
 
Siku
 chache baada ya mshambuliaji wa kimataifa wa Senegal Pappis Demba Cisse
 kutoa kauli yakugoma kuvaa nembo ya kampuni ya Wonga ambayo hutoa 
mikopo yenye riba , mchezaji wa pili ametoka na kuungana na Cisse kwenye
 msimamo huo wa kutovaa logo ya Wonga kwa kuwa kampuni hiyo inafanya 
biashara ambayo kwa mujibu wa misingi ya dini ya kiislamu ni Haramu.
Kiungo wa Ivory Coast ambaye atakuwepo uwanjani siku ya jumapili 
kucheza dhidi ya Taifa Stars Ismael Cheikh Tiote amesema kuwa atazungmza
 na wanasheria wake kuangalia  wa kutoivaa nembo hiyo . Tiotte kama 
ilivyo kwa Cisse ni muislamu anayefuata misingi yote ya dini hiyo na kwa
 mujibu wa sheria za dini yake riba kwenye mkopo unaotolewa kwa mtu 
mwingine ni haramu.
Newcastle United imesaini mkataba wa miaka minne na kampuni ya Wonga 
mkataba ambao umeifanya klabu hiyo kuingia kwenye utata na wachezaji 
wenye imani ya dini ya kiislamu . Newcastle United ina wachezaji 
wasiopungua watano ambao wamezungmzia kutokuwa tayari kuvaa nembo ya 
Wonga jambo linaweza kusababisha klabu hiyo kulazimika kuwauza wachezaji
 kama Pappis Cisse , Tiotte na wenzao kwani hawako tayari kutumiwa 
kwenye kampeni za matangazo ya kampuni hiyo.
.jpg)