuva baada ya kuchezewa vibaya 
na mlinzi wa Coastal Abdi Banda, huku watu wakisubiria mwamuzi amuadhibu
 Banda alimpatia kadi Msuva na kiungo wa Coastal Crispin Odula.
Dakika
 ya 90 mwamuzi Martin Sanya aliipatia Coastal Union penati ya utata 
kufuatia kiungo Haruna Moshi 'Boban' kumdanganya mwamuzi kuwa mlinzi 
Nadir Haroub 'Cannavaro' ameunawa mpira ndani  ya eneo la hatari na 
penati hiyo ilipigwa na Jerry Santo na kuwapatia bao la kusawzisha.
Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika Young Africans 1 - 1 Coastal Union.
Mara
 baada ya mchezo kocha mkuu wa Yanga Ernie Brandts amemtupia lawama 
mwamuzi wa mchezo Martin Sanya kwa kushindwa kuumudu mchezo na kusema 
katika mchezo wa  amekuwa mchezaji bora baada ya kushindwa kulimudu 
pambano.
Young Africans: 1.Ally Mustapha 
'Barthez', 2.Juma Abdul, 3.David Luhende, 4.Nadir Haroub 'Cannavaro' 
5.Mbuyu Twite, 6.Salum TelelaHamis Thabit , 7.Saimon Msuva, 8.Frank 
Domayo, 9.Didier Kavumbagu, 10.Jerson Tegete/Hussein Javu, 11.Haruna 
Niyonzima.
Coastal Union: 1.Shaban Hassan 'Kado',
 2.Juma Hamada, 3.Abdi Banda, 4.Marcus Ndehele, 5.Juma Nyosso, 6.Jerry 
Santo, 7.Uhuru Seleman/Seleman Kassim, 8.Haruna Moshi 'Boban', 9.Lutimba
 Yayo/Kenneth Masumbuko, 10.Crispin Odula, 11.Danny Lyanga/Razack 
Khalfani