Mchungaji Christopher Mtikila akifurahia ushindi baada ya kushinda kesi dhidi yake.
 
 
MWENYEKITI wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ameshinda kesi ya uchochezi iliyokuwa inamkabili.
Akizungumza
 baada ya kushinda kesi hiyo, Mtikila amesema, "Ushindi huu niliutarajia
 maana hata asubuhi kabla ya kuja mahakamani niliongea na Yesu na sasa 
amenijibu".
Mara baada ya kushinda kesi hiyo lilizuka timbwili 
lingine baada ya mtu mmoja kujitokeza akiwa na RB (Report Book) 
akimtuhumu Mchungaji Mtikila kuwa alimtishia kumuua na ni mwizi wa 
viwanja. Baada ya kutaka kukamatwa na polisi mmoja aliyekuwa na cheo cha
 Koplo, Mchungaji alikataa kwa madai kuwa yeye ni kiongozi wa kitaifa 
hivyo hawezi kukamatwa na polisi mwenye cheo cha Koplo, labda polisi 
mwenye cheo cha SSP (Senior Superintendent of Police). Kwa kauli hiyo 
polisi alishindwa kumtia nguvuni.
 
  
Mtikila
 amkimsikiliza Koplo wa Polisi mwenye RB Namba : KMR/RB/10482 yenye 
maelezo ya kutishia kuuwa kwa maneno na wizi wa viwanja iliyofunguliwa 
na bwana Gotta Ndungulu.
 
 
* 
"Hukumu dhidi ya Mwenyekiti wa Chama cha DP, Mchungaji Christopher 
Mtikila, iliyoahirishwa mara mbili kwa sababu ya hakimu kuwa na dharura,
 ilisomwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu a Hakimu Mkazi 
Mfawidhi, Illivin Mugeta aliyeisikiliza kesi hiyo ya kutoa maneno ya 
uchochezi.
Mtikila alikuwa akikabiliwa 
na mashitaka ya kusambaza waraka wa uchochezi dhidi ya Rais Jakaya 
Kikwete, kwamba anataka kuuangamiza Ukristo.
Mshitakiwa
 Mtikila alifunga ushahidi kwa kuwa na mashahidi wawili wa utetezi, 
akihofia kupoteza fedha za Serikali kwa kuwaleta mashahidi wengi ambao 
hawana kitu tofauti na mashahidi wengine waliokuwa wamewasilisha 
ushahidi wao mahakamani hapo.
Mtikila, 
anadaiwa kwamba, Aprili, 2010 Dar es Salaam, alisambaza waraka aliokuwa 
akidai ni wa kuunusuru Ukristo wenye lengo la kuangamizwa na Jihad ya 
Rais Jakaya Kikwete na kwamba Wakristo wajitoe mhanga kukomesha ugaidi, 
“Kikwete anaangamiza Ukristo, amekuwa jasiri wa kuingiza Uislamu katika 
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alidai Mtikila katika waraka
 wake huo.
Alidai waraka uliosambazwa 
alisaini akiwa kama Mwenyekiti wa Kamati ya Kuunusuru Ukristo na 
walichapisha nakala 100,000, lakini aligoma kutaja mahali 
walipochapishia nakala hizo. Maelezo yote hayo yalitolewa mahakamani 
kama kielelezo na ofisa wa polisi, SSP, Ibeleze Mrema aliyemuhoji 
Mtikila Aprili 14, 2010."